Wahisani wakibana kisawasawa, mbali na Wafanyabiashara kukamuliwa, hata sitting allowance za Wabunge zinaweza kutoweka

Wahisani wakibana kisawasawa, mbali na Wafanyabiashara kukamuliwa, hata sitting allowance za Wabunge zinaweza kutoweka

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kutokana uchaguzi huu ulivyokwenda, binafsi naona kuna uwezekano wa asilimia 70 mpaka 80 wa wahisani na mashirika ya fedha ya kimataifa, kusitisha kutoa fedha zao kwa hii serikali unless zinafanyika jitihada kubwa sana za kidiplomasia huku serikali ikilazimika kuji-commit kwa baadhi ya mambo: demokrasia, utawala bora na kuheshima haki za binadamu, vinginevyo tutalimia meno.

Katika kulimia meno huko, ni pale tutapolazimika kuongezea makusanyo na kubana matumizi kufidia nakisi itayotokana na kukosekana kwa fedha za wahisani.

Nini kinaweza kutokea?

Kwasababu hakuna vyanzo vipya vya mapato, uwezekano uliopo ni kuongeza wigo wa kodi kwa wafanyabiashara na hata wafanyakazi, na serikali kulazimika kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na hali hii ikiendelea kwa muda mrefu, basi hata sitting allowance za wabunge zinaweza kuguswa huko mbeleni.

Tukumbuke tuna deni la Taifa tunalohitaji kulihudumia kila mwezi, na wakati huo huo, tuna miradi ya matrilioni inayotakiwa kukamilika katika ungwe hii ya mwisho ya Mzee Baba na sidhani kama atakubali kushindwa kuikamilisha labda akosa hela kabisa.

Na ikitokea anakosa hela kabisa, basi wewe mwananchi wa kawaida jiulize utakuwa katika hali gani na pia jiulize kama elimu bure nayo itaendelea.

Naishia hapo, wache nisepe zangu kuelekea shambani mvua zimeanza.
 
Kutoka na uchaguzi huu ulivyokwenda, binafsi naona kuna uwezekano wa asilimia 70 mpaka 80 wa wahisani na mashirika ya fedha ya kimataifa, kusitisha kutoa fedha zao kwa hii serikali unless zinafanyika jitihada kubwa sana za kidiplomasia huku serikali ikilazimika kuji-commit kwa baadhi ya mambo: demokrasia, utawala bora na kuheshima haki za binadamu, vinginevyo tutalimia meno....

Ndio vizuri..Donors wabane kila kitu.

Kwasababu Tanzania kuna mtawala mshenzi..mwizi wa kura.
 
Mpiga ramli....
Kutoka na uchaguzi huu ulivyokwenda, binafsi naona kuna uwezekano wa asilimia 70 mpaka 80 wa wahisani na mashirika ya fedha ya kimataifa, kusitisha kutoa fedha zao kwa hii serikali unless zinafanyika jitihada kubwa sana za kidiplomasia huku serikali ikilazimika kuji-commit kwa baadhi ya mambo: demokrasia, utawala bora na kuheshima haki za binadamu, vinginevyo tutalimia meno...
 
Acheni hizi akili za kipumbavu na za kinafiki za kujifanya nyinyi ni sehemu ya jamii mkiwa hadharani halafu gizani mnaendekeza fitina.

Zitto Kabwe na Lissu wanakwenda kupotea kisiasa kwa sababu ya kuendekeza hulka hizi za kipumbavu. Ni hulka zisizoweza kufanikiwa hata mara moja.

Wahisani wana maslahi yao ya kiuchumi humu nchini hawawezi kuwaamini watu ambao hawana majukumu halali ya kuongoza nchi.

Hawawezi kuwaamini watu wasiokubalika mbele ya jamii ya kitanzania sana sana watawatumia tu na baadae watawapuuza mazima.
 
Jamaniee, naomba mlio karibu na salary slip muwe mnakaa nae kwa umakini asije akajinyonga
 
Bila hata bungeni inatakiwa wapunguziwe posho na maslai wabunge ili kuokoa pesa zikatumike kujenga nchi mfano kwa wiki tu wabunge 375 Mara laki 3 kwa siku ni pesa nyingi Sana.

Posho ya laki 3 ni nyingi Sana kwa maisha ya watz, wapewe elf 10 mishahara yao ipunguzwe nao wajibane Kama sisi wananchi Hadi tukiwa na maendeleo kuliko ulaya ndo waanze kupewa maslai makubwa.

Hii itasaidia kuwapata wawakilishi wa kweli wa wananchi na sio wachumia tumbo wanaotaka ubunge kwa ajili ya kusaka utajiri
 
Miradi mikubwa ya Maendeleo ya Vitu kukwama kuendelea, kama kwa mfano kuna uwezekano daraja la baharini jijini Dar es Salaam kuwa gofu linaloelea baharini na kielelezo tosha kwa waTanzania na ulimwengu kuwa wahisani na wadau wa maendeleo a.k.a "kugeuka" mabeberu na kuwa jipu la kuitangaza jinsi serikali ya CCM Mpya ilivyosusiwa, kuwekewa vikwazo na kutengwa na Jumuiya ya Kimataifa.
 
Kwa vyovyote vile lazima ifike mahali tanzania ijitegemee yenyewe kiuchumi hiweze kufinance miradi yake yenyewe kwa kiwango kikubwa bila kutegemea pesa za wahisani, huo ndio msingi wa kujitawala.

Safari dio hii tulishaanza tokea awamu ya tano iingie madarakani. challenge lazima tutapitia during transition period.

Challenge za ndani na nje kutoka mataifa makubwa na sera zao za kinyonyaji na ukoloni mamboleo, na wadau wa ndani ambao hawaamini katika tanzania huru kiuchumi.

Hii safari lazima ifike kivyovyote vile hakuna kurudi nyuma, safari ndio ishaanza. Either your survive or you perish, the choice is yours.
 
Anayeumia ni wewe , jipime akili utaelewa. Just support na hutapoteza chochote. Rafiki yako Lisu yuko ulaya anskula bata wewe utakula jasho na kazi Mara 4 zaidi
Jipime akili wewe kwanza ambae upo hapa kutetea dhuluma..
Acha tuumie kuliko kukaa raha mustarehe kutawaliwa na hilo jambazi la kura na bakaji la demokrasia..
Huyu mwizi wa kura akishabinywa kisawasawa na donors ndio itapatikana Katiba mpya na tume huru ya uchaguzi..
Make up your mind Dude..
Vipi umepagawa..unaishi kwa Shemeji nini??!
 
Back
Top Bottom