Dr Restart
JF-Expert Member
- Jul 15, 2021
- 4,949
- 24,046
Huo utaratibu hakuna. Ila je, unaelewa taratibu sahihi kabisq za miamala ya simu inavyopaswa kuwa?
Wakati inaanza, M-PESA walikuwa na kitabu cha logbook. Mteja akitoa fedha, anajaza taarifa zake muhimu ikiwemo namba ya muamala, kiasi, kitambulisho chake, sahihi,nk.
Hii yote iliweka ili kuepusha usumbufu mwingi. Wizi vile vile.
Sasa siku hizi kuna wimbi kubwa sana la kurudisha miamala. Mteja anaenda kwa wakala. Anaomba kutoa fedha, anapewa go ahead.
Anachofanya, anamtumia mwenzake namba ya kutolea. Anapewa hela na kuondoka. Kisha akishaondoka mahali hapo, anawasiliana na mwenzake simu inapigwa huduma kwa wateja kuzuia muamala..
Wanachoangalia mtandaoni, kwanza wanaushililia huo muamala immediately. Kisha watapiga simu kwa wakala kujiridhisha. Wakala ukisema umetoa hela, wanawaunganisha na mteja. Mzungumze.
Mteja anakataa, wakala naye anabisha. Sasa wanarudi kwenye location. Mteja katoa fedha yupo Narung'ombe huko. Wewe wakala upo Dar. Wapi na wapi?
Ukijitetea pengine alitoa namba kwa nduguye, basi unakosa. Umejaza logbook? Jibu hapana.
Mteja anarudishiwa fedh zake na wakala kula hasara .
Mantiki ya kuona sms ni kujiridhisha tu. Sidhani kama kumuonyesha sms chap bila kumkabidhi simu yako, ukaamua kuziba salio kwa kidole ni jambo gumu.
Si haki, lakini wana sababu yenye mashiko kidogo. Vinginevyo tuwe tunajaza vitabu vya miamala.
Wakati inaanza, M-PESA walikuwa na kitabu cha logbook. Mteja akitoa fedha, anajaza taarifa zake muhimu ikiwemo namba ya muamala, kiasi, kitambulisho chake, sahihi,nk.
Hii yote iliweka ili kuepusha usumbufu mwingi. Wizi vile vile.
Sasa siku hizi kuna wimbi kubwa sana la kurudisha miamala. Mteja anaenda kwa wakala. Anaomba kutoa fedha, anapewa go ahead.
Anachofanya, anamtumia mwenzake namba ya kutolea. Anapewa hela na kuondoka. Kisha akishaondoka mahali hapo, anawasiliana na mwenzake simu inapigwa huduma kwa wateja kuzuia muamala..
Wanachoangalia mtandaoni, kwanza wanaushililia huo muamala immediately. Kisha watapiga simu kwa wakala kujiridhisha. Wakala ukisema umetoa hela, wanawaunganisha na mteja. Mzungumze.
Mteja anakataa, wakala naye anabisha. Sasa wanarudi kwenye location. Mteja katoa fedha yupo Narung'ombe huko. Wewe wakala upo Dar. Wapi na wapi?
Ukijitetea pengine alitoa namba kwa nduguye, basi unakosa. Umejaza logbook? Jibu hapana.
Mteja anarudishiwa fedh zake na wakala kula hasara .
Mantiki ya kuona sms ni kujiridhisha tu. Sidhani kama kumuonyesha sms chap bila kumkabidhi simu yako, ukaamua kuziba salio kwa kidole ni jambo gumu.
Si haki, lakini wana sababu yenye mashiko kidogo. Vinginevyo tuwe tunajaza vitabu vya miamala.