Wakatoliki (TEC) wameanza, huenda wakafuata waprotestant (CCT), wapentekoste(PCT) na wasabato. Rais Samia nakushauri achana na DP world!

Wakatoliki (TEC) wameanza, huenda wakafuata waprotestant (CCT), wapentekoste(PCT) na wasabato. Rais Samia nakushauri achana na DP world!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Dalili ya mvua ni mawingu, unaweza ukapuuzia mawingu lakini manyunyu yakianza hupaswi tena kuyapuuzia maana mvua ikishashika kasi huna tena ujanja, ni kuloa tu.

Wasomi waliokosoa mkataba wa bandari kupewa DP world huenda yalikuwa ni mawingu tu, vyama vya siasa (hususani CHADEMA) na wanaharakati walipoingia na kukaa mstari wa mbele kupinga mkataba wa bandari hiyo ilikuwa ni manyunyu ya mvua, na sasa kanisa katoliki kupitia baraza la maaskofu (TEC) wamekuja na mvua kamili ya mashambulizi kuupinga huo mkataba wa bandari.

Kwa wale tunaoweza kuona mbali, muda sio mrefu walutheri (KKKT) watakuja na tamko la kuuzika huo mkataba wa bandari kabla ya mwamvuli wa waprotestant (CCT) kuja na tamko na mwishoni mwamvuli wa wapentekoste (PCT) watagongelea msumari zaidi kuuzika huu mkataba. Safari hii usishangae hadi wasabato kuingia frontline na matamko ya kuupinga huu mkataba.

Kwa kifupi sana, Kanisa hapa Tanzania limejipanga kuleta full scale ya mashambulizi dhidi ya serikali ya mama Samia kuhusu huu mkataba wa bandari na hii ni kutokana na makosa ya kiufundi ya CCM na wapiga debe wa serikali kulazimisha hili suala lionekane linapingwa kwa mlengo wa kidini ili kuwazima wakosoaji. Sasa wakosoaji wameamua kuja na mlango ule ule ambao watawala wameutengenza.

Ushauri wangu kwa mama Samia na serikali yake ni kusoma alama za nyakati tu na kuachana haraka na huu mkataba wa bandari. Huu mziki wa kanisa ni mnene mnoo, wamejipanga vizuri mnoo na wana nguvu ya kupitiliza. Wakati ni ukuta, ukishindana nao utaumia, wakati sahihi wa kuachana na mkataba wa bandari na Dp world ni sasa. Mama Samia tunakupenda sana na tunakutakia mema.
 
Kwa hiyo Serikali inaendeshwa na Taasisi za kidini?

Hata kama mkataba ungekuwa haufai jambo ambalo halipo. Ni precedent mbaya sana kwa Serikali kuonekana inaendeshwa na Taasisi za kidini.

Hilo halipo na halitakuja kutokea duniani. Hakuna Taasisi yenye nguvu kuliko Serikali.

Haijatokea na haitakuja kutokea Duniani.

Hizo sifa mnawapa kwa sababu stori zenu za vijiweni tu.
 
Kwa hiyo Serikali inaendeshwa na Taasisi za kidini?..
duh, serikali na dini zote ni watu... labda tukuulize katika nchi hii kuna mwanasiasa alipata urais bila kuwaomba viongozi wa dini wamuamini?

Unasema halipo unajua mapinduzi ya kiislam ya IRAN kati ya rais wa IRAN na Ayatolah nani mkuu wa nchi?

Acha upumbavu jomba. Binafsi sipingi uwekezaji wa DUBAI PORT WORLD lakini kulingana na suala hili lilipofikia serikali iachane nalo.

The lost
 
Wabakie huko huko kanisani maslahi ya nchi yataamuliwa na serikali na sisi wananchi kupitia wawakilishi wetu watulie , waache kutikisa kiberiti acha dp world ije ilete tija wamezoea wizi tu kule bandarini
 
duh, serikali na dini zote ni watu... labda tukuulize katika nchi hii kuna mwanasiasa alipata urais bila kuwaomba viongozi wa dini wamuamini..
Mantiki ya hoja yangu ni kwamba hakuna Serikali duniani inayoendeshwa na matamko ya taasisi za kidini.

Never. Na hii ni kwenye muktadha wa Serikali za nchi zinazojitanabaisha sio za kidini.

Mfano uliotoa wa IRAN sio sahihi. Iran ni Islamic Republic of Iran.

Wao wana Baraza la Kidini tena la Kiislamu ambalo ni sehemu ya Uongozi wa nchi
 
Kwa hiyo Serikali inaendeshwa na Taasisi za kidini?

Hata kama mkataba ungekuwa haufai jambo ambalo halipo. Ni precedent mbaya sana kwa Serikali kuonekana inaendeshwa na Taasisi za kidini.

Hilo halipo na halitakuja kutokea duniani. Hakuna Taasisi yenye nguvu kuliko Serikali.

Haijatokea na haitakuja kutokea Duniani.

Hizo sifa mnawapa kwa sababu stori zenu za vijiweni tu.
Vatican inatawala dunia
 
Mantiki ya hoja yangu ni kwamba hakuna Serikali duniani inayoendeshwa na matamko ya taasisi za kidini. Never. Na hii ni kwenye muktadha wa Serikali za nchi zinazojitanabaisha sio za kidini.

Mfano uliotoa wa IRAN sio sahihi. Iran ni Islamic Republic of Iran. Wao wana Baraza la Kidini tena la Kiislamu ambalo ni sehemu ya Uongozi wa nchi
Serikali inapata mamlaka yake toka kwa wananchi, hivyo iwasikilize wananchi. Dini zimeikumbusha tu kuwa zinalea wananchi kiroho na ndio wanaonung'unika. Kusema kwa niaba yao sio kuiendesha serikali bali kuikumbusha kuwa isipende kulazimisha mambo.
Binafsi sipendi nchi ifike mahali KUTAMKIANA kuwe ndio jibu lakini katika hili sioni nini kingefanyika kuishtua serikali maana kila njia halali serikali imepinga mpaka mahakama inatoa hukumu huku inashangaza pia! (Simu zilipigwa?) Mimi tangu mwanzo nilikataa jibu la (kuziba masikio), lilikuwa jibu la KIBURI na siku zote kiburi hutangilia kabla anguko halijawasili.
 
Dalili ya mvua ni mawingu, unaweza ukapuuzia mawingu lakini manyunyu yakianza hupaswi tena kuyapuuzia maana mvua ikishashika kasi huna tena ujanja, ni kuloa tu.

Wasomi waliokosoa mkataba wa bandari kupewa DP world huenda yalikuwa ni mawingu tu, vyama vya siasa (hususani CHADEMA) na wanaharakati walipoingia na kukaa mstari wa mbele kupinga mkataba wa bandari hiyo ilikuwa ni manyunyu ya mvua, na sasa kanisa katoliki kupitia baraza la maaskofu (TEC) wamekuja na mvua kamili ya mashambulizi kuupinga huo mkataba wa bandari.

Kwa wale tunaoweza kuona mbali, muda sio mrefu walutheri (KKKT) watakuja na tamko la kuuzika huo mkataba wa bandari kabla ya mwamvuli wa waprotestant (CCT) kuja na tamko na mwishoni mwamvuli wa wapentekoste (PCT) watagongelea msumari zaidi kuuzika huu mkataba. Safari hii usishangae hadi wasabato kuingia frontline na matamko ya kuupinga huu mkataba.

Kwa kifupi sana, Kanisa hapa Tanzania limejipanga kuleta full scale ya mashambulizi dhidi ya serikali ya mama Samia kuhusu huu mkataba wa bandari na hii ni kutokana na makosa ya kiufundi ya CCM na wapiga debe wa serikali kulazimisha hili suala lionekane linapingwa kwa mlengo wa kidini ili kuwazima wakosoaji. Sasa wakosoaji wameamua kuja na mlango ule ule ambao watawala wameutengenza.

Ushauri wangu kwa mama Samia na serikali yake ni kusoma alama za nyakati tu na kuachana haraka na huu mkataba wa bandari. Huu mziki wa kanisa ni mnene mnoo, wamejipanga vizuri mnoo na wana nguvu ya kupitiliza. Wakati ni ukuta, ukishindana nao utaumia, wakati sahihi wa kuachana na mkataba wa bandari na Dp world ni sasa. Mama Samia tunakupenda sana na tunakutakia mema.
Umesikilizwa Vema
 
Back
Top Bottom