Wafanyakazi sasa kujiachia na Riba hadi asilimia 14 kutoka benki ya CRDB

Wafanyakazi sasa kujiachia na Riba hadi asilimia 14 kutoka benki ya CRDB

Feld Marshal Tantawi

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2014
Posts
655
Reaction score
1,069
Benki ya CRDB imezindua kampeni maalumu ijulikanayo kama “Jiachie Utakavyo” ambapo wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi sasa kufurahia riba ya hadi asilimia 14. Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa habari Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati, Boma Raballa alisema benki imefanya maboresho makubwa katika mikopo ya wafanyakazi ili kuwapa unafuu na kuwawezesha kufikia malengo yao waliyojiwekea.

“Jiachie Utakavyo inamaanisha kuwa wafanyakazi sasa wana wigo mpana zaidi wa kukopa, kwa gharama nafuu, kwa muda mrefu na uhuru wa kuchagua wanachotaka,” alisema Boma Raballa. Raballa alisema pamoja na kumpa uhuru mteja wa kujiachia kwa kuutumia mkopo atakavyo, Benki ya CRDB pia imempa uhuru mteja kuchagua muda wa kulipa mkopo anaoendana na matakwa yake na kiwango cha riba anachotaka kulipa.

“Kwenye jiachie utakavyo mteja ana uhuru wa kuchagua muda wa kulipa iwe ni mwaka 1, 2, 3, mpaka 7, na vivile mteja atakuwa anachagua riba anayotaka kuanzia asilimia 14 mpaka 16,” alisema Boma Raballa huku akibainisha kuwa kampeni hiyo ya “Jiachie Utakavyo” inawapa fursa wafanyakazi kukopa hadi shilingi milioni 100.

Akizungumzia kuhusiana na maboresho hayo ya mikopo ya wafanyakazi, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Stephen Adili alisema Benki ya CRDB inatambua mchango mkubwa unaotolewa na wafanyakazi wa taasisi za Umma mna sekta binafsi, hivyo basi maboresho hayo ni motisha kwa wafanyakazi kusaidia kufikia malengo yao.

“Tunafahamu changamoto tulizopitia katika kipindi hiki, na wafanyakazi wetu wamekuwa mstari wa mbele kukatika kutuhudumia katika kila nyanja, kampeni hii ya Jiachie Utakavyo ni sehemu ya shukrani kwa wafanyakazi wote, lakini pia kuwasaidia kufikia malengo yao,” alisema Adili.

Kwa upande wake Meneja mwandamizi Mikopo ya Wafanyakazi, Farida Hamza alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wafanyakazi wote nchini kuchangamkia fursa hiyo ya “Jiachie Utakavyo”, huku akibainisha kuwa mteja ana uhuru wa kutumia mikopo hiyo atakavyo ikiwa ni pamoja na kulipia ada za Watoto, kijiendeleza kimasomo, kuanzisha na kuendeleza biashara na matumizi mengine apendayo.

“Mikopo hii si kwa wateja wa Benki ya CRDB tu ni kwa wafanyakazi wote nchini, kama mfanyakazi anamkopo benki nyengine, Benki ya CRDB inautaratibu wa kununua mikopo ili kuwafanya wafanyakazi wote waweze kujiachia watakavyo na Benki yao pendwa ya CRDB,” alisema Farida huku akibainisha mikopo hiyo inatolewa ndani ya saa 24 mteja napokamilisha maombi ya mkopo.

Ili kupata mkopo huo wafanyakazi wanatakiwa kutembelea tawi la Benki ya CRDB lililo karibu na kujaza fomu ya maombi ya mkopo ambapo atatakiwa kuambatanisha vielelezo vifuatavyo; Kitambulisho kinachotambuliwa - cha utaifa/ kura/ leseni ya udereva na kitambulisho cha kazi, Hati ya mshahara (Salary slip) iliyothibitishwa kwa kipindi cha miezi mitatu, Mkataba wa kazi/ barua ya uteuzi, barua ya utambulisho, barua ya uthibitisho kazini.
 
Gari ni muhimu kwa miaka hii,
litakusaidia kwenda kuishi utakako hata kama ni Kibaha, kuliko enzi zile kubanana Magomeni Mapipa/Idrisa

Gari litakufanyia shughuli nyingi ikiwemo Hospital, sokoni, kupeleka watoto shule kuliko kudandia UDA

Petrol imeshuka na itashuka licha ya magari nayo kushuka
kujenga nyumba ifuate baada ya gari, kwani huwezi tu kutoka Chuo unaanza ajira eti uuantembea kwa miguu na bodaboda kupakia cement hadi Mbezi au Mabwepande kuchimba msingi wa nyumba

MAMBO YA KIZAMANI SANA HAYO, NYUMBA WAACHIENI wenye familiakubwa au wastaafu
 
Sikiliza wewe.. nikichukua for 14 wanatakiwa tukubaoiane kwamba hiyo 14 haitabirika hadi miaka 7 iishe.

Most or banks ni waongo, unachukua mkopo.kwa hiyo 14 mwakani utasikia stoey za uchumi inabidi iende 19.

Kuweni makini , pamoja na hiyo 14 bank inatafuta faida
Benki ya CRDB imezindua kampeni maalumu ijulikanayo kama “Jiachie Utakavyo” ambapo wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi sasa kufurahia riba ya hadi asilimia 14. Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa habari Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati, Boma Raballa alisema benki imefanya maboresho makubwa katika mikopo ya wafanyakazi ili kuwapa unafuu na kuwawezesha kufikia malengo yao waliyojiwekea.

“Jiachie Utakavyo inamaanisha kuwa wafanyakazi sasa wana wigo mpana zaidi wa kukopa, kwa gharama nafuu, kwa muda mrefu na uhuru wa kuchagua wanachotaka,” alisema Boma Raballa. Raballa alisema pamoja na kumpa uhuru mteja wa kujiachia kwa kuutumia mkopo atakavyo, Benki ya CRDB pia imempa uhuru mteja kuchagua muda wa kulipa mkopo anaoendana na matakwa yake na kiwango cha riba anachotaka kulipa.

“Kwenye jiachie utakavyo mteja ana uhuru wa kuchagua muda wa kulipa iwe ni mwaka 1, 2, 3, mpaka 7, na vivile mteja atakuwa anachagua riba anayotaka kuanzia asilimia 14 mpaka 16,” alisema Boma Raballa huku akibainisha kuwa kampeni hiyo ya “Jiachie Utakavyo” inawapa fursa wafanyakazi kukopa hadi shilingi milioni 100.

Akizungumzia kuhusiana na maboresho hayo ya mikopo ya wafanyakazi, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Stephen Adili alisema Benki ya CRDB inatambua mchango mkubwa unaotolewa na wafanyakazi wa taasisi za Umma mna sekta binafsi, hivyo basi maboresho hayo ni motisha kwa wafanyakazi kusaidia kufikia malengo yao.

“Tunafahamu changamoto tulizopitia katika kipindi hiki, na wafanyakazi wetu wamekuwa mstari wa mbele kukatika kutuhudumia katika kila nyanja, kampeni hii ya Jiachie Utakavyo ni sehemu ya shukrani kwa wafanyakazi wote, lakini pia kuwasaidia kufikia malengo yao,” alisema Adili.

Kwa upande wake Meneja mwandamizi Mikopo ya Wafanyakazi, Farida Hamza alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wafanyakazi wote nchini kuchangamkia fursa hiyo ya “Jiachie Utakavyo”, huku akibainisha kuwa mteja ana uhuru wa kutumia mikopo hiyo atakavyo ikiwa ni pamoja na kulipia ada za Watoto, kijiendeleza kimasomo, kuanzisha na kuendeleza biashara na matumizi mengine apendayo.

“Mikopo hii si kwa wateja wa Benki ya CRDB tu ni kwa wafanyakazi wote nchini, kama mfanyakazi anamkopo benki nyengine, Benki ya CRDB inautaratibu wa kununua mikopo ili kuwafanya wafanyakazi wote waweze kujiachia watakavyo na Benki yao pendwa ya CRDB,” alisema Farida huku akibainisha mikopo hiyo inatolewa ndani ya saa 24 mteja napokamilisha maombi ya mkopo.

Ili kupata mkopo huo wafanyakazi wanatakiwa kutembelea tawi la Benki ya CRDB lililo karibu na kujaza fomu ya maombi ya mkopo ambapo atatakiwa kuambatanisha vielelezo vifuatavyo; Kitambulisho kinachotambuliwa - cha utaifa/ kura/ leseni ya udereva na kitambulisho cha kazi, Hati ya mshahara (Salary slip) iliyothibitishwa kwa kipindi cha miezi mitatu, Mkataba wa kazi/ barua ya uteuzi, barua ya utambulisho, barua ya uthibitisho kazini.
 
Safi sana kama ni kweli,Je sie wafanyabiashara ndogo ndogo tumejumuishwa?
 
1591041367508.jpg
 
Safi sana kama ni kweli,Je sie wafanyabiashara ndogo ndogo tumejumuishwa?
Mkuu Benki Kuu BOT ndiye anayetoa Mikopo hiyo kwa hiyo Benki km CRDB alikuwa ana taasisi ndogo kama Saccos ambapo alizikopesha, wapo AKIBA benki na ana vikundi vidogo vidogo, na wafanyabiashara wenye Leseni na TIN, hiyo CRDB iliweza kuwakopesha Madiwani na Wabunge Nchi nzima ikiwakata Mishahara yao haitashindwa biashara hiyo
Kuna mahali Waziri Mpango wa Fedha na Mipango alisema watapunguza Riba kwa Mabenki, baada ya wote kuwa chini yao, nina hakika hawatashindwa, na hapo keshawabana wakopeshaji wa mitaani
 
Ukiona kiwango Cha Riba Kinatamkwa "............Hadi Asilimia 14" na siyo Fixed ujue kuna Janja Janja ITAHUSIKA.

It's a kind of marketing lip service.
 
Nyinyi mkalipie kwanza vile vitambulisho vyenu vya Ujasiriamali kwanza maana vimeshatoka! Hii ofa ni kwa Wafanyakazi tu!! Yaani wanataka watukopeshe mpaka milioni 100!! Mbona mtaani kutachimbika.

Hakika CRDB ni Baba lao!
Aiseee kweli baba lao sie wajasiliamali imekula kwetu,nyie wafanyakazi mtumie hela zenu vizuri msije kufungiwa ndani na watoto wa kitanga mkatapakanya 100m.
 
Back
Top Bottom