Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,843
- 31,057
Kwa mambo yanayoendelea hapa nchini Kwa sasa, ni dhahiri kuwa CCM ishaanza rasmi kumnadi mgombea wake wa Urais wa mwakani, ambaye ni Samia Suluhu Hassan.
Tumeshuhudia katika ziara alizofanya majuzi kwa madai kuwa ni ziara za kiserikali katika mikoa ya Rukwa na Morogoro, ambapo ziara hizo bila mashaka yoyote ni za kampeni ya Urais wa mwakani mwaka 2025 na si za kiserikali, kama wanavyodai wenyewe CCM.
Tukizingatia kuwa ujumbe wa Rais, katika ziara hizo ulikuwa na mawaziri kadhaa na Kila wanapotembelea, kazi kubwa ilikuwa ni kuwapa nafasi hao mawaziri wake Ili waeleze miradi ambayo wameitekeleza katika maeneo yao.
Hao mawaziri wanaoambatana na Rais, hawajapungua kumi!
Najaribu kufikiria ni kwanini sasa, CCM ndiyo wameona ni muda muafaka wa mawaziri hao kunadi kazi walizozifanya na miradi waliyoiteleleza na siyo kabla ya hapo??
Niwaombe wapinzani nao wasibweteke, ni lazima waunganishe nguvu hivi sasa na wamtangaze mgombea wao wa upinzani, ambaye naye atafanya kazi Moja ya kuzunguka nchini kote na kuanza kujinadi akiwa mgombea wa upinzani, kinyume Cha hapo itakuwa "Too Late"
Nakumbuka kuwa mwaka 2015, wakati upinzani wa nchi hii, ulipotoa upjnzani mkubwa sana Kwa CCM, katika historia ya toka siasa za vyama vingi uanzishwe, mwaka 1992, nyakati hizo vyama vya upinzani viliungsnisha nguvu ya pamoja, katika umoja waliouita UKAWA, na kumweka mgombea mmoja, ambaye alikuwa marehemu Edward Lowassa.
Kitu kingine ambacho Kambi ya upinzani inapaswa ifahamu ni kuwa, wao wanalazimika kuunganisha nguvu zao Ili kupambana na hiki chama kikongwe Cha CCM ambacho kimeotesha mizizi katika vyombo vya ulinzi na usalama nchini.
Matokeo ya kuunganisha nguvu hizo Kwa upande wa upinzani, ni ushindi mkubwa sana walioupata kuanzia wenyeviti wa mitaa na vitongoji, madiwani, wabunge na hata mgombea Urais, Kwa tiketi ya UKAWA, hayati Edward Lowassa, alivuna kura nyingi (pamoja na kumuibia) ambazo hazikuwahi kupatikana katika chaguzi zote katika historia ya toka uanzishwe mfumo huu wa vyama vingi.
Ni lazima vyama vya upinzani vitambue ukweli huu kuwa UMOJA NI NGUVU na UTENGANO NI UDHAIFU
Tumeshuhudia katika ziara alizofanya majuzi kwa madai kuwa ni ziara za kiserikali katika mikoa ya Rukwa na Morogoro, ambapo ziara hizo bila mashaka yoyote ni za kampeni ya Urais wa mwakani mwaka 2025 na si za kiserikali, kama wanavyodai wenyewe CCM.
Tukizingatia kuwa ujumbe wa Rais, katika ziara hizo ulikuwa na mawaziri kadhaa na Kila wanapotembelea, kazi kubwa ilikuwa ni kuwapa nafasi hao mawaziri wake Ili waeleze miradi ambayo wameitekeleza katika maeneo yao.
Hao mawaziri wanaoambatana na Rais, hawajapungua kumi!
Najaribu kufikiria ni kwanini sasa, CCM ndiyo wameona ni muda muafaka wa mawaziri hao kunadi kazi walizozifanya na miradi waliyoiteleleza na siyo kabla ya hapo??
Niwaombe wapinzani nao wasibweteke, ni lazima waunganishe nguvu hivi sasa na wamtangaze mgombea wao wa upinzani, ambaye naye atafanya kazi Moja ya kuzunguka nchini kote na kuanza kujinadi akiwa mgombea wa upinzani, kinyume Cha hapo itakuwa "Too Late"
Nakumbuka kuwa mwaka 2015, wakati upinzani wa nchi hii, ulipotoa upjnzani mkubwa sana Kwa CCM, katika historia ya toka siasa za vyama vingi uanzishwe, mwaka 1992, nyakati hizo vyama vya upinzani viliungsnisha nguvu ya pamoja, katika umoja waliouita UKAWA, na kumweka mgombea mmoja, ambaye alikuwa marehemu Edward Lowassa.
Kitu kingine ambacho Kambi ya upinzani inapaswa ifahamu ni kuwa, wao wanalazimika kuunganisha nguvu zao Ili kupambana na hiki chama kikongwe Cha CCM ambacho kimeotesha mizizi katika vyombo vya ulinzi na usalama nchini.
Matokeo ya kuunganisha nguvu hizo Kwa upande wa upinzani, ni ushindi mkubwa sana walioupata kuanzia wenyeviti wa mitaa na vitongoji, madiwani, wabunge na hata mgombea Urais, Kwa tiketi ya UKAWA, hayati Edward Lowassa, alivuna kura nyingi (pamoja na kumuibia) ambazo hazikuwahi kupatikana katika chaguzi zote katika historia ya toka uanzishwe mfumo huu wa vyama vingi.
Ni lazima vyama vya upinzani vitambue ukweli huu kuwa UMOJA NI NGUVU na UTENGANO NI UDHAIFU