Waislamu wazindua program 2010

Waislamu wazindua program 2010

Ni bora wawe hawana Diploma kuliko kuwa na zile za St.. St,, ambazo zinakubeba toka Certificate mpaka PhD.



au zile za islamic, islamic .. islamic....! zinazomtoa mtu mwenye Phd mpaka certificate ya madrassa. ! HAHAHAHAHAHAHAH....!

THE LATE MO.
 
Tujiulize kati ya hao masheikh wanaopigania haki ya Waislam ni wangapi hata wana diploma kujua haki ya kataba ya nchi kutobadilishwa?

Usikashifu dini yetu wengi wamesoma wana certificate za MADRASA na ni walimu wazuri wa MADRASA
 
jamani jamani huu udini utatupeleka wapi? sifa za kiongozi bora ni kuwa muumini wa dini fulani tu na si dini nyingine? mimi nafikiri sifa kubwa ya kiongozi ni uzalendo. Tukianza kuchagua watu kwa misingi ya dini tutafika kweli?
 
Wakatoliki itawaudhi hiyo program. lakini nchi ni ya wote . You can fool some people some time But ou can't all the people all the time.

Hafif....fikra finyu sana....kwanini huisi wakatoliki ndo watakaochefuka na hii programu ya waislamu?Madhehebu mengine ya kikistru unayaweka wapi?Dini nyingine zikiwemo za asili zinafurahi hilo?Fikiri kwanza...acha hisia hisia...
 
Nimefurahi sana mwangozo huu umetoka wakati nipo Tanzania. Nitakuwepo mpaka ijumaa na namba ninayotumia ni 0777 420000 ( ya dereva wangu)


Nafikiri kinachokusumbua wewe ni kutaka watu uwaendeshe kama makondoo. Yaani wewe unataka kila mtu aisifie Chadema, Ukatoliki na mengine.

hakika nipo na natumai mwenzangu Tumaini naye yupo huru sana kuchangia kwa mujibu wa mawazo yake na sio kushinikizwa ka kashfa na matusi. Tunaomba utuletee hoja na si kingine.

Barubaru,
Hapa tatizo langu si CHADEMA. Ila kuingiza habari za dini kwenye kila mjadala. Kama ni dini kuna kitengo chake.

Kama mtu akija na kuichambua CHADEMA vizuri basi mie hainipi wasiwasi.

Kumbuka mie ni MPINZANI mkubwa wa Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema mwaka huu. Nina imani Zitto alifanya makosa kugombea na Mbowe alifanya makosa kuanza siasa chafu kwa Zitto. Kama mambo yangelienda kwa uwazi na ukweli, hii aibu isingelikuwepo.
 
Barubaru,
Hapa tatizo langu si CHADEMA. Ila kuingiza habari za dini kwenye kila mjadala. Kama ni dini kuna kitengo chake.

Kama mtu akija na kuichambua CHADEMA vizuri basi mie hainipi wasiwasi.

Kumbuka mie ni MPINZANI mkubwa wa Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema mwaka huu. Nina imani Zitto alifanya makosa kugombea na Mbowe alifanya makosa kuanza siasa chafu kwa Zitto. Kama mambo yangelienda kwa uwazi na ukweli, hii aibu isingelikuwepo.
Mhhhh! wewe ukiacha kuingiza udini wako na sisi tutaacha lakini wewe unafikiri ukifanya insult kwa uislamu wenye dini zetu tutanyamaza..ikitaka kuheshimiwa jiheshimu
 
imeshindwa kujibu hoja unakuja kutisha watu hapa..hatudanganyiki!

shura inataka kiongozi wa kitaifa, muadilifu mwenye kufahamu historia sahihi ya Tanzania, mwenye kujua kwamba ubaguzi ni aibu taifa...na ustawi wake...what is bakwata bana toa hoja ndugu??
1. Nashukuru kwa majibu yako ndugu, lakini sijamtisha mtu yeyote zaidi ya kueleza ukweli wa mambo! Sijui kama umejiuliza kwamba shura ya maimamu inapotafuta kiongozi wa kitaifa kwenye misikiti pekee, huyo kiongozi atawaongoza akina nani?
2. Na wanaposema kwamba wanataka kiongozi ambaye hatahusisha uislamu na ugaidi, huyo kiongozi hatakuwa mwadilifu, in the first place, kwa sababu hatakuwa anasema ukweli, atakuwa MNAFIKI mkubwa! Soma maneno ya Quran kuhusu UGAIDI: "Mola wako Mlezi alipo wafunulia Malaika: Hakika Mimi ni pamoja nanyi, basi watieni nguvu walio amini. Nitatia woga katika nyoyo za walio kufuru. Basi wapigeni juu ya shingo na wapigeni kwenye kila ncha za vidole." (Quran 8:12).
3. Sasa hapa mimi nawatisha watu au marehemu Muhammad ndio anayetishia uhai wa watu wasio na hatia kupitia Quran? Kuwa na huruma na nafsi yako ambayo inakutaka useme ukweli siku zote!
 
1. Nashukuru kwa majibu yako ndugu, lakini sijamtisha mtu yeyote zaidi ya kueleza ukweli wa mambo! Sijui kama umejiuliza kwamba shura ya maimamu inapotafuta kiongozi wa kitaifa kwenye misikiti pekee, huyo kiongozi atawaongoza akina nani?
2. Na wanaposema kwamba wanataka kiongozi ambaye hatahusisha uislamu na ugaidi, huyo kiongozi hatakuwa mwadilifu, in the first place, kwa sababu hatakuwa anasema ukweli, atakuwa MNAFIKI mkubwa! Soma maneno ya Quran kuhusu UGAIDI: "Mola wako Mlezi alipo wafunulia Malaika: Hakika Mimi ni pamoja nanyi, basi watieni nguvu walio amini. Nitatia woga katika nyoyo za walio kufuru. Basi wapigeni juu ya shingo na wapigeni kwenye kila ncha za vidole." (Quran 8:12).
3. Sasa hapa mimi nawatisha watu au marehemu Muhammad ndio anayetishia uhai wa watu wasio na hatia kupitia Quran? Kuwa na huruma na nafsi yako ambayo inakutaka useme ukweli siku zote!

Hoja yako imekaa KIDINI na ume-quote quran "out of context" yaani kutafsiri quran unatakiwa usome huo ujumbe (sura) in a "holistic manner" i.e. umetolewa wapi? kwa ajili ya nani? na wakati gani? ok. kwahiyo swala lako la maradhi yako ya udini wako sintajibu ok au weka kule kwenye dini ntakusaidia..
Kwakuwa ulikuwa na hoja moja tu yenye kuhitaji ufafanuzi

1. Kiongozi wa kitaifa kutafutwa misikitini pekee kiongozi huyo ataongoza kina nani? ...Hiyo si kweli shura inapeleka mwongozo kwa watanzania wote ni mikutano yake inafanyika kwenye public places all over the country...kwa hiyo ni kwa wananchi wote unaweza kuhudhuria ili uweze kupata historia sahihi ya nchi na matatizo ya msingi ya nchi hii nzuri...unlike waraka ambao husambazwa na kufundishwa kwenye jumuiya za kikatoliki na kufundishwa na mapadre huo ndio umekaa kibaguzi si kitaifa
 
Ahali yangu Fundi mchundo.

Hakika mimi nimeununua jana majira ya saa sabaa mchana baada ya swala la Adhuhur pale msikiti wa Mtoro kariakoo kwenye duka la radio Quran.

Nimefurahi sana mwangozo huu umetoka wakati nipo Tanzania. Nitakuwepo mpaka ijumaa na namba ninayotumia ni 0777 420000 ( ya dereva wangu)


Nafikiri kinachokusumbua wewe ni kutaka watu uwaendeshe kama makondoo. Yaani wewe unataka kila mtu aisifie Chadema, Ukatoliki na mengine.

hakika nipo na natumai mwenzangu Tumaini naye yupo huru sana kuchangia kwa mujibu wa mawazo yake na sio kushinikizwa ka kashfa na matusi. Tunaomba utuletee hoja na si kingine.

1. Nilisema hii ni biashara na wewe kwa kuununua umedhihirisha. Hao wakatoliki wanaowakera hawakuuza waraka wao. Huu ni mpango wa ulaji wa watu wachache wanaojifanya ndiyo wawakilishi wa waislamu wote.
2. Kulikuwa na haja gani kutuambia kuwa simu unayoitumia ni ya dereva wako? Au ndiyo kutudhihirishia bado ile dhana ya utwana?
3.Nitakutakaje usifie Chadema au ukatoliki wakati mimi mwenyewe sijawahi kufanya hivyo? Wamisheni wote si wakatoliki kama ambavyo pengine unadhani.
4. Naam, Tumaini ana haki ya kuchangia kama mtu mwingine. Na vivyo hivyo ana haki ya kujibiwa kadri anavyoileta hoja yake.
5. Hoja yangu ni kuwa hii ni programu jina tu. Ni mpango ambao umeletwa kuendelea kuwagawa wamisheni na waislamu. Wakati huu unatamka wazi kuwa mgombea achaguliwe kutokana na ahadi zake kwa waislamu, huo wa wenzenu haukufanya hivyo. Hatari ya kuweka litmus test kama hii ni kuwa watajitokeza walaghai au wachochezi watakaoitumia kwa ajili ya ajenda zao.

Amandla.......
 
Exactly, wao walipinga progarmme na waraka wa Wakatoliki wakisema ni kuchanganya dini na siasa. Na walisema mambo mengi sana 'negative' kuhusu Wakatoliki na Wakristo kwa ujumla.

Hao hao leo wanakuja na similar issue na hawaoni kama walichowafanyia Wakatoliki wao wenyewe. Huo ni unafiki mkubwa. "Sisi hatufanyi hivi..." kumbe na wao wanafanya. Si wanadai Qur'an inajitoshereza haihitaji waraka wala mwongozo. Sasa mwongozo na programme ni vya nini, kama siyo fix tu.

Kwenye psychology kuna 'expression' inaitwa 'split personality'. Ni mtu kusema kitu fulani na baadaye kusema hajasema hivyo. Au kupinga kitu na baadaye kukifanya kitu kilekile ulichokipinga.

Mimi hainiingii akilini, unless waseme walichokuwa wanapinga ilikuwa geresha tu. Umenielewa? Nilitegemea wao wasingezindua mwongozo wala progarmme ili wawe mfano kwa wote. Lakini kumbe hawana jipya ni kuji'contradict' tu. What a shame!

Kwa taarifa yako waliopinga waraka wa wakatoliki ni BAKWATA ambayo si waislam wote wanaifuata. Kina Ponda wamekuwa against BAKWATA kwa miaka mingi.
 
Wanasema tatizo kubwa ni udini na wana imply kuwa viongozi wakristo ndiyo mafisadi....Soma kwa makini...Ningependelea kuona mwongozo wa kitaifa zaidi.

Kusema kuna udini hakuna uhusiano na implication kwamba viongozi wakristo ndio mafisadi.

Ina maana mkristo akisema kuna udini ina maana anasema Waislamu ndio mafisadi? I dont think so.

Kama mtu anaamini mafisadi wengi ni waialamu ama wakristo ana uhuru wa kusema waziwazi. Kusema kuna tatizo la udini haiwezi kuwa na maana kwamba wasio dini ya msemaji ndio mafisadi.
 
Hii progamme ina agenda nyingi zilizojificha na kuna wanaofuata mkumbo tu bila kujua hasa ndani yaliyomo ni nini.

Kuna the so called wapigania uhuru wenye grievances za miaka mingi walioona hawakutendewa na kupewa heshima ya kutosha hasa na utawala wa awamu ya kwanza.Wameandika vitabu weeee wakaona havijawaletea matunda..sasa wanakuja na program.

Ngoja tuone hii nchi itafika wapi kwa ubiinafsi wa watu wachache wenye kutumia majority innocent ignorant poor and the down trodden!
 
KAMATI ya Siasa ya Shura ya Maimamu jana ilizindua programu ya Elimu ya Uraia yenye lengo la kutekeleza kwa vitendo waraka wake kuhusu uchaguzi mkuu wa mwakani.

Programu hiyo inataja sifa za msingi za chama na mgombea anayepaswa kuchaguliwa, masuala ambayo yalisababisha utata mkubwa baada ya nyaraka hizo za Shura ya Maimamu na Kanisa Katoliki kutolewa.

Mpango huo umo kwenye kitabu cha kurasa 76 na unataka Waislaam kuutekeleza kwa vitendo mwongozo uliozinduliwa na kamati hiyo Agosti 26 mwaka huu.

Programu hiyo ilizinduliwa jana kwenye Msikiti wa Mtoro jijini jijini Dar es Salaam na balozi wa zamani wa Tanzania katika nchi za Ufaransa na Italia, Abbass Sykes. Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo, Sykes alisema: "Nchi hii ni ya Watanzania wote, hakuna chama wala mtu mwenye hati miliki ya kutawala nchi hii."

Alisema kila chama na mtu bila ya kujali rangi, dini, kabila au mahali alipotoka, ana haki ya kuomba uongozi ili mradi awe amegombea nafasi ya uongozi kwa kufuata taratibu na sheria zilizopo.

Sifa za mgombea zinatajwa katika mada nambari tano ya kitabu hicho cha 'Elimu ya Uraia' kikitaja bayana sifa za mgombea anayetakiwa kupigiwa kura na Waislamu. "Awe kiongozi mwadilifu, anayejua matatizo makuu ya nchi na wananchi na mjuzi wa kuyatatua.

Matatizo makuu ya nchi ni udini, ubaguzi dhidi ya Waislaam au baadhi ya watu, rushwa, uchafuzi wa mkataba wa Muungano na ukosefu wa maadili kwa viongozi," inasema sehemu hiyo katika ukurasa wa 65.

"Awe kiongozi mwenye utashi wa kuwasaidia wananchi wote bila ya kujali tofauti zao, ajali zaidi maslahi ya umma kuliko ya chama chake, awe tayari kusaidia urejeshaji wa haki za wananchi zilizotaifishwa na serikali ikiwa ni pamoja na shule, ardhi na majengo."

Kitabu hicho kinaeleza kuwa ili mgombea apigiwe kura, anapaswa awe anafahamu haki na dhuruma walizofanyiwa Waislaam kwa kutotendewa haki sawa na dini nyingine na awe tayari kufuta makubaliano baina ya serikali na kanisa.

"Kiongozi huyo lazima awe tayari kutomwaga damu ya Waislaam kama ilivyotokea mara kadhaa katika misikiti, maandamano ya kudai haki au katika mahubiri ya kidini."

Kuhusu chama kinachostahili kuingia madarakani, kitabu hicho kinafafanua kuwa ni kile ambacho serikali yake haitawazuia Waislaam kufuata na kutangaza dini yao kwa uhuru na ambayo haitabadilisha sheria za Waislaam zinazohusu mambo ya mirathi, ndoa na talaka.

Kamati hiyo ya siasa ya Shura ya Maimamu, ilikumbushia migogoro mbalimbali baina ya serikali na Waislaam na kwamba chama kinachofaa ni lazima kiwe tayari kuunda tume huru kuchunguza mauaji ya Waislaam yaliyotokea miaka iliyopita.

"Kiwe chama ambacho serikali yake, itakubali kufanyika kwa uchunguzi wa mauaji ya waislaam katika maandamano ya kutetea Qur-an 1988, mauaji ya msikitini Morogoro 1994, mauaji ya kinyama msikitini Mwembechai 1998, mauaji ya imamu wa msikiti wa Mwembetanga 2001 na mauaji katika maandamano ya Waislaam ya kupinga kufungwa kwa mwenzao aliyesema Yesu si Mungu mwaka 2001," inafafanua sehemu ya kitabu hicho.

"Kiwe chama ambacho serikali yake haitakuwa tayari kupokea maagizo, sheria na misamiati mipya dhidi ya Waislaam kama vile magaidi au siasa kali na kuwasikiliza masheikh na maimamu pamoja na viongozi wengine wa taasisi za kiislaam."

Awali katibu wa kamati ya siasa ya Shura ya Maimamu, Sheikh Ponda Issa Ponda alisema: "Muongozo (wa awali) umefanikiwa sana hasa mikoani, katika mikoa ya kanda ya kusini zaidi ya asilimia 90 ya viongozi walishinda katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji ni Waislaam wanaojielewa."

"Asilimia 75 ya wilaya zote za Tanzania zimefanya warsha na makongamano kuuchambua mwongozo, hotuba za Ijumaa zenye mwelekeo mmoja zimeanza jijini Dar es Salaam, Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislaam limetanga kura ya maslahi kuwa ajenda yao kuu 2010 na Taasisi 15 zimesaini makubaliano ya pamoja kuelekea uchaguzi mkuu."

Kwa mujibu wa sheikh Ponda, program mpya ya elimu ya uraia itatekelezwa katika mifumo ya machapisho, warsha, semina, makongamano, mikutano ya hadhara na hotuba kali za Ijumaa zenye mwelekeo mmoja katika miskiti yote nchini.

Source: Mwananchi
Tunawatakia mafanikio mema
 
Asiyejua maana usimfunze maana. Tuacheni na program yetu ya mwongozo wa 2010.

Kwani kutoa mwongozo ni kosa kisheria?
Kutoa program ya mwongozo ni kosa kisheria?
Mbona DCI au hata mwanasheria mkuu hajasem lolote?

Sasa nyie wakristo kinawauma nini?
 
Asiyejua maana usimfunze maana. Tuacheni na program yetu ya mwongozo wa 2010.

Kwani kutoa mwongozo ni kosa kisheria?
Kutoa program ya mwongozo ni kosa kisheria?
Mbona DCI au hata mwanasheria mkuu hajasem lolote?

Sasa nyie wakristo kinawauma nini?

Kwani nyinyi mlipoulalamikia waraka wa wakatoliki ilikuwa ni kwa sababu wao walivunja sheria?

Sasa kwa nini mliileta hii habari humu kama hamkutaka wamisheni wachangie?

Kitu tuchoogopa wengine ni kuwa hicho mnachotaka kiwe kikitokea hatutawaona mstari wa mbele. Kazi hiyo mtawaachia hao wafuasi wenu ambao wengi hawana nafasi nzuri kama za kwenu.

Amandla......
 
Ni bora wawe hawana Diploma kuliko kuwa na zile za St.. St,, ambazo zinakubeba toka Certificate mpaka PhD.
kama ya Slaa. mimi siku zote humwita Slaa kwangu sio DR.
PIA JITAHIDI UPATE UJUMBE WA IJUMAA WA OKTOBA 24 KUTOKA MSIKITI WA IDRISA WENYE KICHWA CHA HABARI KAULI ZA SLAA NA ASKOFU KILAINI HAZINA NIA NJEMA NA WAISLAM.
AU SOMA GAZETI LA JAMBO LEO TOLEO 111 LA OKTOBA 19,2009 KUONESHA NIA MBAYA YA SLAA
 
Hii progamme ina agenda nyingi zilizojificha na kuna wanaofuata mkumbo tu bila kujua hasa ndani yaliyomo ni nini.

Kuna the so called wapigania uhuru wenye grievances za miaka mingi walioona hawakutendewa na kupewa heshima ya kutosha hasa na utawala wa awamu ya kwanza.Wameandika vitabu weeee wakaona havijawaletea matunda..sasa wanakuja na program.

Ngoja tuone hii nchi itafika wapi kwa ubiinafsi wa watu wachache wenye kutumia majority innocent ignorant poor and the down trodden!

Ubinafsi na udini ulianzia kwenye waraka wa Maaskofu tusije kusahau "source" tukaanza kurukia matokeo..source ni waraka!

Watu wengi tulishauri serikali iwakemee wakristo na udini wao pamaoja na agenda ya ubinafsi na ajenda zao zingine za siri wakakataa na wakristo wakaja juu kuutetea..

Wacha kulalamika usisahau source, niliwahi kusema nchi hii kutakuwa na vyama viwili "christian party ans islamic party at the end of the day..naamini tutafika huko wananchi watachagua kwa mrengo huo good move..
 
Ubinafsi na udini ulianzia kwenye waraka wa Maaskofu tusije kusahau "source" tukaanza kurukia matokeo..source ni waraka!

Watu wengi tulishauri serikali iwakemee wakristo na udini wao pamaoja na agenda ya ubinafsi na ajenda zao zingine za siri wakakataa na wakristo wakaja juu kuutetea..

Wacha kulalamika usisahau source, niliwahi kusema nchi hii kutakuwa na vyama viwili "christian party ans islamic party at the end of the day..naamini tutafika huko wananchi watachagua kwa mrengo huo good move..

Arm-chair General mwingine!

Amandla......
 
Back
Top Bottom