Waganda watumia Biblia kumshawishi Museveni kung’oka, Hongera Magufuli

Waganda watumia Biblia kumshawishi Museveni kung’oka, Hongera Magufuli

Benmpo

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2015
Posts
450
Reaction score
423
Kwa kile kinachoonekana kuwa hali imekuwa tete nchini Uganda, baada ya mchakato kwa kubadili vifungu vya katiba vitakavyomwezesha Rais Mu7 kuwa na nafasi zaidi ya kugombea Urais wa nchi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao. Baada ya tetesi kwamba huenda Mu7 anaogopa kushtakiwa mahakamani kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu baada ya kutoka madarakani, Waganda walipendekeza kwamba kiwekwe kifungu katika katiba kitakacho mlinda pindi atakapo achia madaraka, lakini inaonekana juhudi hizo hazizai matunda kwani mchakato unaendelea kwa kasi kubwa.

Katika hatua ya kushangaza, limeibuka kundi linalofanya kampeni zake kumtaka Mu7 amrithishe kiti hicho mwanaye Meja Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ambaye pia ni mshauri wake katika masuala ya uongozi. Kikundi hicho kimetohoa kifungu cha Biblia kutoka Yn 3:16 na kusema “Kwa maana jinsi hii Mu7 aliipenda Uganda, hata akamtoa mwanaye kuwa Rais wa Uganda”, wakitarajia kuwa juhudi hizo labda zitafanikiwa kumweka benchi Mu7 na kumpata Rais mpya, kijana, lakini akiwa ni mwanaye.

Sisi Watanzania tumpongeze sana Rais Magufuli (The President Incumbent) kwa kuonesha nia wazi wazi kwamba atatawala kwa mujibu wa katiba ya JMT. Ni suala la kujivunia kuwa na viongozi wa namna hii, kwani tunaona nchi nyingi zinazotuzunguka Marais wao wanavyokuwa ving’ang’anizi. Pia tuna kila sababu ya kuwapongeza Marais wetu wote waliostaafu kwa kuridhia kwa moyo mmoja na kwa amani kabisa kuachia madaraka pale muda wa uongozi wao ulipokoma. Tuiombee nchi yetu, Tudumishe amani yetu.

Benmpo
 
Stupid!!! M7 aliingia madarakani kwa mtutu wa bunduki huyu unaemwelezea alitumia njia hiyo? Pumbavu kabisa wewe. huyujui vitu vya kulinganisha au ni upuuzi wa kichekechea na kukimbia umande?
 
Huko Lumumba huwa hampeani "tuisheni" kabla ya kupeana majukumu. Pia kabla ya kukabidhiana "Laptop" hakuna kupeana kinachotakiwa kuwekwa mitandaoni. Hao tagu wale vijana 46 kupewa nyadhifa hapo Lumumba mnaendesha mambo yenu hobela hobela!
 
Akili za kuvukia barabara , za kufikiri zimewekwa kabatini Lumumba
 
Na muuseveni ajawahi kukubali kama antaga'gania madarakani usiamini wanasiasa wa Africa tuombe mungu atuepushe hayo tu
 
Na muuseveni ajawahi kukubali kama antaga'gania madarakani usiamini wanasiasa wa Africa tuombe mungu atuepushe hayo tu

Mkuu waeleweshe hao wanaojitia ujuaji huku kichwani hamna kitu, sijui ubongo wao umetengenezwa na nini
 
Stupid!!! M7 aliingia madarakani kwa mtutu wa bunduki huyu unaemwelezea alitumia njia hiyo? Pumbavu kabisa wewe. huyujui vitu vya kulinganisha au ni upuuzi wa kichekechea na kukimbia umande?

We mjinga ngoja nikusaidie kufikiri, maana bichwa lako kubwa lakini halifanyi kazi yake. Njia ya aliyotumia mtu kuingia madarakani na kung'ang'ania madarakani au kutong'ang'ania ni vitu viwili tofauti. Unaweza ingia madarakani kwa mtutu wa bunduki simply kwa sababu hupendezwi na dictator aliyepo madarakani then ukatengeneza mazingira ya chaguzi za kidemokrasia. Pia waweza ingia madarakani kwa uchaguzi wa kidemokrasia then ukang'ang'ania, ukabadilisha vifungu vya katiba ukaendelea kutawala.

Kumbuka Mwalimu Nyerere mwaka 1982 alishasema kwa nature ya katiba yetu, jinsi ilivyotoa mamlaka makubwa kwa Rais, kama atapatikana mtu wa kuitumia vibaya basi itakuwa majanga maana atakuwa kama Mungu, nevertheless hajapatikana Rais mwenye uroho huo licha ya katiba kumpa mazingira hayo.

Hivi karibuni:
1) Tumemsikia Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi akisema ingependeza kama Rais Magu angetawala zaidi ya miaka 10,
2) Tumeona movement ya [HASHTAG]#MAGUFULIBAKI[/HASHTAG] ikiendeshwa na kikundi fulani cha watu,
3) Tumeona Mbunge akiazimia kupeleka hoja binafsi bungeni, itakayojadili juu ya ukomo wa Rais kwa kipindi cha miaka mitano ili muda huo uongezwe.

Mbali na hayo yote Rais Magufuli hajashawishika kama ambavyo ingewezekana kwa Marais kadhaa wa nchi zinazotuzunguka. Kwa nini asipongezwe ka hilo? Kwani angetengeneza mazingira kwa kampeni ya [HASHTAG]#MAGUFULIBAKI[/HASHTAG] ku-propagate hoja zao, mngefanya nini?
Narudia tena, namna ulivyoingia madarakani na kung'ang'ania madarakani au kutong'ang'ania ni vitu viwili tofauti.
 
Akili za kuvukia barabara , za kufikiri zimewekwa kabatini Lumumba

Bora mie hata hizo ninazo maana wewe hata za kwenda chooni umenyimwa, piga picha mwenyewe unajifanyiaje!!
 
Huko Lumumba huwa hampeani "tuisheni" kabla ya kupeana majukumu. Pia kabla ya kukabidhiana "Laptop" hakuna kupeana kinachotakiwa kuwekwa mitandaoni. Hao tagu wale vijana 46 kupewa nyadhifa hapo Lumumba mnaendesha mambo yenu hobela hobela!

The stupidest comment from the so-called verified user. Pathetic!!
 
Sio kuogopa tu kushtakiwa pia anaona nchi yake inaenda kupata utajiri kwa kupitia mafuta hivyo anataka utajiri huo upitie mikononi mwake...
 
We mjinga ngoja nikusaidie kufikiri, maana bichwa lako kubwa lakini halifanyi kazi yake. Njia ya aliyotumia mtu kuingia madarakani na kung'ang'ania madarakani au kutong'ang'ania ni vitu viwili tofauti. Unaweza ingia madarakani kwa mtutu wa bunduki simply kwa sababu hupendezwi na dictator aliyepo madarakani then ukatengeneza mazingira ya chaguzi za kidemokrasia. Pia waweza ingia madarakani kwa uchaguzi wa kidemokrasia then ukang'ang'ania, ukabadilisha vifungu vya katiba ukaendelea kutawala.

Kumbuka Mwalimu Nyerere mwaka 1982 alishasema kwa nature ya katiba yetu, jinsi ilivyotoa mamlaka makubwa kwa Rais, kama atapatikana mtu wa kuitumia vibaya basi itakuwa majanga maana atakuwa kama Mungu, nevertheless hajapatikana Rais mwenye uroho huo licha ya katiba kumpa mazingira hayo.

Hivi karibuni:
1) Tumemsikia Rais Mstaafu Mwinyi akisema ingependeza kama Rais Magu angetawala zaidi ya miaka 10,
2) Tumeona movement ya [HASHTAG]#MAGUFULIBAKI[/HASHTAG] ikiendeshwa na kukundi fulani cha watu,
3) Tumeona Mbunge akiazimia kupeleka hoja binafsi bungeni, itakayojadili juu ya ukomo wa Rais kwa kipindi cha miaka mitano ili muda huo uongezwe.

Mbali na hayo yote Rais Magufuli hajashawishika kama ambavyo ingewezekana kwa Marais kadhaa wa nchi zinazotuzunguka. Kwa nini asipongezwe ka hilo? Kwani angetengeneza mazingira kwa kampeni ya [HASHTAG]#MAGUFULIBAKI[/HASHTAG] ku-propagate hoja zao, mngefanya nini?
Narudia tena, namna ulivyoingia madarakani na kung'ang'ania madarakani au kutong'ang'ania ni vitu viwili tofauti.
Haya maelezo yote ulimanisha nini? Stupid
 
Sio kuogopa tu kushtakiwa pia anaona nchi yake inaenda kupata utajiri kwa kupitia mafuta hivyo anataka utajiri huo upitie mikononi mwake...

Hii nayo yaweza kuwa sababu, na ndio maana wanasema wampe Urais Mwanaye. Mu7 wamemchoka kwa kweli
 
Aaah nyie walumumba mko kama misukule tu

Huo ndo ugonjwa mlionao, maana kila mtu anayefikiri tofauti na ninyi basi ni wa Lumumba. Ndio maana mkapewa lile jina la Wanyama mbumbumbu wanaoingia tu katika hatari bila tahadhari. Aliyewapa lile jina alitafakari sana, kweli akawatendea haki
 
Back
Top Bottom