Wafanyakazi wamemkubali Rais Samia, wamekula “Bata”

Wafanyakazi wamemkubali Rais Samia, wamekula “Bata”

jmushi1

Platinum Member
Joined
Nov 2, 2007
Posts
26,329
Reaction score
25,263
Wanajamvi, Leo nimesikiliza madam President Samia Suluhu Hassan mwanzo mwisho. Mimi siyo mfanyakazi, lakini niliikubali hotuba yake na kuona busara nyingi sana ndani yake.

Hata hivyo, sikuwa najuwa wafanyakazi wenyewe wameipokeaje hotuba hiyo. Jibu nililipata mtaani.

Kwa kifupi sana, wafanyakazi leo wamekula bata mbaya kabisa. Wakiwa wenye furaha na matumaini.

Siyo tu matendo yao yalionyesha hayo, bali hata nyuso zao. Sikuamini mimi mwenyewe nikaanza kuwauliza maswali kiudadisi tu. Walinihakikishia kuwa furaha yao imetokana na hatua za mama kwenye hotuba ile! Nilishangazwa na uelewa wao! Nikajuwa nao wakiona kama mimi nilivyoona!

Pamoja na kwamba hawakuongezewa mishahara, lakini hatua alizochukuwa kama mfano punguzo la PAYE kwa asilimia moja, malipo ya deni la mikopo ya vyuo kwa asilimia sita pamoja na utegemezi wa bima kutoka miaka 18 hadi 21, ni zaidi hata ya nyongeza za mishahara.

Na ukizingatia kwamba ameahidi kuanzia mwaka ujao kufanya hayo, basi amewakhosha haswa wafanyakazi siku ya leo. Hata mimi nilifurahi sana kuona furaha zao!

Kitu pekee cha kuhofia, ni hofu yenyewe. Mama yuko vizuri.
 
Nakubaliana na wewe kwa 100%
Kusema ukweli, ni jambo zuri. Kwasababu hata kwenye uchumi, “ consumer confidence” ndilo jambo la msingi kabisa kwenye uchumi wa nchi. Wanejitokeza na kutumia pesa zao. Mzunguko wa pesa umeshaanza rasmi. Wafanyabishara nao wamepata matumaini makubwa.
 
Serikali hii imelemewa na mzigo wa madeni na mamiradi ya matrilioni hata mwakani hsitakuwa na uwezo wa kuongeza mishahara.

Subiri kusikia viaingizio vingine hiyo mwakani.

Ulivyoandika mkuu ni kana kwamba unaiombea serikali ishindwe kuongeza mishahara ili upate cha kuandika kwenye mitandao sio?...Jikiteni katika kufanya kazi sio maneno tu,mama anania nzuri na sisi wananchi wake kama wewe huna jema utakufa na kiroho chako.

#chawa_wa_samia_suluhu_hassan
 
Ulivyoandika mkuu ni kana kwamba unaiombea serikali ishindwe kuongeza mishahara ili upate cha kuandika kwenye mitandao sio?...Jikiteni katika kufanya kazi sio maneno tu,mama anania nzuri na sisi wananchi wake kama wewe huna jema utakufa na kiroho chako.

#chawa_wa_samia_suluhu_hassan
Kilichonifurahishza ni kuwa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 5 mfululizo, Rais hajatukemea sisi wafanyakazi!

Kila mtu anakumbuka namna mwendazake, alivyotumia hizi hotuba za mei mosi kutukemea vikali sisi wafanyakazi na kuapa kuwa haongezi mishahara hadi pale atakapomaliza miradi yake mikubwa aliyoanzisha!

Sasa kiko wapi mbona miradi hajaikamilisha na Mungu amekatisha maisha yake na kumtwaa!
 
Kilichonifurahishza ni kuwa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 5 mfululizo, Rais hajatukemea sisi wafanyakazi!

Kila mtu anakumbuka namna mwendazake, alivyotumia hizi hotuba za mei mosi kutukemea vikali sisi wafanyakazi na kuapa kuwa haongezi mishahara hadi pale atakapomaliza miradi yake mikubwa aliyoanzisha!

Sasa kiko wapi mbona miradi hajaikamilisha na Mungu amekatisha maisha yake na kumtwaa!
Alikuwa na roho mbaya sana. Ndio maana wenye roho mbaya wenzie kazi ilikuwa kuwapakazia watu kesi kuteka kuuwa watu kutesa na kuwaweka kwenye viroba ufukweni alafu Bado akataka tumuombee.

Very shame
 
Mkuu wafanyakazi wa sekta binafsi mishahara imechelewa kisa kupataikana kwa hitilafu huko benki kuu. Sidhani kama wote wamekula bata. Mishahara haijaingia benki mbalimbali mpaka leo.
 
Back
Top Bottom