Wakandarasi wa barabara (Nyanza Roadworks) hawafukii mashimo walipochukua vifusi, maeneo ya Iyumbu, Block C, Dodoma na kusababisha HATARI

Wakandarasi wa barabara (Nyanza Roadworks) hawafukii mashimo walipochukua vifusi, maeneo ya Iyumbu, Block C, Dodoma na kusababisha HATARI

2Y2

New Member
Joined
Dec 27, 2023
Posts
1
Reaction score
0
Habari,

Tunaomba ushauri ili tupate msaada kutoka kwa mamlaka husika. Mimi ni mmoja wa wakazi wa Block C, Iyumbu West, Dodoma.

Tuna changamoto ya mashimo / makorongo makubwa yaliyochimbwa na kampuni ya Nyanza Roadworks wakitafuta kifusi kwa ajili ya matengenezo ya barabara, na mpaka sasa wameyaacha hivyo hivyo bila kuyafukia / site restoration (Nimeambatanisha picha).

Tumejaribu kwenda NEMC tukakwama na wakasema hawawezi kutusaidia, tulitakiwa kwenda wakati wanachimba ndio wangewasimamisha.
20231217_123715.jpg
20231217_123721.jpg
20231217_123727.jpg
20231217_123812.jpg
20231217_123910.jpg
20231217_123913.jpg
20231217_123918.jpg
 
Back
Top Bottom