Wakati Rais Magufuli amegoma kusaini hukumu za waliohukumiwa kifo Rais Trump ameendelea kunyonga hadi wiki yake ya mwisho!

Hata wafungwa wa federal government Rais hafanyi hiyo kazi ya kusaini wanyongwe, anayeidhinisha ni mwanasheria mkuu. Rais anaweza kutoa msamaha kutonyongwa kama akijisikia.
We ndio hujui,kuna wafungwa wamehukumiwa na federal government na waliohukumiwa na state governments.hao wanaoidhinishwa kunyongwa na magavana walihukumiwa na state governments.
 
Ishu sio kufungwa na federal govt,lakini kuna aina ya mauaji ambayo federal govt ndio huwa inaidhinisha kisho.
Ngoja nikuelimishe..iko hivi,kama wewe ni mkazi let's say wa Jimbo la Texas,ukaenda kufanya uhalifu jimbo la California,hiyo case utashtakiwa katika federal court. But ukifanya uhalifu kwenye state yako unayoishi bas hiyo case utashtakiwa katika mahakama za state husika.ni hivyo tu mkuu.
 
Hata wafungwa wa federal government Rais hafanyi hiyo kazi ya kusaini wanyongwe, anayeidhinisha ni mwanasheria mkuu. Rais anaweza kutoa msamaha kutonyongwa kama akijisikia.
Nakubaliana na wewe mkuu.
 
Pia Ukifanya kosa kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya federal government kama kambi za jeshi, national park ni federal cases
 
Athabu ya kifo ni adhabu ya kipumbavu kuliko zote.

Funga mtu kifungo cha maisha afie huko
Ila wewe jambazi akuuwe na familia yako ibaki kwenye mateso wakati yeye jambazi akiendesha familia yake kwa remote!
 
Katika mifuasi ya Ccm hili jamaa ni pumbavu namba moja. Sasa kuna uhusiamo gani wa death penalty huko Usa na hapa Tanzania
Kabisa mkuu. Sheria ya kunyonga ya Marekani ni sheria ya majimbo (states) na kuna majimbo mengine hayana adhabu ya kifo. Rais wa Marekani hahusiki na adhabu ya kunyonga. Hiki kijamaa kilicholeta hii thread ni kipumbavu kisichoelewa chochote bali kimekurupuka tu kujiandikia baada ya kuona kwenye taarifa za habari za CNN, Aljazeera na media kubwa za kimataifa.
 
Wangekuwa wamehukumiwa kunyongwa kina Lissu huko, angesaini siku hiyo hiyo.

Hao wafungwa hawana maslahi naye tu ya kisiasa na madaraka.
 
Kamanda Mbwakachoka by Muroto!
 
Kuidhinisha mtu kuuwawa siyo lazima kutia saini tu, hata maelekezo ya ishara au kwa lugha ya mafumbo yote ni uuaji tu.
 
Serikali ya Marekani haina msemaji zaidi ya Trump, sasa nitabishanaje na mtu ambaye hajawahi kuwepo,yuko kwenye fikra zako tu!
Achana na hili bumunda limeamka na kilevi cha mitaputapu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…