Wajuzi naomba mnitoe ushamba, hivi star wa movie za mapigano anapatikanaje?

Wajuzi naomba mnitoe ushamba, hivi star wa movie za mapigano anapatikanaje?

NIMEONA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2019
Posts
3,862
Reaction score
5,693
Zamani nilifikiri inatokana na uwezo wa kupigana wa mtu, hivyo niliamini Jack chan, Jet Li, Jack Bauer na wengine ni mafundi haswaa wa kupigana kuzidi wanaocheza nao. Lakini najiuliza ina maana ni kweli kwamba wale wengine wote hawajui kuwazidi?

Nikiangalia picha nyingi za mapigano ni nakshi za kompyuta tu, uharaka, uzito wa ngumi hadi mtu mwenye kilo 88 anarushwa juu huko n.k. Najiuliza, kama ni michezo tu ya kompyuta sasa inakuaje star anakuwa Jet Li tu?! Mwingine nae si anaweza tu kuchezesha au kuna ishu ya mtaji inahusika?

Yaani Angelina Jolie nae anapiga watu, kweli?!

Ni nini hiko kinamfanya mtu awe star wa hizi picha?

Tuelewesha jamani, si mzaha!
 
Ulikuwa sahihi zamani, miaka ya 70 na 80 computer haikuwa advanced sana hivyo kina Bruce Lee, Van Dame, Jet li, Jackie Chan etc wanafahamu kupigana ukweli ukweli, Arnold alikuwa ni Body Builder, Chuck Norris ana Black belt ya Taekwondo, Karate, Judo na michezo kibao ya Mapigano.

Ila siku hizi sababu computer imekuwa advanced anatafutwa TU muuza sura anawekwa, weakness zake zinatatuliwa na computer.
 
Anapatikana kulingana na matakwa ya waandaaji (producers) wa filamu husika.

Hata kama ni wewe mwenyewe unaandaa filamu yako, ukijiamulia kuwa star katika hiyo filamu yako na unaona itakulipa sokoni, inawezekana kabisa.
 
Ulikuwa sahihi zamani, miaka ya 70 na 80 computer haikuwa advanced sana hivyo kina Bruce Lee, Van Dame, Jet li, Jackie Chan etc wanafahamu kupigana ukweli ukweli, Arnold alikuwa ni Body Builder, Chuck Norris ana Black belt ya Taekwondo, Karate, Judo na michezo kibao ya Mapigano.

Ila siku hizi sababu computer imekuwa advanced anatafutwa TU muuza sura anawekwa, weakness zake zinatatuliwa na computer.
Ahsante sana!
 
Anapatikana kulingana na matakwa ya waandaaji (producers) wa filamu husika.

Hata kama ni wewe mwenyewe unaandaa filamu yako, ukijiamulia kuwa star katika hiyo filamu yako na unaona itakulipa sokoni, inawezekana kabisa.
Alaa kumbe!
 
Zamani walikua wakweli Bruce Lee wanasema alipata majeraha wakiwa wanatengeneza movie hata Chuck Norris aliwahi pata majeraha akiwa kazini ilibidi apumzike kidogo kwa muda walipotaka kutoa movie nyingine...Van Dame anavuta gari na unaliona sio sasa hivi ujanja ujanja tuu..
 
Zamani nilifikiri inatokana na uwezo wa kupigana wa mtu, hivyo niliamini Jack chan, Jet Li, Jack Bauer na wengine ni mafundi haswaa wa kupigana kuzidi wanaocheza nao. Lakini najiuliza ina maana ni kweli kwamba wale wengine wote hawajui kuwazidi?

Nikiangalia picha nyingi za mapigano ni nakshi za kompyuta tu, uharaka, uzito wa ngumi hadi mtu mwenye kilo 88 anarushwa juu huko n.k. Najiuliza, kama ni michezo tu ya kompyuta sasa inakuaje star anakuwa Jet Li tu?! Mwingine nae si anaweza tu kuchezesha au kuna ishu ya mtaji inahusika?

Yaani Angelina Jolie nae anapiga watu, kweli?!

Ni nini hiko kinamfanya mtu awe star wa hizi picha?

Tuelewesha jamani, si mzaha!
Anapangwa kabla "senema" haijachezwa.Anakuwa mshindi katika kila eneo.Akili,ujanja,ubunifu,mbinu,nguvu na kudumu hadi neno "the End" lionekane.
 
Mkuu mbona simple sana!
Hiyo ndio maana ya "MAIGIZO" yaani "UNAIGIZA" hakuna kinachotakiwa kuwa kweli yote ni kuigiza tu hakuna kupigana kweli ngumi za uso.
Hiyo ya watu kujua kupigana kweli ilikuwa enzi hizo sana tena kwa kwenye movie zenye budget ndogo.
Mtu anaweza akawa anajua kupigana lakini hajui kuigiza. sasa hilo ni tatizo ambalo litasababisha movie nzima kuflop na kusababisha hasara kubwa kwa studio.

Lakini siku hizi ni muigizaji anaingia gym kufanya mazoezi ya kujenga mwili na misuli (wengine hujifunza kabisa aina za mapigano kama kong fu na judo au krav maga kama nyongeza au kufanya mwili uwe sharp pekee) baada ya hapo director na writer tayari wanakuwa na scene ya mapigano itakavyokuwa vichwani mwao inaitwa fight choreography, alafu kunakuwa na watu special kabisa ambao ni wapiganaji officials kabisa wao kazi yao wanaapply maagizo ya director na writer yaani ile fight choreography na kusaidia actors wapigane vipi mbele ya camera kwa kufuata maagizo ya director.

Hapo wakichanganya na special effects, visual effects (vfx), computer generated imagery (CGI) na animations kwa msaada wa greenscreen basi hapo kazi imekwisha na unaweza kufanya movie iwe vyovyote unavyoweza kuimagine kichwani kwako, ila budget yake ni kubwa sana, na ndio sababu movie nyingi za zamani walitumia actors wanaoujua kupigana kweli ili kupunguza gharama za production ya movie.
Lakini kwa studio kubwa hilo sio tatizo.

Kwenye studio kubwa hakuna kupigana ngumi kweli lakini muda wengine actors huumia vibaya mpaka kusimamisha shooting kwa muda mpaka wapone au kama itahitajika scene yenye uhalisia sana basi watatumia watu wanaitwa stunt doubles hawa ni watu maalum ambao huajiriwa kwa ajili ya kufanya mambo ya hatari tu kwenye movies ikiwemo mapigano. mfano Tom Cruise alivunjika ankle wakati akishoot mission impossible fallout ilikuwa scene ya kuruka ghorofa mpaka ghorofa lakini akamaliza scene baada ya hapo akaenda hospital kwa miezi kadhaa na baadae wakaendelea na shooting.

Au wataruka yote hayo, alafu kwenye scenes za mapigano watachukua tu stunt doubles wanaofanan na actors wenyewe lakini ambao ni wapiganaji professional then watarecord scenes za mapigano alafu wataedit sura ya actor na stunt double alafu tayari movie imekamilika.

Kwenye movies kubwa watu hawaangalii nani anajua kupigana bali wanaangalia uwezo wako wa kuigiza yaani acting skills na elimu yako ya maswala ya sanaa sababu actors wakubwa wengi wanakuwa wamesomea uigizaji kwenye vyuo maalum lakini bila kusahau umaarufu wa jina, hayo mengine ni nyongeza tu.
Muigizaji bora anayejua anachokifanya atacheza scene yoyote kwa ufasaha na uhalisia hasa akipata director bora aliyesomea na mzoefu anayejua maana movie choreography na movie cinematography na mambo mengine mengi kwenye sanaa ya movie.

Muone brad pitt kwenye fury.
Leonardo dicaprio kwenye inception.
Keanu reeves kwenye John Wick, humu keanu alifanya mazoezi ya shooting na judo lakini jamaa sio fighter professional ni mtu mmoja cool sana lakini zile fight choreography zinamfanya awe professional assassin mnyama asiyekamatika.
matt damon kwenye Jason Bourne.

Tom Cruise, huyu mzee angalia movie zake zote hasa mission impossible na jack reacher na yeye hatumii stunt doubles bali anafanya kila kitu mwenyewe kiume maigizo yote hata kuruka nje ya ghorofa na ndege na kuning'inia nje ya ndege huyu mzee ni legend.
Colin Firth kwenye Kingsman the secret service, hii movie ina scene moja ya hatari sana pale kanisani acha kabisa na yote ni sababu ya director na ule upangaji wa fight choreography, director amefanya unyama sana kwenye ile scene, respect.

Chris evans kwenye captain america, humu wanatumia computer yaani vfs na green screen.
Bob Odenkirk kwenye nobody, huyu mzee unaweza sema ni ndugu wa damu na babayaga john wick.
Daniel craig kwenye james bond hasa no time to die na yule bidada mrembo Ana de Armas anachapa mkono kinyama, sasa jiulize yule dada mrembo namna ile na usoft wote ule anawezaje hata kurusha ngumi mpaka mtu aisikie acha mtu kuanguaka.
Alafu bado kidogo niisahau The Equalizer kazi ya mzee mzima mr Denzel Washington.
Na huyo mrembo uliyemtaja Angelina Jolie kama Evelyn Salt kwenye movie ya SALT 2010 au movies za Tomb Raider 2001-2003.

Hao actors wote hapo juu sio wapiganaji kweli kwenye maisha halisi ni watu tu wa kawaida kama sisi huku, bali wenyewe ni waigizaji tu ambao wanajua kuigiza na kusomea kuigiza hivyo wakipata writer na director bora na mwenye uzoefu basi wataigiza kila kitu kama inavyotakiwa ikiwemo scene za mapigano.

Mzee nikiendelea kuandika hapa naona sitamaliza sababu movies nilizoangalia ni mamia au maelfu mpaka sasa ila kiufupi kwenye main cinema industry au niseme Hollywood kitu kinachoamua Movie iwe vipi ni Actors wanaojua kuigiza na Budget ya movie yaani pesa za kutosha na baada ya hapo kinachofuata ni Writer na Director bora anayejua anachokifanya ukipata hivyo vinne movie itakuwa vyovyote vile inavyotakiwa kuwa.

Limitation ni Imagination pekee, nimeandika rough sana lakini nadhani inaeleweka.
Over and out.
 
Mkuu mbona simple sana!
Hiyo ndio maana ya "MAIGIZO" yaani "UNAIGIZA" hakuna kinachotakiwa kuwa kweli yote ni kuigiza tu hakuna kupigana kweli ngumi za uso.
Hiyo ya watu kujua kupigana kweli ilikuwa enzi hizo sana tena kwa kwenye movie zenye budget ndogo.

Lakini siku hizi ni muigizaji anaingia gym kufanya mazoezi ya kujenga mwili na misuli (wengine hujifunza kabisa aina za mapigano kama kong fu na judo au krav maga kama nyongeza au kufanya mwili uwe sharp pekee) baada ya hapo director na write tayari wanakuwa na scene ya mapigano itakavyokuwa vichwani mwao inaitwa fight choreography, alafu kunakuwa na watu special kabisa ambao ni wapiganaji officials kabisa wao kazi yao wanaapply maagizo ya director na write yaani fight choreography na kusaidia actors wapigane vipi mbele ya camera. hakuna kupigana ngumi kweli lakini au kama itahitajika hivyo basi watatumia watu wanaita stunt doubles hawa ni watu maalum ambao huajiriwa kwa ajili ya kufanya mambo ya hatari tu kwenye movies ikiwemo mapigano.

Au wataruka yote hayo na kwenye scenes za mapigano watachukua tu stunt doubles wanaofanan na actors wenyewe lakini ambao ni wapiganaji professional then watarecord scenes za mapigano alafu wataedit sura ya actor na stunt double alafu tayari movie imekamilika.

Kwenye movies kubwa watu hawaangalii nani anajua kupigana bali wanaangalia uwezo wao wa kuigiza yaani acting skills na elimu yako ya maswala ya sanaa bila kusahau umaarufu wa jina, hayo mengine ni nyongeza tu.
Muigizaji bora anayejua anachokifanya atacheza scene yoyote kwa ufasaha na uhalisia hasa akipata director bora na mzoefu anayejua maana movie choreography na movie cinematography.

Muone brad pitt kwenye fury.
Leonardo dicaprio kwenye inception.
Keanu reeves kwenye John Wick, humu keanu alifanya mazoezi ya shooting lakini jamaa sio fighter ni mtu mmoja cool sana lakini zile fight choreography zinamfanya awe professional assassin mnyama asiyekamatika.
matt damon kwenye Jason Bourne.
Tom Cruise, huyu mzee angalia movie zake zote hasa mission impossible na jack reacher na yeye hatumii stunt doubles bali anafanya mwenye kiume maigizo yote hata kuruka nje ya ghorofa na ndege na kuning'inia nje ya ndege huyu mzee ni legend.
Colin Firth kwenye Kingsman the secret service, hii movie ina scene moja ya hatari sana pale kanisani acha kabisa na yote ni sababu ya director na ule upangaji wa fight choreography, director na amefanya unyama sana kwenye ile scene respect.
Chris evans kwenye captain america, humu wanatumia computer yaani vfs na green screen.
Bob Odenkirk kwenye nobody.
Daniel craig kwenye james bond hasa no time to die na yule bidada mrembo Ana de Armas anachapa mkono sasa jiulize yule dada mrembo namna ile na usoft wote ule anawezaje hata kurusha ngumi mpaka mtu aisikie acha kuanguaka.

Alafu bado kidogo niisahau The Equalizer kazi ya mzee mzima mr Denzel Washington.
Mzee nikiendelea kuandika hapa naona sitamaliza sababu movie nilizoangalia ni mamia au maelfu mpaka sasa ila kiufupi kwenye main cinema industry au niseme hollywood kitu kinachoamua Movie iwe vipi ni Budget ya movie yaani pesa za kutosha na baada ya hapo kinachofuata ni Writer na Director bora anayejua anachokifanya ukipata hivyo vitatu movie itakuwa vyovyote vile inavyotakiwa.

Limitation ni Imagination pekee, nimeandika rough sana lakini nadhani inaeleweka.
Over and out.
Ahsante sana kwa elimu hii!!
 
Kumbe hata kwenye movie ya Roho Tua ni usanii mtupu. Kwamba ukweli ni kidogo na longo longo ndiyo nyingi.
 
Woote waigize, ila aliyeigiza X(porn) jua kafanywa kweli.
😂 😂
Hata hao wapo wa uongo mkuu, Kuna kitu kinaitwa Body Dubbing, ana act mwengine then wanaweka TU sura ya mwengine.

Movie nyingi ukiona Actress analiwa ujue sio yeye wamefanya Body Dubbing.
 
Back
Top Bottom