Strong ladg
Senior Member
- Jul 15, 2021
- 170
- 445
Wafanyakazi wa kampuni ya kutengeneza magari ya Volkswagen ya huko Ujerumani walianza mgomo mnamo Jumatatu ya tarehe 2 Disemba 2024.
Wafanyakazi hao walianza mgomo kupinga hatua zilizotangazwa na uongozi ambazo ni kupunguza pensheni pamoja na kufunga viwanda vitatu vya kampuni hiyo nchini Ujerumani.
Uongozi wa Volkswagen ulisema kwamba hatua hizo ni za lazima ili kukabiliana na hali ngumu ya kiuchumi inayoikumba kampuni hiyo. Ripoti ya fedha ya robo ya tatu ya mwaka 2024 ilionesha kuwa faida ya Kampuni ya Volkswagen ilishuka kwa asilimia 64.
Endapo Volkswagen itavifunga viwanda vyake vitatu vya nchini Ujerumani, familia nyingi zitaathirika kwa sababu Volkswagen ndio kampuni inayoongoza kwa kuajiri wafanyakazi wengi zaidi nchini humo.
Kampuni ya Volkswagen imejikuta katika hali mbaya ya kiuchumi kutokana na ushindani mkali kutoka nchini China. Vilevile gharama za uzalishaji zimeongezeka katika viwanda vingi vya nchini Ujerumani baada ya nchi zinazounda umoja wa ulaya (EU) kuacha kununua gesi moja kwa moja kutoka Urusi ikiwa ni sehemu ya vikwazo walivyoiwekea nchi ya Urusi baada ya kuanza kwa vita ya Ukraine mwaka 2022.
Chanzo/ Source: DW
"Volkswagen workers strike at factories across Germany – DW – 12/02/2024" Volkswagen workers strike at factories across Germany – DW – 12/02/2024
Wafanyakazi hao walianza mgomo kupinga hatua zilizotangazwa na uongozi ambazo ni kupunguza pensheni pamoja na kufunga viwanda vitatu vya kampuni hiyo nchini Ujerumani.
Uongozi wa Volkswagen ulisema kwamba hatua hizo ni za lazima ili kukabiliana na hali ngumu ya kiuchumi inayoikumba kampuni hiyo. Ripoti ya fedha ya robo ya tatu ya mwaka 2024 ilionesha kuwa faida ya Kampuni ya Volkswagen ilishuka kwa asilimia 64.
Endapo Volkswagen itavifunga viwanda vyake vitatu vya nchini Ujerumani, familia nyingi zitaathirika kwa sababu Volkswagen ndio kampuni inayoongoza kwa kuajiri wafanyakazi wengi zaidi nchini humo.
Kampuni ya Volkswagen imejikuta katika hali mbaya ya kiuchumi kutokana na ushindani mkali kutoka nchini China. Vilevile gharama za uzalishaji zimeongezeka katika viwanda vingi vya nchini Ujerumani baada ya nchi zinazounda umoja wa ulaya (EU) kuacha kununua gesi moja kwa moja kutoka Urusi ikiwa ni sehemu ya vikwazo walivyoiwekea nchi ya Urusi baada ya kuanza kwa vita ya Ukraine mwaka 2022.
Chanzo/ Source: DW
"Volkswagen workers strike at factories across Germany – DW – 12/02/2024" Volkswagen workers strike at factories across Germany – DW – 12/02/2024