Wakati mwingine tunachukiwa na watu kwasababu hawakupenda tuwe hivi leo

Wakati mwingine tunachukiwa na watu kwasababu hawakupenda tuwe hivi leo

Magical power

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2022
Posts
2,158
Reaction score
5,626
Wakati mwingine wanakuchukia kwasababu unavyopendwa na unakuubalika kwa watu au na mtu fulani hapo kazini/ofisini au ulipo

Yawezekana kwasababu ya connection hizo ulizonazo na namna unavyoitwa kila mahala. Yawezekana wanakuchukia kwasababu ya kipawa, neema au uwezo ulionao mkubwa kiasi kwamba wanakuona tishio kwenye maisha yao

Zipo chuki ni juu yetu kwasababu ya kukubalika kwetu au kupendwa na kuthaminiwa na watu fulani. Yawezekana kwasababu ya vipawa na neema tulizonazo ndani mwetu zmewafanya watu watuchukie au watutamanie kuanguka

Yawezekana ni kwasababu ya nafasi tulizonazo kazini au mafanikio ya wazazi au watoto wetu waliyonayo yamekuwa mwiba sana kwao ndio maana wameamua kutuinulia chuki na maapio ya kutuangusha au kuwaangusha ili wafurahie
 
UKIONA ANAKUKWEPA USIMSUMBUE TENA YAWEZEKANA HATAKI JIONGEZE TU NDUGU

Jifunze sana katika ukimya wa watu na pale ukapopuuzwa na kukwepwa kwenye hitaji lako au changamoto zako. Wakikukwepa au wakikupuuza usiwasumbue tena ili ulinde amani ya moyo wako na uone cha kufanya kwa wakati ili usipoteze focus yako kwa kuendelea kumtegemea mtu asiye muwazi kwako

Msaada si haki yako, ukiona anakukwepa basi usimsumbue tena maana wapo watu wakiombwa msaada wanataka uanze kujinyeyekeza kwake anajiona wa thamani sana kwasababu umemshirikisha au umewaomba akusaide katika hilo linakutia ugumu. Wakati mwingine Mungu anatuepusha na masimango pale tutakapofanikiwa wasije kusema nisingekuwa mimi asingekuwa. Pia, anakufundisha kujiamini na kujipambania

Ukiona anakukwepa ilihali mliahidiana muonane (aje au uende) basi usimsumbue tena katika hilo. Wapo watu huwa hawawezi kukuambia haiwezekani ila watakukwepa tu mpaka uchoke na ujiongeze.

Ukiona hapokei simu zako wala hajibu sms zako baada ya maongezi fulani mliyoongea basi hakuwa na dhati juu ya hilo. Jiongeze acha kumsunbua tena katika hilo

Yawezekana akikuambia nitafute siku fulani kwa ajili ya jambo lako ila ulipomtafuta hiyo siku hapokei simu wala hajibu sms zako juu ya hilo basi usimsumbue tena.

Yawezekana kuna kitu umemshirikisha akakiona kisha akaa kimya wala hakusema chochote inawez ikawa umemtumia ujumbe na unaonekana umeusoma na amekaa kimya basi usimsumbue tena kwa sms ikiwa amekupuuza

1739117408775.jpg
 
Wakati mwingine tunawakumbuka maex wetu si kwa uzuri wao, muonekano ila kwa matendo yao waliotufanyia nyakati zile tuliokuwa pamoja

Yako mambo ukimtendea mtu unaacha alama isiofutika. Hata akienda kwa mtu mwingine atatamani afanyiwe kama vile alivyokuwa anafanyiwa na ex wake ile kuoneshwa upendo

Kuna watu walitendewa mema na mazuri walindekezwa sana na mtu wake wa nyuma kiasi kwamba sisi tunaonekana hatufanyi kitu kwasababu sisi si wabunifu na hatuna huruma

Ukiwa na utu, upendo na huruma yapo mambo utayafanya ukihisi ni ya kawaida kwako kumbe ni makubwa sana kwa mtu unayamfanyia.

Huwa nasema, yapande mema ndani mwake hata kama ubinadamu au hali yeyote ikiingilia mahusiano yenu usifutike kwenye moyo wake, kumbukumbu zake za mambo mema uliyowahi kumfanyia kipindi kile mlipokuwa mnapendana

Mfanye aishi na mtu mwingine kimwili ila kuna mambo hatayapata kwa mtu huyo kwasababu uliyafanya kwa upendo na kiwango kikubwa kwake. Muwekee kuhuri ya mambo yale mema yasiyofutika kirahisi kwenye maisha yake yote popote atakapokuwa akukumbuke ubaki kuwa mfano wa mtu bora na mwema kwake daima

1739117465943.jpg
 
BARUA YA WAZI KWA KAKA ZANGU WAOAJI

Kaka mpendwa habari za furaha yako, habari za kila njema lako! Hongera kwa kuzaliwa mwanaume na hongera kwa mengi ambayo siwezi kuyasema hapa kwa kuandika pekee.

Leo naomba kuwaongelea yule single mother wenye THAMANI. Yawezekana mnawaogopa kwasababu fulani au mmeaminishwa vibaya na jamii zenu kuhusu single mother lakini si wote

Naomba uelewe single mother ni dada zetu, binamu zetu, mama zetu nk najua hili unalijua yawezekana hata wewe yuko mdada amekuwa single mother kwasababu yako au zake binafsi. Siwezi jua kwa nini mlitengana ila ipo sababu

KAKA ANGU MWEMA unaweza kumkimbilia asiye na mtoto na akawa AZAM TV burudani kwa wote ndani ya ndoa akakuzalia watoto wasio wa damu yako kwahiyo uswahukumu kwa mapito yao, hali zao si kila single mother ni mbaya au ana sifa za hovyo kama ujuavyo

Kaka mpendwa wapo single mother wenye THAMANI na wenye nia kweli ya kuwa wake wa mume mmoja. Wapo single mother wapambanaji na wenye uchungu na maisha, wasiojali ugumu au hali ya maisha wao wanachojua ni kuhakikisha familia inapata mahitaji. Siongelei single mom WADANGAJI

Kaka MPENDWA achana na kauli za kuwa single mother hupasha VIPORO na wazazi wenza hapana inategemea na mtazamo au huruka za mwanamke husika. Single mother mwenye THAMANI hujua THAMANI yake wala hawezi kurudia MATAPISHI. Single mother anajua kunyenyekea, kuishi kulingana na maisha yapatikanayo, anayo IMANI na pendo kubwa linalomwangika akupea hutolijutia

SWALA la kupasha viporo hata single father wapo wanaopasha viporo kwahiyo kwenye swala la kupasha viporo hata wanaume wapo wenye tabia hiyo. Kwahiyo si wanawake tu kaka wapo single mother wenye AKILI timamu wale wanaojielewa wale MALI SAFI kabisa wapo

Kaka mpendwa ukikutana na single mother anayejielewa utawashawishi hata jamaa zako wawaoe maana hawatajuta. Single mother hata akiwa na shape huwa haimpi kiburi, hata akiwa na pesa hazimpi kiburi, hata akiwa na nini hawezi kuona kuwa ni kitu cha kujivunia ila huhitaji kuiishi NDOTO yake ya kuwa mke wa mtu na mama bora wa familia atakayoipata

Kaka angu nikutoe HOFU achana na maneno ya watu kuhusu single mother kuwa hafai kuwa mke. SINGLE MOTHER na wengi wamepuvuka KIROHO na KIAKILI. Hawana pruu pruu nyingi

Kuna single mother ni wazuri kila idara kuanzia mahakamani, jikoni, kichwani (akili za maisha) hawana mambo mengi. Mapito, maumivu yao yamewafundisha na kuwajenga kuwa watu imara. Kuna single mother wanajielewa sana wanajipenda ukimpata utaenda kutoa sadaka

KAKA ANGU mwema tabia ya kupasha viporo hata asiye na mtoto anaweza kupasha viporo au kuchepuko mbona tunawoana huku mtaani sio single mother ila wanarukaruka sana na wamezaa na watu wengine wakiwa ndani ya ndoa wapo pia wanaopasha viporo na ex wao

Mbona wanawake wao hawawazii vibaya hao single father kuwa hawafai au wao wanapasha viporo mbona wanawake tunawatazama vibaya kama wao hawana akili, hawajitambui, wasaliti mkatae kwasababu yeye si chaguo lako tu kaka

HAPA SIONGELEI SINGLE MOM WADANGAJI MAKURUMBEMBE WAGALATIA ILA SINGLE MOTHER WENYE THAMANI WALE MALI SAFI


1739117533291.jpg
 
DADA ANGU MWEMA KAA MBALI NA HAO WANAUME WADANGAJI HAO OMBAOMBA

Kuna wanawake wanatumikishwa sana kwenye mahusiano wanakopwa hela sana, waachiwa madeni mwanaume anaomba hela tu ukisema huna anasusa. Dada angu huyo si mwanaume mkimbie haraka. Huyo hana malengo na wewe Mara nyingi huwa ana familia au mwanamke wake wewe amekufanya daraja, amekufanya mtaji. Kuna wanaume wanataka kuhudumiwa hao wanaume ni WADANGAJI wakubwa sana

Dada mwanaume anayekupenda hawezi kuwa mtu wa kukuambia nikopee, naomba hela nk wala hajakuoa. Ukiona hivyo jua huyo mpitaji

Kuna wakati huwa nawawazia hivi kwa nini huwa hamnisikilizi nawapa code sana ila mna tekwa akili mnatumikishwa kimwili na uchumi

Siwapi tena code mteseke, muachiwe madeni, mtumikishwe kimwili, kisaikolojia na kiuchumi

1739117600258.jpg
 
NAKUKUMBUSHA TU RAFIKI YANGU MWEMA

Usiache kupenda tena, yawezekana ajaye ndiye aliyekusudiwa kuwa wako. Ukiachana na mtu usisuse ila jisahihishe kisha daka chombo tena

Rafiki yangu penda kama hujawahi kupenda tena, jisahihishe kisha rudi tena kwenye safari ya maisha uyatamaniyo usikubali kuishia njiani kwasababu umeumizwa au umeachana na mtu baada ya kubaini huyo hakuwa sahihi kwako.

Kwasababu hakuondoka nayo basi unayo thamani kuhitajika kwa mwingine. Kama kwa nini uyasusie mahusiano. Usikubali kuishilia kwasababu ameondoka au umemuondoa kwenye maisha yako mtu asiye sahihi kwako

Usijione hufai baada ya kuondoka kwake au baada ya kumuondoa kwenye maisha yako. Ukaamua kuishilia, ukajitenga mahusiano

Bado unayo thamani ya kufurahia mahusiano wala usijione wewe ni wa fungu la kukosa tu. Jisahihishe kisha daka ingia tena maana hajaondoka nayo ameondoka na yake

Muhimu uwe nayo tu kisha jipende, jithamini na ujiongezee thamani na uwe mtu na nusu. Utapendwa tu wala usiendee kulialia au kususa

1739117695792.jpg
 
DADA ANGU MWEMA KAA MBALI NA HAO WANAUME WADANGAJI HAO OMBAOMBA

Kuna wanawake wanatumikishwa sana kwenye mahusiano wanakopwa hela sana, waachiwa madeni mwanaume anaomba hela tu ukisema huna anasusa. Dada angu huyo si mwanaume mkimbie haraka. Huyo hana malengo na wewe Mara nyingi huwa ana familia au mwanamke wake wewe amekufanya daraja, amekufanya mtaji. Kuna wanaume wanataka kuhudumiwa hao wanaume ni WADANGAJI wakubwa sana

Dada mwanaume anayekupenda hawezi kuwa mtu wa kukuambia nikopee, naomba hela nk wala hajakuoa. Ukiona hivyo jua huyo mpitaji

Kuna wakati huwa nawawazia hivi kwa nini huwa hamnisikilizi nawapa code sana ila mna tekwa akili mnatumikishwa kimwili na uchumi

Siwapi tena code mteseke, muachiwe madeni, mtumikishwe kimwili, kisaikolojia na kiuchumi

View attachment 3230621



OK ok
 
WAKATI MWINGINE TUNACHUKIWA NA WATU KWASABABU HAWAKUPENDA TUWE HIVI LEO

Wakati mwingine wanakuchukia kwasababu unavyopendwa na unakuubalika kwa watu au na mtu fulani hapo kazini/ofisini au ulipo

Yawezekana kwasababu ya connection hizo ulizonazo na namna unavyoitwa kila mahala. Yawezekana wanakuchukia kwasababu ya kipawa, neema au uwezo ulionao mkubwa kiasi kwamba wanakuona tishio kwenye maisha yao

Zipo chuki ni juu yetu kwasababu ya kukubalika kwetu au kupendwa na kuthaminiwa na watu fulani. Yawezekana kwasababu ya vipawa na neema tulizonazo ndani mwetu zmewafanya watu watuchukie au watutamanie kuanguka

Yawezekana ni kwasababu ya nafasi tulizonazo kazini au mafanikio ya wazazi au watoto wetu waliyonayo yamekuwa mwiba sana kwao ndio maana wameamua kutuinulia chuki na maapio ya kutuangusha au kuwaangusha ili wafurahie
Mda mwingne wala hakuna anaekuchukia wala kujali kuhusu wewe ni kujishtukia tu.
 
Back
Top Bottom