Tunaomba ushauri ili tupate msaada kutoka kwa mamlaka husika. Mimi ni mmoja wa wakazi wa Block C, Iyumbu West, Dodoma.
Tuna changamoto ya mashimo / makorongo makubwa yaliyochimbwa na kampuni ya Nyanza Roadworks wakitafuta kifusi kwa ajili ya matengenezo ya barabara, na mpaka sasa wameyaacha hivyo hivyo bila kuyafukia / site restoration (Nimeambatanisha picha).
Tumejaribu kwenda NEMC tukakwama na wakasema hawawezi kutusaidia, tulitakiwa kwenda wakati wanachimba ndio wangewasimamisha.