Wajumbe Bunge la Katiba wanamwakilisha Rais, sio Wananchi

Wajumbe Bunge la Katiba wanamwakilisha Rais, sio Wananchi

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Wajumbe wa bunge la katiba wanaotokea upande wa CCM wamekuwa wakisingizia kufanya maamuzi kwa niaba ya wananchi. Huu ni upotoshaji na unafiki mkubwa sana.

Suala hili limejitokeza hasa pale CCM wanapoweka msimamo wa pamoja wa kichama kuhusu matumizi ya kura ya wazi. Hoja wanayotoa ni kwamba kupiga kura ya siri kutawafanya wananchi 'waliowatuma' bungeni waone jinsi wanavyowawakilisha. Huo ni unafiki uliopindukia! Kuna mtu leo anaweza kusimama na kudai kwamba wajumbe wa bunge la katiba walichaguliwa na wananchi kuwawakilisha kwenye bunge la katiba?

Kila mtu anafahamu kwamba wajumbe wa bunge la katiba waliteuliwa na rais na hakuna mwananchi yeyote aliyepiga kura kuwachagua wajumbe hao. Sasa iweje CCM watuambie kwamba wametumwa na wananchi bungeni?

Ninachofahamu ni kwamba wajumbe wa bunge la katiba wanamwakilisha Rais aliyewateua (kwa makundi au kama mtu mmoja mmoja). Ila baada ya kufika bungeni kundi moja limejiunda kuwakilisha matakwa ya wananchi (UKAWA) na lingine limebaki kutetea maslahi ya chama (CCM
 
wanakera kweli mkuu, wangetumia akili kidogo tu, wasingesema hayo maneno ambayo ama yanawafanya watz kuwa hawana akili kabisa au la hawajui kusikia na kuchambua mambo, mfano hili la kura ya siri ama ya wazi, ni dhahiri kuwa kura ya wazi ina lengo jingine nyuma ya pazia. kwani wakikubali kupiga kura ya siri wao wanaoshabikia ya wazi watapata hasara gani kwa vile wale wanaotaka ya siri wameshaonesha hofu ya kumlikwa na pengine kupewa adhabu na viongozi wao wa juu. kura ya siri itawasaidia kuamua kwa haki kwa jamii yao bila mashinikizo. Hakuna cha kutumwa na wananchi hapo! kwanza sijawaona hata wakikusanya maoni ama kuwaelimisha hao wananchi juu ya katiba.
 
Ndio maana watu wenye hekima na busara wanashauri hili bunge la rais livunjwe liundwe bunge la wananchi. Ikiwa CCM kweli wanawawakilisha wananchi kwanini wameamua kuweka misimamo ya KICHAMA katika kuamua mambo yanayohusu katiba ya WANANCHI? Waseme tu kwamba wanawakilisha maslahi ya mafisadi na wachumia tumbo wachache walioigeuza nchi hii kuwa shamba la bibi. Hapo walau tutawaelewa kidogo. Wanafiki wakubwa!!
 
Haiingii akilini kwa chama chenye wanachama milioni 5 kudai kuwa wanawakilisha wawazo ya wananchi milioni karibu 40 wasiokuwa na chama chochote! Kwanini wasiboreshe katiba zao badala ya kuparamia Katiba ya Wananchi wote?
 
Rais anawakilisha watanzania wote...watanzania ndiyo unaowaita wananchi. Rais ameteua wajumbe kwa niaba ya wananchi....uzuri wajumbe hao ni miongoni mwa watanzania wapatao milioni 46 hivi ambao unawaita watanzania. Upo hapo Mkuu?
 
Rais anawakilisha watanzania wote...watanzania ndiyo unaowaita wananchi. Rais ameteua wajumbe kwa niaba ya wananchi....uzuri wajumbe hao ni miongoni mwa watanzania wapatao milioni 46 hivi ambao unawaita watanzania. Upo hapo Mkuu?

Mkuu, wewe ni kazi bure kabisa. kama rais ndio anaamua kwa niba ya wananchi, basi kusingekuwa na haja ya wananchi kupiga kura kwenye uchaguzi wa wabunge na madiwani--wananchi wangekuwa wanamuachia rais anawateua viongozi na watawala hao kwa niaba yao. si rais ndiye mwakilishi wa wananchi bhana, kwani tatizo liko wapi? angeachiwa ateue tu!
 
Mkuu, wewe ni kazi bure kabisa. kama rais ndio anaamua kwa niba ya wananchi, basi kusingekuwa na haja ya wananchi kupiga kura kwenye uchaguzi wa wabunge na madiwani--wananchi wangekuwa wanamuachia rais anawateua viongozi na watawala hao kwa niaba yao. si rais ndiye mwakilishi wa wananchi bhana, kwani tatizo liko wapi? angeachiwa ateue tu!
Naweza kweli kuwa bure kwa mujibu wa fikra zako hilo silikatai. Lakini kumbuka...baada ya Rais kutangazwa na tume ya uchaguzi ya taifa kuwa ndiye rais...tayari huyo ni mwakilishi wa wananchi. Ndiyo maana hata Kagame alivyomkwaruza 'tulikuja' juu kumtetea sisi wananchi maana yeye ndiye mwakilishi wetu. Hoja yangu ililenga hapo. Tusonge mbele.
 
Just to pick one point. The analysis is in principle, what ought to happen, not of the happenning practice.

Just because wamechaguliwa na rais, haina maana kwamba hawawajibiki kwa wananchi na hawawakilishi wananchi.

Kwa sababu hata rais anawajibika kwa wananchi na kuwawakilisha.

After all, wanasimika katiba ya nchi, haiyumkiniki wasiwajibike kwa wananchi.
 
Naweza kweli kuwa bure kwa mujibu wa fikra zako hilo silikatai. Lakini kumbuka...baada ya Rais kutangazwa na tume ya uchaguzi ya taifa kuwa ndiye rais...tayari huyo ni mwakilishi wa wananchi. Ndiyo maana hata Kagame alivyomkwaruza 'tulikuja' juu kumtetea sisi wananchi maana yeye ndiye mwakilishi wetu. Hoja yangu ililenga hapo. Tusonge mbele.

Mifano yako haisadifu hoja tunayoiongelea. Basi kama Rais ndiye mwakilishi wa kila wazo la mtanzania, hata hii katiba mpya tunayoitunga angeitunga mwenyewe kwa niaba ya wananchi. kusingekuwa na haja ya kukusanya maoni ya wananchi. Pia kusingekuwa na haja ya kuitisha chaguzi ndogo kama hizi za Kalenga na Chalinze. Tungemuachia Rais atuamulie. Si ndivyo unavyotaka wewe? Fahamu kwamba hili bunge la katiba ni jipya kabisa. Usilichanganye hili bunge maalum la katiba (BMK) na lile bunge la JMT. Sijui kama unanipata.
 
Mifano yako haisadifu hoja tunayoiongelea.....

Soma post namba nane ya uzi huu. Baada ya hapo itathimini hoja yako kama kweli rais siyo mwakilishi wa wananchi. Ukidhibitisha kuwa bado rais siyo mwakilishi wa wananchi, basi nashauri tukubaliane kutokukubaliana.
 
Wajumbe wa bunge la katiba wanaotokea upande wa CCM wamekuwa wakisingizia kufanya maamuzi kwa niaba ya wananchi. Huu ni upotoshaji na unafiki mkubwa sana.

Suala hili limejitokeza hasa pale CCM wanapoweka msimamo wa pamoja wa kichama kuhusu matumizi ya kura ya wazi. Hoja wanayotoa ni kwamba kupiga kura ya siri kutawafanya wananchi 'waliowatuma' bungeni waone jinsi wanavyowawakilisha. Huo ni unafiki uliopindukia! Kuna mtu leo anaweza kusimama na kudai kwamba wajumbe wa bunge la katiba walichaguliwa na wananchi kuwawakilisha kwenye bunge la katiba?

Kila mtu anafahamu kwamba wajumbe wa bunge la katiba waliteuliwa na rais na hakuna mwananchi yeyote aliyepiga kura kuwachagua wajumbe hao. Sasa iweje CCM watuambie kwamba wametumwa na wananchi bungeni?

Ninachofahamu ni kwamba wajumbe wa bunge la katiba wanamwakilisha Rais aliyewateua (kwa makundi au kama mtu mmoja mmoja). Ila baada ya kufika bungeni kundi moja limejiunda kuwakilisha matakwa ya wananchi (UKAWA) na lingine limebaki kutetea maslahi ya chama (CCM

Na ndiyo maana wenzetu Uganda waliomba kwa kura kuwa Mbunge/ Mjumbe wa Bunge la kutunga Katiba, na haikuwa kwa Wabunge wa Uganda! Hapa tukiri kabisa tulikosea, hawa Wabunge wa Bunge wa Bunge la JMT, na Wabunge wa BLW hawakupaswa kuwemo kwenye hili Bunge la Katiba, kwa hapo kweli tuliteleza!
 
Just to pick one point. The analysis is in principle, what ought to happen, not of the happenning practice.

Just because wamechaguliwa na rais, haina maana kwamba hawawajibiki kwa wananchi na hawawakilishi wananchi.

Kwa sababu hata rais anawajibika kwa wananchi na kuwawakilisha.

After all, wanasimika katiba ya nchi, haiyumkiniki wasiwajibike kwa wananchi.

kama wanawajibika kwa wananchi kwanini wajifungie ndani kuweka msimamo wa kichama na kuyatupilia mbali maoni ya wananchi (serikali 3) badala yake walazimishe serikali 2 zinazopendekezwa na chama? mitazamo kama hii inadhihirisha kabisa kwamba uwakilishi wa wanananchi haupo. bunge hili lilipaswa litokane na wabunge waliopigiwa kura na wananchi. hapo ndipo uwakilishi wa wananchi ungeonekana.
 
kama wanawajibika kwa wananchi kwanini wajifungie ndani kuweka msimamo wa kichama na kuyatupilia mbali maoni ya wananchi (serikali 3) badala yake walazimishe serikali 2 zinazopendekezwa na chama? mitazamo kama hii inadhihirisha kabisa kwamba uwakilishi wa wanananchi haupo. bunge hili lilipaswa litokane na wabunge waliopigiwa kura na wananchi. hapo ndipo uwakilishi wa wananchi ungeonekana.

Your argument is a non sequitur.

Kama hawafanyi wanachotakiwa kufanya, hilo halimaanishi kwamba hawatakiwi kufanya wanachotakiwa kufanya.

Tofautisha kutokufanya unachotakiwa kufanya na unachotakiwa kufanya.

Tuchukue mfano kwamba watoto wanatakiwa kuwatunza wazazi wao pindi wazee wanapozeeka.

Kama mtoto kakataa kumtunza mzazi wake, hilo halimaanishi hana wajibu wa kumtunza mzazi.

Ndiyo maana katika jibu langu la awali nimetofautisha principle na practice makusudi.

Kwa kujua kuwa, ingawa tuna principle, in practice si wote wanafuata principle.

Kutofuata principle in practice hakuondoi ile principle.

Kilatini wanasema "abusus non tollit usum".
 
Mkuu Kiranga, kushindwa kwa wabunge wa BMK kufanya kile walichotakiwa kufanya kunachagizwa na ukweli kwamba hao watu (wananchi) ambao wanatakiwa kufanyiwa hicho amabacho hakifanywi, hawahusiki moja kwa moja kuwaweka pale bungeni. Kwa hiyo, hawawajibiki kwao (wananchi) kwa namna yoyote ile.

Mambo mengi wanayofanya ni yale ambayo ama yatamfurahisha yule aliyewateua au kikundi (chama) wanachotoka. Nafasi ya wananchi katika utunzi wa katiba hii, haitambuliki-ijapokuwa maoni waliyotoa ndiyo yaliyozaa hiyo rasimu wanayoijadili. Laiti kama wabunge hawa wangechaguliwa na wananchi, hata nafsi zingekuwa zinawasuta pale ambapo wanakwenda kinyume na maoni ya wenye katiba (wananchi).

Hii ni sawa kabisa na mfano wako uliotoa kuhusu baba na mtoto. Ili mtoto ajione kwamba anawajibika kwa baba, ni sharti huyo baba awe amemzaa mtoto husika. Maana yake ni kwamba, ukaribu wao wa kidugu, utamfanya mtoto ajisikie vibaya pale anapomuona baba yake akiteseka wakati anao uwezo wa kumsaidia.

The same case applies to BMK. Wabunge wa BMK hawaoni umuhimu wa kujali matakwa ya wananchi, kwa kuwa wananchi hawajahusika kuwachagua kuingia bungeni. Ndio 7bu wanajitahidi kulinda maslahi ya chama (kwa lengo la kumfurahisha mwenyeketi wa chama chao aliyewateua) kuliko maslahi ya wananchi ambao wametengwa mbali kabisa na katiba hii.
 
Mkuu Kiranga, kushindwa kwa wabunge wa BMK kufanya kile walichotakiwa kufanya kunachagizwa na ukweli kwamba hao watu (wananchi) ambao wanatakiwa kufanyiwa hicho amabacho hakifanywi, hawahusiki moja kwa moja kuwaweka pale bungeni. Kwa hiyo, hawawajibiki kwao (wananchi) kwa namna yoyote ile.

Nimeshaligusia hili hapo juu. You have a valid point. Kwamba the further removed are they from their appointing mandate, the more diluted their sense of responsibility will be. I can go deeper into information theory and show how the nodes between the source of information and the recipient corrodes efficiency in the system. Huwezi kuwa unatoa copy ya copy ya copy with default settings halafu utegemee quality i improve.

I am not disputing that.

What I am disputing is the reductivist overgeneralization kwamba hawa watu hawawajibiki kwa wananchi kwa sababu aliyewateua ni rais, na wakichaguliwa na wananchi ndiyo tutapata fidelity of responsibility. Huyo rais anawajibika kwa nani? Hiyo katiba ni ya nani? Mbona tuna wabunge wa bunge la jamhuri wamechaguliwa na wananchi na hawana hiyo fidelity of responsibility?

In a serendipitously counterintuitive way, ukishaanza kwa kusema wabunge hawawajibiki kwa wananchi unawanyima wananchi nafasi ya kuwawajibisha. Unawapa legitimacy ya kusema "I serve at the pleasure of the president" kama utaondoa caveat nyingine ya kusema "the president serves at the pleasure of the president", at least in principle. And thus, they, by induction, serve at the pleasure of the people.

Mambo mengi wanayofanya ni yale ambayo ama yatamfurahisha yule aliyewateua au kikundi (chama) wanachotoka. Nafasi ya wananchi katika utunzi wa katiba hii, haitambuliki-ijapokuwa maoni waliyotoa ndiyo yaliyozaa hiyo rasimu wanayoijadili. Laiti kama wabunge hawa wangechaguliwa na wananchi, hata nafsi zingekuwa zinawasuta pale ambapo wanakwenda kinyume na maoni ya wenye katiba (wananchi).

There is a fallacy in this argument. And that fallacy is that kuchaguliwa na wananchi ni litmus test ya responsibility. Ingekuwa hivyo, bunge letu la siku zote lisingekuwa na indiscipline.

Kama nilivyoandika mwanzo hapo, suala la rais kuwa na mamlaka makubwa sana katika kuteua hawa wabunge ni la hatari. As a matter of fact mimi nimeanza kulisema hili suala la rais kuwa na madaraka makubwa hata kabla hii habari ya wabunge wa bunge la katiba. Nyerere mwenyewe aliyefaidika na hili alilisema kama jambo ambalo si zuri sana, alisema kama angetaka kuwa dikteta mbaya sana angeweza, ndani ya sheria. Leo hii rais hakatazwi kujimegea kipande chochote cha Tanzania na kuamua kufanya lolote analolitaka (kamkatia mshikaji wake Hashim Thabit kiwanja Obay bila maelezo, nani atamuuliza wakati katiba imempa mamlaka? Rais anaweza kuumba ofisi yoyote bila rhyme or reason, akampa mjomba wake asiye na kazi, ujuzi wala usomi, na huwezi kufanya lolote.

Tunategemea tu kwamba rais awe benevolent and self limiting with a lot of natural modesty. Siku tukipata kichaa aliyeficha makucha yake mpaka aupate urais tutajuta.

Kwa hiyo, mimi nitakuwa wa kwanza kupinga uhalali wa rais kuteua wabunge wa bunge la katiba. Especially kama rais huyo huyo ndiye mwenyekiti wa CCM. Vipi siku interests za CCM na interests za taifa zitakapogongana? Rais atateua watu kwa kigezo cha kutetea interests za nchi au interests za CCM? Wengine wanaweza kusema hiki ndicho kinatokea sasa.

Kwa hiyo, nikisema kwamba principle ya wabunge kuwa responsible kwa wananchi inabaki pale pale hata kama wabunge wameteuliwa na rais, simaanishi kutetea habari ya rais kuteua wabunge, namaanisha kwamba hata kama tunahitaji kumpunguzia rais madaraka na wabunge hawa wachaguliwe na wananchi - something that may prove impractical for a constitutional body like this in the middle of election seasons and all the other questions revolving around the hoopla of representation of religious bodies etc etc

Hii ni sawa kabisa na mfano wako uliotoa kuhusu baba na mtoto. Ili mtoto ajione kwamba anawajibika kwa baba, ni sharti huyo baba awe amemzaa mtoto husika. Maana yake ni kwamba, ukaribu wao wa kidugu, utamfanya mtoto ajisikie vibaya pale anapomuona baba yake akiteseka wakati anao uwezo wa kumsaidia.

Tukirudi kwenye mfano huo - nearing the territory of stretching an analogy here-, mtoto kuwajibika kumtunza baba, hakumzuii kutaka kumtunza babu aliyemzaa baba pia. Lakini pia, kama ni wajibu wa mtoto kumtunza baba, na imefikia wakati mpaka mjukuu inambidi azidishe kumtunza babu, inabidi tujiulize baba mbona hajamtunza babu?

Kwa maana nyingine, kilichotakiwa kutokea in principle hapa ni a chain of delegation. In principle, wananchi wamemchagua rais wakampa kazi ya kuangalia interests zao, rais akawateua wabunge wamsaidie kuangalia interests za wananchi. Basi kama kuna wabunge hawaangalii interests za wananchi, utakuwa na haki ya kuhoji si tu uzuri wa huu mfumo wa wananchi kum delegate rais awafanyie hii kazi (labda wabunge wanaweza kuwa na responsibility kwa wananchi zaidi kama watachaguliwa na wananchi moja kwa moja - natumai utakubali kodi itakayozidishwa kwako kama mwananchi ili kupata haki hii-) kwa hiyo concern yako ni genuine. Lakini inabidi pia tumuhoji rais kwa nini kateua wabunge ambao hawafanyi kazi zao, za kuwa deputies wa deputy wa wananchi?

The same case applies to BMK. Wabunge wa BMK hawaoni umuhimu wa kujali matakwa ya wananchi, kwa kuwa wananchi hawajahusika kuwachagua kuingia bungeni. Ndio 7bu wanajitahidi kulinda maslahi ya chama (kwa lengo la kumfurahisha mwenyeketi wa chama chao aliyewateua) kuliko maslahi ya wananchi ambao wametengwa mbali kabisa na katiba hii.

Ungekuwa na a stronger argument katika hili kama bunge letu la jamhuri ya muungano lingekuwa na tofauti kubwa sana katika kujali maslahi ya wananchi.

This is not to say nina support rais kuteua wabunge wa bunge la katiba.

It is just saying kwamba unaweza kupata gharama za uchaguzi, ukachagua wabunge wa baraza la katiba, karibu wote wakawa kina Dr. Maji Marefu, wataalamu wa sheria na mengine yanayohusika katika katiba moja kwa moja wasiwemo, ukaingia gharama za mamilioni ya dola, bila kupata responsibility unayoitaka.

Tanzania tuna utamaduni wa kutokuwajibishana na accountability kama alivyosema Amani Karume. Kuanzia kwenye familia baba hakosei. Wangapi washamshuhudia baba akiiomba samahani familia kwa kuikosea?

Mpaka hapo tutakapobadilisha utamaduni, huko mbele tunachuzana tu.Watu wakichaguliwa na wananchi au wakiteuliwa na rais hawatakuwa na tofauti kubwa sana kama hakutakuwa na la msingi litakalobadilika katika utamaduni wetu.

Waingereza wanasema "you can't teach an old dog new tricks". Mijitu imekulia katika clientelism for decades (CCM na upinzani), huwezi kusema itabadilika leo kwa sababu imechaguliwa na wananchi.

Ni kama kusema eti nywele za mtu zitaacha kuwa kipilipili siku zote eti kwa sababu kaweka relaxer mara moja!
 
Mkuu Kiranga, Tanzania na neno principle ni kama Mbingu na Dunia. Mathalan, the very day our current President stepped into office, that I believe, was the day the word principle waved us goodbye! Tukirudi kwenye uwajibikaji, amini usiamini, tofauti na ilivyo kawaida kote duniani kwenye watu wanaojua principle ni nini na kuiheshimu, hapa kwetu ni Watanzania ndio wanatakiwa wawajibike kwa Raisi instead of vice versa. Kwenye uwakilishi ndio balaa kabisa, Raisi wetu anamwakilisha kwanza Kikwete, pili familia ya Kikwete, tatu washikaji wa Kikwete na mwisho CCM...Raisi wetu hajawahi kuwawakilisha wananchi, Watanzania...he just doesn't know how and that's the naked truth!
 
Mkuu Kiranga, Tanzania na neno principle ni kama Mbingu na Dunia. Mathalan, the very day our current President stepped into office, that I believe, was the day the word principle waved us goodbye! Tukirudi kwenye uwajibikaji, amini usiamini, tofauti na ilivyo kawaida kote duniani kwenye watu wanaojua principle ni nini na kuiheshimu, hapa kwetu ni Watanzania ndio wanatakiwa wawajibike kwa Raisi instead of vice versa. Kwenye uwakilishi ndio balaa kabisa, Raisi wetu anamwakilisha kwanza Kikwete, pili familia ya Kikwete, tatu washikaji wa Kikwete na mwisho CCM...Raisi wetu hajawahi kuwawakilisha wananchi, Watanzania...he just doesn't know how and that's the naked truth!

Yeye mwenyewe hajalelewa katika mfumo unaoheshimu principle na uwakilishi. Hakuchaguliwa kwa merit.

To begin with, kaingia bungeni kwa viti maalum!

Tutategemeaje ateue wabunge wa bunge la katiba kwa merit na principle instead of Machiavellian machinations za party factionalism politics?

Tunategemeaje Kikwete awe na principles kama malaika wakati majority hatuna principle? Kuheshimu principle Tanzania ni exception, si rule.

Airport ukishuka tu, watu wanakuomba rushwa bila aibu. Mtu umerudi nyumbani kutoka mbali, unakaribishwa kwa rushwa!

Ukitoka mtumishi wa Swissport anakuambia kinagaubaga kwamba umkatie ili kuondoa bugudha zisizo lazima!

Wanaotaka principle ni nani? Ni vijana - maana wazee tutasema wamepitwa na wakati- hawahawa wanaotoroka kazini serikalini na kuacha wenzao wasaini kwa niaba yao? Huku wenyewe wameenda kwenye shughuli zao?

Ni madereva wasioheshimu sheria za usalama wa barabarani na trafiki wala rushwa?

Ni hawa kinababa wenye nyumba ndogo utitiri wakati hawahudumii familia?

Ni hawa wanaowacheka wachache waliostaafu bila kuiba na kuonekana wamechoka?

Let's face it. Kikwete kama mtu aliye juu kabisa katika uongozi wa Tanzania, ana sehemu kubwa sana ya lawama kwa matatizo tuliyonayo sasa per "Noblesse Oblige". To whom much is given, much will be required.

Lakini haya matatizo yetu yaliyo deep katika tamaduni zetu, yanayoanza pale siku mtoto anapozaliwa, kwa mtoto huyo - na hata kabla kama unataka kujali historia-, matatizo yaliyotufanya tuweze kumchagua Kikwete mara mbili pamoja na udhaifu wake wote, yananionesha kuwa tuna matatizo zaidi ya Kikwete, zaidi ya CCM, zaidi ya upinzani, zaidi ya siasa.

Tuna matatizo deep kwenye utamaduni huko.

Matatizo yanayoturuhusu kuwa na utamaduni wa kwamba mgombea wa CCM kama ni rais tayari, basi hapati serious challenge kutoka katika chama, anapitishwa tu.

Matatizo yanayoturuhusu kumuacha mtu aliyekuwa na scandal ya IPTL kwenda kuwa rais.

Matatizo yaliyoturuhusu kuacha mtu aliyekwishajiuzulu kwa kushindwa kutimiza wajibu wake - hata kama wa kiuangalizi tu- aweze kuwa rais. I am talking about Mwinyi. Na tusipokaa sawa sasa hivi tunamrudisha Lowassa, kujiuzulu badala ya kuwa a disgrace inaweza kuwa kama a prerequisite!

Kwa hiyo anytime naona mtu ana focus sana kwenye watu, Kikwete this, wabunge that, naona haangalii mzizi hasa wa matatizo.

Utamtoa Kikwete na kumuweka nani mwingine ambaye hajaguswa na matatizo yetu ya kiutamaduni?

Utasema uache wabunge waliochaguliwa na rais, utake wabunge waliochaguliwa na wananchi, utawatoa wapi wabunge ambao hawajaguswa na utamaduni wa top down decrees and lack of grassroots directed politics?

Kama tunataka mabadiliko tuanze kuangalia jamii nzima critically, sio hawa viongozi tu.

Hawa viongozi ni vioo tu vya jamii yetu ilivyo.
 
Back
Top Bottom