Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Mungu awasimamie watumishi wake Amen.Binafsi tangu nikiwa na Miaka minne Wazazi wangu walikuwa wananunua tapes za Mwl Mwakasege,amekuwa mwalimu mwema sana kwangu Kwa Miaka takribani 30.Mungu amuongezee.
 
Mkuu, nilieleza kuwa hao niliowaweka ni ambao kwa namna Moja ama nyingine nimebarikiwa na huduma zao.

Nilivisoma vitabu kadhaa vya Uebert Angel, japo kuna baadhi ya mambo ambayo mwanzoni vilinitia mashaka kuhusu huduma yake, niliamua kupuuzia baada ya kubaini kuwa mentor wake ni Pastor Chris.

Pastor Chris naye nilikuwa nina mashaka naye, lakini mashaka yaliisha nilipogundua kuwa rafiki yake wa karibu ni Benny Hinn.

Hata Benny Hinn, nilikuja kumkubali vilivyo baada ya kugundua ukaribu alikokuwa nao na Reinhard Bonnke.

Unauona mnyororo ulivyo? Bonnke, Benny Hinn, Pastor Chris, Uebert Angel.

Lakini sivyo tu, huwa nina "falsafa" yangu kwa habari ya watumishi. Kwamba, katika mafundisho yao, nitatofautisha chuya na wali. Nikikutana na chuya, nitatema lakini wali nitaumeza.

"Sibugii" kila kitu kisemwacho na mtumishi. Nikijiridhisha kuwa akisemacho kipo nje ya Biblia, nakiweka kando nasubiria kingine.
Kiongozi wa KIROHO wa Benny Hin nazani ni Catherine kuhlman na huwaga anaenda kutembelea kaburi lake Anasema Ile roho ya Catherine ime incarnate kwake

Sasa sijui hii nini kama sio uchawi
 
Hivi Mitimingi ni nabii,nayakubali sana mafundisho yake ya ndoa na mahusiano.
 
kuna siku nilienda semina ya Mwakasege, niliondoka katikati ya mahubiri aliposema Cain na Abel ni mapacha(tena akarudia mara mbili kusema haya (NI MAPACHA SOMENI BIBLIA YENU VIZURI,,halafu katikati ya mahubiri kuna lugha anaongea ambazo hazieleweki,,ndio wanaita kunena kwa lugha
Kwangu mimi mpaka sasa kwa hapa Tanzania ni hawa.
1. Mwalimu Christopher Mwakasege
2. Pastor Carlos Kirimbai

Jamaa wanaijua bible fresh, wanaisoma kila siku, na wanatamani kila mtu aisome Bible fresh na kuitambua. Yote kwa yote wanakufanya umjue Yesu at personal level bila kubabaishwa na chochote au yoyote.

Naambiwa walifanikiwa kuukwepa upepo wa kidini (kidhehebu) uliokuwa ukivuma vilivyo miaka ya 90, na wamefanikiwa pia kuuvuka huu upepo wa sasa wa tamaa za mali na umungu mtu unaotikisa kanisa la Tz kwa zaidi ya 80%.

Yote kwa yote jamaa wanaweza kukushawishi umjue Yesu na kuijua Bible fresh hata kama wewe sio mkristo au wewe ni mpagani.
 
Yeyote unayeona ametumiwa vizuri na Roho Mtakatifu kuhubiri injili, nashauri usimpe sifa yeye wala kumshabikia kama ulivyopanga orodha. Mpe utukufu, sifa, heshima na shukrani Roho Mtakatifu anayewatumia. Nachelea kusema unaweza kujikuta unawaabudu pasipo kujitambua!

Aidha, hakuna awezaye neno lolote pasipo Yesu Kristo aliyetukomboa na kutununua kwa damu yake ya thamani. Mtukuze Yeye daima, si kiumbe au chombo anachokitumia. Ni ushauri tu!
 
Mchungaji Joshua Maponga, ukiskiza sentensi 2 tu huwezi acha kumskiza.

Pan africanist, and true son of Africa & bible hero
 
Je? Kuna watumishi wa mungu ukifka tu wanataja matatizo yako before ujawaelezea? Hii imekaaje wataalam??

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
Kwanza rekebisha andika Mungu kwa kuanza na M kubwa.

Najibu swali lako, ndio wapo watumishi wa namna hiyo. Ila kama alivyosema mdau hapo juu hutakiwi kubebwa na hii ya kutajiwa majina ya baba yako sjui watoto mara uambiwe una jirani anaitwa Mbanga nk

Ukisoma Biblia imeeleza kila kitu kuhusu watumishi feki na wasio feki, na kila mtumishi amepewa sifa zake uamuzi ni wako yupi umfuate yupi usimfuate. Nasikitika wengi wanatekwa na hawa wanaopiga ramli za kutajiwa majina... Utasikia mtumishi anamuuliza mshirika....

Mtumishi: unaitwa John ennh

Mshirika: Ndio baba mchungaji/Nabii

Mtumishi: Mke wako wa kwanza uliachana naye, huyu wa sasa umekuja nae kanisani na anaitwa Kivuli..

Mshirika: Amen mtumishi nimekuja nae

Mtumishi: Mimi na wewe tulishawahi kuonana kabla ya leo?

Mshirika: Hapana leo ndio mara ya kwanza..

Sehemu hii ndiyo watumishi wengi hujizolea kondoo wasiojielewa kwa kutajiwa taarifa zake ambazo anaamini hakuna mwingine anaezijua basi inakuwa ithibati ya kuamini maelezo yote anayopewa.

Tusome neno la Mungu bila kuchoka, tumuombe Mungu bila kukoma, yeye ni yule yule jana leo na hata milele. Mwisho tuwe makini sana na hawa wahubiri wa mafuta dunia iko hovyo kuliko, nafsi nyingi zinatekwa kwenye uharibifu.
 
Yule anahubiri au anasuta na kufanya comedy. Anahubiri saa Zima bila kuweka hata kifungu kimoja cha Biblia zaidi ya kufanya utani na kuchomekea maneno ya mtaani. Mtu mwenye akili timamu hawezi kaa na kumsikiloza mgogo hata mara 1.
We jamaa unaelewa sana, nikiperuzi mtandaoni nikiona clip ya Mgogo huwa nairuka [emoji1787][emoji1787]

Hafanyi rejea yeyote toka kwenye Bible, yule mwamba komedi balaa, wanawake ndio wanapenda kumsikiliza fuatilia utagundua.
 
Uko sahihi sana. Nafkiri mada ilitakiwa kuzitaja kazi za watumishi na si kulinganisha sifa bila vigezo.
Nitatoa mfano, Paulo, mtumwa wa Yesu Kristo anasema yeye ni zaidi ya wale thenashara. Lakini zaidi katika nini? Ni katika kufungwa, katika kufunga, katika dhoruba na katika mapigo. Yaani zaidi katika taabu ya injili. Lakini pia yeye ndiye aliyefanya kazi ya kusambaza injili zaidi kwa mataifa. Lakini pamoja na yote hakuwadharau wenzake, isipokuwa aliwaonya kwa upendo.

Pia, ikumbukwe hizi karama za roho hutolewa na roho kadri apendavyo roho mtakatifu. Mwingine mwalimu, mwinjilisti, utume na unabii.

Neno linatuagiza tuzijaribu kila roho, tupime au tuwatambue watumishi kwa matunda yao na maisha yao kwa ujumla. Na pia tuangalie nani kawaachia joho, yaani tuangalie baba zao wa kiroho.

Paulo aliitwa na Yesu akapewa Philipo, kuna Elisha na Eliya, kuna Musa na Haroun, Joshua na Caleb, kuna Paulo na Timotheo. Watoto wa Kulola na Lazaro unapata TAG / EAGT hapo kwa DSM hapo ma nguli kama Katunzi, Kakobe na wengi ambao wameanzisha huduma na zimesimama imara mpaka sasa.

Hivi ndivyo vipimo vya kibiblia. Ni muhimu kukumbuka kuwa hiyo ni mifano michache. Wapo watumishi wa Mungu wanafanya kazi kubwa hasa vijijini na wanatumika kweli kweli lakini hawaimbwi sana masikioni mwa watu. Ukiwa mfatiliaji wa injili utalielewa hili.
[emoji120]
 
Back
Top Bottom