Waganga wa jadi limekuwa tatizo nchini sasa tuwakatae

Kyambamasimbi

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
762
Reaction score
1,597
Habar wanajf.

Kutokana na matukio yanaoendelea katika nchi yetu hasa Kanda ya Ziwa, na kati imefanya niandike huu Uzi, kwamba Hawa watu sasa imekuwa shida.

Kwani wanachangia uvunjifu wa amana kwa kuua watu wazima na watoto wasio na hatia maskini ya Mungu, ni kuwa tiba asili ni utamaduni wetu lakini sio hivyo wanavyofanya hao wanaojiita wataalamu wa tiba asili kwa kutumia viungo vya binadamu kutibu.

Aidha serikali na wananchi tupige vita waganga uchwara katika jamii na tuwakatae na kuwaondoa katika jamii kwani wanachochea mauaji katika jamii yetu.

Nafikiri Singida wameelewa na Dodoma. Nawasilisha.
 
Ikitokea nikashika mpini, hao watu watapotea.
 
Tatizo lipo kwa Hao wananchi wanaoishi mazingira ya jirani na waganga wenye ramli chonganishi na sio serikali. Wanakijiji wanaoishi na waganga wa kienyeji hawatoi taarifa kwenye ofisi zao za vijiji juu ya uwepo wa Hao jamaa kwenye vijiji vyao. Baada ya ndugu zao na watoto kupotea katika mazingira yasiyoeleweka ndipo wanaanza kutoa taarifa kwa polisi.
 
Kwa kweli tunapaswa kubadilika
 
Kanda ya ziwa kunatisha kwa ushirikina, kwanini 🙄
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…