Wajama biashara gani inayolipa?

Gastone.W.Makishe

New Member
Joined
Jul 2, 2013
Posts
3
Reaction score
0
Wana JF mimi ni mwanafunzi natarajia kuhitimu elimu yangu ya sekondari mwaka huu.Ninaomba ushauri wenu wa kufanya biashara gani kipindi nikiwa nyumbani kuliko kukaa tu bila lolote....ninakamtaji kama 150,000 hivi fremu ipo ni yetu lakini ikija kwenye kuchagua aina ya biashara ni mtihani mkubwa...Sasa wanaJF nipeni idea nifanye biashara gani.(SIO VIBAYA KILA MTU AKATAJA BIASHARA ALAFU NIKACHAGUA)AhSnTeNi
 
150K? you need a really smart head, seriously!
 
Kama home kuna friji fanya biashara ya Fruit Salad na juice. Nunua matunda, kata vipande vdogovidogo kwa mchanganyiko mbalimbali, uza ktk sahani. Pia kamua juice freshi na uuze. Kama upo sehemu penye watu wengi, naamini itakulipa.
 
Cheki kitaa, Huwezi anzisha biashara ya Kukaanga Chips au Mihogo?
Pia unaweza kupika Maandazi, Vitumbua, Keki, Half cake. Ukawa unauza kitaa na ukiweza Kuongea na Maduka ya Jirani ukawa unapeleka na kusupply hivi vitu, cheki na wenye migahawa pia hasa wauza Juice na Maziwa.
Bila Kusahahau Cribs za Mihogo, Ndizi, Viazi pia unaweZa kupeleka madukani.
Pia unaweza kuuza Matunda Ndizi, Machungwa na mengineo.

Ila kumbuka tunaenda kwenye mfungo kwa sasa na kitu kinacholipa ni mihogo, Viazi, Matikiti, Tambi na vyakula vingine.

All in all Hiyo frem achana nayo kama vipi ipangishe upate kodi uongeze kwenye Mtaji.
 
unapatikana wapi? kwa mtaji wako huo mdogo unaweza kuanzisha biashara nyingi tu ndogondogo,
ningefahamu unapatikana mtaa/kijiji gani ningekushauri accordingly na mazingira uliyopo funguka vizuri upewe ushauri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…