Wakati wa uchaguzi baadhi walisema jirani zetu wako vizuri kwa kuwa na tume huru na Katiba Mpya

Wakati wa uchaguzi baadhi walisema jirani zetu wako vizuri kwa kuwa na tume huru na Katiba Mpya

ambagae

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2009
Posts
3,334
Reaction score
1,385
Wakati wa uchaguzi wa jirani na ndugu zetu kuna baadhi ya wenzetu Watanzania walisifu sana kuwa wenzetu wako mbali kidemokrasia tujifunze kutoka kwao lakini kwa yanayoendelea kama mambo yenyewe ya demokrasia yako hivyo ni bora tuendelee na katiba iliyopo na tume ya uchaguzi iliyopo kuliko kuelekea huko waliko wenzetu kwa sasa.
 
Katiba yetu mpya inabidi iweke mfumo wa serikali ya mseto kama Ujerumani au Israel, sio mfumo wa mshindi kuchukua kila kitu.
Kabisa kabisa huo ndio utakuwa muarobaini. Hapo kama zilikuwepo mbeleko zitaacha Hiyo kazi ya kubeba beba watu. Naona Kenya 🇰🇪 wanaelekea huko huko.
 
Wakati wa uchaguzi wa jirani na ndugu zetu kuna baadhi ya wenzetu Watanzania walisifu sana kuwa wenzetu wako mbali kidemokrasia tujifunze kutoka kwao lakini kwa yanayoendelea kama mambo yenyewe ya demokrasia yako hivyo ni bora tuendelee na katiba iliyopo na tume ya uchaguzi iliyopo kuliko kuelekea huko waliko wenzetu kwa sasa.
Hilo bado sahihi, wenzetu wako mbali kidemokrasia. Ila chawa ndio tatizo. Bado elimu ya uraia bado inahitajika, si tu ibaki katika makaratasi kama Katiba nzuri n.k.

La msingi wananchi waelewe maana na faida ya demokrasia vinginevyo faida yake hakuna.

Ni lazima tuwafikie akina mdudu CHADEMA na kuwaelimisha hata baada ya katiba mpya. Hawa akina mdudu CHADEMA ndio wanaoleta vurugu huko KENYA.
 
Wakati wa uchaguzi wa jirani na ndugu zetu kuna baadhi ya wenzetu Watanzania walisifu sana kuwa wenzetu wako mbali kidemokrasia tujifunze kutoka kwao lakini kwa yanayoendelea kama mambo yenyewe ya demokrasia yako hivyo ni bora tuendelee na katiba iliyopo na tume ya uchaguzi iliyopo kuliko kuelekea huko waliko wenzetu kwa sasa.
Kwani Marekani hawaandamani? Wanaandamana sababu anaenda kinyume na matakwa ya wananchi
 
Wakati wa uchaguzi wa jirani na ndugu zetu kuna baadhi ya wenzetu Watanzania walisifu sana kuwa wenzetu wako mbali kidemokrasia tujifunze kutoka kwao lakini kwa yanayoendelea kama mambo yenyewe ya demokrasia yako hivyo ni bora tuendelee na katiba iliyopo na tume ya uchaguzi iliyopo kuliko kuelekea huko waliko wenzetu kwa sasa.
Kufikiri kwamba kufuata katiba iliyopo ndiko kutakuendelea kutuletea amani, ni mawazo finyu. Kwa sababu wananchi uvumilivu ukiwashinda kitachoweza kutokea kinaweza kuwa zaidi ya hicho cha KENYA.

La msingi ni kusoma alama za nyakati, dunia inabadilika, generation mpya inakuja kila mwaka, na mabadiliko ndio maisha.

Mahitaji ya leo sio yale ya Jana, kama tunakubaliana kwa maandishi jinsi ya kuendesha nchi ni lazima turudi katika karatasi na kalamu tuandike sheria/katiba kutokana na mahitaji yetu leo.
 
Kufikiri kwamba kufuata katiba iliyopo ndiko kutakuendelea kutuletea amani, ni mawazo finyu. Kwa sababu wananchi uvumilivu ukiwashinda kitachoweza kutokea kinaweza kuwa zaidi ya hicho cha KENYA.
La msingi ni kusoma alama za nyakati, dunia inabadilika, generation mpya inakuja kila mwaka, na mabadiliko ndio maisha.

Mahitaji ya leo sio yale ya Jana, kama tunakubaliana kwa maandishi jinsi ya kuendesha nchi ni lazima turudi katika karatasi na kalamu tuandike sheria/katiba kutokana na mahitaji yetu leo.
Na huu ndio ukweli
 
Wakati wa uchaguzi wa jirani na ndugu zetu kuna baadhi ya wenzetu Watanzania walisifu sana kuwa wenzetu wako mbali kidemokrasia tujifunze kutoka kwao lakini kwa yanayoendelea kama mambo yenyewe ya demokrasia yako hivyo ni bora tuendelee na katiba iliyopo na tume ya uchaguzi iliyopo kuliko kuelekea huko waliko wenzetu kwa sasa.
Uko sahihi kabisa. Hawa jamaa sijui ni kwa nini wanapenda kusifia sana hii nchi jirani na kututaka tu kopi na kupesti mambo ya huko. Waliuana sana baada ya uchaguzi mkuu ule. Mauaji yale ndio yakasababisha katiba mpya waliyodhani itakuwa mwarobaini ya machafuko hayo. Walijidanganya, machafuko yameendelea kila baada ya chaguzi kuu.

Tatizo siyo katiba mpya. Tatizo la nchi zetu ni uchu wa madaraka. Utakuta mtu anang'ang'ania na kulazima awe raisi au mbunge. Kila uchaguzi mkuu lazima awe mgombea. Ni vyema katiba yetu tukairekebisha kwa kuweka kipengele hiki:

1 (a): Mgombea wa uraisi au ubunge akishindwa kwenye uchaguzi mkuu hataruhusiwa tena kuwa mgombea kwa nafasi hizo kwenye chaguzi zijazo hadi baada ya miaka kumi, yaani vipindi viwili hatakuwa mgombea

2 (b): Mtu akishinda ugombea wa nafasi ya uraisi au ubunge ataruhusiwa kugombea tena nafasi hizo kwa mara ya mwisho kwenye uchaguzi mkuu utakaofuata, yaani baada ya miaka mitano. Baada ya hapo hataruhusiwa kugombea nafasi hizo maishani mwake au baada ya miaka 20 kupita.

Hii ndiyo itakuwa mwarobaini ya fujo hizi za kisiasa zinazopelekea vifo vya wananchi.

 
Uko sahihi kabisa. Hawa jamaa sijui ni kwa nini wanapenda kusifia sana hii nchi jirani na kututaka tu kopi na kupesti mambo ya huko. Waliuana sana baada ya uchaguzi mkuu ule. Mauaji yale ndio yakasababisha katiba mpya waliyodhani itakuwa mwarobaini ya machafuko hayo. Walijidanganya, machafuko yameendelea kila baada ya chaguzi kuu.

Tatizo siyo katiba mpya. Tatizo la nchi zetu ni uchu wa madaraka. Utakuta mtu anang'ang'ania na kulazima awe raisi au mbunge. Kila uchaguzi mkuu lazima awe mgombea. Ni vyema katiba yetu tukairekebisha kwa kuweka kipengele hiki:

1 (a): Mgombea wa uraisi au ubunge akishindwa kwenye uchaguzi mkuu hataruhusiwa tena kuwa mgombea kwa nafasi hizo kwenye chaguzi zijazo hadi baada ya miaka kumi, yaani vipindi viwili hatakuwa mgombea

2 (b): Mtu akishinda ugombea wa nafasi ya uraisi au ubunge ataruhusiwa kugombea tena nafasi hizo kwa mara ya mwisho kwenye uchaguzi mkuu utakaofuata, yaani baada ya miaka mitano. Baada ya hapo hataruhusiwa kugombea nafasi hizo maishani mwake au baada ya miaka 20 kupita.

Hii ndiyo itakuwa mwarobaini ya fujo hizi za kisiasa zinazopelekea vifo vya wananchi.


Muarobaini ni haki bin haki ikitendeka na ionekane inatendeka !! Uchu wa madaraka upo pande zote za wanaoingia kwenye uchaguzi sio upande mmoja tu !! Tuwe wakweli !!
 
Muarobaini ni haki bin haki ikitendeka na ionekane inatendeka !! Uchu wa madaraka upo pande zote za wanaoingia kwenye uchaguzi sio upande mmoja tu !! Tuwe wakweli !!
Kwani huko nchi jirani hakuna hiyo haki bin haki? Si tunaamini haki bin haki inapatikana? Si walifikishana hadi Supreme Court, lakini mambo yako Vilevile. Mwarobaini ni hicho kipengele kuingizwa kwenye katiba yetu. Kitawahusu wa vyama vyote. Mtu akishindwa kwenye uchaguzi mkuu akafanye shughuli zingine na asahau kuja kugombea tena. Watu kama akina Raila na Tundu hawangalisumbua tena nchi zao. Na nchi zingalitulia tuli.
 
Katiba yetu mpya inabidi iweke mfumo wa serikali ya mseto kama Ujerumani au Israel, sio mfumo wa mshindi kuchukua kila kitu.
Lengo lenu mnataka tu vyeo na kuchumia matumbo yenu
 
Wakati wa uchaguzi wa jirani na ndugu zetu kuna baadhi ya wenzetu Watanzania walisifu sana kuwa wenzetu wako mbali kidemokrasia tujifunze kutoka kwao lakini kwa yanayoendelea kama mambo yenyewe ya demokrasia yako hivyo ni bora tuendelee na katiba iliyopo na tume ya uchaguzi iliyopo kuliko kuelekea huko waliko wenzetu kwa sasa.
Upinzani wa wasaka Tonge huu.
 
Katiba ni kama ndoa...
Ndoa zote ambazo huzijui undani ..unazitazama Kwa nje unaona ndo ndoa za mfano
 
Wakati wa uchaguzi wa jirani na ndugu zetu kuna baadhi ya wenzetu Watanzania walisifu sana kuwa wenzetu wako mbali kidemokrasia tujifunze kutoka kwao lakini kwa yanayoendelea kama mambo yenyewe ya demokrasia yako hivyo ni bora tuendelee na katiba iliyopo na tume ya uchaguzi iliyopo kuliko kuelekea huko waliko wenzetu kwa sasa.

Uwezo wako wa kupambanua mambo ni mdogo
 
Kuna jamaa nilimsikia anasema wao wakenya wana katiba nzuri na tume huru but wakati wa uchaguzi anadai kunambongo alienda huko na akahamishia utz huko ndo mambo yakawa hvyo kama tulivyoona na tunavyoona
 
Back
Top Bottom