Wakati unatibu majeraha yako nyamaza. Kuna watu hawakuelewi na kamwe hawatokuelewa

Wakati unatibu majeraha yako nyamaza. Kuna watu hawakuelewi na kamwe hawatokuelewa

Daudi Kempu

Member
Joined
Dec 6, 2024
Posts
26
Reaction score
56
Kadri unavyoendelea kujieleza kwa watu wasiokuelewa, ndivyo unavyoongeza nafasi ya wao kukuumiza ama kukifumua kidonda chako upya.

Mtu asiyekuelewa, atajitahidi kukuonyesha kila kinachokukuta ni uzembe na makosa yako mwenyewe.

Mtu asiyekuelewa, atakuhukumu, atakufanya ujishuku na pengine utaanza kujihukumu na kupuuza mchakato wako wa kujiponya.

Mtu asiyekuelewa ni wazi hakuamini, hata ukimwambia unapambana kuushona moyo wako uuvae tena, atakukatisha tamaa, atakwambia huwezi.

Mtu asiyekuelewa, atakukosea na abadani hatoona kosa lake; kuna mara ataona alikukosea kwakuwa ulitaka akukosee.

Nyamanza tu, ikibidi kuongea wakati wa mchakato, ongea na mtu mmoja anayekuelewa, atakayekwambia una nguvu na uwezo wa kupona na kusonga mbele.

Wakati mwingine, hata mgonjwa anachohitaji ni kuambiwa inuka uende na si jicho la huruma lisilo na imani.

Katika hali yoyote unayopitia mpendwa, inuka, angalia ulipo chanika, jishone, songa mbele.

Ikiwa unapumua, tambua kuwa, unayo nafasi ya kukabili na kubadili chochote. Usijikatie tamaa.
 
Kadri unavyoendelea kujieleza kwa watu wasiokuelewa, ndivyo unavyoongeza nafasi ya wao kukuumiza ama kukifumua kidonda chako upya.

Mtu asiyekuelewa, atajitahidi kukuonyesha kila kinachokukuta ni uzembe na makosa yako mwenyewe.

Mtu asiyekuelewa, atakuhukumu, atakufanya ujishuku na pengine utaanza kujihukumu na kupuuza mchakato wako wa kujiponya.

Mtu asiyekuelewa ni wazi hakuamini, hata ukimwambia unapambana kuushona moyo wako uuvae tena, atakukatisha tamaa, atakwambia huwezi.

Mtu asiyekuelewa, atakukosea na abadani hatoona kosa lake; kuna mara ataona alikukosea kwakuwa ulitaka akukosee.

Nyamanza tu, ikibidi kuongea wakati wa mchakato, ongea na mtu mmoja anayekuelewa, atakayekwambia una nguvu na uwezo wa kupona na kusonga mbele.

Wakati mwingine, hata mgonjwa anachohitaji ni kuambiwa inuka uende na si jicho la huruma lisilo na imani....

Katika hali yoyote unayopitia mpendwa, inuka, angalia ulipo chanika, jishone, songa mbele.... ikiwa unapumua, tambua kuwa, unayo nafasi ya kukabili na kubadili chochote. Usijikatie tamaa..
una maumivu gani ndugu
 
binadamu inabid tupitie katika kila jaribio ili kukufanya imara
kweli huwezi kumsema mtu aliyetendwa na mapenz akataka kujiua
na wengi wanaoelewa dunia hii vitu vyote vya mwili havikai ni kama upepo yawe mapenz pesa kitu chochote unachokiona wewe kina muda mfupi wa kuishi
usiteseke eti kisa huna mtoto pesa nyumba hapana
tafuta amani tafuta upendo jitafute utaona Nuru na Nuru ni Yesu kristo kutoka kuumbwa kwa dunia ..
 
binadamu inabid tupitie katika kila jaribio ili kukufanya imara
kweli huwezi kumsema mtu aliyetendwa na mapenz akataka kujiua
na wengi wanaoelewa dunia hii vitu vyote vya mwili havikai ni kama upepo yawe mapenz pesa kitu chochote unachokiona wewe kina muda mfupi wa kuishi
usiteseke eti kisa huna mtoto pesa nyumba hapana
tafuta amani tafuta upendo jitafute utaona Nuru na Nuru ni Yesu kristo kutoka kuumbwa kwa dunia ..
Amina ubarikiwe sana
 
Back
Top Bottom