Hawa watu huwa wa kusukumwa sana ili wakupe huduma ambazo ni wajibu wao kuzitoa, ni nadra sana kupata Hotel, mgahawa au Bar bongo ambapo wahudumu wake sio wa kususuasua na wako on point muda mwingi na kwa wateja walio wengi
Shida ni kwamba hawalipwi vizuri, wako kwenye hizo kazi kupoteza muda tu au huwa wanapatikana kwa kuokotwa mtaani na wamiliki pasipo kuwa na vigezo vyovyote vile ??
View attachment 3053318
Nadhani tuwe na utaratibu wa kutoa Tip, au keep change,
Nchi kama Marekani , unachangamkiwa kuhudumiwa , kutokana kwamba kuna Tip,
Hawa wenzetu kazi zao maslahi ni kidogo sana, wana msongo wa mawazo, hivi unawaona askari Traffic jinsi walivyo active huko mabarabarani, ? Unafikiri ni kwamba wanaipenda sana kazi yao?
Rushwa ndio inawafanya wawe active vile,. Hata akiwa off , sio ajabu kumkuta barabarani.
Sasa tuwe na utaratibu wa kuwapa hawa wahudumu angalau 5% ya bei ya chakula ulichokula. Hata kwenye baa iwe hivyo, mtu unatumia sh 30000/- kula au kunywa , mtoto wa watu wakakuhudumia hapo, unaagiza tu, nipe maji, nipe tooth pick, nipe sijui toilet paper, mwisho kabisa nipe change yangu, halafu huyo unaenda kwenye gari lako!!!! Bila kumpa hata 1000!!!!, hata aibu huna ?!!! SHAME TO YOU. Miafrika ndivyo tulivyo, mfyuuuuu,
Tumekuwa na riho mbayaaaaa.
Unaletewa maji , unaletewa chakula, huduma zote unapewa kwa upendo, unamaliza kula hata kusema ansante kwa kunihidumia na wewe shika hii, unaondoka tu na mitako yako, nyamafu kabisa, shame, shame, shame to to you all.
Mna roho mbaya sana nyie,
Unawezaje kutumia sh 60000, na limeza umechafua na maugali yako na mamifupa umeacha hapo kama mbwa , hata 2000 mbili ya nauli unashindwa kumpa mhudumu? Nyambafu kabisa nyie.
Nilishaenda kwenye baa fulani na mwanamke, tumehudumiwa vizuri, tunaondoka , naacha tip, eti yule mwanamke ananikataxa! Nilitaka kumlamba kibao, na toka siku hiyo sitaki hata kumwona, maana tabia hio ndio ina mliflect jinsi alivyo rohoni.
Hivi huoni aibu kabisaaa, unaenda na gari , unanunua au unaagiza chakula cha 15000, unakula , halafu unaondoka hivihivi hata kuacha 1000/-?!???! Duuu, watu mna roho mbaya.
Hivi unadhani huyo mhudumu analipwa sh ngapi?
Mnapenda sana kudharau watu nyie,.
Tip ndio mpango mzima ndugu, kama ulikuwa hujui ndio ujue leo.