Hapa huenda tunachanganya vitu viwili, kugushi cheti na kutumia cheti toka chuo ambacho hakina accreditation ni vitu viwili tofauti.
Tumshukuru Prof. Ndullu maana japo yeye kajaribu. Ni rahisi sana kupata matokeo halali ya form four na six na kisha kulinganisha.
Tatizo liko kwa serikali ambayo imeshindwa kutunga sheria zenye meno za kuwashughulikia wale wanaogushi vyeti vya elimu za juu.
Kwa mfano huwezi kumshitaki Nchimbi kwa kugushi cheti, ingawaje kama nchi inaweza isitambue cheti chake na hivyo kumfanye yeye asijiite Dr.
Pia kuna jambo lingine ambalo linachanganya Tanzania. Nafikiri hata uwe na Ph.D unapoomba kazi lazima utoe na matokeo ya form four, hapo ndipo kugushi kunaanza. Wengine huko nyuma walikuwa na matokeo mabaya au kuna watu wamesahau matokeo yao.
Kwenye hili mimi nampongeza prof. Ndullu, japo ni hatua ndogo lakini angalau yeye ameanza. Laiti spika Sitta na yeye akaanza na wabunge, JK na mawaziri wake nk. huenda tukasogea kidogo.