Wahadhiri wa Vyuo Vikuu na mishahara ya Wabunge na Wakurugenzi Mashirika ya Umma

Wahadhiri wa Vyuo Vikuu na mishahara ya Wabunge na Wakurugenzi Mashirika ya Umma

Manelezu

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2015
Posts
1,908
Reaction score
2,774
Habari wana bodi, nimekuwa nikisoma baadhi ya articles zinazo ongelea mchango wa vyuo vikuu marekani katika uchumi wa taifa hilo especially kutengeneza innovators "silicon valley".

Kwa kiasi kikubwa maendeleo ya taifa la marekani yamechangiwa sana na innovations zinazofanywa na taasisi zake za elimu ya juu kama "think tank" ya nchi, kuanzia sera za uchumi, sera za mambo ya nje, etc.

Ukiangalia Taifa letu, wahadhiri wa vyuo vikuu ambao ndio wazalishaji wa wataalamu mbalimbali wamekuwa wakilipwa pesa kidogo sana ukilinganisha na wakurugenzi wa mashirika ya Umma au wabunge( ambao hawana mchango wa maana kwenye taifa hili uki compare na mchango unaotolewa na wahadhiri wa vyuo vikuu. Jiulize kibajaji au musukuma anawezaje kulipwa mshahara na marupurupu kuliko Prof au Dr, wa chuo kikuu?

Mimi ningemuomba Rais Samia waangalie hawa watu kama kweli tunataka hili taifa lisonge mbele. Licha ya kuongezewa mishahara serikali ipeleke pesa za kufanya tafiti mbalimbali na maamuzi ya wanasiasa yazingatie recommendations za wataalamu wetu.

Mtu ana PhD analipwa mshahara wa mil 3 au 4 na hapo bado makato kweli unategemea atakuwa na morale ya kufundisha? Au ndio atakuwa busy kufanya kazi zake za nje? Serikali inatakiwa kuona wapi inaweza kuwekeza pesa na zikawa na tija kwa taifa hili.
 
Wakati unamtetea huyo anayelipwa mil 3-4 unasahau yule mwl wa foundation anayepokea laki 3.!! Unafikiri innovations zinaanzia wapi mkuu?
Kama umeamua kuwatetea au kuwapigia debe walimu basi nakuomba usiwagawe
Lakini pia kumbuka na mwalimu wa darasa la AWALI na la KWANZA wanaofundisha KKK(kusoma, kuhesabu na kuandika). Usisahau madarasa yale watoto wengine hawajajitambua wanajisaidia humo humo. Huyu mwalimu huyu!!!
 
Habari wana bodi, nimekuwa nikisoma baadhi ya articles zinazo ongelea mchango wa vyuo vikuu marekani katika uchumi wa taifa hilo especially kutengeneza innovators "silicon valley".

Kwa kiasi kikubwa maendeleo ya taifa la marekani yamechangiwa sana na innovations zinazofanywa na taasisi zake za elimu ya juu kama "think tank" ya nchi, kuanzia sera za uchumi, sera za mambo ya nje, etc.

Ukiangalia Taifa letu, wahadhiri wa vyuo vikuu ambao ndio wazalishaji wa wataalamu mbalimbali wamekuwa wakilipwa pesa kidogo sana ukilinganisha na wakurugenzi wa mashirika ya Umma au wabunge( ambao hawana mchango wa maana kwenye taifa hili uki compare na mchango unaotolewa na wahadhiri wa vyuo vikuu. Jiulize kibajaji au musukuma anawezaje kulipwa mshahara na marupurupu kuliko Prof au Dr, wa chuo kikuu?

Mimi ningemuomba Rais Samia waangalie hawa watu kama kweli tunataka hili taifa lisonge mbele. Licha ya kuongezewa mishahara serikali ipeleke pesa za kufanya tafiti mbalimbali na maamuzi ya wanasiasa yazingatie recommendations za wataalamu wetu.

Mtu ana PhD analipwa mshahara wa mil 3 au 4 na hapo bado makato kweli unategemea atakuwa na moral ya kufundisha? Au ndio atakuwa busy kufanya kazi zake za nje? Serikali inatakiwa kuona wapi inaweza kuwekeza pesa na zikawa na tija kwa taifa hili.
Hoja nzuri lakini CCM watakuja kukupinga.Tunapitishwa katika Tanuri la Uvuli na Mauti.
 
Mkuu una hoja ya msingi sana, ila nchi hii tulishawaachia wanasiasa waitafune wanavyotaka........nafikiri hii nchi ndo itakuwa ya kwanza kwa wataalamu wake kulipwa kiduchu, angalia mishahara wanayolipwa graduates huko serikalini ni aibu tupu.....mtu una PhD mshahara wako haufiki mil. 3, lakini kuna vilaza mjengoni hawana elimu ya kueleweka wanakunja mkwanja wa hatari. Hapo unakuwa unahamasisha vijana wakite mizizi kwenye ushirikina ili waweze kushinda ubunge badala ya kuwekeza muda kusaka elimu ya viwango vya juu.......
 
Watu wenye elimu kubwa kama hizo wasipotumia elimu zao kutengeneza pesa basi hii nchi itakuwa imelaaniwa. Kama vijana wadogo tu kabisa wenye degree wameweza kupenya na kufanya mambo makubwa bila msaada wa serikali, sasa tusemeje kwa maprofesa?

Tatizo tulilo nalo ni kwamba tuna mijitu ina PhD za kupika, majitu yanasoma tu elimu ya kikasuku tu ali mradi yaonekane kwenye jamii yana PhD. Lakini ukiyaweka nje ya system ya serikali kwa kufundisha vyuo vikuu vya umma hayawezi hata kusurvive.

Hii nchi imeangushwa sana na wasomi wa vyeti tu na sio wasomi wenye maarifa.
 
Back
Top Bottom