Wakandarasi wababaishaji sitaki -Kikwete

Wakandarasi wababaishaji sitaki -Kikwete

Tusimlaumu JK bure kwenye hili. Mtatatizo ya procurement method yetu yamejali sana mambo ya CYA kuliko ufanisi. Tunapendelea open tenders kwenye miradi kwa kuogopa kuwa ukifanya vinginevyo utaonekana umekula. Tatizo la open tenders ni kuwa makandarasi wa maana hawaingii maana wanajua toka wali hawawezi kushindana na makandarasi uchwara kutoka China na kwingineko. Tukumbuke kuwa kutenda kuna gharama zake. Ndiyo maana Skanska aliishafunga virago na Noremco wanasuasua. Kama tunataka ubora na ufanisi ni lazima tuangalie uwezekano wa kutumia zaidi limited tenering ambapo makandarasi watakuwa pre-qualified. Technocrats wetu waanze kufanya hivi bila kuogopa shutuma za kula na mafisadi.

Kwa wale ambao wanadhani solution ni kuwapa wazawa badala ya wageni wanakosea. Ukweli ni kuwa ni makandarasi wachache wazawa wenye uwezo wa kitaalamu na kiufundi wa kuzimudu kazi hizi! Dhana ya makandarasi wetu wengi ni kupunguza gharama kwa kuajiri wataalamu wachache ( ni makandarasi wangapi wazawe wenye Quantity Surveyors qualified na wanaopewa madaraka kamili ya ku'price tenda zao?)na kutegemea zaidi kupenyeza rupia ili wapate engineer's estimate. Wakiipata hii wanafanya kila njia kufanya tenda yao iwe chini ya hii bila kujali gharama zao halisi! Mimi naamini makandarasi wetu walio makini badala ya kugombea hizo tenda kubwa wangejenga uwezo wao katika specialised areas ili waweze kushirikiana na hao wageni kama sub-contractors.

Mwisho, namuunga mkono mhandisi Mmasai kuwa uwezo wetu wa kutayarisha tenda documents pamoja na kusimamia mikataba una walakin mkubwa. Inabidi tufanye jitihada kubwa katika maeneo haya maana bila tenda air-tight na usimamizi makini tutaendelea kuliwa!
 
Mh Rais kwakweli anatushtusha wengi!
Ama ni ule msemo wa "Usijudge Kitabu Based on its Cover?!" Ndio unatugeuka Watanzania?
 
Fundi,

.........nilifikiri hata ktk Open Tendering kunatakiwa kuwe na post-qualification kabla ya kufungua makabrasha ya mkandarasi...........

Limited Bidding ni nzuri.........tatizo la wawakilishi wetu TANROADS kwanini hawaipendi hiyo......... ni 10%...........
 

Kwa wale ambao wanadhani solution ni kuwapa wazawa badala ya wageni wanakosea. Ukweli ni kuwa ni makandarasi wachache wazawa wenye uwezo wa kitaalamu na kiufundi wa kuzimudu kazi hizi! Dhana ya makandarasi wetu wengi ni kupunguza gharama kwa kuajiri wataalamu wachache ( ni makandarasi wangapi wazawe wenye Quantity Surveyors qualified na wanaopewa madaraka kamili ya ku'price tenda zao?)na kutegemea zaidi kupenyeza rupia ili wapate engineer's estimate. Wakiipata hii wanafanya kila njia kufanya tenda yao iwe chini ya hii bila kujali gharama zao halisi! Mimi naamini makandarasi wetu walio makini badala ya kugombea hizo tenda kubwa wangejenga uwezo wao katika specialised areas ili waweze kushirikiana na hao wageni kama sub-contractors.

Mwisho, namuunga mkono mhandisi Mmasai kuwa uwezo wetu wa kutayarisha tenda documents pamoja na kusimamia mikataba una walakin mkubwa. Inabidi tufanye jitihada kubwa katika maeneo haya maana bila tenda air-tight na usimamizi makini tutaendelea kuliwa!

FM,

Suala hapo sio kuwapa wazawa bali kuhakikisha kunakuwa na technology transfer ambayo ina maana kubwa zaidi ya kuwapa wazawa.

Kwa mfano ukiwapa mradi KAJIMA basi wanaungana na kampuni ya TZ ambayo hata ina asilimia 20. Hawa Wazawa wanajifunza kuanzia tendering process mpaka kusimamia, kujenga na kumanage project.

Kinachonisikitisha nyumbani ni haya mawazo ya kukimbilia solutions za haraka haraka badala ya kuwa na long term strategies. Unaweza kuogopa cost leo lakini madhara yake ni kuingia cost kubwa sana hapo baadaye.
 
Fundi,

.........nilifikiri hata ktk Open Tendering kunatakiwa kuwe na post-qualification kabla ya kufungua makabrasha ya mkandarasi...........

Limited Bidding ni nzuri.........tatizo la wawakilishi wetu TANROADS kwanini hawaipendi hiyo......... ni 10%...........

Open tenda kama inavyosema ni kuwa kila mwenye uwezo na anayeamini ana'meet' criteria anaweza kuingia kwenye mpambano. Kinachoangaliwa mara nyingi ni general qualifications kama :class of registration, performance bond,vifaa, watu n.k. Baada ya hapo ndipo hayo makabrasha yanafunguliwa. Ni mara chache kunakuwa na muda wa kuweza kuangalia performance ya makandarasi kwa undani. Hii inapendwa kwa sababu superficially inaonekana iko wazi na hata kama atapatikana mkandarasi bomu hakuna atakayeweza kuwanyooshea kidole evaluation team maana ndiyo transparency tunayoitaka.

Limited tenda ziko za aina mbili kama sijakosea:

1) Matandazo yanakaribishwa kwa ajili ya pre-qualification. Katika hatua hii, kipimo ni uwezo, experience na sifa za mkandarasi. Kutokana na hii, shortlist inatayarishwa ya wale wachache wanaoonekana kuwa ndio bora zaidi ili wa'submit' tenda. Makandarasi wakubwa wanaipenda hii kwa sababu kwanza hawaingii gharama ya ku'price' bids bila kujua washindani hao ni nani. Hii inawafanya waamini kuwa wana realistic chance za kushinda kwa hiyo ni worth the expence.

2)Wataalamu kutokana na uzoefu wao wanawakaribisha makandarasi ambao wana hakika wanaiweza hiyo kazi ili wasubmit bids. Hii tatizo lake ni kwamba inamhamishia mzigo mtaalamu maana mkandarasi akitokea kuwa bomu itajulikana kabisa kuwa hakuwa makini. Kwa kuogopa kuwajibika na shutuma za kula 10% wengi wanaikimbia. Mimi kwa imani yangu kuwa kwa miradi sensitive na complex hii ni njia pekee inayofaa maana unahakika competent contractors watabid! Tatizo lingine ni kuwa World Bank na wafadhili wengine wanaamini kuwa sisi wote ni corrupt kwa hiyo hatuwezi kutayarisha shortlist isiyotanguliza interest zetu! Japokuwa kuna ukweli katika hizi tuhuma lakini naamini hii inaweza kuwa controlled kama wataalamu wetu wakijua kuwa their heads will roll kama mkandarasi atashindwa kutimiza wajibu wake katika muda na standards zilizokubalika!

Ukweli ni kuwa tenda procedure zote zinaweza kuwa manipulated hata zinazoonakana kuwa ziko wazi. Kwa mawazo yangu hizi limited zina nafuu kwa sababu ni rahisi ku'trace' kamchezo kabaya kalitokea wapi! swali la kwa nini amepewa mkandarasi asiye na uwezo litawaangukia wale ambao tumewapa dhamana ya kulinda interest zetu! wakikubali kuwa influenced na wakubwa zao au vijisenti, watagundulikana tu.
 

Mfano mzuri wa udhaifu wa Tender documents zetu ni kwenye vipengele viwili:

1) liquidated damages inatakiwa iwe punitive kiasi ambacho mkandarasi aisikie anapokatwa kutokana na kuchelewesha kazi. Mara nyingi kiasi kinachowekwa ni kidogo na hakimstui mkandarasi.

2) Defect liability period ambayo ni muda ambao mkandarasi atakuwa bado anawajibika baada ya kukabidhi kazi mara nyingi ni mfupi mno. Utakuta kwenye miradi ya majengo, muda huu unawekwa wa miezi sita wakati mojawapo ya kipimo kizuri cha kuhakikisha jengo limejengwa lipasavyo ni uhimili wake wa mvua. Kama mvua ya maana haijanyesha katika muda huo ndio mshitiri ameliwa!

Upande mwingine ambao haujadiliwi sana ni wajibu wa consultants wetu. Mkandarasi mara zote anatekeleza kile alichoelekezwa na consultant kwa hiyo kama design au specifications zina matatizo toka awali hakuna ambacho mkandarasi anachoweza kufanya! Mara nyingi muda tunaotoa kwa ajili ya kufanya haya matayarisho ni mfupi mno maana focus yetu ni kuhakikisha mkandarasi anaingia kwenye site haraka iwezekanavyo. Haraka hizo zinafanya consultants wasiwe makini na hasara yake ni kubwa mno. Kwa wenzetu hapa ndipo wanapoelekeza juhudi zao. Ukiwa na design na specifications zilizo kamilika ni vigumu kwa mkandarasi makini kuharibu kazi kama atasimamiwa vizuri.

Eneo lingine linalochangia ni mshitiri(mara nyingi ni serikali) kutoelewa wajibu wake dhidi ya mkandarasi na consultant. Ucheleweshaji wa malipo pasipo na sababu na kutaka kutoa maelekezo moja kwa moja kwa mkandarasi pasipo kupitia kwa consultant kunachangia sana uzembe katika miradi yetu. Matokeo ni maombi ya extensions of time na variations kibao ambazo zinachangia sana katika kuongeza gharama ya mradi. Mshitiri akiwa makini katika ulipaji wa certificates katika wakati unaotakiwa na kufanya maamuzi yote KABLA ya hajaingia kwenye mkataba na mkandarasi kungeokoa na kurahisisha sana usimamizi wa miradi yetu. Hauwezi kumlaumu mkandarasi ikiwa analipwa miezi sita baada ya muda wa kulipa unapopita!
 
FM,

Suala hapo sio kuwapa wazawa bali kuhakikisha kunakuwa na technology transfer ambayo ina maana kubwa zaidi ya kuwapa wazawa.

Kwa mfano ukiwapa mradi KAJIMA basi wanaungana na kampuni ya TZ ambayo hata ina asilimia 20. Hawa Wazawa wanajifunza kuanzia tendering process mpaka kusimamia, kujenga na kumanage project.

Kinachonisikitisha nyumbani ni haya mawazo ya kukimbilia solutions za haraka haraka badala ya kuwa na long term strategies. Unaweza kuogopa cost leo lakini madhara yake ni kuingia cost kubwa sana hapo baadaye.

Mkuu Mtanzania, ukweli ni kwamba apart from the fact kuwa kuna ka unwritten law kwenye Consultancy industry in Tanzania kuwa "Foreign Registered Firms lazima waingie ubia na Local Firms", still Local Firms zetu bado zinasuasua sana kutoa qualified personnel in the field.... Mfano rahisi jiulize how many qualified Pavement Engineers, Traffic Engineers etc wapo hapa nchini kuweza ku compete na Foreign chaps?? So pamoja na kupewa pasi hii still Local Engineers tunaishia kwenye minor works kama structural condition surveys, traffic counts, axle load surveys etc.... Hii ni based on experience Mkuu....

Kingine kuhusu issue ya wazawa kujiunga na makampuni ya nje.... Mfano ulioutoa wa Kajima, Mkuu hapo ndipo penye sababu Kajima mwishoni aliiwezesha kampuni inaitwa Estates ya kule Mbeya... Hawa Estates wamekuwa Sub-Con wa Kajima wa muda mrefu na wamekuwa anafanya kazi nyingi sana za Kajima... Sasa swali ni kuwa je Estates ni ya wazawa, kwangu jibu ni ndiyo (hata kama ni of Asian Origin lakini ni wazawa wa Tz)!! wale waliweza kujiunga na Kajima among other things ni wka vile walikuwa na capital amabayo ilikuwa rahisi wao kuwezeshwa, ni wanagapi wenye kuweza hili??

Wakuu haya ni mawazo yangu tuu.....
 
Mkuu Mtanzania, ukweli ni kwamba apart from the fact kuwa kuna ka unwritten law kwenye Consultancy industry in Tanzania kuwa "Foreign Registered Firms lazima waingie ubia na Local Firms", still Local Firms zetu bado zinasuasua sana kutoa qualified personnel in the field.... Mfano rahisi jiulize how many qualified Pavement Engineers, Traffic Engineers etc wapo hapa nchini kuweza ku compete na Foreign chaps?? So pamoja na kupewa pasi hii still Local Engineers tunaishia kwenye minor works kama structural condition surveys, traffic counts, axle load surveys etc.... Hii ni based on experience Mkuu....

Kingine kuhusu issue ya wazawa kujiunga na makampuni ya nje.... Mfano ulioutoa wa Kajima, Mkuu hapo ndipo penye sababu Kajima mwishoni aliiwezesha kampuni inaitwa Estates ya kule Mbeya... Hawa Estates wamekuwa Sub-Con wa Kajima wa muda mrefu na wamekuwa anafanya kazi nyingi sana za Kajima... Sasa swali ni kuwa je Estates ni ya wazawa, kwangu jibu ni ndiyo (hata kama ni of Asian Origin lakini ni wazawa wa Tz)!! wale waliweza kujiunga na Kajima among other things ni wka vile walikuwa na capital amabayo ilikuwa rahisi wao kuwezeshwa, ni wanagapi wenye kuweza hili??

Wakuu haya ni mawazo yangu tuu.....

Mkuu,

Nimekuelewa lakini bado tatizo ni lile lile la serikali isiyo na long term strategies. Suala la kuwawezesha Wazawa haliishii kuwapa nafasi za kushiriki kwenye tendering process. Ni pamoja na kuwawezesha kifedha.

Ni pamoja na kushirikiana kwa karibu na hivyo vyama kwa mfano vya Wahandisi kutambua weaknesses zilizopo na namna ya kuzirekebisha. Kwa mfano kama kuna watalaamu hatunao, tunashindwa nini kusomesha wakati kuna vijana wengi tu wenye uchu wa elimu?

Angalia mfano wa China, makampuni mengi yanayokuja Afrika sasa yanapewa kila kitu chini ya udhamini wa serikali ya China. Wanapewa mikopo nafuu sana, wanasaidiwa na serikali kutumia contacts za kisiasa kuzishawishi nchi husika ili warekebishe baadhi ya sheria za nchi nk.

Tupende tusipende ni kosa kubwa kwa nchi maskini kuendelea kutegemea wageni kwa kila kitu. Ni nchi za West chache sana ambazo makampuni yao yamekuwa na uwezo mkubwa kiasi kwamba hata ukiruhusu ushindani wa asilimia 100 kunakuwa hakuna matatizo.

Kila nchi zingine zote zinazoendelea, lazima kuwe na juhudi ya kuwasaidia Wazawa ili washiriki kwenye uchumi wa nchi yao.

Bahati mbaya kwa Tanzania mgeni ana nafasi ya kusaidiwa kuliko Mtanzania mwenzetu. Hii ni kila sehemu kuanzia juu mpaka chini.

Tutaendelea kusema makampuni yetu ni ya Wababaishaji lakini ukweli ni kwamba wanasiasa wetu ndio wababishaji na matokeo yake wanajenga jamii ya Watanzania ya wababaishaji.

Ukiniuliza mimi nikuambie ninavyowaona Watanzania wa leo, zaidi ya asilimia
80 ya Watanzania ninaoonana nao Tanzania na nje ya nchi ni Wababishaji tu. Inafika mahali mtu unakuna kichwa, inakuwaje watu kama hawa wanapanda mpaka kufika huko juu.

Kuleta maendeleo sio kazi ndogo, lazima sisi kama nchi na kama mtu mmoja mmoja tukubali kuchukua maamuzi magumu, hata kama yatakuwa na uchungu wa mwarobaini hapa mwanzoni lakini angalau yawe na positive impacts kwa siku za mbeleni.

Mfumo wetu mzima wa siasa na uchumi ni ubabaishaji mkubwa sana. Matokeo yake kila mmmoja wetu anamwona mwingine ni mbabaishaji wakati kiukweli karibu sisi wote ni wababaishaji na hatutaki hata kubadilika. Tunakimbilia
majibu ya haraka haraka kwenye mamambo magumu ya kitaifa.

Ukiona rais wa nchi anaongea hivyo, hawa wa chini je? Tusahau wazo la maisha bora kwa kila mtanzania.
 
Hivi hizi tenda za miradi mbali mbali huwa zinapelekwa Ikulu kwanza Rais azipitie ndipo zipitishwe au?
 
Wakuu hapo naomba nipingane na sababu zilizotolewa kwamba eti ni bei inasababisha yote haya.... Jamani kwa wale tunaofahamu mambo ya procurement of these jobs ni kwamba kabala hujajua jamaa ni cheap au expensive lazima uwe ushampitisha kuwa yeye ni mzuri... Sasa hili la bei rahisi na kazi mbovu ina maana:
1. Wanafungua tender documents kiholela - Kimsingi/kiutaratibu ni kwamba kwanza unafungua "Technical Proposal" then unafungua "Financial Proposals" only from qualified only those technically qualified firms!! Sasa kama mmeangalia mkaona jamaa ni mbangaizaji who open his financial??

2. Our Technical requirements set forth in our bids are very poor kiasi kwamba hata mimi Maasai nisiyekuwa na ujuzi wala pesa for that case ninaweza kuwa qualified.....

3. Hawa wakuu wanajua kipengele kinaitwa "Liquidated Damages" amabcho kinaendana sambamba na "Out put/stage based payment based on certificate/inspection" ambapo kuna minimum na mazimum payments za kumlipa kandarasi kwa kuzingatia muda, production and bila kusahau kuwa kuna "Performance Bond"??

Sasa wakuu ili niweze kuwakubalia hao jamaa kuwa kuchagua rahisi ndio expensive lazima wanihakikishie kuwa hayo mawili hapo juu sio ndio wachawi wetu kwenye sekta hii... Wao lazima wakubali kuwa wao wenyewe ndio tatizo sio hata yule kandarasi aliyeshindwa kazi sababu walipmitisha kuwa technically - Manpower, equipments, materials source, technical capacity, time schedule etc were all complient to technical requirement!!!!!

Jamani tutaendelea kuwasikiliza hawa jamaa na vijisababu vyao uchwara mpaka lini?? Mbaya zaidi ni pale amabapo wameshamdanganya hata Rais kuwa eti ni kutaka cheap ndipo kumetuponza wakati we all know kuwa kama sio 10% then ni kutokujua kabisa??

Naomba kuwakilisha!!!
SOBAI PAPA MKUU UNATISHA KEEP IT ON.
 

Mkuu Mtanzania,
Naelewa sentiments zako lakini ukifanya kazi na wengi wa makandarasi wetu wazawa unaweza kulia! Wengi hawaambiliki na hawakawii kusingizia kuwa ulikuwa unadai rushwa unapowakosoa. Badala ya kutaka kujijenga professionally wao wanaona cha muhimu zaidi ni kuwaweka sawa washitiri! Wako wachache ambao kweli wanajitahidi. Na hawa ndio wanaoshirikishwa na hayo makampuni makubwa maana wako tayari kujifunza. mimi naamini mojawapo ya matatizo makubwa kwetu ni kutokutaka kuambiana ukweli. Tunadai upendeleo bila hata kuonyesha nia ya kujitahidi ili tu'deserve' huo upendeleo. Mwisho wa siku, ni yule anaye'deliver' ndiye atakayebaki anasimama. Unfortunately, hatuna luxury ya kuwabeba wanaokataa kubebwa. Responsibility yetu ni kwa jamii nzima na si kisekta kimoja. Naamini hao makandarasi wababaishaji wakiona kuwa tuko serious, watajirekebisha. On the other hand as long as wanajua kuwa madai yao ya upendeleo kwa ajili tu wao ni wazawa yanasikilizwa hawata kuwa na sababu ya kujirekebisha.
 

Mkuu Mtanzania,
Naelewa sentiments zako lakini ukifanya kazi na wengi wa makandarasi wetu wazawa unaweza kulia! Wengi hawaambiliki na hawakawii kusingizia kuwa ulikuwa unadai rushwa unapowakosoa. Badala ya kutaka kujijenga professionally wao wanaona cha muhimu zaidi ni kuwaweka sawa washitiri! Wako wachache ambao kweli wanajitahidi. Na hawa ndio wanaoshirikishwa na hayo makampuni makubwa maana wako tayari kujifunza. mimi naamini mojawapo ya matatizo makubwa kwetu ni kutokutaka kuambiana ukweli. Tunadai upendeleo bila hata kuonyesha nia ya kujitahidi ili tu'deserve' huo upendeleo. Mwisho wa siku, ni yule anaye'deliver' ndiye atakayebaki anasimama. Unfortunately, hatuna luxury ya kuwabeba wanaokataa kubebwa. Responsibility yetu ni kwa jamii nzima na si kisekta kimoja. Naamini hao makandarasi wababaishaji wakiona kuwa tuko serious, watajirekebisha. On the other hand as long as wanajua kuwa madai yao ya upendeleo kwa ajili tu wao ni wazawa yanasikilizwa hawata kuwa na sababu ya kujirekebisha.


FM,

Hapa ndipo panaponitatiza kuhusu Tanzania yetu. Kila mtu anasema watu wetu
hawabebeki, hawajituma, wanaongea tu.

Mimi siko Tanzania kwahiyo sina uhakika sana na baadhi ya mambo. Ila kwa kutumia mfano wangu najua kwamba kwa Watanzania tunaangushana sisi wenyewe kwa wenyewe.

Mimi nimehangaika sana kwenye hizo ofisi za serikali, TRA, mabank ya Tanzania. Kuna hata kejeli zingine unapewa na mtu ambaye hata hajui nini maana ya biashara.

Bahati nzuri wengine sio wakata tamaa na hatukubali kuwa bullied, tunaendelea mbele kupambana. Aidha ile ahadi ya mwana TANU ya kwamba sitakubali kutoa au kupokea rushwa ilituingia kichwani. Matokeo yake ni kukwamishwa huku na huku.

Ninachotaka kusema ni kwamba kila shilingi ina pande mbili. Hao tinaowaita wababaishaji si ajabu system ndio imewafanya wawe wababaishaji.

Kwa msimamo wangu quality ni paramount, ubabaishaji kwenye kazi yoyote ile haukubaliki hata siku moja. Ninachotofautiana na wengine ni kwamba mimi naamini kuna solutions za kuwasaidia hawa Watanzania wasiwe wababaishaji. Kuna watakaoshindwa lakini wapo wengi watakaofanikiwa. Ndio maana nikaongelea technology transfer.

Kutokana na mihangaiko yangu TZ na pia kazi yangu huku Ulaya ambayo inanipa nafasi ya kusimamia baadhi ya projects za maana kwenye telecom hapa Europe, nina uhakika kabisa matatizo ya ubabaishaji TZ yanaweza kupungua sana kama kila mshiriki atakuwa na nia njema ya kuwasaidia wahusika.

Mtu aliyekaa na hawa wazungu kwa muda mrefu kama sisi wengine, anajuwa wazi walivyo wajinga, bahati nzuri kwa wenzetu systems zao ndio ziko smart kiasi kwamba hata wajinga wanaonekana werevu. Laiti Watanzania wachache wenye nafasi, wengi wao wakiwa hata members hapa JF, wangetumia nafasi zao hizo kusaidia Tanzania iendelee, tungeweza kusogea mbele.

Miaka mitano ijayo ninategemea kutunga kitabu kwa kutumia experience yangu
juu ya ujinga wa Mtanzania. Tanzania imeoza kuanzia chini mpaka juu, hata tubadili uongozi wa juu bado itatuchukua miaka mingi sana kabla ya kuanza kuona mabadiliko ya kweli.
 
Hapa ndipo panaponitatiza kuhusu Tanzania yetu. Kila mtu anasema watu wetu
hawabebeki, hawajituma, wanaongea tu.


Sio wote, Mkuu, ambao hawabebeki. Wako ambao wanajitahidi na kweli mara nyingi ni system inayowaangusha. Tatizo ni hizi blanket solutions ambazo zinawafanya wengi wetu kudai kupendelewa bila kuonyesha jitihada zako hata kidogo. Unfortunately, wengi wako hivyo.

Mimi ninachosema ni kuwa tutangulize responsibility amasivyo tutajenga taifa ambayo iko addicted kwa hand-outs. Pawe na vipimo na mpango wowote wa upendeleo ijulikane tangu mwanzo ni wa mpito tu. Katika hii global world hatuwezi kutegemea kulindwa maisha yetu yote.
 
Watanzania, tufike mahali pa kutokulaumu kwa kila jambo, Kikwete hana vichwa mia!! na hana mikono mia, Unajua ukiwa nyumbani kwako na mitoto mijambazi, kila ukijipindua tu, imepita na kijiko! oooooo!!! mara sufuria, haujakaa sawa godoro! Kikwete anajitahidi sana ila hii mijamaa imemzidi nguvu, nafikiri ajipange upya, kila kukicha utasikia hili mara lile, jamani huyu naye ni mwanadamu. Hivyo tusishangae kwa kauli anazosisitiza, hii yote ni kutaka kunusuru pesa zetu, najua mtabisha.
 
Watanzania, tufike mahali pa kutokulaumu kwa kila jambo, Kikwete haja vichwa mia!! na hana mikono mia, Unajua ukiwa nyumbani kwako na mitoto mijambazi, kila ukijipindua tu, imepita na kijiko! oooooo!!! mara sufuria, haujakaa sawa godoro! Kikwete anajitahidi sana ila hii mijamaa imemzidi nguvu, nafikiri ajipange upya, kila kukicha utasikia hili mara lile, jamani huyu naye ni mwanadamu.

Isayamwita,

Nimecheka sana huu ujumbe wako.

Uko sahihi kabisa, Tanzania ya leo karibu kila mtu ni jambazi tu.

Ila sio kweli kwamba JK anajitahidi na kazidiwa tu maana mambo kama ya EPA yako wazi mno, angeacha msumeno ukate tu.

Kiujumla tatizo la Tanzania ni kubwa mno kuliko watu wengi hapa JF tunavyoliona. Ukitaka kujua Tanzania iko vipi, uwe mtu mwenye principles na kisha jaribu kufanya kitu TZ. Unapata kizunguzungu, usumbufu mkubwa unafanywa nawatu kama sisi tu, tena ambao wengi wao wanashinda hapa JF wakiwatukana mafisadi.

Fundi Mchundo anasema tuangalie responsibilities, hiyo ni sawa wala hakuna anayepinga hicho kitu. Lakini je kama huyo mhusika hajui hata nini maana ya responsibility utafanya nini?

Ndiyo mambo ya kwamba hakuna nyanya zenye quality TZ, kwahiyo waagize nyanya toka SA. Kufundisha kundi la vijana kulima nyanya zenye quality na kufanya packaging nzuri kweli kunahitaji muda na pesa ngapi?

Hapo ndipo tunapotofautiana. Wengine tungependa serikali iwe pro-active kwa kuwasaidia Watanzania wenye matatizo ili wakuze ubora wa kazi zao na kisha waweze kushindana. Njia za kuwasaidia ziko nyingi.

Hakuna anayesema wapewe hizo kazi tu hata kama hawana uwezo.

Nyerere aliwahi kusema ni sawa na kumpiganisha Tyson na bingwa wa ngumi wa wilaya hapo TZ. Mzee wetu alikuwa sahihi. Suala ni je unamuacha huyu boxer kijana au unamsaidia ili aongeze uwezo kabla ya kumpambanisha na Tyson.
 
Mkuu,

Nimekuelewa lakini bado tatizo ni lile lile la serikali isiyo na long term strategies....Suala la kuwawezesha Wazawa haliishii kuwapa nafasi za kushiriki kwenye tendering process. Ni pamoja na kuwawezesha kifedha.

........ Kwa mfano kama kuna watalaamu hatunao, tunashindwa nini kusomesha wakati kuna vijana wengi tu wenye uchu wa elimu?.....

......Bahati mbaya kwa Tanzania mgeni ana nafasi ya kusaidiwa kuliko Mtanzania mwenzetu. Hii ni kila sehemu kuanzia juu mpaka chini.

Mkuu Mtanzania, I salute Mkuu..... Yaani umegusa kule kwenye matatizo na umeyaweka bayana.... Kwanza kabla sijajaribu kuweka my two cents on your issues above, naomba nikushukuru kwa swala zima la ubebwaji!! Hapo kaka naomba nisiongeze maneno wala chumvi lakini ni ukweli uliopitiliza kwalo!!! Nikirudi kwenye points naomba nichangie kama hivi:

1. Long term stratergy ya Serikali yetu.... Hapo kwa kweli kuna udhaifu mkubwa sana, hapa siongelei kwenye top level bali kwenye idara zetu na mfano rahisi ni ile thread iliyokuwa inahusu mambo ya budget.... Being an Engineer naamini kwamba tatizo la ku maintain barabara linakuwa gumu sio kwa kukosa ujuzi, muda, au vitendea kazi bali ni kutokana na pesa.... PESA pekee.... Lakini ile article ya TANROADS Singida shocked me kabisa... Inapofika 75% of FY imeshakatika nawe upo below 50% in expenditure of your Budget then ujue una matatizo kwenye PLANNING & STRATEGIZING!!

2. Kuhusu kusomesha watu kwa kweli hapa ndipo pagumu... Kuna vitu viwili vya kuangalia, kwanza ni kusomesha wanafunzi na pili ni kuwawezesha kutumia walichokisoma shuleni in real life.... Unfortunatelly hili la pili la uwezeshwaji linakuwa gumu sababu unakuta mtu alikuwa MoW then, kisha akapelekwa kufanya what they call "Highway Maintenance Engineering for Developing Countries".... Read the title Mkuu, kisha akirudi unategemea aje afanye miujiza ya kumzidi ujanja yule aliyesoma cutting edge technology applicable to first world na sio developing world?? Fuatilia hili utaona what I mean in this..... NO OFFENCE INTENDED IN THIS WAKUU

3. Hili la nchi kuwawezesha watu wake I give you the following examples kisha uone Tz ipo katika nafasi gani kusaidia wazawa:
i. KONIKE anapata kazi ya Kilwa Road, anaingiza vifaa duty/tax free kwamba akimaliza anaondoa vifaa vyake (akishamaliza kazi anaviuza who cares). Morani yeye ana vifaa vyake bongo, spares zina kodi na hategemi kupata exemption yoyote je kweli ataweza ku compete na KONOIKE ambaye yupo exepmted for this specific project?

ii. Morani ana wahandisi wake wa ndani wanakatwa kodi ya mapato, NSSF etc etc etc (michango ya mwenge hakuna siku hizi) amounting to around 30% of his pay.... Kampuni X ya kigeni inakuja na wahandisi inawalipa murua na kodi wanalipa ni 2.5% inaitwa withholding tax or something!!

iii. Morani ana bid kwa miradi in TZS wakati yeye kipato chake kisheria na mahesabu yake yote yapo in TZS, lakini lami and other materials ananua in $$.... With the fluctuation in TZS against Foreign currencies unafikiri Morani atakuwa stable kweli kwenye hii miradi?? Imagine anaanza $$ ikiwa at 1000tZS then contract ya 2 years in shoot mpaka 1300 TZS, Morani kila kitu yupo in TZS bali importation ni lazima in $$ je ataweza kusimama huyu Mmasai kweli?

Ni my 2 cents which may not be too good but nadhani kwangu nafikiri ni baadhi ya vitu vinavyotuumiza!!! And by the way, watu ambao wapo kwenye decission making are they held responsible and accountable in anyways incase there is a failure such as in Sam Nujoma, Manyoni Road etc? If not why???
 
Wakuu, naona baada ya Raisi kupiga mkwara kule maeneo CRB naon leo eti wanshusha lawama na mkwara kuhus Kandarasi bomu.... Duh, sijui lakini the move to me is waaaay too late and maneno matupu hayavunji mfupa.... Kama Regulator wa Kandarasi nchini CRB lazima wafanye vitu kama:
1. Periodic work site inspection kuangalia safety procedure
2. Periodic offices inspection kuhakikisha makampuni yana up to date records including registration docs etc
3. Kupandisha kandarasi mardaraja kutegemea na performance, sasa hapa wanatumia basis gani??

Kimantiki majukumu ya CRB katika industry ni mengi sana (apart from those few stated) ambapo before they even piga mkwara they should be able to pre-empt matatizo and issue warnings to the public/clients

Article yenyewe ni kwenye Tanzania Daima la leo hii hapa chini

CRB yawajia juu makandarasi
na Ratifa Baranyikwa

SIKU chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwashutumu makandarasi kwa kutotimiza wajibu wao, Bodi ya Usajili ya Makandarasi nchini (CRB), imesema kuwa haitasita kuwafutia usajili na hata kuwafukuza kazi makandarasi wazembe.

Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake jana kuhusiana na suala hilo, Msajili wa bodi hiyo, Boniface Muhegi, alisema kuwa wao kama bodi wanaungana na Rais Kikwete kuwakemea makandarasi wazembe.

"Tunawaomba waajiri wanaoingia mkataba watupe taarifa… tukifanya uchunguzi, tukigundua tatizo ni mkandarasi, hatutasita kufuata sheria, ili tubaki na wale wanaozingatia sheria," alisema.

Alisema kuwa makandarasi lazima wafanye kazi kwa kuzingatia mikataba yao, hususan kwa kukamilisha kazi katika muda uliopangwa.

Aidha, akizungumzia kuhusu kile kilichotokea Singida hadi kusababisha Rais kuwakemea makandarasi, Muhegi alisema kuwa barabara iliyojengwa kuanzia eneo la Isuna hadi Mwanza, haina matatizo na kazi imefanyika vizuri, lakini tatizo ni kuanzia Isuna kurudi nyuma, ambako kazi ya kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo ilichelewa kutokana na kubadili makandarasi.

[I]Courtesy:[/I]http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/5/8/habari21.php
 

Mfano................

1) liquidated damages........

2) Defect liability period..........

Upande mwingine ambao haujadiliwi sana ni wajibu wa consultants wetu. Mkandarasi mara zote anatekeleza kile alichoelekezwa na consultant kwa hiyo kama design au specifications zina matatizo toka awali hakuna ambacho mkandarasi anachoweza kufanya! Mara nyingi muda tunaotoa kwa ajili ya kufanya haya matayarisho ni mfupi mno maana focus yetu ni kuhakikisha mkandarasi anaingia kwenye site haraka iwezekanavyo. Haraka hizo zinafanya consultants wasiwe makini na hasara yake ni kubwa mno. Kwa wenzetu hapa ndipo wanapoelekeza juhudi zao. Ukiwa na design na specifications zilizo kamilika ni vigumu kwa mkandarasi makini kuharibu kazi kama atasimamiwa vizuri.

Eneo lingine linalochangia ni mshitiri(mara nyingi ni serikali) kutoelewa wajibu wake dhidi ya mkandarasi na consultant. Ucheleweshaji wa malipo pasipo na sababu na kutaka kutoa maelekezo moja kwa moja kwa mkandarasi pasipo.....Hauwezi kumlaumu mkandarasi ikiwa analipwa miezi sita baada ya muda wa kulipa unapopita!

Mkuu FM, well put in all aspect. Kuna ka small case we were working on ilikuwa ni evaluation ya "Premature Road Failure in Some Major Road in Southern African Region" hii sio Tanzania manake hapa kwetu kwa kweli vitu kama "Premature Fauilure" ni misamiati migumu na kama mradi utaishia kufeli katika kipindi kifupi kuliko ada huwa tunatumia maneno kama "Mambo ya Mungu, ni kutokana na mvua, nk nk nk".... Ile kesi kwa kifupi imegusia kwenye vipengele vyote alivyoviweka FM katika maelezo yake hapo juu... Bahati nzuri tulikuwa tuna mrepresent Client... Pamoja na kwamba kulikuwa na vitu kama alivyosema FM, "Client too pushy, Client kuingilia maamuzi, kuchelewa kwa malipo nk nk nk" ambavyo vyote vilichangia kama:
1. Client pushing kandarasi kuanza na kumsukuma kwa kasi sana kazi - Works started without detail design leading to some variations unecessairly

2. Client kuingilia baadhi ya maamuzi - again variation

3. Malipo kuchelewa - hii ilitokana upande mmoja kutokana na too many variations ambapo approvals zilikuwa zinachukua muda saana with Client/Consultant.... Sasa bahati mbaya ilinyesha mvua mapema kuliko anticipated na base course ikanyonya maji sana... Since hakukuiwa na muda wa kusubiri "Client pushing" kandarasi akapiga mzigo with approvals from consultant....

Sasa with those scenario hapo juu kilichotokea Consultant ana kesi ya kujibu "Insurance Claim" ya millions of $$ under a very funny named case of "PROFESSIONAL NEGLIGENCE"........... Mpo hapo wakuu?? So bottom line pamoja na kwamba waChina wanachemsha sana na miradi yetu hapa nyumbani, je hakuna anayejiuliza hawa waChina wanasimamiwa na nani "Consultant"..... Na hao maConsult nao mbona hatuwaongelei na kuwahukumu under "PROFESSIONAL NEGLIGENCE" sababu wao ndio vichwa hasa wa mradi?? Jamaa bahati mbaya hakuwa ready for this with things to cover him under "Professional Indemnity" so sijui kampuni hiyo watafikia wapi zaidi ya kufilisiwa..... Hii inatakiwa sana hapa nyumbani na hizi kampuni zetu nyiiiingi kama uyoga za Consultants hasa miradi ya barabara ambapo tumeishia kujenga mapitio ya maji ambayo yanaishia kuwa mahandaki after a few months (years is too much)

Naomba kuwakilisha............
 
Back
Top Bottom