Elections 2010 Wafanyakazi: Tutampigia kura Jakaya Kikwete

Elections 2010 Wafanyakazi: Tutampigia kura Jakaya Kikwete

Mimi hii habari inatia kichefuchefu sitaki hata kuisoma na hao waliohojiwa nao loh!! kweli maisha bora kwa kila mtanzania aliyehojiwa na kujibu upupu huu
Pole sana.Vumilia tu Baada ya muda hali itakuwa shwari. na utajilaumu kwa nini hukusoma mapema.I wish you all the best
 
Kama source ni global publishers hakuna haja ya kupotez muda kujadili , UMBEA MTUPU
 
Kwanza mwandishi si mtafiti tusimlaumu: Kitaalam sampuli ya wafanyakazi aliowahoji sidhani matokeo yake yanatosha kujumuisha kwa wafanyakazi wote nchini. Pili kusema mishahara imeongezeka ni sawa ila swali dogo la kujiuliza ni kiasi gani cha bidhaa cha nyongeza ya shilingi inaweza kununua. Ukishapata jibu utajua kitaalam hakuna nyongeza yoyote ambayo ni dhahiri....Mungu awanusuru Watanzania kwa vile hata wasomi kama nyinyi waaandishi mnashindwa kujenga hoja....itakuwa kwa wakulima huko vijijini ambao hata hawana mishahara!!!
 
s5kavs.jpg

Rais Jakaya Kikwete


Na Waandishi Wetu
Wakati Shirikisho la Vyama vya Wanyakazi nchini (TUCTA) likidaiwa linajipanga kutoa tamko la kuwataka wafanyakazi wote nchini kutompigia kura Rais Jakaya Kikwete kwenye Uchaguzi Mkuu 2010, inaonekana mambo ni kinyume.

Sehemu kubwa ya wafanyakazi wanaeleza kufurahishwa na utawala wa JK, hivyo kuwa tayari kumuongezea kipindi kingine cha uongozi cha miaka mitano (2010-2015).

Wafanyakazi waliozungumza na gazeti hili kwa wiki nzima iliyopita, Dar es Salaam, walieleza kufurahishwa na kazi ya JK aliyoifanya Ikulu kwa miaka mitano, hivyo wanaamini ataendeleza mazuri endapo ataongezewa kipindi kingine.

Walisema kuwa Rais Kikwete ameweza kuonesha moyo mzuri kwa kuongeza mishahara ya wafanyakazi mara kwa mara pia kukabiliana na ufisadi, hivyo hawaoni sababu ya kuliunga mkono TUCTA endapo litasema JK asipigiwe kura.
Baadhi ya maoni ya wafanyakazi kama walivyozungumza ni kama ifuatavyo;

ITUS BILLA
Mfanyakazi wa Kampuni ya Big Bell.
Anasema: “Nafurahia kipindi chote cha Kikwete kuwepo madarakani, maana mengi aliyoahidi ametekeleza. Nawashauri Watanzania wenzangu tumuongezee kipindi kingine aweze kuleta maendeleo zaidi. Kuhusu nyongeza ya mshahara mimi naona maisha yatakuwa yale yale kwani kila mshahara ukitangazwa kupanda na bidhaa nazo zinapandishwa.”


2z8utlu.jpg

Itus Billa

SULEIMAN MAZINGE
Anasema: “Utawala wa Rais Jakaya Kikwete ni mzuri kwani nchi ina amani na hakuna njaa wala migogoro na hilo ndilo jambo kubwa, mambo mengine ni majaaliwa. Kuhusu ongezeko la mishahara hapo hakutakuwa na jipya kwani uzoefu unaonesha mishahara ikipanda na huduma nazo zinapanda.”

devc3q.jpg

Suleman Mazinge

ANNA LUWENA
Anasema: “Utawala wa Rais Kikwete ni mzuri na anaomba uendelee ingawa hauna tofauti kubwa na tawala zingine zilizopita. Kuhusu kupanda kwa mishahara ni bora ingebaki palepale kwani ongezeko la mishahara litasababisha kuongezeka maradufu kwa gharama za huduma mbalimbali.”

r938nc.jpg

Anna Luwena


HUSSEIN MAKUBI
Anasema: “Utawala wa Rais Kikwete ni mzuri kwani ameendeleza mazuri yaliyoachwa na marais waliopita. Kuhusu mishahara mwanzoni wananchi watafurahia ongezeko hilo lakini siku zinavyokwenda huduma nazo taratibu zitapanda na kufanya hali kuwa ile ile.”

BABY OMARY
Anasema: “Utawala wa Rais Kikwete ni mzuri hakuna dosari kubwa iliyojionesha ukilinganisha na tawala zilizopita.
Ongezeko la mishahara linatokana na kusonga kwa dunia lakini halina uhusiano wowote na ubora wa maisha kwani hapo zamani mfanyakazi alilipwa 6000/ (elfu sita) mfanyakazi huyo sasa hivi analipwa 600,000/ (laki sita) lakini maisha yake ni yaleyale afadhali ya zamani.

xek569.jpg

Baby Omary

HADIJA HASSAN
Mfanyakazi wa Kampuni ya Vodacom anasema: “Utawala wa Rais JK ni mzuri na hasa kwa kuwa ametoa ajira kama alivyoahidi, hivyo kuwakomboa Watanzania. Ongezeko la mishahara anasema litakuwa na mafanikio kwa wenye malengo lakini wasio na malengo wataendelea kuumia.”


GHONCHE MATEREGO
Katibu Mtendaji wa BASATA, anasema: “Rais Kikwete uongozi wake ni mzuri sana pia ni mtu anayeona mbele zaidi ndiyo maana anawapa vijana kipaumbele tena anapenda kuwarithisha ili baadaye wawe viongozi wanaofaa kuongoza nchi. Amekuwa ni mchango mkubwa sana kwa vijana, lakini hajawaacha wazee anawataka kuelimisha vijana wao ili waweze kujikwamua kimaisha.

“Kwa upande wa mshahara kuongezwa hilo nalo ni jambo la heri na serikali imetimiza ahadi yake kwani kilikuwa ni kilio cha siku nyingi na sasa imefikia mahali na kuongeza tunashukuru kwa kutimiza ahadi hiyo.”

MBAZI OMBENI
Karani wa BASATA, anasema: “Utawala wa Rais Kikwete siyo mbaya sana lakini kuna ahadi ambazo naomba kama akichaguliwa tena awamu ya pili azitekeleze. Shule za Kata zimejengwa nyingi lakini vitendea bado tatizo, naomba aliangalie hilo pamoja na mfumuko wa bidhaa sokoni.

“Suala la mishahara kuongezwa nashuru kwa sababu kilikuwa kilio chetu cha siku nyingi.”

SOURCE: Global Publishers aka. Shigongo

Hii siyo sehemu ya udaku. Pia sitegemei Global publishers watoe kitu kilichokinyume na mkuu wakati juzi katoka kumwomba Shigongo avumilie next term atapata kilichompeleka mwanza.
 
Mmi pia nitampa kura yangu Jakaya mwana wa Kikwete .Anaelezeka.
Tatizo lako ni ufahamu mdogo ulionao. Kikwete anaelezeka vipi? amewadanganya kuhusu ufisadi mnapiga makofi, Hataki kubadilisha katiba mnapiga makofi. Kitu ninacho kiona kwako ni kuwa huna uzalendo wa kweli unachoangalia ni tumbo lako tu, ndo maana unasema kikwete(mafisadi) wanaelezeka. Tafakari sana kwa kina kuhusu nchi yako imetoka wapi na inaelekea wapi. Mambo yanapokuwa mabaya tunawalaumu viongozi, badala ya kujilaumu sisi wenyewe,tunapewa nafasi ya kutafakari na kuchagua viongozi wanaotufaa sisi tunakimbilia CHAMA,HATUTAKI KUFIKIRI.
 
Nia tunayo,elimu tunayo,sababu tunayo.kazi ikiyobaki ni moja tu.TUTAMPA KURA ZETU
Sioni ajabu kusema kuwa utampa kikwete kura, Maana nina amini kitu kimoja watu wanaofaidika na ufisadi wa CCM, wataipigia kura CCM. bila kujali madhala yatakayotupata hapo baadaye kama nchi. Ninakumbuka nilipata kufanya kazi katika Halmashauri moja. Katika halmashauri ile watu walimchukia sana Dr. Silaa(mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za serikali za mitaa) walikuwa wakisema huyu Silaa ni mtu asiyependa rushwa, hivyo anaharibu ulaji wao. Hao wote najua hawatampigia Kura Dr. Silaa kwama si kiongozi mzuri bali watamnyima kura kwa sababu ni muadilifu.Ndo maana naona wazalendo wa nchi hii ni wachache kabisa.
 
Sishangai watakaompa kura kikwete maana wengi ni wale waliokosa elimu hivyo wakazibwa milango yao yote ya FAHAMU
Nakubaliana na wewe kabisa ndio maana CCM imekuwa ikitamba na kufanya inavyotaka kwasababu wanajua watanzania ni wajinga na ni wavivu kufikiri.
 
Mimi hii habari inatia kichefuchefu sitaki hata kuisoma na hao waliohojiwa nao loh!! kweli maisha bora kwa kila mtanzania aliyehojiwa na kujibu upupu huu
Tatizo kubwa watu wengi sana hawafanyi a realistic country wide evaluation ya situation kisiasa ilivyo nchini.CCM watashinda tu, tena kwa wingi wa kura.
CCM iko madarakani,CCM wanabajeti kubwa,CCM ina wanachama wengi tu mijini na mikoani.Kutegemea chama chochote kingine kushinda is at best wishful thinking!
Ride with the winner.
 
Hao wengine wanaonekana kuwa machagu kule Ohio. "2010 HATUDANGANYIKI"
xek569.jpg


Shigongo anatuletea machangudoa eti wafanyakazi wamesema, huyu changu kabisa namfahamu hushinda pale kinondoni makaburini, kwa wakazi wa kinondoni tembelea kuanzia saa 2 usiku utamkuta buku tu. HATUDANGANYIKI.
 
xek569.jpg


Shigongo anatuletea machangudoa eti wafanyakazi wamesema, huyu changu kabisa namfahamu hushinda pale kinondoni makaburini, kwa wakazi wa kinondoni tembelea kuanzia saa 2 usiku utamkuta buku tu. HATUDANGANYIKI.

Naye mfanyakazi na mpiga kura
 
Tatizo kubwa watu wengi sana hawafanyi a realistic country wide evaluation ya situation kisiasa ilivyo nchini.CCM watashinda tu, tena kwa wingi wa kura.
CCM iko madarakani,CCM wanabajeti kubwa,CCM ina wanachama wengi tu mijini na mikoani.Kutegemea chama chochote kingine kushinda is at best wishful thinking!
Ride with the winner.
Akili mfilisi kabisa Mandela angesema ride with the winner Afrika kusini isingekuwa hivi leo, ukikata tamaa kata kivyako subiri wengne wakupiganie.
 
Kumbe zile habari za kusema kuwa JK hafai ni uzushi tu, wafanyakazi wanamfagilia.
 
Ni vema kuhoji wafanyakazi kujua wana msimamo gani. Ila wasi wasi wangu mbona umehoji kwenye sector moja tu? Hawa uliowahoji ni manager wa bar na wahudumu wake(bar maids). Kibaya zaidi hawakuwa kwenye akili zao, kwani walikuwa wameshiba offer ya keep change za wateja.

SLAA FOR PRESIDENT 2010, DON'T BE DESEIVED!!
 
Wana JF wala msikonde. Nimepata habari hivi punde kwamba picha za JK alizoanguka Jangwani ziko YouTube. Naomba mwenye nazo a-post nione tafadhali, then nitamjibu Shigongo
 
Akili mfilisi kabisa Mandela angesema ride with the winner Afrika kusini isingekuwa hivi leo, ukikata tamaa kata kivyako subiri wengne wakupiganie.
Sawa Mkuu but you have not argued your case to win this ballot.Mandela na South Africa kwa taairfa yako is another case altogether, the majority was behind Mandela, just as the majority is behind CCM.
Matusi mengi hayajawahi kushinda kura, it just reflects ones stupidity.
 
Back
Top Bottom