Wafanyabiashara waliopo Barabara ya Mpanda Hotel - Kigoma watengewe eneo la biashara, walipo sio salama kwao

Wafanyabiashara waliopo Barabara ya Mpanda Hotel - Kigoma watengewe eneo la biashara, walipo sio salama kwao

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
WhatsApp Image 2024-11-06 at 21.03.51_9e945121.jpg
Sisi Wananchi wa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi tunaomba uongozi wetu wa Manispaa uchukue hatua za haraka kuwaondoa wajasiriamali wanaoweka bidhaa pembezoni mwa Barabara ya Mpanda Hotel kwenda Kigoma kwa kuwa ni hatari kwa usalama wao na wale wanaotumia Vyombo vya Moto

Wananchi wa hapa tumekuwa tukipaza sauti kwa muda mrefu kuhusu hali hiyo kuanzia ngazi ya uongozi wa mtaa hadi wilaya lakini hakuna mafanikio yoyote.

Naomba wajasiriamali waondolewe barabarani kwa sababu iko siku isiyofahamika gari litaacha barabara na kusababisha mambo ambayo sipendi kuona yakitokea.

Nashauri Serikali itafute eneo zuri na salama ambalo litawawezesha wajasiriamali kuweka bidhaa zao, siwapingi wenzetu kufanya biashara ila tatizo ni kutokuzingatia usalama.
WhatsApp Image 2024-11-06 at 21.04.03_9a48ba0d.jpg

WhatsApp Image 2024-11-06 at 21.04.15_03b22dcc.jpg
 
Sisi Wananchi wa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi tunaomba uongozi wetu wa Manispaa uchukue hatua za haraka kuwaondoa wajasiriamali wanaoweka bidhaa pembezoni mwa Barabara ya Mpanda Hotel kwenda Kigoma kwa kuwa ni hatari kwa usalama wao na wale wanaotumia Vyombo vya Moto

Wananchi wa hapa tumekuwa tukipaza sauti kwa muda mrefu kuhusu hali hiyo kuanzia ngazi ya uongozi wa mtaa hadi wilaya lakini hakuna mafanikio yoyote.

Naomba wajasiriamali waondolewe barabarani kwa sababu iko siku isiyofahamika gari litaacha barabara na kusababisha mambo ambayo sipendi kuona yakitokea.

Nashauri Serikali itafute eneo zuri na salama ambalo litawawezesha wajasiriamali kuweka bidhaa zao, siwapingi wenzetu kufanya biashara ila tatizo ni kutokuzingatia usalama.
Ila hizo nyanya zinavutia sana
 
Uchaguzi unapokaribia ccm hujitia ina huruma sana na wananchi
 
Back
Top Bottom