Waganga wa kienyeji wametusaidia. Tusiwabeze

Waganga wa kienyeji wametusaidia. Tusiwabeze

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Leo ukiwa unaimba kwaya unarukaruka unawatukana waganga wa kienyeji na kusahau kuwa huenda sasa ungekuwa unaitwa marehemu. Ila waganga wa kienyeji ndio waliokutoa kwenye mikono ya adui zako kipindi ukiwa mtoto au kijana.

Nakumbuka nikiwa darasa la tatu siku moja nikiwa shule nilipata stroke ya miguu na ghafla nikawa Kiwete.

Nikafuatwa kwa baiskeli nikarudishwa home.

Nikawa mtu wa kukaa ndani tu, siumwi mahali popote ila miguu siwezi kuinyakua.

Siku moja nikawa najadiliana na mdogo wangu ambaye ni rika moja na mimi. Baba mmoja kasoro mama tu. Nikamwambia twende kwa mganga wa kienyeji mtaa wa pili. Nilijua nitakwenda kwa msaada wa mtu. Ile nainuka tu nikawa mzima, nilitembea mpaka kwa mganga.

Akapiga ramli bure, akanitibu bure. Nikapona moja kwa moja. Nikarudi shule nikaendelea kufanya vizuri na sasa nimegraduate shahada yangu ya kwanza ya International Relations & Diplomacy na sasa nimekuwa mlinzi mwenye degree.

Sijawahi kwenda kwa waganga miaka hii ila jana usiku nimekumbuka fadhila za yule mganga, nawaza nikampe zawadi (sio kupata huduma).

Ni miaka karibu 20 sasa sijamuona machoni. Nimewauliza kijijini wanasema bado yupo. Kumtibu mtu bure kwa tatizo kubwa kiasi kile ni upendo wa ajabu sana, hawa wachungaji wakikuponya sikio tu watakurusha kwenye tv kila siku ili kuvutia watu kwao.
 
Sasa kama ulipotaka kwenda, ukawa mzima ukaweza kutembea mwenyewe ulifata nini huko?

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilikuwa mzima kwa maana niliweza kutembea mwenyewe, lakini bado mwili ulikuwa mzito.

Ila katika yote, kama ulishindwa kutembea kwa wiki moja then siku ukiinuka tu ili ukokotwe uende kwa witch unajikuta unatembea mwenyewe lazima safari iendelee mbele
 
Una maana gani unaposema umekuwa mlinzi mwenye degree
 
Mtoto alitaka kumchukua msukule baba yake, baba alishtuka akaenda kwa mganga na akaambiwa imebaki wiki tu aondoke duniani. Mganga akamgeuzia kibao Yule mtoto akafa kwa ajali ya bajaji. Baba akapona na akasema kaburi la mwanae liongezewe m moja kwenda chini. Mganga kamuokoa mzee!

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app

Hakuna ushahidi wa hila ya mtoto hapo, Mzee alishtuka vipi!
 
Kuna jua,kuna mvua
Kuna mwanamke,kuna mwanaume
Kuna Nuru-mchana,kuna Giza-Usiku
Kuna nchi kavu, kuna majini

Kuna Nguvu za giza na kuna nguvu za Nuru

Kama mtu hushawahi kuuchukia usiku
Kama mtu hujawahi kumchukia mwanamke sababu wewe ni mwanaume
Kama hujawahi kuchukia bahari sababu upo nchi kavu
Kama hukawahi kuchukia anga sababu upo ardhini


Basi amini nawaambia nguvu za giza hazina shida yeyote bali matatizo yenu yangeweza kutatulia vzr kwenye nguvu za Nuru tena bila changamoto nyingi hapo sijasema ukiamua kulala mchana ukafanya kazi usiku ni tatizo ila ni bora zaidi utumie usiku kulala kuliko mchana atakaye lala mchana hatapati usingizi mzuri kama atakayelala usiku i gawa wote watalala.

Ni vizuri zaidi kulima msimu wa mvua haina maana ukilima kiangazi haitavuna ila itakutana na changamoto za maji.

Wazee wetu hawakuwa na dini hivyo walitumia zaidi nguvu za giza kutatua mambo yao..

Nguvu za giza ni kama kisu,wewe unatumiaje

Nachosema ni hivi open mind ni muhimu na hii inahitaji uwe na uelewa mkubwa kdg kujua kila jambo linapande mbili..[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mkuu, unaongea kwa shukrani as if wewe ni Mh. waziri, mbunge, katibu mkuu, Managing Director serikalini? Ila nawashukuru tu mwaka huu wa uchaguzi hamkuua maalbino baada ya dunia kupiga kelele.
 
Kwani mabalozi wote wamesomea International Relationship?

Ulitoroka kwa mganga, rudi hujapona vizuri... waganga huikanyaga dawa [kuiruka] kama hujalipa ili tatizo likurejee.

"International Relationship" ni mdudu gani?

Kufanya kazi ubalozini sio kuwa Balozi.
 
Back
Top Bottom