WAJIBU WA VIJANA WA TANZANIA

WAJIBU WA VIJANA WA TANZANIA

DolphinT

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2016
Posts
2,014
Reaction score
2,979
Kwanini vijana wa Tanzania hawajadili mambo muhimu? Ni swali linalopaswa kutafakariwa kwa kina hasa tunaposhuhudia kundi kubwa la vijana likitumia muda na rasilimali zao kuwasifia viongozi pasipo kutathmini kwa kina viashiria vya moja kwa moja vya utendaji wao wa kazi unaolenga kuboresha maisha ya wananchi kisiasa, kiuchumi, na kijamii. Vijana hawa wamejikita zaidi katika kuwania nafasi za uongozi kupitia sifa za kijinga, kama vile kuwa wapambe na wafuasi wa kusifia kila jambo, hali ambayo haileti mchango wowote wa maana katika maendeleo ya taifa. Ni muhimu kuelewa kwamba kumsifia kiongozi haikatazwi, lakini sifa zinazozidi kiasi zinaharibu dhana ya uwajibikaji na kuondoa uwajibikaji wa kweli unaotakiwa kutoka kwa viongozi. Badala yake, vijana wanapaswa kujadili na kuhoji masuala ya msingi yanayoathiri maisha yao moja kwa moja, kama vile upatikanaji wa nishati kwa gharama nafuu ili kuwasaidia katika shughuli za uzalishaji na ujasiriamali, sera za kumiliki ardhi kwa haki, na fursa bora za mikopo ambazo zinaweza kupanua wigo wa uchumi wa vijana na taifa kwa ujumla.

Vijana wa leo wanapaswa kuwa sauti ya mabadiliko kwa kuibua mijadala muhimu kuhusu elimu bora na elimu ya ufundi, ili kuhakikisha wahitimu wanakuwa na ujuzi wa kujitegemea katika soko la ajira ambalo linakabiliwa na changamoto kubwa. Vilevile, ni jukumu lao kuwashinikiza viongozi kuonyesha namna wanavyoshughulikia athari za mabadiliko ya tabianchi na kujenga uchumi endelevu unaoendana na changamoto hizo. Aidha, vijana wasio na ajira rasmi na wale waliopo vyuoni wanapaswa kuishinikiza serikali kuboresha huduma za afya zinazoweza kumudu gharama, huku wakitilia mkazo umuhimu wa bima ya afya kwa wote kama njia ya kuhakikisha maisha na afya za watu zinahifadhiwa. Badala ya kutegemea nafasi chache za uteuzi, vijana wanapaswa kuwa wakosoaji wa kujenga, wanaohoji na kuhimiza uwajibikaji, badala ya kuishia kuwa mashabiki wa kawaida wa viongozi wa sasa. Taifa linahitaji kizazi cha vijana wenye ujasiri wa kuhoji na kusimamia maslahi ya jamii, si kizazi la vijana waliolemaa kwa sifa zisizo na tija na kutegemea uteuzi pekee kama njia ya kufanikisha ndoto zao.
 
Vijana waki Tanzania tuliletwa duniani tukiwa na lengo moja tu kichwani mwetu. Kushabikia Simba na Yanga

Maendeleo hayatuhusu kabisa tushawaaachia serikali na viongozi ishu za maendeleo.
Hatuko kama vijana wa nchi nyingine
Ukitaka tuingie #Road zuia simba na Yanga
 
Moja ya mada nzuri sana kwa siku ya leo...!!

Hakika hiki kizazi chetu Cha vijana kinatia kinyaa sana kwa tunayoyashuudia hapa nchini hasa kwa awamu hii...

Vijana wamejivika upofu, hawajali kabisa future ya taifa hili, wamekuwa ni watu wa kutetea maovu na ushenzy unaofanywa na mafisadi.

Vijana wameacha taaluma zao na kuamua kuwa wapambe wa wahujumu uchumi na wabadhirifu wa pesa za umma wa nchi hii, maana wamegundua hiyo ndio njia Rahisi ya kuwafanya wao waishi hapa mjini.

Kuna mambo mengi sana ya msingi ya kuhoji yanayotokea kwenye jamii yetu, lakini hawana muda nayo, wako bize na kuwalamba makalio wanasiasa... Mfano mwepesi tu mfululizo wa matukio ya utekaji yaliyotokea hivi karibuni ambayo waathirika karibu wote ni vijana.

-ilipaswa mpaka kufikia leo hii wale waliotaka kumteka Tarimo Bonge kule kibamba wawe wameshakamatwa baada ya kuishinikiza serikali kwa nguvu

-Ilipaswa mpaka Sasa hivi yule mmiliki wa lile jengo la kariakoo na mamlaka ziliompa kibali Cha kufanya ule ujinga wote wawe wameshachukuliwa hatua, maana kimemgharimu maisha ya watu wengi sana na Tena vijana.

-Ilipaswa mpaka Sasa hivi muafaka wa suala la ajira hasa zile ambazo serikali imezitangaza kwa muda mrefu ndani ya mwaka huu uwe umeshapatikana(Kuna ajira serikali imezitangaza tangu mwezi wa kwanza lakini mpaka leo hii watu hawajaitwa hata kwenye interviews).

Kuna mambo meeengi sana ambayo vijana wa taifa hili walipaswa kuihoji serikali itoe majibu, lakini badala yake ndio kwanza vijana tuko bize kuisifu na kuipa siafa za uongo..
 
Kwanini vijana wa Tanzania hawajadili mambo muhimu? Ni swali linalopaswa kutafakariwa kwa kina hasa tunaposhuhudia kundi kubwa la vijana likitumia muda na rasilimali zao kuwasifia viongozi pasipo kutathmini kwa kina viashiria vya moja kwa moja vya utendaji wao wa kazi unaolenga kuboresha maisha ya wananchi kisiasa, kiuchumi, na kijamii. Vijana hawa wamejikita zaidi katika kuwania nafasi za uongozi kupitia sifa za kijinga, kama vile kuwa wapambe na wafuasi wa kusifia kila jambo, hali ambayo haileti mchango wowote wa maana katika maendeleo ya taifa. Ni muhimu kuelewa kwamba kumsifia kiongozi haikatazwi, lakini sifa zinazozidi kiasi zinaharibu dhana ya uwajibikaji na kuondoa uwajibikaji wa kweli unaotakiwa kutoka kwa viongozi. Badala yake, vijana wanapaswa kujadili na kuhoji masuala ya msingi yanayoathiri maisha yao moja kwa moja, kama vile upatikanaji wa nishati kwa gharama nafuu ili kuwasaidia katika shughuli za uzalishaji na ujasiriamali, sera za kumiliki ardhi kwa haki, na fursa bora za mikopo ambazo zinaweza kupanua wigo wa uchumi wa vijana na taifa kwa ujumla.

Vijana wa leo wanapaswa kuwa sauti ya mabadiliko kwa kuibua mijadala muhimu kuhusu elimu bora na elimu ya ufundi, ili kuhakikisha wahitimu wanakuwa na ujuzi wa kujitegemea katika soko la ajira ambalo linakabiliwa na changamoto kubwa. Vilevile, ni jukumu lao kuwashinikiza viongozi kuonyesha namna wanavyoshughulikia athari za mabadiliko ya tabianchi na kujenga uchumi endelevu unaoendana na changamoto hizo. Aidha, vijana wasio na ajira rasmi na wale waliopo vyuoni wanapaswa kuishinikiza serikali kuboresha huduma za afya zinazoweza kumudu gharama, huku wakitilia mkazo umuhimu wa bima ya afya kwa wote kama njia ya kuhakikisha maisha na afya za watu zinahifadhiwa. Badala ya kutegemea nafasi chache za uteuzi, vijana wanapaswa kuwa wakosoaji wa kujenga, wanaohoji na kuhimiza uwajibikaji, badala ya kuishia kuwa mashabiki wa kawaida wa viongozi wa sasa. Taifa linahitaji kizazi cha vijana wenye ujasiri wa kuhoji na kusimamia maslahi ya jamii, si kizazi la vijana waliolemaa kwa sifa zisizo na tija na kutegemea uteuzi pekee kama njia ya kufanikisha ndoto zao.
Kwa mwandiko huo afu unataka vijana wajadili?? Nini 😁poor keyboard writing
 
kwa mfano leo Yanga amefungwa hapa kijiweni pamewaka tupo live mpaka usiku
 
Vijana waki Tanzania tuliletwa duniani tukiwa na lengo moja tu kichwani mwetu. Kushabikia Simba na Yanga

Maendeleo hayatuhusu kabisa tushawaaachia serikali na viongozi ishu za maendeleo.
Hatuko kama vijana wa nchi nyingine
Ukitaka tuingie #Road zuia simba na Yanga
View attachment 3162217

Hizo team za simba na yanga zinatakiwa ziwe zinafungwa mara kwa mara ili kuwafanya watu waache kushabikia ujinga.
 
Kwa mwandiko huo afu unataka vijana wajadili?? Nini 😁poor keyboard writing
Would you please consider the content and themes portrayed rather than the keyboard typos? Why adonihem fallacy marrying you?
 
Vijana kukata mauno tu
Kubishana mipira kufatilia udaku umbea kusikia miziki na sahv waneletewa visungura

Iva
 
Back
Top Bottom