Uchaguzi 2020 Wagombea 460 wajitokeza kuutaka ubunge Kagera kupitia CCM, milango yafungwa

Uchaguzi 2020 Wagombea 460 wajitokeza kuutaka ubunge Kagera kupitia CCM, milango yafungwa

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Wagombea 460 wajitokeza kuchukua fomu za kugombea ubunge Kagera zoezi la uchukuaji fomu lafungwa.

=========
Mchakato wa kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ulianza tarehe 14/07/2020 na kumalizika 17/07/2020 saa kumi jioni.

Katika mkoa wa Kagera wagombea 460 wa ubunge walichukua fomu na kuzirudisha na hivyo umebaki mchakato wa vikao vya mapendekezo.

Katika hao wagombea 460 ambao wamegawanyika katika sehemu mbili (wagombea wa viti maalum na wagombea wa majimbo) katika majimbo yote wagombea waliochukua fomu na kuzirudisha ni 404.

Na jumuiya wanayo jumuiya ya wazazi, vijana na UWT na wote wamefanya mchakato huu na kupata wagombea 56 na hivyo kufanya jumla ya wagombea 460 na mchakato ulifungwa rasmi tarehe 17/07/2020 na kubaki utaratibu wa vikao vya ndani vya mapendekezo.

Kuna majimbo 9 ya uchaguzi, Bukoba mjini wagombea waliochukua fomu na kuzirudisha ni 57, Bukoba vijijini wagombea 42, Muleba kaskazini wagombea 17, Muleba kusini wagomnea 52, Biharamulo wagombea 51, Ngara wagombea 43, Kyelwa wagombea 52, Karagwe wagombea 36 na Misenyi ( Nkenge)wagombea 54. Zoezi lilikamilika vizuri na hivyo taratibu za ndani ya chama zinaendelea.
 
Safi SANA-JPM atakuwa na wakati Mgumu sana katika kuwakata hawa watu.
 
Bukoba vijijini Rweikiza harudi tena
Huyo ni tycoon ndani ya ccm hakuna wa kumgusa labda ahamue yeye kutogombea na jambo ambalo haliwezekani
Ubunge kwake sio vijisent vya posho na mshahara ni fursa ya kuendesha biashara zake bila ya kubughuziwa na mtu
 
Huyo ni tycoon ndani ya ccm hakuna wa kumgusa labda ahamue yeye kutogombea na jambo ambalo haliwezekani
Ubunge kwake sio vijisent vya posho na mshahara ni fursa ya kuendesha biashara zake bila ya kubughuziwa na mtu
Tatizo linaanzia kwa watu wa Bukoba Vijijini ingekuwa ni majimbo mengine angeshatolewa zamani
 
Huyo ni tycoon ndani ya ccm hakuna wa kumgusa labda ahamue yeye kutogombea na jambo ambalo haliwezekani
Ubunge kwake sio vijisent vya posho na mshahara ni fursa ya kuendesha biashara zake bila ya kubughuziwa na mtu
Karamagi hajachukua fomu?
 
Hongereni mno wasomi wa bongo, wahaya ni watu makini kwenye elimu nawafagilia, ni watani zangu mimi ni muha napiga jembe mwanzo mwisho kuhakikisha wahaya wanapata msosi na kusoma vizuri hata digrii tano bado mtu hajaridhika! siku hizi wahaya wamekuwa safi mno mambo ya kupenda sifa za kijinga hawana, big up sana vijana wa kihaya, na huko Bukoba hasa mitaa yangu ya Hamugembe pale kama nawaona walivyochangamkia fursa na kuchukua forms kama zote!!Yuko best wangu wa kihaya tulifanana jina na tulisoma pamoja for six years, he was my companion and my role model manake mimi tangu nikiwa mdogo sikuwa nikiheshimu wazee!! sorry guys!

Shikamoo Mh Rais Magufuli, ama kwa hakika wewe ni chuma cha pua umetunyoosha kweli kweli!! utitiri huu wa watia nia umewatoa kwenye spotlight wanasisiemu wote waliokuwa wamejificha kina Jecha, Gwajima, Master J, na pia wengine kina Haji Adam nao wameingilia siasa huko ACT , kweli vyuma vimekaza kila msanii katupa MIC na kukimbilia siasa!! pia utitiri umethibitisha njaa kali walizonazo raia wengi pamoja na kuongezeka kwa ari za watu kushiriki siasa, ari za watu kukipenda chama cha kijani, ari ya kwenda bungeni kuvuna kodi za wanyonge, kukua kwa demokrasia ndani ya chama zamani mfano mbunge mmoja tu tena ni wa milele kama lets say Wassira anasinzia bungeni sababu ni mzee , kijana yoyote mwingine akitangaza nia jimboni kwake anakufa, utitiri huu wa watia nia ni ushahidi wa kuongezeka tatizo la ajira na umaskini , kuharibika maslahi ya sekta binafsi na biashara na matajiri wengi kuporomoka kiuchumi na sasa kuishi kishetani!!

naiota siku haki itatendeka sisiem tupate viongozi wa haki , yaani wajumbe kila mmoja apige kura kwa mgombea anaemtaka bila kuwa ameshawishiwa kwa posho takrima rushwa au ahadi!wagombea hao tu ndio wataweza kuendeleza nchi hii sio manyang’au yaliyojazana bungeni mengi yameenda kwa rushwa na ubabe tu!!

ili kufikia lengo la kupata viongozi bora aliowaota Mwalimu namshauri Polepole na Bashiru waandae form za tathmini zenye maswali mia ya kisomi wapewe kila mjumbe wa sisiem nchi nzima na wajaze na waandike tathmini zao binafsi na kila mjumbe apewe form zingine tano aandike tathmini yake kwa wajumbe wenzake watano kwa siri, tathmini zioneshe jinsi yeye binafsi (form yake) na wenzake ( five evaluation forms) wameshiriki mchakato wa kura za maoni kwa haki kwa kuchagua mgombea makini wa ubunge na udiwani! Wajumbe wataobainika kupendelea mgombea flani watolewe ujumbe tupewe sisi tuko kijiweni huku Kawe hatuna kazi hatuna pesa wala matumaini yoyote ya maisha bora.


najua nitakwenda mavumbini bila kuiona siku hiyo,but nafurahi nimesema kuwa nchi hii imejaa viongozi uozo mtupu ,manyang’au kina Chenge na genge lake hawatoki bungeni kuachia vijana , haya ni majitu yasiyo na huruma na raia ambao kodi zao ndio matumbo yao! majitu yamesahau kama kuna kifo wakati kila siku yanaenda mavumbini mmoja mmoja!

Hongera Mh Rais Magufuli umeanza kupunguza udini katika teuzi zako za karibuni kuna waislam kidogo si haba nawe utabarikiwa sana inshaallah we pray for you. Sasa huwezi kuteua waislam huku alieshawishi jambo hilo wewe uache udini na kupunguza kasi ya mfumo kristo Roman Catholic , Mh Sheikh Ponda kuendelea kumuweka ndani selo , it doesnt make sense! Sheikh Ponda hana madhara yoyote kisiasa ni baridi mno hagombei nafasi yoyote ya kisiasa hakuna sababu ya kumuweka ndani na kwanza waraka wake ni wa kisomi unaishia kwa wasomi wachache wa mtandaoni, ZZK, DJ Mbowe au Membe au Sugu ni hatari zaidi kwa CCM kuliko Sheikh Ponda hana kitisho chochote wasomi wa kiislam wana sisiem wapiga kura wako tunakuomba Mh Magufuli uamuru Sheikh Ponda atolewe, kumbuka Mkulu hawa Masheikh na Mapadri na Maasofu ndio unawaambia kila siku wakuombee!! au mkishashiba na Korona ikiondoka mnatusahau??
 
Wagombea 460 wajitokeza kuchukua fomu za kugombea ubunge Kagera zoezi la uchukuaji fomu lafungwa.

=========
Mchakato wa kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ulianza tarehe 14/07/2020 na kumalizika 17/07/2020 saa kumi jioni.

Katika mkoa wa Kagera wagombea 460 wa ubunge walichukua fomu na kuzirudisha na hivyo umebaki mchakato wa vikao vya mapendekezo.

Katika hao wagombea 460 ambao wamegawanyika katika sehemu mbili (wagombea wa viti maalum na wagombea wa majimbo) katika majimbo yote wagombea waliochukua fomu na kuzirudisha ni 404.

Na jumuiya wanayo jumuiya ya wazazi, vijana na UWT na wote wamefanya mchakato huu na kupata wagombea 56 na hivyo kufanya jumla ya wagombea 460 na mchakato ulifungwa rasmi tarehe 17/07/2020 na kubaki utaratibu wa vikao vya ndani vya mapendekezo.

Kuna majimbo 9 ya uchaguzi, Bukoba mjini wagombea waliochukua fomu na kuzirudisha ni 57, Bukoba vijijini wagombea 42, Muleba kaskazini wagombea 17, Muleba kusini wagomnea 52, Biharamulo wagombea 51, Ngara wagombea 43, Kyelwa wagombea 52, Karagwe wagombea 36 na Misenyi ( Nkenge)wagombea 54. Zoezi lilikamilika vizuri na hivyo taratibu za ndani ya chama zinaendelea.
View attachment 1510190
Hakuna aliyekosea kujaza form?
 
Kila nafasi ina wastani wa wagombea 50!? Nshomile mmetisha mbayaaaa!
 
Back
Top Bottom