Wafanyabiashara wa Tanzania msipoteze uaminifu kwa manufacturers wa nje waliowaamini kwa kutolipia mizigo mliyopewa kwa mali kauli. peni pesa za watu

Wafanyabiashara wa Tanzania msipoteze uaminifu kwa manufacturers wa nje waliowaamini kwa kutolipia mizigo mliyopewa kwa mali kauli. peni pesa za watu

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Nimeandika kwa masikitiko makubwa sana baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya marafiki zangu manufacturers kutoka nchini India ambao hutengeneza na kuuza vifaa vya hospitali. Kuna wenzetu wameingia tamaa na kuishia kudhulumu watu waliowaamini na kuwapa mzigo bila kulipa chochote kwa makubaliano ya kulipa baadae.

Hii ni tabia mbaya sana na inawaharibia wafanyabiashara wadogo wanaoanza kutoaminiwa. Malalamiko ni makubwa na tayari ubalozi wa India hapa nchini una taarifa za hawa watanzania wenzetu wenye tabia za kipuuzi. Kwa leo ninayahifadhi majina yao ila ninawasihi waongee na hao manufacturers na kukubaliana jinsi ya kulipa madeni.

Pamoja na lawama wanazotupiwa ila wahindi ni watu poa sana kufanya nao biashara. Kukuinua ni fasta. Binafsi nina ushuhuda wao. Vilevile ninawashauri wafanyabiashara kuwa waache upuuzi wa kushangilia ushindi kabla ya mechi kwisha. Ukipata faida iongezee kwenye biashara (recapitalize) hadi biashara iimarike kiasi cha kutosha ndo uanze mambo ya kununua magari, plot na kujenga nyumba. Kwa mfano hawa wanaotuhumiwa kukimbia na hela za watu ni watu wenye majina town kwa kuendesha magari mazuri na kuishi poa kumbe kuna dhuluma wanafanya.
 
Uaminifu ni mali unaweza kusema ni tunu pia ukiweza kuwa mwaminifu hata kama hauna maokoto ni kama yapo tu maana unaweza kupewa mzigo na usilipe chochote hao watu wapo wachache sana saivi.
 
Nakubaliana na wewe lakoni hili tatizo la dola Tanzania ndio linaua kabisa credibility ya wafanya biashara kupokea credit kutoka viwandani. Mnakubaliana siku 30/60/90, halafu muda umepita benki zote hazina dola kucover miamala.

Pia wahindi wagumu kipokea currency yao INR kama malipo japo zipo benki za Tanzania zinazokuwa na INR wanalazimisha dola, mwisho hasara tupu
 
Back
Top Bottom