Waislamu wenyeji na wageni nchini China wakaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhani

Waislamu wenyeji na wageni nchini China wakaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhani

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG111170104158.jpg


VCG111329712245.jpg


Ramadhan ni mwezi wa Baraka kwa Waislamu wote duniani. Katika kipindi chote cha mwezi mtukufu wa Ramadhan, Waislamu wanafunga na kusali ili kuomba msamaha kwa Mungu wafutiwe dhambi zao. Kawaida kila mwislamu duniani anajiandaa mapema kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Waislamu wa China nao halikadhalika wana taratibu zao mbalimbali za kuukaribisha mwezi katika kipindi hiki.

Dini ya kiislamu imekuwepo nchini China kwa takriban miaka 1,400. Ingawa kundi la waislamu sio kubwa sana wakiwa ni watu million 40 ambao ni sawa na asilimia 2.85% ya idadi yote ya Wachina, wengi wao wakiwa ni dhehebu la Sunni, lakini wana uhuru mkubwa wa kuabudu na kutekeleza sharia mbalimbali za kiislamu, ikiwemo ibada ya kufunga.

Kwa waislamu wa China na duniani kwa ujumla, kuangalia mapema saa ya kuanza kufunga na kufungua pamoja na kuangalia mwandamo wa mwezi, ni kazi muhimu sana ili kujua siku na muda wa kuanza kufunga na kuftari.

Waislamu wote wanafahamu kuwa Ramadhani ni mwezi wa kukaa chini na kutafakari, lakini sambamba na hilo pia ni wakati wa kuonesha uvumulivu na subra ya hali ya juu kabisa, kwa kujizuia kula na kunywa kwa muda wote kuanzia asubuhi hadi jioni na kuchuma thawabu kwa wingi kwa kufanya ibada mbalimbali, hivyo huu umekuwa ni mwezi wenye umuhimu mkubwa ndani ya kalenda ya Kiislamu.

Kwa Waislamu wa China, katika mwezi huu mtukufu wanasali, kuwasaidia watu masikini, kufunga, na kujizuia kutenda dhambi. Kuna desturi moja ambayo inavutia sana kwenye kipindi hiki. Tunaelewa kuwa futari ni mlo muhimu sana kwa siku kwani baada ya kutekeleza ibada ya funga kutwa nzima, unapowadia wakati wa kufungua waislamu ni lazima wale bila kujali kama wapo nyumbani ama njiani.

Ili kuhakikisha watu wanakula kwa wakati, Waislamu wanaoishi karibu na misikiti huwa wanaandaa futari na kupeleka msikitini kwa ajili ya kuwafutarisha kwa wakati wasafiri ama watu wasiojiweza. Lakini tangu kuzuka kwa janga la COVID-19, mambo mengi yameshuhudiwa yakibadilika kutokana na kuchukuliwa hatua kali za kulinda watu wasiambukizwe, na kufanya taratibu nyingi kusitishwa katika kipindi hiki cha mwezi mukufu wa Ramadhani hapa nchini China.

Moja ya mambo hayo ni kufungwa kwa misikiti. Awali baada ya hali kuwa nzuri, nyumba za ibada kama vile misikiti, mahekali na makanisa zote zilifunguliwa, lakini kutokana na kutotabirika kwa virusi na tabia yake ya kujirejearejea, imesababishwa kufungwa tena kwa nyumba za ibada tangu mwezi Disemba mwaka 2021. Kutokana na hatua hizo swala muhimu kama vile tarawehe, madarsa yanayoendeshwa nyakati za jioni yote yamefungwa.

Waislamu wenyeji pia hufurahia sana kuwakaribisha waislamu wageni wanaoishi nchini China. Makaribisho haya huwa yanafanyika kwa kuwaalika waislamu wenzao kusali pamoja na kufutari pamoja wakati jioni.

Mimi nikiwa kama muislamu ninayeishi hapa China, nimeshuhudia ukarimu mkubwa wa Waislamu wenyeji katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani. Kawaida linapokuja swala la chakula, Wachina huwa hawana hiyana na kuonyesha ukarimu wa hali ya juu. Na hii si kwa waislamu tu, bali hata Wachina ambao si waislamu wanawaalika marafiki zao waislamu na kufutari nao pamoja wakati wa jioni.

Mialiko hii huwa inafanyika katika siku za wikiendi. Tunafahamu kuwa Wachina ni wachapa kazi sana, katika siku za katikati ya wiki mara nyingi wanakuwa hawana nafasi ya kualikana kutokana na pilika za kazi. Hivyo inapofika siku za wikiendi huzitumia vizuri kualikana na kuftari pamoja na kufurahia mwezi mtukufu wa Ramadhani na familia zao.

Katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani, waislamu wenyeji na wageni wa China ni lazima kuhakikisha wananunua vyakula halali wanapokwenda sokoni. Tofauti na nilikotokea Tanzania, ambapo unapokwenda sokoni kununua chakula, hujali sana kama chakula hiki ni halali au la, hapa China ni lazima umakini huo uwepo, kwasababu kama nilivyosema awali kwamba idadi ya waislamu sio kubwa sana. Hata hivyo, kwenye masoko, vyakula vyote ambavyo ni halali vinawekwa alama ya “vyakula vya kiislamu”, na pia migahawa yote ya kiislamu inawekwa alama ya “halali” juu ya mlango.
 
Wachina na dini wapi na wapi
Hao waislam ni wahamiaji kutoka nchi zinazopakana na china km afghanistan,tajkstan, kazakhstan,pakstan nk
 
Hata hivyo, kwenye masoko, vyakula vyote ambavyo ni halali vinawekwa alama ya “vyakula vya kiislamu”, na pia migahawa yote ya kiislamu inawekwa alama ya “halali” juu ya mlango.
Hizi dini hizi..eti chakula halali
 
Wachina na dini wapi na wapi
Hao waislam ni wahamiaji kutoka nchi zinazopakana na china km afghanistan,tajkstan, kazakhstan,pakstan nk
Huyu aliweka hii post yuko China, we uko wapi mkuu?
 
Acheni ubaguzi eti chakula vya uislam, mabudha he?
 
waislam wananyanyaswa sana China,duniani mzima inalijua hilo,jimbo la magharibi ya China liitwalo Xinjiang lina Waislam wengi ,..watu hawaruhusiwi kuandika Kiarabu,misikiti inavunjwa,

Waislam wanafungwa katika kambi ili wasomeshwe wageuzwe wawe wachina wa kawaida waachane na Uislam, nk
 
waislam wananyanyaswa sana China,duniani mzima inalijua hilo,jimbo la magharibi ya China liitwalo Xinjiang lina Waislam wengi ,..watu hawaruhusiwi kuandika Kiarabu,misikiti inavunjwa,

Waislam wanafungwa katika kambi ili wasomeshwe wageuzwe wawe wachina wa kawaida waachane na Uislam, nk
Kinachoogopwa hapa ni ugaidi
 
Kinachoogopwa hapa ni ugaidi
Nafikiri wakiwaachia waishi maisha wanayoyataka kutokana na mila zao, ugaidi hautotokea

kuanza kuwazuia wasifanye wanayoyataka hapo ndio itaweza kuebua vikundi vinavyopinga yale wanayofanyiwa
 
Back
Top Bottom