*MISEMO YA WATU WENYE WIVU/HUSDA*
1.Siwezi kununua gari kwa mkopo.
2.Huyo bwana wake ni mkubwa kuliko yeye, alifuata pesa tuu!
3.Iphone kitu gani, simu simu tuu bora mawasiliano.
4.Siwezi kula chakula cha kwenye fridge.
5.Anajifanya amesoma lakini hata haolewi.
6.Siwezi kuendesha Vits, bora nitembee kwa miguu
7.Kuolewa ni stress tuu bora nikae single.
8.Microwave inaleta cancer.
9.Anaendesha V8 halafu anaishi uswazi.
10.Hiyo nguo anajifanya amenunua laki tatu wakati ni elfu thelathini tuu kariakoo.
11.Hiyo Kazi aliipata baada ya kutembea na bosi.
12.Hata kama ana degree, maisha yake sawa tuu na yetu.
13.Kwani Mercedes ina miguu mitano, gari gari tuu!
14.Siwezi kununua gari wakati sina nyumba.
15.Anaenda gym kila siku lakini ana umbo bayaaa!
16.Anajifanya kuongea kizungu wakati kwao shamba tuu.
17.Anaringaaa! Ataachwa tuu huyo.
18.Ana umbo zuri lakini hajui kuvaa.
19.Usione amenenepa hivyo anatumia ARV.
20.Hakuna jipya kwenye ndoa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji38]UKIONA HUWA UNAWAZA NA KUSEMA MANENO HAYA, NI MAWAZO YA KIMASIKINI, UJUE UNA IBILISI WA HUSDA NDANI YA MOYO WAKO. PAMBANA NA HALI YAKO NDUGU[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]