Wajua, kuna 2 Types of Leaders. Born Leaders na Manmade Leaders? Je, Wajua tutamfaidi zaidi Rais Samia kipindi cha 2025-2030 kuliko sasa If Only?

Wajua, kuna 2 Types of Leaders. Born Leaders na Manmade Leaders? Je, Wajua tutamfaidi zaidi Rais Samia kipindi cha 2025-2030 kuliko sasa If Only?

Wanabodi,
Kila nipatapo fursa, huja na makala za Kwa Maslahi ya Taifa, leo makala yangu ni makala ya dhana dhanifu, kuhusu Tanzania ya 2025 -2030.

Makala ya leo kwanza inafundisha kujua types mbili za leaders, kuna born leaders, na made leaders, na kwenye made leaders kuna manmade leaders na selfmade leaders. Na ndani ya makundi hayo makubwa mawili pia kuna sub groups za leaders ambao ni leaders leaders na leaders ambao ni technocrats leaders.

Kwa vile kwa sasa rais wetu ni Rais Samia, hivyo nashauri tuanze na Samia Ili kupata Viongozi Bora baadae, Watanzania tujifunze kuwasoma watu kwa asili zao. Mjue Samia alivyo kwa asili yake

Je wajua kuwa licha ya Tanzania na Watanzania kumfaidi Rais Samia kwa makubwa anayoyafanya sasa, japo Rais Samia ni born leader yaani God made leader lakini ameupata uongozi kwa manmade kwa kushikwa mkono na watu, kwa jina lake kupendekezwa na watu, kuwa VP, na ndipo hatimaye kuupata urais wa JMT kwa kudra tuu za Mwenyeezi Mungu, hivyo kama sasa tuu hivi alivyo ni rais kwa kudra tuu, amefanya makubwa haya anayoyafanya na anaendelea kuyafanya mambo makubwa mazuri ya kupendeza ya neema na mafanikio, can you imagine 2025 - 2030 tutakapokuwa tumempa rasmi, kwa kumchagua kupitia sanduku la kura, itakuwaje?.

Sii wengi wanajua kuwa japo sasa tutamfaidi sana Rais Samia, lakini tutamfaidi zaidi na zaidi iwapo Rais Samia ataendelea na urais wa 2025 - 2030, kuliko sasa?. Ni kwanini,
Andamama nami!.

Naomba kabla ya kusoma bandiko hili, umezuka mtindo mtu yoyote akimpongeza kiongozi yoyote, ananyooshewa vidole vya uchawa!. Hili sio bandiko la uchawa wala mimi sio chawa wa Mama wala chawa wa mtu yoyote na hili nimelisema wazi Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza!

Naomba kukiri nimekuwa inspired kupandisha bandiko hili kutokana na hoja ya mwana JF huyu

Mkuu MTAZAMO , kwanza niendelee kukupongeza wewe ni miongoni mwa wana JF very objective.

Kuna viongozi wanasiasa wa aina mbili, born leaders na made leaders na sub groups mbili.
1. Born leaders who are responsible to the people!.
2. Made leaders who are (a)manmade leaders who are responsible to those who made them!.
(b) Self Made Leaders who are not politician leaders but technocrats, who are responsible only to themselves!.

1. Born leaders, ni viongozi wanaozaliwa na karama ya uongozi, ambao ni leaders responsible to the people, hawa ni wale viongozi wanasiasa waliozaliwa na kipaji cha uongozi kwa wito wa utumishi wa watu, hawa ni selfless leaders ambao kwao ni taifa kwanza, na wameutafuta uongozi kwa juhudi zao wenyewe binafsi kihalali bila kubwebwa na mtu au kutumia rushwa au ukwasi wao kununua uongozi, hivyo wanawajibika kwa watu, na hawawajibiki kulipa hisani kwa yeyote!. Hawa ni viongozi kama Nyerere, Karume Snr, Jumbe, Kawawa, Mkapa na wengine, they are born leaders, wameutafuta uongozi kwa juhudi zao binafsi bila kubwebwa na yeyote au kutumia rushwa, hivyo they were indebted to no one!, na wanaongoza kwa mifano.

Naomba kuliruka kundi la pili la
born leaders ambao pia ni Made leaders na kurukia kundi la Self Made Leaders who are technocrats, are responsible only to themselves!, kwenye kundi hili ndio kuna Magufuli, huyo ni self made leader ambaye alikuwa a technocrat ndio maana aliongoza kwa mtindo wa nyapara style ya mkono wa chuma na hakuwa indebted kulipa fadhila kwa yeyote ndio maana alitawala as if he own this country ni mali yake na anaweza kufanya lolote na chochote na hakuna wa kumuuliza.

Sasa nirudi kwa kundi la pili la
2. Made leaders , kwenye kundi hili pia kuna born leaders ambao wameminywa na kunyimwa fursa, hivyo mpaka watokee watu wawashike mkono, wawanyanyue na kuinuka, who are leaders who are responsible not only to people, but also to those who made them!. Kundi hili lina Mwinyi Snr, Karume Jnr, JK, Mwinyi Jnr na Samia. Unaweza kuangalia Samia aliishaonyesha uwezo siku nyingi sana angalia toka lini tumemtaja New Cabinet: Baadhi ya Majina ni Haya Hapa!

Na wakati tukiangazia sifa za Mwanamke kuweza kuwa rais wa Tanzania, jina la Samia Suluhu Hassan liliibuka kinara Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material?

Japo they are born leaders, but they had to be made leaders hivyo they are not only responsible for the people, but indebted to those who made them, who they are hivyo kuwa ni watu wa shukrani!, hivyo wale mnaopiga kelele mara muondoe huyu, mara muondoe yule!, mtapiga sana kelele za mlango, ama kama kelele za chura kisimani!.

Japo ni kweli baada ya Rais Samia kuupata urais kwa kudra tuu za Mwnyeenzi Mungu, Rais Samia angependa kuona Watanzania wakichagua rais Mwanamke na yeye ana nia ya dhati ya kuwania urais 2025 ila ana changamoto Kuu mbili.

Changamoto ya kwanza ni jee ni yeye aliyepangiwa na YEYE kwa 2025?. Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!

Changamoto ya pili ni HII sauti !.

Awamu hii ya kwanza ndio awamu pekee ya kudra, hisani na fadhila, Watanzania tukimchagua Rais Samia kwa awamu ya pili, hii sasa itakuwa ni awamu yake ya self made leader, besides being a born leader, atakuwa hawajibiki kulipa fadhila kwa yeyote na hapo sasa ndio Tanzania na Watanzania tutamfaidi vizuri zaidi the real Samia I know, ambaye ni Samia huyu niliyemzungumza hapa! Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth!”

Ila sasa kufuatia possibility ya ile changamoto ya pili kuja kuwa kweli, naendelea kumsisitiza Rais Samia, kama anaweza kuacha alama ya katiba kabla ya 2025, atakuwa amefanya jambo jema ili hiyo 2025, hata asipo, atakuwa ameacha alana!.

Otherwise lets put our fingers crossed and pray for her ili 2025 awe Samia, Tanzania na Watanzania tumfaidi Rais Samia kikamilifu!

Mungu Mbariki Rais Samia aendelee 2025,
Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali
Rejea za Mwandishi kuhusu uwezo wa wanawake kwenye uongozi
Mkuu Pascal, ili kulinda heshima na taaluma yako hachana kabisa kutuletea makala za aina hii. Moja ya sifa ya mwandishi wa habari, ni kuhabarisha umma matukio kwa usahihi. Na pale anapotoa maoni binafsi basi hayo maoni yanapaswa kuaksi ukweli wa jambo lenyewe.

Uchaguzi mkuu uliopelekea Samia kuwa Rais wa nchi baada ya JPM kufariki ulikuwa ni batili. Ni uhani uliofanyika kwa kupoka matakwa ya umma wa Tanzania na kujitangazia ushindi batili na baadae kuunda serikali. Urais wa Samia ni zao la kihalifu. Hii inathibitishwa mbali na jinsi tulivyo ona kipindi cha uchaguzi pia matamko ya viongozi waandamizi ndani ya chama na serikali yanathibitisha hili. Mfano, Kinana na Makamba wameliweka wazi hili la uchaguzi wa 2020 siku chache zilizopita, ukiachia mbali matamko ya Rais Samia mwenyewe hasa kipindi anatangaza zile 4Rs zake.

Haramu siku zote haiwezi kuhalalishwa na jambo lolote lile. CCM chama nilichokipenda kwasasa kimegeuka kuwa genge la Viongozi mafisadi, wezi wa mapato na rasilimali za nchi. Wanalindana ktk wizi. Kimekuwa chama cha kurithishana madaraka kwa watoto na ndugu zao kidogo na kwa chawa wanaojikomba. Sifa ya kuwa kiongozi sasa hivi ni konekshini na uchawa. Ndiyo huu mwendo unaousifia? Mwanasheria na mwandishi wa habari nilidhani utakuwa na akili pembuzi zaidi yetu tusiokuwa wataaluma. Kwa kiwango chako inasikitisha sana, ingawa sishangai kwasababu ndiyo zao la mfumo hasa kuanzia kipindi cha JPM. Sifiasifia na kutukana wapinzani kesho unakula uteuzi. Alifanya hivyo Jerry Muro na wenzake wakafanikiwa sasa ni zamu yako!!!
 
Si kwamba Nakubaliana na Kila kitu alichowasilisha mleta mada, lakini, hapa nilipoopa maneno kutoka bandiko lako ninaomba ufafanuzi.

Unadhani, Nyerere (Baba wa Taifa) alikuwa anahitaji fadhila gani kutoka kwa Mkapa(R.I.P) ambazo unadhani wakati huo alikuwa anazikosa kutoka sehemu nyingine ama kwa watu wengine ??

Na uwe specific kwenye majibu yako, sihitaji majibu ya jumla jumla!!!

Nyerere alihitaji kanisa katoliki liendelee kushika hatamu Tz basi
 
Hii ni zawadi yangu kwa Birthday ya Mama leo, nilipanga kumpa wiki ya mwisho ya October 2025,

Ili zawadi hii iwe na manufaa kwake, nikisubiri mpaka hiyo 2025, it might be a bit too little too late, kuna ubaya hiyo zawadi, kutolewa mapema mwaka huu ili iweze kutumika mwaka kesho?.

Zawadi yenyewe ni Salaam tuu za Birthday zenye ki parcel fulani!

HBD Mhe. Rais Samia kwa kutimiza miaka 64!, nakupongeza sana na kukuombea afya njema!.

Mwakani 2025 utakuwa unatimiza umri wa miaka 65 na 2030 utakuwa na umri wa miaka 70, hivyo zawadi yangu ya pekee kwako ni HII na kukusisitizia, sio lazima kuizingatia saana kivile, ila ni muhimu kuisikiliza na kujisikilizia kama na wewe pia uliambiwa kama nilivyoambiwa mimi, kwasababu yule YEYE, sometimes ana tabia na mtindo wa kuwaambia watu wake, kupitia kwa watu wengine!, hivyo just listen and try to make sense of this, a think about it, if makes any sense to you, ikitokea it doesn't make any sense to you, then dismiss it as just another set of crap!.

Ila ikitokea na wewe pia uliambiwa, but you are not very sure kama ni YEYE au ni yeye, then don't take a chance!, usipuuze!, maana hicho kitu chenyewe, is nothing compared!.

If this being the case, then tunakuomba sana sana sana, ututekelezee haya mambo tunayokulilia nayo tangu umeingia kwenye usukani, tekeleza tuu yale yaliyomo ndani ya uwezo wako, maana kusubiria post 2025, it might be too little too late!. Please Mama!.

Na ikitokea wewe hujaambiwa mpaka 2025 inaingia na hujawahi kuambiwa na mtu mwingine yeyote, then ipuuze HII itakuwa sio sauti yake YEYE bali itakuwa ni sauti ya yeye tuu ambaye sio YEYE!.

Hivyo endelea na ule mpango wako wa 2025!, na Watanzania wanaolitakia mema taifa letu hili, wote tutakuwa Tuko nyuma yako,
Tuko pamoja nawe,
Tuko nawe!.

Mungu Akubariki Sana!.
HBD Mamaa!.
Paskali

Pascal , CCM ni CCM tu hata awe vipi , zaidi ya miaka 60 wako madarakani hamna kitu chochote cha maana walichokifanyia nchi zaidi ya mipasho na majisifu na kuirudisha nyuma nchi kimaendeleo.

Leo humjui aliyesoma wala asiyesoma . watu wako mbioni kila mmoja analia njaa , labda wewe unayetupiwa mafupa labda unaona unafaidi na kupata ujasiri wa kuja kuwasifu humu JF.

Wapo hapo madarakani kwa sababu ya nguvu ya dola tu lakini vyenginevyo kungekuwa na uchaguzi huru na wa haki wangelishaondoka zamani sana tokea enzi zile za Nyerere alipopinduliwa na majeshi miaka ya 60s.

wawashukuru sana , jeshi, polisi, usalama na vyombo vyengine vya usalama kwa uharamia wanaoufanya wakati wa uchaguzi.

watu walishawachoka miaka mingi sana
 
Back
Top Bottom