Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Shehe Mkuu wa Tanzania (BAKWATA) Amewaagiza Mashehe Nchi Nzima kuitumia siku ya Ijumaa ijayo kuliombea Taifa kwa lengo la kuliepusha na Majanga .
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amewaagiza masheikh na maimamu nchini kufanya dua maalumu ya kumuomba Mungu aliepusha Taifa na maafa mbalimbali kama yaliyotokea wilayani Katesh mkoani Manyara.
Maafa hayo yaliyosababisha vifo vya watu 89 hadi sasa yalitokea alfajiri ya Desemba, 2023 katika Mji Mdogo wa Katesh na vitongoji vya karibu vikiwemo vya Jorodom, Ganana, Katesh na Dumbeta pamoja na vijiji vya Gendabi na Sarijandu.
Katika janga hilo watu 139 walijeruhiwa kati yao 120 wameruhusiwa huku 17 wakiendelea na matibabu hospitalini.
Mufti Zubeir ametoa maagizo hayo leo Jumanne Desemba 12, 2023 wakati akizungumza na wanahabari kuhusu masuala mbalimbali yaliyojitokeza likiwemo la maafa ya Hanang, huku akitoa pole kwa waathirika wa tukio hilo.
Maafa hayo yaliyosababisha vifo vya watu 89 hadi sasa yalitokea alfajiri ya Desemba, 2023 katika Mji Mdogo wa Katesh na vitongoji vya karibu vikiwemo vya Jorodom, Ganana, Katesh na Dumbeta pamoja na vijiji vya Gendabi na Sarijandu.
Katika janga hilo watu 139 walijeruhiwa kati yao 120 wameruhusiwa huku 17 wakiendelea na matibabu hospitalini.
Mufti Zubeir ametoa maagizo hayo leo Jumanne Desemba 12, 2023 wakati akizungumza na wanahabari kuhusu masuala mbalimbali yaliyojitokeza likiwemo la maafa ya Hanang, huku akitoa pole kwa waathirika wa tukio hilo.