Wahitimu wa elimu ya juu, ujumbe wenu huu hapa

Wahitimu wa elimu ya juu, ujumbe wenu huu hapa

RIGHT MARKER

Senior Member
Joined
Apr 30, 2018
Posts
129
Reaction score
473
Mhadhara 32:

Lipo kundi la vijana waliohitimu elimu ya juu ambao watazeeka bila hata kumiliki viwanja vya kujenga nyumba ambavyo kwa sasa vinapatikana hadi kwa Tsh 1,000,000. Ni kwasababu kundi hili la vijana wenye elimu za juu wanasubiri ajira za ofisini zitakazoendana na GPA zao za vyuoni. Hawataki kufanya kazi halali za kutoka jasho, wanasubiri kazi za kwenye viyoyozi.

Wapo baadhi ya wahitimu wa elimu ya juu wanajishughulisha na kazi ndogo ndogo za mitaani pasipo kutazama elimu zao, hakika wapewe maua yao. Lakini wengi waliohitimu elimu za juu wapo mtaani hawataki kujishughulisha, mbaya zaidi huwadharau vijana wenzao ambao wanatafuta pesa kupitia kazi halali ndogo ndogo.

Naongea na wewe mhitimu wa elimu ya juu; dharau yako ndio inakufanya mpaka sasa huna kibarua cha kukuingizia pesa, huna mtaji, huna hata senti tano mfukoni, kwa ujumla huna mbele wala nyuma licha ya kuwa una vyeti vya elimu ya juu. Vijana wengi wanaojiita wasomi kitu pekee wanachomiliki ni smartphone walizotoka nazo vyuoni kwa pesa ya Boom.

Na hao ndio vijana ambao kutwa hawamalizi kulalamika kupitia comments za social media huku wakiwa wamekaa vijiweni au ufukweni. Si kwamba wanalalamika kwasababu ya fikra pana walizonazo bali ni njaa za kujitakia wenyewe, yes! ni njaa. Akitokea mbunge au waziri yoyote akiwaambia; "vijana mliohitimu elimu ya juu anzeni kujiajiri" - watampinga kwa comments nyingi za kejeli na matusi, kamwe hawataki kuukubali ukweli kwamba nafasi za kuajiriwa ni chache kuliko wingi wao, hii ni kwasababu kila mhitimu wa elimu ya juu ana ndoto ya kuwa waziri.

Akikutana na ujumbe mtandaoni usemao EWE MSOMI JIAJIRI, atachukua iphone yake aliyoinunua kwa Tsh 3,500,000 kisha atacomment; "Mtaji wa kujiajiri uko wapi, mbona wewe hukujiajiri" - asijue kwamba simu yake ni mtaji tosha.

Wahitimu wengi wa elimu ya juu hata kama watapewa mashamba ya bure, mbegu za bure, mashine za umwagiliaji, na mbolea za bure kamwe hawatoweza kulima - utamsikia; "sikusomea kulima nimesomea uhasibu" - yaani wanasubiri viti vya maofisini tu.

Right Marker
Dar es salaam
 
Mhadhara 32:

Lipo kundi la vijana waliohitimu elimu ya juu ambao watazeeka bila hata kumiliki viwanja vya kujenga nyumba ambavyo kwa sasa vinapatikana hadi kwa Tsh 1,000,000. Ni kwasababu kundi hili la vijana wenye elimu za juu wanasubiri ajira za ofisini zitakazoendana na GPA zao za vyuoni. Hawataki kufanya kazi halali za kutoka jasho, wanasubiri kazi za kwenye viyoyozi.

Wapo baadhi ya wahitimu wa elimu ya juu wanajishughulisha na kazi ndogo ndogo za mitaani pasipo kutazama elimu zao, hakika wapewe maua yao. Lakini wengi waliohitimu elimu za juu wapo mtaani hawataki kujishughulisha, mbaya zaidi huwadharau vijana wenzao ambao wanatafuta pesa kupitia kazi halali ndogo ndogo.

Naongea na wewe mhitimu wa elimu ya juu; dharau yako ndio inakufanya mpaka sasa huna kibarua cha kukuingizia pesa, huna mtaji, huna hata senti tano mfukoni, kwa ujumla huna mbele wala nyuma licha ya kuwa una vyeti vya elimu ya juu. Vijana wengi wanaojiita wasomi kitu pekee wanachomiliki ni smartphone walizotoka nazo vyuoni kwa pesa ya Boom.

Na hao ndio vijana ambao kutwa hawamalizi kulalamika kupitia comments za social media huku wakiwa wamekaa vijiweni au ufukweni. Si kwamba wanalalamika kwasababu ya fikra pana walizonazo bali ni njaa za kujitakia wenyewe, yes! ni njaa. Akitokea mbunge au waziri yoyote akiwaambia; "vijana mliohitimu elimu ya juu anzeni kujiajiri" - watampinga kwa comments nyingi za kejeli na matusi, kamwe hawataki kuukubali ukweli kwamba nafasi za kuajiriwa ni chache kuliko wingi wao, hii ni kwasababu kila mhitimu wa elimu ya juu ana ndoto ya kuwa waziri.

Akikutana na ujumbe mtandaoni usemao EWE MSOMI JIAJIRI, atachukua iphone yake aliyoinunua kwa Tsh 3,500,000 kisha atacomment; "Mtaji wa kujiajiri uko wapi, mbona wewe hukujiajiri" - asijue kwamba simu yake ni mtaji tosha.

Wahitimu wengi wa elimu ya juu hata kama watapewa mashamba ya bure, mbegu za bure, mashine za umwagiliaji, na mbolea za bure kamwe hawatoweza kulima - utamsikia; "sikusomea kulima nimesomea uhasibu" - yaani wanasubiri viti vya maofisini tu.

Right Marker
Dar es salaam
Unahisi nani alaumiwe??
 
Nakereka sana mtu anawekeza miaka 18 shule, kisha unamuambia awe dereva bodaboda, awe Saidia fundi. Kwa nini msibadili mfumo wa elimu angalau watu wajifunze kazi za mikono kwa muda mrefu. Kuliko kuandaa ma officer ambao hamtaki kuwatumia kwenye nyaja mlinzowaandaa.
 
Nakereka sana mtu anawekeza miaka 18 shule, kisha unamuambia awe dereva bodaboda, awe Saidia fundi. Kwa nini msibadili mfumo wa elimu angalau watu wajifunze kazi za mikono kwa muda mrefu. Kuliko kuandaa ma officer ambao hamtaki kuwatumia kwenye nyaja mlinzowaandaa
Mfumo wa elimu ni wa kufumuliwa na kujengwa upya, hauendani na kasi ya mabadiliko ya dunia
Unatengeneza wasomi tegemezi wengi kuliko wasomi wanaotengeneza ahira
 
Mfumo wa elimu ni wa kufumuliwa na kujengwa upya, hauendani na kasi ya mabadiliko ya dunia
Unatengeneza wasomi tegemezi wengi kuliko wasomi wanaotengeneza ahira
Sasa tujiulize Mimi na wewe mkuu, kwa nini hawataki kubadili mfumo wa elimu?. Wao watawala ndio wafaidika wakubwa wa hii mifumo mibovu ya elimu.
 
Sasa tujiulize Mimi na wewe mkuu, kwa nini hawataki kubadili mfumo wa elimu?. Wao watawala ndio wafaidika wakubwa wa hii mifumo mibovu ya elimu.
Wanafaidika nao direct or indirect. Kwanza unatengeneza wapiga kura wengi, jamii inyime elimu bora na uchumi, halafu angalia maadili yatakavyo poromoka. Mwanasiasa akileta tu pesa wanahama kirahisi
 
Nakereka sana mtu anawekeza miaka 18 shule, kisha unamuambia awe dereva bodaboda, awe Saidia fundi. Kwa nini msibadili mfumo wa elimu angalau watu wajifunze kazi za mikono kwa muda mrefu. Kuliko kuandaa ma officer ambao hamtaki kuwatumia kwenye nyaja mlinzowaandaa.
Sawa kabisa nadhani mfumo wetu wa elimu una changamoto tunapaswa kufanya mabadiliko tena makubwa.
 
Swala la kuwa na simu njanja kwa dunia ya sasa ni unavoidable tena kwa wasomi wa vyuo kwa sababu ajira nyingi zinapatikana kwenye mitandao ya kijamii na zinaobwa kwa kutumia internet lkn pia ata kukaa updated na maswala ya kidunia ikiwa ni pamoja nakujiongezea maarifa.
 
Wewe ni mjinga sana(huelewi
unachosema), nyie ndio mnafikiri wasomi wote wana iphone na hawajitumi kwa kuangalia vijana wachache wa huko dar. Kiukwel vijana wanajituma sana, tatizo ni mifumo mibovu ya elimu. Hata kwenye utafutaji pia vikwazo ni vingi sana kwa kijana kujikwamua. Hebu toka hapo dar kwa shemeji yako tembea mikoani huku uone vijana wasomi wanvyombana na changamoto wanazopitia.
 
Shida ya ajira ipo duniani kote hata wakibadilisha mfumo wa elimu shida haiwezi kuisha Cha muhimu kwa mzazi ni kumuuliza mwanao ana taka fani Gani au talent Gani ambayo itamuwezesha kuja kupambana na maisha Yake ya badae kusoma sana kwa sasa sio njia ya kuja kuwa waziri au kuajiriwa soma wastani Anza kupambana na maisha
 
 
Mhadhara 32:

Lipo kundi la vijana waliohitimu elimu ya juu ambao watazeeka bila hata kumiliki viwanja vya kujenga nyumba ambavyo kwa sasa vinapatikana hadi kwa Tsh 1,000,000. Ni kwasababu kundi hili la vijana wenye elimu za juu wanasubiri ajira za ofisini zitakazoendana na GPA zao za vyuoni. Hawataki kufanya kazi halali za kutoka jasho, wanasubiri kazi za kwenye viyoyozi.

Wapo baadhi ya wahitimu wa elimu ya juu wanajishughulisha na kazi ndogo ndogo za mitaani pasipo kutazama elimu zao, hakika wapewe maua yao. Lakini wengi waliohitimu elimu za juu wapo mtaani hawataki kujishughulisha, mbaya zaidi huwadharau vijana wenzao ambao wanatafuta pesa kupitia kazi halali ndogo ndogo.

Naongea na wewe mhitimu wa elimu ya juu; dharau yako ndio inakufanya mpaka sasa huna kibarua cha kukuingizia pesa, huna mtaji, huna hata senti tano mfukoni, kwa ujumla huna mbele wala nyuma licha ya kuwa una vyeti vya elimu ya juu. Vijana wengi wanaojiita wasomi kitu pekee wanachomiliki ni smartphone walizotoka nazo vyuoni kwa pesa ya Boom.

Na hao ndio vijana ambao kutwa hawamalizi kulalamika kupitia comments za social media huku wakiwa wamekaa vijiweni au ufukweni. Si kwamba wanalalamika kwasababu ya fikra pana walizonazo bali ni njaa za kujitakia wenyewe, yes! ni njaa. Akitokea mbunge au waziri yoyote akiwaambia; "vijana mliohitimu elimu ya juu anzeni kujiajiri" - watampinga kwa comments nyingi za kejeli na matusi, kamwe hawataki kuukubali ukweli kwamba nafasi za kuajiriwa ni chache kuliko wingi wao, hii ni kwasababu kila mhitimu wa elimu ya juu ana ndoto ya kuwa waziri.

Akikutana na ujumbe mtandaoni usemao EWE MSOMI JIAJIRI, atachukua iphone yake aliyoinunua kwa Tsh 3,500,000 kisha atacomment; "Mtaji wa kujiajiri uko wapi, mbona wewe hukujiajiri" - asijue kwamba simu yake ni mtaji tosha.

Wahitimu wengi wa elimu ya juu hata kama watapewa mashamba ya bure, mbegu za bure, mashine za umwagiliaji, na mbolea za bure kamwe hawatoweza kulima - utamsikia; "sikusomea kulima nimesomea uhasibu" - yaani wanasubiri viti vya maofisini tu.

Right Marker
Dar es salaam
Ni kweli ila try to think , kama mtu wa bachelor auze karanga la saba aytafanya Kaz gan .......
Serikali inatakiwa iandae degree holder mwenye mtazamo tofauti na mtu ambae ajasoma
 
Back
Top Bottom