Uchaguzi 2020 Waitara, Nyamhanga waigawa Tarime kwa maslahi yao binafsi kisiasa

Uchaguzi 2020 Waitara, Nyamhanga waigawa Tarime kwa maslahi yao binafsi kisiasa

nokwenumuya

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2019
Posts
820
Reaction score
2,896
WAITARA, NYAMHANGA WAIGAWA TARIME KWA MASLAHI YAO BINAFSI KISIASA
  • Ni Naibu Waziri na Katibu Mkuu Wizara ya TAMISEMI.
  • Dhamira ni kuwarahisishia mipango yao kugombea majimbo ya Tarime Mjini na Vijijini.
  • Wagawanya Kata wakipuuza mapendekezo ya Mabaraza ya Madiwani.
  • Washikilia msimamo wa kuigawa tarafa ya INCHUGU ulioasisiwa na CHADEMA.
Kama tunavyofahamu, mwaka huu 2020 tuna uchaguzi mkuu katika nchi yetu, na moja ya hatua ambazo huchukuliwa kipindi hiki ni ugawaji mpya wa kata na majimbo, na baada ya hatua hiyo, Wizara inayohusika na ugawaji huo, WIZARA YA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) huwasilisha mapendekezo hayo kwa TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI kwa ajili ya kutangaza kwa ajili ya uchaguzi mkuu pindi Bunge linapovunjwa.

Mchakato huo wa ugawaji huanzia ngazi za chini, katika Wilaya/Halmashauri husika, kisha Mkoani na baadae mapendekezo hupelekwa TAMISEMI kwa ajili ya kuyathibitisha au kushauri panapowezekana.

Wilaya ya Tarime ina majimbo mawili, Jimbo la Tarime Mjini, na Jimbo la Tarime Vijijini. Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Wilaya ya Tarime iligawanywa katika Halmashauri mbili, ambapo Tarime Mjini ilipewa kata 8, na vijijini kata 26. Baadae ikaonekana Halmashauri ya Tarime Mjini kwanza imetengewa eneo dogo, pili kuna Wananchi kufuata huduma Nyamwaga (Makao Makuu ya Tarime Vijijini) ikaonekana ni mbali sana, na tatu haina vyanzo vya mapato, hivyo ikaonekana ni busara ugawaji wa kata ufanyike upya ili kuondoa Changamoto hizo zilizojitokeza baada ya ugawaji ambao haukuwa sahihi.

Mchakato ulianza na mwaka jana 2019 Halmashauri zote za Wilaya ya Tarime zikapendekeza kuwa kata 8 ziongezeke katika Halmashauri ya Tarime Mjini, ambazo ni Komaswa, Manga, Kiyole, Bumera, Mwema, Susuni, Sirari, na Regicheli. Halmashauri hizi zote mbili zinaongozwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Mapendekezo haya ambayo hayakushirikisha wananchi wa kata husika yaliibua malalamiko toka Tarafa ya INCHUGU, kwa sababu wananchi wa Tarafa hiyo hawakutaka igawanywe, walitaka ni kheri tarafa na kata zote ziende katika jimbo moja kuliko kugawanywa huku na huku, jambo ambalo walisema kimila halikubaliki, na walilalamikia hatua hiyo ya CHADEMA kutoa mapendekezo hayo bila kuwashirikisha wananchi na hasa WAZEE wa MILA.

Malalamiko hayo waliyapeleka TAMISEMI ili yafanyiwe kazi, wakiamini kuwa mapendekezo yao yatafanyiwa kazi ukizingatia kuwa Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Injinia Joseph Nyamhanga, ni mtu wa Tarime hivyo anajua juu ya mila na ubaya wa kuigawa INCHUGU. Pili walimshirikisha Naibu Waziri, Mh. Mwita Waitara juu ya hilo. Waliamini uwepo wa hao unaweza kuwasaidia kwani wote bahati nzuri ni watu wa Tarime na hayo malalamiko wanayafahamu vizuri. Na hata wasingekuwa watu wa Tarime bado wangewaelimisha juu ya mila za kuigawanya INCHUGU.

Kinyume na matarajio ya kilio cha Wazee wa Tarafa ya INCHUGU, wawili hao wamekaa na kukubaliana kwenda kinyume kidogo na mapendekezo ya Mabaraza ya Madiwani baada ya kung’amua kuwa kama mapendekezo hayo yataachwa jinsi yalivyo yatawagonganisha wao katika uchaguzi Mkuu wa 2020, maana wote wana dhamira ya kwenda kugombea Ubunge katika majimbo hayo.

Mh. Mwita WAITARA, Naibu Waziri TAMISEMI, na INJINIA Joseph NYAMHANGA, Katibu Mkuu TAMISEMI wote walikuwa na dhamira ya kugombea Jimbo la Tarime Vijijini katika uchaguzi wa mwaka huu, 2020. Kwa kuwa wote wako TAMISEMI waliamua kwa kauli moja ni bora mmoja aende Tarime Mjini na mwingine aende Tarime Vijijini. Katika makubaliano hayo walikubaliana kuwa Mh. Waitara abaki Tarime Vijijini, na Injinia NYAMHANGA aende Tarime Mjini.

Changamoto ambayo waliiona kwa pamoja ni kuwa kata ya BINAGI, ambako ndipo anapotoka Injinia NYAMHANGA imependekezwa iendelee kubaki jimbo la Tarime Vijijini, hivyo itampa yeye changamoto kugombea mjini pasipo kuwepo na kata ambayo ndiko chimbuko la familia yake, hivyo wakaamua kuwa kwa namna yoyote lazima kata hiyo irudi jimbo la Tarime Mjini, bila kuzingatia mapendekezo wala ramani ya hiyo kata ilivyokaa.

Hivyo kinyume na taratibu za ugawaji, ambapo Katibu Mkuu huwa mtu wa mwisho katika mchakato huo, aliamua kuomba nyaraka za mapendekezo ya ugawaji wa Tarime, na kuamua kulifanyia kazi moja kwa moja bila kuwashirikisha watu wa chini yake, na akachora ramani mpya na kuiingiza kata ya Binagi katika jimbo la Tarime Mjini, ili aweze kuwa na nguvu katika kugombea jimbo hilo.

Jambo baya walilofanya ni kutoangalia maslahi ya umma wa wana INCHUGU, ambao walipendekeza tarafa hiyo isigawanywe bali iende ama Tarime Mjini yote, au Tarime Vijijini. Jambo ambalo sio tu kupuuza Wazee wa MILA wa tarafa hiyo, bali kuendeleza tabia waliyofanya madiwani wa CHADEMA wa kutoona umuhimu wa kuwashirikisha WAZEE katika mchakato wa ugawaji mpya wa mipaka ya kata na Jimbo hilo.

Baada ya kukamilisha mipango yao, wakakubaliana Mh. Waitara afanye ziara mwezi huu wa pili katika Wilaya ya Tarime, kwamba awakusanye wenyeviti wa vijiji na mitaa, atoe semina ya uongozi kama Naibu Waziri TAMISEMI ili kuwajengea uwezo katika ufanyaji wao wa kazi. Lakini ziara hiyo malengo yao ni kuendelea kuwa karibu na hao viongozi wa ngazi za chini ili kuwasaidia kufanikisha malengo yao(maana si mkakati wa nchi nzima), hivyo muda si mrefu mtamuona akienda Tarime kufanya ziara hiyo, labda abadilishe mbinu baada ya kuweka mipango yao wazi, lakini hadi sasa huo ndio mpango kazi ulio mezani kwao.

Baada ya kupata taarifa hii kwa mtu wa ndani wa Mh. Waitara, ambaye ni mkazi wa INCHUGU aishie Dar es Salaam, ambaye alijaribu kuwashauri kinyume basi nikaona bora kuiweka taarifa hii wazi huenda ikasaidia katika mchakato huo kuangaliwa upya, kwani kwa hali ilivyo hivi sasa Katibu Mkuu TAMISEMI, na Naibu Waziri tayari wamekwishazika mapendekezo ya wale Wazee wa INCHUGU ambao kimsingi wanawakilisha jamii nzima ya wakazi wa TARAFA hiyo.


Ni Mimi,
Venance Marwa
Mwana TARIME.

NOKWE AGHONGWE.
 

Attachments

WAITARA, NYAMHANGA WAIGAWA TARIME KWA MASLAHI YAO BINAFSI KISIASA
  • Ni Naibu Waziri na Katibu Mkuu Wizara ya TAMISEMI.
  • Dhamira ni kuwarahisishia mipango yao kugombea majimbo ya Tarime Mjini na Vijijini.
  • Wagawanya Kata wakipuuza mapendekezo ya Mabaraza ya Madiwani.
  • Washikilia msimamo wa kuigawa tarafa ya INCHUGU ulioasisiwa na CHADEMA.
Kama tunavyofahamu, mwaka huu 2020 tuna uchaguzi mkuu katika nchi yetu, na moja ya hatua ambazo huchukuliwa kipindi hiki ni ugawaji mpya wa kata na majimbo, na baada ya hatua hiyo, Wizara inayohusika na ugawaji huo, WIZARA YA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) huwasilisha mapendekezo hayo kwa TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI kwa ajili ya kutangaza kwa ajili ya uchaguzi mkuu pindi Bunge linapovunjwa.

Mchakato huo wa ugawaji huanzia ngazi za chini, katika Wilaya/Halmashauri husika, kisha Mkoani na baadae mapendekezo hupelekwa TAMISEMI kwa ajili ya kuyathibitisha au kushauri panapowezekana.

Wilaya ya Tarime ina majimbo mawili, Jimbo la Tarime Mjini, na Jimbo la Tarime Vijijini. Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Wilaya ya Tarime iligawanywa katika Halmashauri mbili, ambapo Tarime Mjini ilipewa kata 8, na vijijini kata 26. Baadae ikaonekana Halmashauri ya Tarime Mjini kwanza imetengewa eneo dogo, pili kuna Wananchi kufuata huduma Nyamwaga (Makao Makuu ya Tarime Vijijini) ikaonekana ni mbali sana, na tatu haina vyanzo vya mapato, hivyo ikaonekana ni busara ugawaji wa kata ufanyike upya ili kuondoa Changamoto hizo zilizojitokeza baada ya ugawaji ambao haukuwa sahihi.

Mchakato ulianza na mwaka jana 2019 Halmashauri zote za Wilaya ya Tarime zikapendekeza kuwa kata 8 ziongezeke katika Halmashauri ya Tarime Mjini, ambazo ni Komaswa, Manga, Kiyole, Bumera, Mwema, Susuni, Sirari, na Regicheli. Halmashauri hizi zote mbili zinaongozwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Mapendekezo haya ambayo hayakushirikisha wananchi wa kata husika yaliibua malalamiko toka Tarafa ya INCHUGU, kwa sababu wananchi wa Tarafa hiyo hawakutaka igawanywe, walitaka ni kheri tarafa na kata zote ziende katika jimbo moja kuliko kugawanywa huku na huku, jambo ambalo walisema kimila halikubaliki, na walilalamikia hatua hiyo ya CHADEMA kutoa mapendekezo hayo bila kuwashirikisha wananchi na hasa WAZEE wa MILA.

Malalamiko hayo waliyapeleka TAMISEMI ili yafanyiwe kazi, wakiamini kuwa mapendekezo yao yatafanyiwa kazi ukizingatia kuwa Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Injinia Joseph Nyamhanga, ni mtu wa Tarime hivyo anajua juu ya mila na ubaya wa kuigawa INCHUGU. Pili walimshirikisha Naibu Waziri, Mh. Mwita Waitara juu ya hilo. Waliamini uwepo wa hao unaweza kuwasaidia kwani wote bahati nzuri ni watu wa Tarime na hayo malalamiko wanayafahamu vizuri. Na hata wasingekuwa watu wa Tarime bado wangewaelimisha juu ya mila za kuigawanya INCHUGU.

Kinyume na matarajio ya kilio cha Wazee wa Tarafa ya INCHUGU, wawili hao wamekaa na kukubaliana kwenda kinyume kidogo na mapendekezo ya Mabaraza ya Madiwani baada ya kung’amua kuwa kama mapendekezo hayo yataachwa jinsi yalivyo yatawagonganisha wao katika uchaguzi Mkuu wa 2020, maana wote wana dhamira ya kwenda kugombea Ubunge katika majimbo hayo.

Mh. Mwita WAITARA, Naibu Waziri TAMISEMI, na INJINIA Joseph NYAMHANGA, Katibu Mkuu TAMISEMI wote walikuwa na dhamira ya kugombea Jimbo la Tarime Vijijini katika uchaguzi wa mwaka huu, 2020. Kwa kuwa wote wako TAMISEMI waliamua kwa kauli moja ni bora mmoja aende Tarime Mjini na mwingine aende Tarime Vijijini. Katika makubaliano hayo walikubaliana kuwa Mh. Waitara abaki Tarime Vijijini, na Injinia NYAMHANGA aende Tarime Mjini.

Changamoto ambayo waliiona kwa pamoja ni kuwa kata ya BINAGI, ambako ndipo anapotoka Injinia NYAMHANGA imependekezwa iendelee kubaki jimbo la Tarime Vijijini, hivyo itampa yeye changamoto kugombea mjini pasipo kuwepo na kata ambayo ndiko chimbuko la familia yake, hivyo wakaamua kuwa kwa namna yoyote lazima kata hiyo irudi jimbo la Tarime Mjini, bila kuzingatia mapendekezo wala ramani ya hiyo kata ilivyokaa.

Hivyo kinyume na taratibu za ugawaji, ambapo Katibu Mkuu huwa mtu wa mwisho katika mchakato huo, aliamua kuomba nyaraka za mapendekezo ya ugawaji wa Tarime, na kuamua kulifanyia kazi moja kwa moja bila kuwashirikisha watu wa chini yake, na akachora ramani mpya na kuiingiza kata ya Binagi katika jimbo la Tarime Mjini, ili aweze kuwa na nguvu katika kugombea jimbo hilo.

Jambo baya walilofanya ni kutoangalia maslahi ya umma wa wana INCHUGU, ambao walipendekeza tarafa hiyo isigawanywe bali iende ama Tarime Mjini yote, au Tarime Vijijini. Jambo ambalo sio tu kupuuza Wazee wa MILA wa tarafa hiyo, bali kuendeleza tabia waliyofanya madiwani wa CHADEMA wa kutoona umuhimu wa kuwashirikisha WAZEE katika mchakato wa ugawaji mpya wa mipaka ya kata na Jimbo hilo.

Baada ya kukamilisha mipango yao, wakakubaliana Mh. Waitara afanye ziara mwezi huu wa pili katika Wilaya ya Tarime, kwamba awakusanye wenyeviti wa vijiji na mitaa, atoe semina ya uongozi kama Naibu Waziri TAMISEMI ili kuwajengea uwezo katika ufanyaji wao wa kazi. Lakini ziara hiyo malengo yao ni kuendelea kuwa karibu na hao viongozi wa ngazi za chini ili kuwasaidia kufanikisha malengo yao(maana si mkakati wa nchi nzima), hivyo muda si mrefu mtamuona akienda Tarime kufanya ziara hiyo, labda abadilishe mbinu baada ya kuweka mipango yao wazi, lakini hadi sasa huo ndio mpango kazi ulio mezani kwao.

Baada ya kupata taarifa hii kwa mtu wa ndani wa Mh. Waitara, ambaye ni mkazi wa INCHUGU aishie Dar es Salaam, ambaye alijaribu kuwashauri kinyume basi nikaona bora kuiweka taarifa hii wazi huenda ikasaidia katika mchakato huo kuangaliwa upya, kwani kwa hali ilivyo hivi sasa Katibu Mkuu TAMISEMI, na Naibu Waziri tayari wamekwishazika mapendekezo ya wale Wazee wa INCHUGU ambao kimsingi wanawakilisha jamii nzima ya wakazi wa TARAFA hiyo.


Ni Mimi,
Venance Marwa
Mwana TARIME.

NOKWE AGHONGWE.
Waitara huyu huyu aliyemkimbia Makonda jimbo la ukonga?!!
 
Eti Waitara kaapa kuichukua Taaarime ya Heche maajabu, kakimbia hapa Dar na masufulia ya wali kaenda huko kuweka kambi kwani wana Tarime wanataka walii? Muda huu tunaongea kavamia jimbo kwa gari la umma.

Tunamtaka arudi Dar tumpe adabu yake, kama mwanaume kweeli mbona kakimbia town.

Wana Tarime mnajua cha kufanya huko!! Mkishindwa basi mrudisheni Dar jimboni kwake tumpe majibu ya kuisaliti wake!!
 
WAITARA, NYAMHANGA WAIGAWA TARIME KWA MASLAHI YAO BINAFSI KISIASA
  • Ni Naibu Waziri na Katibu Mkuu Wizara ya TAMISEMI.
  • Dhamira ni kuwarahisishia mipango yao kugombea majimbo ya Tarime Mjini na Vijijini.
  • Wagawanya Kata wakipuuza mapendekezo ya Mabaraza ya Madiwani.
  • Washikilia msimamo wa kuigawa tarafa ya INCHUGU ulioasisiwa na CHADEMA.
Kama tunavyofahamu, mwaka huu 2020 tuna uchaguzi mkuu katika nchi yetu, na moja ya hatua ambazo huchukuliwa kipindi hiki ni ugawaji mpya wa kata na majimbo, na baada ya hatua hiyo, Wizara inayohusika na ugawaji huo, WIZARA YA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) huwasilisha mapendekezo hayo kwa TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI kwa ajili ya kutangaza kwa ajili ya uchaguzi mkuu pindi Bunge linapovunjwa.

Mchakato huo wa ugawaji huanzia ngazi za chini, katika Wilaya/Halmashauri husika, kisha Mkoani na baadae mapendekezo hupelekwa TAMISEMI kwa ajili ya kuyathibitisha au kushauri panapowezekana.

Wilaya ya Tarime ina majimbo mawili, Jimbo la Tarime Mjini, na Jimbo la Tarime Vijijini. Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Wilaya ya Tarime iligawanywa katika Halmashauri mbili, ambapo Tarime Mjini ilipewa kata 8, na vijijini kata 26. Baadae ikaonekana Halmashauri ya Tarime Mjini kwanza imetengewa eneo dogo, pili kuna Wananchi kufuata huduma Nyamwaga (Makao Makuu ya Tarime Vijijini) ikaonekana ni mbali sana, na tatu haina vyanzo vya mapato, hivyo ikaonekana ni busara ugawaji wa kata ufanyike upya ili kuondoa Changamoto hizo zilizojitokeza baada ya ugawaji ambao haukuwa sahihi.

Mchakato ulianza na mwaka jana 2019 Halmashauri zote za Wilaya ya Tarime zikapendekeza kuwa kata 8 ziongezeke katika Halmashauri ya Tarime Mjini, ambazo ni Komaswa, Manga, Kiyole, Bumera, Mwema, Susuni, Sirari, na Regicheli. Halmashauri hizi zote mbili zinaongozwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Mapendekezo haya ambayo hayakushirikisha wananchi wa kata husika yaliibua malalamiko toka Tarafa ya INCHUGU, kwa sababu wananchi wa Tarafa hiyo hawakutaka igawanywe, walitaka ni kheri tarafa na kata zote ziende katika jimbo moja kuliko kugawanywa huku na huku, jambo ambalo walisema kimila halikubaliki, na walilalamikia hatua hiyo ya CHADEMA kutoa mapendekezo hayo bila kuwashirikisha wananchi na hasa WAZEE wa MILA.

Malalamiko hayo waliyapeleka TAMISEMI ili yafanyiwe kazi, wakiamini kuwa mapendekezo yao yatafanyiwa kazi ukizingatia kuwa Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Injinia Joseph Nyamhanga, ni mtu wa Tarime hivyo anajua juu ya mila na ubaya wa kuigawa INCHUGU. Pili walimshirikisha Naibu Waziri, Mh. Mwita Waitara juu ya hilo. Waliamini uwepo wa hao unaweza kuwasaidia kwani wote bahati nzuri ni watu wa Tarime na hayo malalamiko wanayafahamu vizuri. Na hata wasingekuwa watu wa Tarime bado wangewaelimisha juu ya mila za kuigawanya INCHUGU.

Kinyume na matarajio ya kilio cha Wazee wa Tarafa ya INCHUGU, wawili hao wamekaa na kukubaliana kwenda kinyume kidogo na mapendekezo ya Mabaraza ya Madiwani baada ya kung’amua kuwa kama mapendekezo hayo yataachwa jinsi yalivyo yatawagonganisha wao katika uchaguzi Mkuu wa 2020, maana wote wana dhamira ya kwenda kugombea Ubunge katika majimbo hayo.

Mh. Mwita WAITARA, Naibu Waziri TAMISEMI, na INJINIA Joseph NYAMHANGA, Katibu Mkuu TAMISEMI wote walikuwa na dhamira ya kugombea Jimbo la Tarime Vijijini katika uchaguzi wa mwaka huu, 2020. Kwa kuwa wote wako TAMISEMI waliamua kwa kauli moja ni bora mmoja aende Tarime Mjini na mwingine aende Tarime Vijijini. Katika makubaliano hayo walikubaliana kuwa Mh. Waitara abaki Tarime Vijijini, na Injinia NYAMHANGA aende Tarime Mjini.

Changamoto ambayo waliiona kwa pamoja ni kuwa kata ya BINAGI, ambako ndipo anapotoka Injinia NYAMHANGA imependekezwa iendelee kubaki jimbo la Tarime Vijijini, hivyo itampa yeye changamoto kugombea mjini pasipo kuwepo na kata ambayo ndiko chimbuko la familia yake, hivyo wakaamua kuwa kwa namna yoyote lazima kata hiyo irudi jimbo la Tarime Mjini, bila kuzingatia mapendekezo wala ramani ya hiyo kata ilivyokaa.

Hivyo kinyume na taratibu za ugawaji, ambapo Katibu Mkuu huwa mtu wa mwisho katika mchakato huo, aliamua kuomba nyaraka za mapendekezo ya ugawaji wa Tarime, na kuamua kulifanyia kazi moja kwa moja bila kuwashirikisha watu wa chini yake, na akachora ramani mpya na kuiingiza kata ya Binagi katika jimbo la Tarime Mjini, ili aweze kuwa na nguvu katika kugombea jimbo hilo.

Jambo baya walilofanya ni kutoangalia maslahi ya umma wa wana INCHUGU, ambao walipendekeza tarafa hiyo isigawanywe bali iende ama Tarime Mjini yote, au Tarime Vijijini. Jambo ambalo sio tu kupuuza Wazee wa MILA wa tarafa hiyo, bali kuendeleza tabia waliyofanya madiwani wa CHADEMA wa kutoona umuhimu wa kuwashirikisha WAZEE katika mchakato wa ugawaji mpya wa mipaka ya kata na Jimbo hilo.

Baada ya kukamilisha mipango yao, wakakubaliana Mh. Waitara afanye ziara mwezi huu wa pili katika Wilaya ya Tarime, kwamba awakusanye wenyeviti wa vijiji na mitaa, atoe semina ya uongozi kama Naibu Waziri TAMISEMI ili kuwajengea uwezo katika ufanyaji wao wa kazi. Lakini ziara hiyo malengo yao ni kuendelea kuwa karibu na hao viongozi wa ngazi za chini ili kuwasaidia kufanikisha malengo yao(maana si mkakati wa nchi nzima), hivyo muda si mrefu mtamuona akienda Tarime kufanya ziara hiyo, labda abadilishe mbinu baada ya kuweka mipango yao wazi, lakini hadi sasa huo ndio mpango kazi ulio mezani kwao.

Baada ya kupata taarifa hii kwa mtu wa ndani wa Mh. Waitara, ambaye ni mkazi wa INCHUGU aishie Dar es Salaam, ambaye alijaribu kuwashauri kinyume basi nikaona bora kuiweka taarifa hii wazi huenda ikasaidia katika mchakato huo kuangaliwa upya, kwani kwa hali ilivyo hivi sasa Katibu Mkuu TAMISEMI, na Naibu Waziri tayari wamekwishazika mapendekezo ya wale Wazee wa INCHUGU ambao kimsingi wanawakilisha jamii nzima ya wakazi wa TARAFA hiyo.


Ni Mimi,
Venance Marwa
Mwana TARIME.

NOKWE AGHONGWE.
TAAARIFA HII SIO SAHIHI KWA KUWA INGEBEBA HOJA BILA KUHUSISHA SIASA

MWANDISHI AMEJENGA HOJA KWA MASLAHI YAKE YA KISIASA KWANI ANGEJENGA HOJA BILA KUWEKA SIASA INGEKUWA NI JAMBO JEMA LA KUTAZAMA ILA UKIISOMA ANA HASIRA NA MHE MWITA WAITARA NA KATIBU ameanza kuwashambulia kisiasa ndipo anasema maamuzi hayakuzingatia mila mila zinahusikaje katika kugawa Kata

Why aeleze sana kuhusu Mhe Waitara na Katibu Mkuu badala ya msingi wa HOJA yake ya mila izingatiwe.

JF naomba moderator muondoe huu Uzi umeshindwa vigezo vya kuwa hoja maana unashambulia nafasi za viongozi wa wizara kisa wametoka Tarime inaonekana nongwa na pia hoja ya msingi why tarafa/kama sio kata isihamie kata nyingine.

Hoja wizara ana ziara Tarime mwanatarime aliyeandika hataki Waziri aende anataka nani aende.

Waitara aliyezunguka nchi nzima na Katibu Mkuu kuhudumia wananchi nyakati hizi akifanya safari iwe nongwa???

Mhusika amejenga hoja ziara hiyo anaenda kutoa semina anasema asifanye hivyo maana sio nchi nzima alipikuwa anatoa semina kwingine mbona hakuleta ya wazo iwe nchi nzima ila ameshindwa kuelewa Wizara hiyo yenye Naibu Waziri na Katibu Mkuu imetoa maelekezo nchi nzima semina zinafanyika wao kupita na kushiriki ni nongwa kwa mwandishi.

Mwandishi ni ana malengo yake kisiasa kwa jimbo mojawapo ndio maana ameleta hoja za kisiasa kwa jambo ambalo hakuihitaji kuweka siasa Bali kujenga hoja.

JF Huu Uzi uondolewe una mirengo ya kushambulia watu kwa maslahi yao sio taifa Tarime tunawahitaji hao viongozi pia nasi tunawahitaji tuwasikie.

Huku Tarime tunalalamika wametuacha wanatuambia majukumu ikisikika wanakuja inakuwa nongwa.

Mwandishi katudharau kuwa wakija wakiongea nasi watatufanya tuwachague tusichague wengine ina maana mwaka 2015 tulichagua kwa kuwa tuliwasikia wagombea walivyokuwa wanaongea DR JPM kuwa Rais wagombea wengine hawakuongea na sisi??

Waje wawahudumie wananchi mambo ya siasa ninyi mnaoumia mnawagombea wenu hebu vicheni hilo izungumze kata tajwa bila kuhusisa siasa na ziara
 
Wana Tarime huyo Msaliti Waitara msimchague kabisa katelekeza Jimbo huku Ukonga,ipo siku atawatelekeza na nyie huko.
Hafai kuwa Kiongozi ni mtu mwenye tamaa sana.
TEAM HECHE FICHA MAHABA YAKO KWA HECHE HATUDANGANYIKI HIVYO
 
Mleta maada kwenye hii taarifa yako Kuna Mambo umeyaandika ukihisi una hoja nzito ila logically sio
Unaposema inchugu usigawanyike kisa misingi ya kimila ya wazee hakuna logic yyt Apo labda tu nikukumbushe

1. kata hiyo ya binagi tarafa ya inchage (magoma,Nyasaricho na nyamwigura) unayoiongelea wewe ndiko Mimi ninakotoka na ilishawahi kugawawanywa ambapo ilipatikana kata ya kitale tarafa ile ile ya inchage (Mogabiri na Nkongore) Sasa Kama iliwezekana ktk tarafa ya inchage wilaya hiyo hiyo ya tarime Mila zile zile zetu za kikurya kwa Nini isiwezekane ktk tarafa ya Inchugu kisa tu kisingizio Cha Mila kwangu mm sioni Kama umejenga hoja yyt Apo zaidi ya majungu kwa uliowalenga.???
2.mimi ninavyoijua geography ya tarafa ya Inchugu na Koo mzima ya inayoishi hiyo tarafa sizani Kama kuwa majimbo mawili ni kikwazo kwani pia koo iliyopo Inchugu ipo pia Kenya na wakati wa Mila huwa inajumuisha mpaka Kenya Sasa Kama inawezekana adi nje ya mipaka ya nchi mtashindwa kushirikiana kisa tu Koo ipo wilaya/majimbo mawili tofauti???

Mm nakushaur ujenge hoja kwenye suala la vitega uchumi,huduma za kijamii,nk na sio suala la Mila kwani Hilo huwa halina mipaka huwa tunajuana tu ata Kama mipaka ipo
 
Sawa John Heche,umesikika vyema
WAITARA, NYAMHANGA WAIGAWA TARIME KWA MASLAHI YAO BINAFSI KISIASA
  • Ni Naibu Waziri na Katibu Mkuu Wizara ya TAMISEMI.
  • Dhamira ni kuwarahisishia mipango yao kugombea majimbo ya Tarime Mjini na Vijijini.
  • Wagawanya Kata wakipuuza mapendekezo ya Mabaraza ya Madiwani.
  • Washikilia msimamo wa kuigawa tarafa ya INCHUGU ulioasisiwa na CHADEMA.
Kama tunavyofahamu, mwaka huu 2020 tuna uchaguzi mkuu katika nchi yetu, na moja ya hatua ambazo huchukuliwa kipindi hiki ni ugawaji mpya wa kata na majimbo, na baada ya hatua hiyo, Wizara inayohusika na ugawaji huo, WIZARA YA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) huwasilisha mapendekezo hayo kwa TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI kwa ajili ya kutangaza kwa ajili ya uchaguzi mkuu pindi Bunge linapovunjwa.

Mchakato huo wa ugawaji huanzia ngazi za chini, katika Wilaya/Halmashauri husika, kisha Mkoani na baadae mapendekezo hupelekwa TAMISEMI kwa ajili ya kuyathibitisha au kushauri panapowezekana.

Wilaya ya Tarime ina majimbo mawili, Jimbo la Tarime Mjini, na Jimbo la Tarime Vijijini. Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Wilaya ya Tarime iligawanywa katika Halmashauri mbili, ambapo Tarime Mjini ilipewa kata 8, na vijijini kata 26. Baadae ikaonekana Halmashauri ya Tarime Mjini kwanza imetengewa eneo dogo, pili kuna Wananchi kufuata huduma Nyamwaga (Makao Makuu ya Tarime Vijijini) ikaonekana ni mbali sana, na tatu haina vyanzo vya mapato, hivyo ikaonekana ni busara ugawaji wa kata ufanyike upya ili kuondoa Changamoto hizo zilizojitokeza baada ya ugawaji ambao haukuwa sahihi.

Mchakato ulianza na mwaka jana 2019 Halmashauri zote za Wilaya ya Tarime zikapendekeza kuwa kata 8 ziongezeke katika Halmashauri ya Tarime Mjini, ambazo ni Komaswa, Manga, Kiyole, Bumera, Mwema, Susuni, Sirari, na Regicheli. Halmashauri hizi zote mbili zinaongozwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Mapendekezo haya ambayo hayakushirikisha wananchi wa kata husika yaliibua malalamiko toka Tarafa ya INCHUGU, kwa sababu wananchi wa Tarafa hiyo hawakutaka igawanywe, walitaka ni kheri tarafa na kata zote ziende katika jimbo moja kuliko kugawanywa huku na huku, jambo ambalo walisema kimila halikubaliki, na walilalamikia hatua hiyo ya CHADEMA kutoa mapendekezo hayo bila kuwashirikisha wananchi na hasa WAZEE wa MILA.

Malalamiko hayo waliyapeleka TAMISEMI ili yafanyiwe kazi, wakiamini kuwa mapendekezo yao yatafanyiwa kazi ukizingatia kuwa Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Injinia Joseph Nyamhanga, ni mtu wa Tarime hivyo anajua juu ya mila na ubaya wa kuigawa INCHUGU. Pili walimshirikisha Naibu Waziri, Mh. Mwita Waitara juu ya hilo. Waliamini uwepo wa hao unaweza kuwasaidia kwani wote bahati nzuri ni watu wa Tarime na hayo malalamiko wanayafahamu vizuri. Na hata wasingekuwa watu wa Tarime bado wangewaelimisha juu ya mila za kuigawanya INCHUGU.

Kinyume na matarajio ya kilio cha Wazee wa Tarafa ya INCHUGU, wawili hao wamekaa na kukubaliana kwenda kinyume kidogo na mapendekezo ya Mabaraza ya Madiwani baada ya kung’amua kuwa kama mapendekezo hayo yataachwa jinsi yalivyo yatawagonganisha wao katika uchaguzi Mkuu wa 2020, maana wote wana dhamira ya kwenda kugombea Ubunge katika majimbo hayo.

Mh. Mwita WAITARA, Naibu Waziri TAMISEMI, na INJINIA Joseph NYAMHANGA, Katibu Mkuu TAMISEMI wote walikuwa na dhamira ya kugombea Jimbo la Tarime Vijijini katika uchaguzi wa mwaka huu, 2020. Kwa kuwa wote wako TAMISEMI waliamua kwa kauli moja ni bora mmoja aende Tarime Mjini na mwingine aende Tarime Vijijini. Katika makubaliano hayo walikubaliana kuwa Mh. Waitara abaki Tarime Vijijini, na Injinia NYAMHANGA aende Tarime Mjini.

Changamoto ambayo waliiona kwa pamoja ni kuwa kata ya BINAGI, ambako ndipo anapotoka Injinia NYAMHANGA imependekezwa iendelee kubaki jimbo la Tarime Vijijini, hivyo itampa yeye changamoto kugombea mjini pasipo kuwepo na kata ambayo ndiko chimbuko la familia yake, hivyo wakaamua kuwa kwa namna yoyote lazima kata hiyo irudi jimbo la Tarime Mjini, bila kuzingatia mapendekezo wala ramani ya hiyo kata ilivyokaa.

Hivyo kinyume na taratibu za ugawaji, ambapo Katibu Mkuu huwa mtu wa mwisho katika mchakato huo, aliamua kuomba nyaraka za mapendekezo ya ugawaji wa Tarime, na kuamua kulifanyia kazi moja kwa moja bila kuwashirikisha watu wa chini yake, na akachora ramani mpya na kuiingiza kata ya Binagi katika jimbo la Tarime Mjini, ili aweze kuwa na nguvu katika kugombea jimbo hilo.

Jambo baya walilofanya ni kutoangalia maslahi ya umma wa wana INCHUGU, ambao walipendekeza tarafa hiyo isigawanywe bali iende ama Tarime Mjini yote, au Tarime Vijijini. Jambo ambalo sio tu kupuuza Wazee wa MILA wa tarafa hiyo, bali kuendeleza tabia waliyofanya madiwani wa CHADEMA wa kutoona umuhimu wa kuwashirikisha WAZEE katika mchakato wa ugawaji mpya wa mipaka ya kata na Jimbo hilo.

Baada ya kukamilisha mipango yao, wakakubaliana Mh. Waitara afanye ziara mwezi huu wa pili katika Wilaya ya Tarime, kwamba awakusanye wenyeviti wa vijiji na mitaa, atoe semina ya uongozi kama Naibu Waziri TAMISEMI ili kuwajengea uwezo katika ufanyaji wao wa kazi. Lakini ziara hiyo malengo yao ni kuendelea kuwa karibu na hao viongozi wa ngazi za chini ili kuwasaidia kufanikisha malengo yao(maana si mkakati wa nchi nzima), hivyo muda si mrefu mtamuona akienda Tarime kufanya ziara hiyo, labda abadilishe mbinu baada ya kuweka mipango yao wazi, lakini hadi sasa huo ndio mpango kazi ulio mezani kwao.

Baada ya kupata taarifa hii kwa mtu wa ndani wa Mh. Waitara, ambaye ni mkazi wa INCHUGU aishie Dar es Salaam, ambaye alijaribu kuwashauri kinyume basi nikaona bora kuiweka taarifa hii wazi huenda ikasaidia katika mchakato huo kuangaliwa upya, kwani kwa hali ilivyo hivi sasa Katibu Mkuu TAMISEMI, na Naibu Waziri tayari wamekwishazika mapendekezo ya wale Wazee wa INCHUGU ambao kimsingi wanawakilisha jamii nzima ya wakazi wa TARAFA hiyo.


Ni Mimi,
Venance Marwa
Mwana TARIME.

NOKWE AGHONGWE.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wana Tarime huyo Msaliti Waitara msimchague kabisa katelekeza Jimbo huku Ukonga,ipo siku atawatelekeza na nyie huko.
Hafai kuwa Kiongozi ni mtu mwenye tamaa sana.
Wana tarime washasema kwani kuna mzigo gani wake aliousahau tarime.
Pili mkakati wa ccm wahamiaji haramu mwisho wao ni chalinze hawaingii dar
 
Eti Waitara kaapa kuichukua Taaarime ya Heche maajabu, kakimbia hapa Dar na masufulia ya wali kaenda huko kuweka kambi kwani wana Tarime wanataka walii? Muda huu tunaongea kavamia jimbo kwa gari la umma.

Tunamtaka arudi Dar tumpe adabu yake, kama mwanaume kweeli mbona kakimbia town.

Wana Tarime mnajua cha kufanya huko!! Mkishindwa basi mrudisheni Dar jimboni kwake tumpe majibu ya kuisaliti wake!!
Tarime sio ukonga inayochagua wasaliti kuwe hata jiwe likigombea haliwezivunja nazi
 
TAAARIFA HII SIO SAHIHI KWA KUWA INGEBEBA HOJA BILA KUHUSISHA SIASA

MWANDISHI AMEJENGA HOJA KWA MASLAHI YAKE YA KISIASA KWANI ANGEJENGA HOJA BILA KUWEKA SIASA INGEKUWA NI JAMBO JEMA LA KUTAZAMA ILA UKIISOMA ANA HASIRA NA MHE MWITA WAITARA NA KATIBU ameanza kuwashambulia kisiasa ndipo anasema maamuzi hayakuzingatia mila mila zinahusikaje katika kugawa Kata

Why aeleze sana kuhusu Mhe Waitara na Katibu Mkuu badala ya msingi wa HOJA yake ya mila izingatiwe.

JF naomba moderator muondoe huu Uzi umeshindwa vigezo vya kuwa hoja maana unashambulia nafasi za viongozi wa wizara kisa wametoka Tarime inaonekana nongwa na pia hoja ya msingi why tarafa/kama sio kata isihamie kata nyingine.

Hoja wizara ana ziara Tarime mwanatarime aliyeandika hataki Waziri aende anataka nani aende.

Waitara aliyezunguka nchi nzima na Katibu Mkuu kuhudumia wananchi nyakati hizi akifanya safari iwe nongwa???

Mhusika amejenga hoja ziara hiyo anaenda kutoa semina anasema asifanye hivyo maana sio nchi nzima alipikuwa anatoa semina kwingine mbona hakuleta ya wazo iwe nchi nzima ila ameshindwa kuelewa Wizara hiyo yenye Naibu Waziri na Katibu Mkuu imetoa maelekezo nchi nzima semina zinafanyika wao kupita na kushiriki ni nongwa kwa mwandishi.

Mwandishi ni ana malengo yake kisiasa kwa jimbo mojawapo ndio maana ameleta hoja za kisiasa kwa jambo ambalo hakuihitaji kuweka siasa Bali kujenga hoja.

JF Huu Uzi uondolewe una mirengo ya kushambulia watu kwa maslahi yao sio taifa Tarime tunawahitaji hao viongozi pia nasi tunawahitaji tuwasikie.

Huku Tarime tunalalamika wametuacha wanatuambia majukumu ikisikika wanakuja inakuwa nongwa.

Mwandishi katudharau kuwa wakija wakiongea nasi watatufanya tuwachague tusichague wengine ina maana mwaka 2015 tulichagua kwa kuwa tuliwasikia wagombea walivyokuwa wanaongea DR JPM kuwa Rais wagombea wengine hawakuongea na sisi??

Waje wawahudumie wananchi mambo ya siasa ninyi mnaoumia mnawagombea wenu hebu vicheni hilo izungumze kata tajwa bila kuhusisa siasa na ziara
Kuwa mpole mheshimiwa Subiri ikuingie wewe...[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mleta maada kwenye hii taarifa yako Kuna Mambo umeyaandika ukihisi una hoja nzito ila logically sio
Unaposema inchugu usigawanyike kisa misingi ya kimila ya wazee hakuna logic yyt Apo labda tu nikukumbushe

1. kata hiyo ya binagi tarafa ya inchage (magoma,Nyasaricho na nyamwigura) unayoiongelea wewe ndiko Mimi ninakotoka na ilishawahi kugawawanywa ambapo ilipatikana kata ya kitale tarafa ile ile ya inchage (Mogabiri na Nkongore) Sasa Kama iliwezekana ktk tarafa ya inchage wilaya hiyo hiyo ya tarime Mila zile zile zetu za kikurya kwa Nini isiwezekane ktk tarafa ya Inchugu kisa tu kisingizio Cha Mila kwangu mm sioni Kama umejenga hoja yyt Apo zaidi ya majungu kwa uliowalenga.???
2.mimi ninavyoijua geography ya tarafa ya Inchugu na Koo mzima ya inayoishi hiyo tarafa sizani Kama kuwa majimbo mawili ni kikwazo kwani pia koo iliyopo Inchugu ipo pia Kenya na wakati wa Mila huwa inajumuisha mpaka Kenya Sasa Kama inawezekana adi nje ya mipaka ya nchi mtashindwa kushirikiana kisa tu Koo ipo wilaya/majimbo mawili tofauti???

Mm nakushaur ujenge hoja kwenye suala la vitega uchumi,huduma za kijamii,nk na sio suala la Mila kwani Hilo huwa halina mipaka huwa tunajuana tu ata Kama mipaka ipo
Weito nami hapo nakusapoti.[emoji106][emoji106]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
huyo mlevi waitara hata CCM wenyewe hawampitishi kwenye kura za maoni ajiandae kwenda kushika chaki.
 
Back
Top Bottom