Kikubwa zaidi kinachosikitisha ni kuona Meneja Rasilimali Watu anashindwa kuwatetea watanzania wenzake, anachoangalia ni yeye mshahara wake pamoja na kuwakumbatia wahindi wasio hata na vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini. Kunduchi beach hoteli ni sehemu iliyojaa unyanyasaji wa hali ya juu kwa wafanyakazi wazawa. Pale Wet n wild water park ambayo ni sehemu ya hoteli, wafanyakaxzi wanalipwa mshahara wa elfu 80 kwa mwezi, hakuna overtime wala nini. Mhindi anaweza kumtusi na kumpiga mzawa asichukuliwe hatua yeyote. HOUR solution wanaotumiwa ktk mashauri ya kinidhamu wanafanya kuwanyanyasa wazawa bila kujali sheria za ajira za nchi hii, wanachoangalia ni pesa yao wanayolipwa kama consultants tu na si sheria zinasemaje, wamegeuka vibaraka wa kuwafurahisha wahindi na si kuangalia taaluma yao. Ama kwa hakika mtu msomi anayejua sheria za ajira na asiye na njaa sana, hawezi kufanya kazi ktk mazingira yale. Natoa angalizo kwa wanaotafuta ajira kuwa Kunduchi Beach hoteli si sehemu ya kufanya kazi. Jamani uhamiaji amkeni na fuatilia hao wahindi na Wakenya wasio na vibali hapo Kunduchi, pia wizara ya kazi na ajira ipamulike.