Wakati wa mvua na mafuriko Dar es Salaam ndipo somo kwamba madaraja ya baharini sio kipaumbele cha kwanza kwa wakazi wa Dar litaeleweka!

Wakati wa mvua na mafuriko Dar es Salaam ndipo somo kwamba madaraja ya baharini sio kipaumbele cha kwanza kwa wakazi wa Dar litaeleweka!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Wanasiasa wa upinzani wanapotoa maoni kwamba kuna vitu vya lazima na msingi zaidi kufanyika Dar es Salaam badala ya kujenga madaraja ya kupita juu ya bahari, huwa wanabezwa sana. Hatukatai hizi flyover zinasaidia sana kupunguza adha ya foleni Dar es Salaam lakini lazima tukiri kwamba flyover sio suluhisho lenye umuhimu sawa na tatizo ambalo linakuwa janga kwa Dar es Salaam, ambapo watu hupoteza maisha na mali zao.

Ni lini ulisikia wakazi wa Dar es Salaam wamepoteza maisha na mali zao kwa ajili ya foleni za Dar za asubuhi na jioni?

Labda sasa wakati wa mvua hizi zinazozaa mafuriko na kuleta majanga ya kupoteza mali za watu na hata maisha, ndipo Watanzania taelewa kwamba madaraja ya kupita juu ya bahari lili Dar es Salaam iwe kama Uaya hayana umuhimu au uharaka kiasi hicho.

Na labda jambo la kukumbuka ni kwamba gharama za daraja moja tu hili la kupita juu ya bahari hapa Dar ni kubwa sana za ukilinganisha na fedha zinazotakiwa kurekebisha miundombinu ya Dar ili watu wasipatwe na majanga wakati mvua za mafuriko zinapotokea.

Kwa hiyo wale mnaoshabikia madaraja ya kuifanya Dar iwe kama Ulaya msilalamike na haya mafuriko - kupanga ni kuchagua, na nyie ndio mnaosema wapinzani wanapinga kila kitu. Sasa ndipo mtajua wapinzani hawapingi kila kitu, bali wanapinga kila uamuzi wa kipuuzi unaofanyika.

1602833423904.png
 
Vipaumbele vya Nchi ni SIFURI. Kuiua Chadema, kununua wanasiasa malaya, kununua ndege kwa trillioni mbili ambazo sasa zinaingiza hasara ya mabilioni, kujenga aiport chato inayotumiwa na mtu mmoja tu na madudu mengine chungu nzima.
Nashauri hawa watu wakapite kwenye flyover kukwepa hii kadhia ya mafuriko!
 
Mvua zinanyesha kwa msimu but foleni ipo mwaka mzima! Hasara inayosababishwa na foleni nikubwa ukilonganisha na mafuriko pia watu tunawaambia hameni mnang'ang'ania alafu mnakuja kipiga kelele hapa.
Foleni inasababisha hasara kwa watu gani?

Unajua hasara wanayopata watu wakati wa mafuriko ni kubwa kiasi gani unapojumlisha wote? Na wanaopoteza maisha utalinganisha na hasara ya foleni?

Na unatakiwa uelewe somo tunapoongelea vipaombele. Hatusemi usijenge flyover, bali nini kinatakiwa kwanza.
 
Mkuu shida siyo hayo madaraja na ma-flyover,shida ipo kwenye Policy(sera)za nchi,leo nilimsikiliza muheshimiwa Rais kwenye kampeni pale Kawe akiwaambia wananchi wa kawe kwamba serikali itatoa bilioni 5 kwa ajili ya marekebisho ya miundombinu nadhani ya kawe,.

Hapa ndipo tatizo lilipo,haiwezekani Jiji la Dar es salaam halina mamlaka yake kisera na kikanuni ya kufanya mambo yake ya maendeleo mpaka Rais aamue nini wafanye! This is Big problem!

Sasa fikiria kama Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuamua ni nini afanye wapi na kwa wakati gani,we unadhani tutafika? Majiji au mikoa yote ilipaswa yajiendeshe kwa mapato yake ya ndani kwa ajili ya maendeleo ya mkoa /jiji husika, serikali kuu ilipaswa ifanye mambo makubwa ya nchi lakini haya ya miundo mbinu,mitaro na madaraja ya hapa Dar es Salaam ilipaswa yafanyike pasipo kuingiliwa na serikali kuu!! VINGINEVYO DAR ES SALAAM ITAENDELEA KUWA JALALA, DAMPO, SHIMO LA MAJI TAKA MPAKA TUKOME!

Kila kitu kwenye hii nchi kimekaa kisiasa,hata kama kinajengwa kidaraja kidogo tu lazima utawakuta watendaji wa serikali wakisifia sana

"TUNAMSHUKURU RAIS MAGUFULI KWA KUTUPATIA HIZI MILIONI 50 KWA AJILI YA UJENZI WA ILI DARAJA, WANANCHI WAMETESEKA KWA MUDA MREFU NA HAWAKUWA NA MTETEZI, ILA RAIS MAGUFULI NI KIONGOZI WA WANYONGE, KAWAKUMBUKA WATU WA NACHINGWEA" Aisee hizi kauli huwa sizipendi hata kidogo!
 
Foleni inasababisha hasara kwa watu gani?

Unajua hasara wanayopata watu wakati wa mafuriko ni kubwa kiasi gani unapojumlisha wote? Na wanaopoteza maisha utalinganisha na hasara ya foleni?

Na unatakiwa uelewe somo tunapoongelea vipaombele. Hatusemi usijenge flyover, bali nini kinatakiwa kwanza
Mkuu unauliza foleni inasababisha hasara gani kwa watu?!
 
Kimsingi kabla ya kuanza project ya Salenda, walipaswa kuanza na ngoma hii ya jangwani.

Inafedhehesha mji sana hii kitu ya jangwani. Mafuriko ya jangwani naona ndiyo yanatudharirisha zaidi.
Ingekuwa wewe ndio Rais hao watu wa jangwani ungewasaidiaje kwa mfano?

Maana hao walishaambiwa wahame hapo hilo eneo sio zuri kwa makazi ya watu na wakapewa viwanja mabwepande wakauza na kurudi tena hapo jangwani ili mradi tu wakae karibu na mjini.
 
Vipuambele vya Nchi ni SIFURI. Kuiua Chadema, kununua wanasiasa malaya, kununua ndege kwa trillioni mbili ambazo sasa zinaingiza hasara ya mabilioni, kujenga aiport chato inayotumiwa na mtu mmoja tu na madudu mengine chungu nzima.
[emoji275][emoji275][emoji275]
 
Nashauri hawa watu wakapite kwenye flyover kukwepa hii kadhia ya mafuriko!

View attachment 1599999
Mbowe angefanya nini? Kama hata ofisi ya makao yake makuu ni kama kibanda tu. Majimbo kama, Kawe, Ubungo, kibamba Chadema mmeyabagaza Sana, mmekula pesa hizi hizi za Magufuli mpaka kwa miguu wapuuzi kweli. Watanzania tunauhakika, chama cha Mbowe hakina uwezo wa kuwasaidia watanzania. Endeleeni kunywa faru John zenu, tumewachoka hasa.
 
Kwa hiyo wale mnaoshabikia madaraja ya kuifanya Dar iwe kama Ulaya msilalamike na haya mafuriko
Kweli kabisa, tena waambie na wale wanaolalamika foleni wasiendelee kulalamika maana jitihada za kuondoa foleni wanazibeza. Maana nimekuta mada eti wanasema wana jambo lao tarehe 28 wakati wanakuja kusema umu JF flyover ya Ubguno haimsaidii mtu wa Bukoba 😀
 
Mbowe angefanya nini?. Kama hata ofisi ya makao yake makuu ni kama kibanda tu. Majimbo kama, Kawe, Ubungo, kibamba Chadema mmeyabagaza Sana, mmekula pesa hizi hizi za Magufuli mpaka kwa miguu wapuuzi kweli. Watanzania tunauhakika, chama cha Mbowe hakina uwezo wa kuwasaidia watanzania. Endeleeni kunywa faru John zenu, tumewachoka hasa.
CCM wasitambe kabisa kuwa na maofisi makubwa na assets nyingi. Mwanzao wao ni tofauti sana na Chadema. Katika nchi inayojali utawala wa Sheria, mali zote za CCM hadi kufikia kuingia mfumo wa vyama vingi zilipaswa kupewa halmashauri za miji.

Kwa hili CCM waone aibu kabisa kuwasema wapinzani.
 
Akili hizi ndio mmawashangaa viongozi wenu na kutegemea siku moja mafuriko yataisha.

Yaani wapuuzi wameamua kukaa bondeni,zisijengwe barabara eti tufanyeje?

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Kwani mafuriko ya Dar yanaathiri wakazi wa bondeni tu? Sikujua kuwa Posta Mpya iko bondeni.
 
Back
Top Bottom