Wafanyakazi 10 wa Mfalme wa OBC, Loliondo wapanda kizimbani

Wafanyakazi 10 wa Mfalme wa OBC, Loliondo wapanda kizimbani

Natimiza ahadi yangu Mtanzania halisi kwa kiapo cha kuipenda,kuitumikia ,kuitetea na kuilinda nchi yangu ya Tanzania.
Ni fahari ya kujivunia kuwepo kwa mfalme wa kiarabu katika chaguo lake katika ardhi ya Tanzania. Nchi za Afrika zenye vivutio vya utalii visivyopishana sana na vyetu hapakuwa na upenyo wa kutushinda. Ni dhahiri Tanzania imesheheni uzuri wa vivutio.
Ni tosha kuthibitisha kuwa Tanzania ipo juu,juu,juu zaidi.
Ni aibu kumkosa . Seuze tunae?!
Tunajivunia , Tunampenda ,Tunamuenzi .
Je? Ni mpita njia? La hasha! Tokea mwaka 1992 mpaka sasa amedumu kwa miaka 27.
Si mgeni tena ni mwenyeji. Tokea uhai wa Baba wa Taifa. Ni sisi.
Emirates airline inayomilikiwa na ndugu ya mfalme huyo ambayo ilishiriki kikamilifu kuutangaza mlima kilimanjaro. Miaka ya nyuma niliwahi kupanda ndege hiyo kutoka dubai kuja dar kwa mara ya kwanza niliuona mlima kilimanjaro kwa juu. Na walitoa maelezo yake huku tukiupita. Sasa imesitishwa.sifahamu kwanini na sijui kwa zile routes za kutoka Nairobi kama zinaendelea kuonyesha Mlima Kilimanjaro.Wengi wa watalii wanatoka huko makundi ya wafanyakazi wa makampuni kuja katika utalii wa hapa nchini na kuupanda mlima Kilimanjaro. Na mengine mengi ambayo Sisi tunaendelea kwa ulaini kula matunda ya ardhi yetu kwa kupitia chaguo lao.
Hawapo hapa sababu ya shida zao ,wala kuwapokea sio ujinga wetu. Tusiwe wapayukaji tukasahau thamani ya uwepo wao. Tuwe Makini na tusiende kombo kwa dhana za upotoshaji.
Enzi za Baba wa Taifa Watanzania tulisifika na kujijengea heshima kwa tabia za upendo na amani husan kwa wageni. Nakumbuka ilikuwa maagizo kuwa mgeni ahudumiwe asipate usumbufu kama mwenyeji.Foleni ya sukari akitokea mgeni huenda moja kwa moja akapata huduma.Watu walikuwa maridhia, sasa tunashuhudia hakuna kumpisha mzee katika kiti.Adabu na heshima zile zimepotea.
Namsifu Baba Magufuli amerudisha heshima ya watanzania. Tukienda Kenya wanatufurahia Tunaaminika ni watu wasio na vitisho, ghasia wala usumbufu.na kwengineko.
Ni matumaini yangu Mheshimiwa Rais Magufuli utaliona na katika Ujenzi wa Taifa letu basi utamaliza vikwazo,Fitina na Usumbufu uso na lazima na Wageni wetu wakae kwa Furaha na Amani.
TUMTANGULIZE MUNGU KATIKA KILA JAMBO LETU
MUNGU IBARIKI ARUSHA
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU IBARIKI AFRIKA
 
E
Wafanyakazi 10 raia wa kigeni wenye asili ya Asia wa kasri la mfalme wa Abu dhabi inayosimamiwa na Kampuni ya Ortelo Business Coparation(OBC) iliyopo eneo la Loliondo wilayani Ngorongoro,Mkoani hapa wamepandishwa kizimbani kwa kosa la kufanyakazi nchini kinyume cha sheria za ajira kwa wageni .

Wakisomewa mashtaka mapema leo mbele ya Hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha, Niku Mwakatobe Mwendesha mashtaka wa Idara ya kazi mkoani hapa, Immanuel Mweta alidai kuwa mnamo Novemba 2018 hadi januari 2019 washtakiwa hao walitenda kosa la kufanya kazi kinyume na sheria ya kuratibu ajira za wageni.

Mweta aliwataja washtakiwa hao kuwa ni Darweshi Jumma,Riaz Aziz Khan,Mohammad Tayyab,Ali Bakhash,Abdulrahman Mohammed,Martin Crasta,Imtiaz Feyaz,Arshad Muhammad,hamza Sharif na Zulfiqar Ali ambao wanashitakiwa kwa kosa la kufanyakazi kinyume cha sheria za uratibu wa wageni na kutokuwa na vibali vya kufanyakazi nchini.

Washtakiwa hao ambao walikuwa hawajui lugha ya Kiswahili wa kiingereza na kutumia mkalimani aliyetambulika kwa jina la Muazamu Husein walikana makosa yao na kusema kuwa kampuni hiyo iliwaleta bila wao kujua chochote na wana uhakika na vibali walivyo navyo.

Washtakiwa hao walikuwa wakiwakilishwa na mawakili wawili Godluck Peter akisaidiana na Daud Haraka wakili haraka aliiomba mahakama kuwapatia dhamana washtakiwa hao kwani kosa linalo wakabili linastahili dhamana.

Wakili wa Upande wa mashtaka ,Mweta alidai hawana pingamizi lolote juu ya dhamana ya washtakiwa ila dhamana ifuate utaratibu wa mahakama.

Hakimu Mwakatobe alisema dhamana kwa washtakiwa wote ipo wazi na kila moja anapaswa kuwa na wadhamini wawili wenye barua za utambulisho na vitambulisho na mali kauli ya thamani ya million Tano.

Washtakiwa hao walikidhi dhamana na wapo nje na kesi hiyo imeahirishwa hadi Tarehe 22 mwezi 2 mwaka huu itakapotajwa tena.

Akiongea nje ya Mahakama,Afisa wa idara ya kazi mkoa wa Arusha, Alfred Mdumi alisema watuhumiwa hao walikamatwa juzi na maofisa wabuhamiaji mkoani hapa wakati wakijaribu kutoroka kuelekea nchini Dubai.




View attachment 1015859View attachment 1015861

Sent using Jamii Forums mobile app
Mfalme mwwnyeheri Jiwe hakuwachekea hawa jamaa
 
Back
Top Bottom