Wakatoliki Tujifunze: Baadhi ya mavazi ya Askofu na maana yake

Wakatoliki Tujifunze: Baadhi ya mavazi ya Askofu na maana yake

Kwa nini Askofu akifa anazikwa ndani ya Kanisa.?
 
Uzi ni mzuri lakini naona umekosea jukwaa...

Mods saidia kuweka kwenye jukwaa sahihi
 
Ndugu yangu sema hivyo vitu vilikuwa vinavaliwa wakati wa utawala wa Rumi au Roman impire hata kabla Yesu hajazaliwa,ila vimekuja kuingizwa kiujanjaujanja pamoja usisahau na utamaduni wa Sanamu wamekuwa nao Roman impare toka enzi na enzi jalibu kuangalia habari zako wangapi watakaozisoma sio kila mtu humu ndani labda hajui,kama kuvaa hayo mavazi basi angevaa Yesu mwenyewe ambaye alikuwa mtume wa Mungu.Lakini yesu mpaka anakufa pamoja na mitume wake walikuwa wanavaa kanzu simple tu,kama walizokuwa wanavaa mitume wengine waliowatangulia
 
Tumsifu Yesu Kristu!
Tumekuwa tukiwaona MaAskofu wetu wakiwa ndani ya Baadhi ya Mavazi ambayo mara Pengine wengine Hatuyafahamu, Basi Haya na Ndiyo Maelezo ya kila Vazi!


1. Pete ya Askofu (Episcopal ring)

View attachment 850469
Hii huvaliwa na Askofu katika “kidole cha pete cha mkono wa kulia” (kidole cha pili kutoka kushoto). Mtume Paulo katika waraka wake kwa Waefeso anatumia lugha ya picha kutoa ujumbe kwa wanandoa akisema “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa…” (Efe. 5:25). Hapa Mtume Paulo anamtazama Kristo kama mume wa Kanisa (Kanisa ni mke na Kristo ni mume). Lugha hii ya picha inaonesha aina fulani ya “muungano wa ndoa” uliopo kati ya Kristo na Kanisa lake kama ilivyo kwa mume na mke. Askofu anamwakilisha Kristo mbaye ni kuhani mkuu. Hivyo kama ambavyo Kristo kuhani mkuu “ameoana/funga ndoa” na Kanisa lake, kadhalika Askofu naye anavikwa pete kuonesha kuwa “amefunga ndoa na Kanisa lake”- ameunganishwa na Kanisa analolitumikia- yaani waamini wake/Jimbo lake). Kama ambavyo pete ni ishara ya uaminifu na mapendo, kadhalika Askofu naye anapaswa kulitumikia kanisa lake/waamini wake/Jimbo lake kwa uaminifu na mapendo.
Kwa nini tunabusu pete ya Askofu? Kitendo cha kubusu pete ya Askofu ni ishara ya kutambua na kuheshimu mamlaka yake ya kuongoza, kufundisha na kutakatifuza.


2. Msalaba wa kifuani (pectoral cross)
View attachment 850468
Msalaba huu humkumbusha Askofu mateso na msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo katika safari nzima ya ukombozi. Msalaba auvaao Askofu humkumbusha Askofu kuwa naye katika kutimiza wajibu wake wa kichungaji atakumbana na mateso na misalaba mingi ambayo atapaswa kuiibeba kwa moyo mkuu- hii ndiyo sababu ya msalaba huo kuvaliwa kifuani (wengi tunaamini moyo hukaa kifuani). Msalaba wa kiaskofu hufungwa ama kwa kamba au mkufu.

3. Fimbo ya kichungaji (Pastoral Staff/ Crosier)

View attachment 850467
Katika jamii ya wafugaji, wachungaji hubeba fimbo wanapokwenda kuchunga mifugo yao. Fimbo hiyo hutumika kuongozea kundi lake la mifugo na hutumika pia kama silaha ya kulilinda kundi la mifugo dhidi ya hatari zozote zitakazojitokeza. Kadhalika fimbo ya Askofu ni ishara ya mamlaka yake ya kichungaji na kiutawala: inaonesha kuwa Askofu amekabidhiwa kundi la kulichunga, kuliongoza na kulitawala. Kundi hilo ni waamini. Hivyo, fimbo ya kichungaji inaashiria kuwa Askofu anao wajibu wa kuwaongoza waamini wake na kuwalinda dhidi ya hatari zozote
za kiimani. Kisheria Askofu anayebeba fimbo ya kichungaji ni Askofu-Jimbo akiwa ndani ya Jimbo lake. Hata hivyo, Askofu asiye wa Jimbo husika anaweza kubeba fimbo ya kichungaji kwa ruhusa ya Askofu-Jimbo wa Jimbo husika. Maaskofu Wastaafu hawabebi fimbo ya kichungaji.


4. Mitra (Miter)

View attachment 850466
Hii ni kofia kubwa ya pembe tatu ambayo kwa nyuma ina tepe mbili. Kufafanua zaidi juu ya maana ya maumbo ya kofia hii tunahitaji muda mwingi. Itoshe kusema tu kwamba Mitra inaashiria “taji ya ushindi” endapo tutashinda mapambano ya Kikristo. Mtume Paulo anasema wazi: “Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake” (2 Tim. 4:7-8). Hivyo, Mitra inamkumbusha Askofu kuwa anapaswa kuliongoza kundi lake katika mashindano ya mbio za hapa duniani kuelekea wokovu hadi tufikie ushindi wa mwisho mbinguni ambapo tutapewa taji ya ushindi inayoashiriwa na Mitra.

5. Zucchetto (kofia ndogo ama nyeupe, au nyekundu au zambarau)
View attachment 850465
Mwanzoni, zucchetto haikuwa sehemu ya mavazi ya liturujia. Miongoni mwa hatua za kuelekea upadre ilikuwa ni kunyolewa kipara cha utosini. Hatua hii iliitwa “tonsure”. Kutokana na baridi kali la nchi za ulaya, ililazimika kuvaa kofia ndogo eneo la kipara ili angalau kupata joto. Kofia hiyo ya kuhifadhi joto kwenye kipara cha utosini ndiyo iliitwa “zucchetto.” Kadiri miaka ilivyopita, zucchetto ikawa vazi la liturujia/ibada. Zucchetto ya rangi nyeupe huvaliwa na Baba Mtakatifu; Zucchetto ya rangi nyekundu huvaliwa na Makardinali na Zucchetto ya rangi ya zambarau huvaliwa na Maaskofu. Vyanzo mbalimbali huonesha kuwa zucchetto ni ishara ya Roho Mtakatifu kama vile Roho Mtakatifu alivyowashukia mitume kama ndimi za moto siku ya Pentekoste (rejea Mdo. 2:1-4). Hivyo, zucchetto huashiria nguvu na mapaji ya Roho Mtakatifu. Kwa kawaida Maaskofu huvua zucchetto zao wawapo mbele ya Baba Mtakatifu ikiwa ni ishara ya heshima na kutambua mamlaka na cheo cha Baba Mtakatifu.

6. Pallium
View attachment 850464
Hili ni vazi ambalo huvaliwa na Baba Mtakatifu, Maaskofu Wakuu na Patriaki wa Yerusalem tu. Ieleweke wazi kuwa siyo kila Askofu Mkuu huvaa Pallium. La hasha! Huvaliwa tu na Maaskofu Wakuu ambao ni Maaskofu-Jimbo (yaani wana majimbo wanayoyaongoza). Hata hivyo, huvaliwa tu na Askofu Mkuu awapo ndani ya majimbo yanayounda Jimbo Kuu lake. Mfano Jimbo Kuu la Mwanza linaundwa na majimbo ya Mwanza, Musoma, Shinyanga, Bunda, Geita, Kayanga, Bukoba na Rulenge-Ngara. Hivyo Askofu Mkuu wa Mwanza anaweza kuvaa Pallium awapo kwenye mojawapo ya majimbo hayo. Akienda Jimbo la Tanga, kwa mfano, hawezi kuvaa Pallium kwa sababu ni nje ya metropolitan yake (nje ya mipaka ya Jimbo Kuu la Mwanza).
Pallium hutokana na sufu (manyoya ya kondoo) yaliyokatwa kutoka kwa kondoo wakati wa sherehe ya Mt. Anyesi ambayo huadhimishwa Januari 21 kila mwaka. Jina Anyesi (au Agnes) limetokana na neno la Kilatin “Agnus” lenye maana ya “Mwanakondoo”. Kwa nini hutengenezwa kutokana na sufu ya kondoo? Kwenye Agano Jipya Kristo anatambulishwa kama “Mwanakondoo wa Mungu” (rejea Yn. 1:29, 36). Kama ambavyo kondoo wanatoa sufu kwa ajili ya kutengeneza Pallium, hivyo hivyo Kristo aliye “mwanakondoo wa Mungu” anajitoa sadaka kwa ajili ya dhambi za ulimwengu. Kadhalika, kitendo cha kuvaa shingoni Pallium iliyotengenezwa kutokana na sufu ya kondoo kinaonesha kuwa Askofu ni Mchungaji Mwema kwani amewabeba kondoo zake (waamini) mabegani. Pallium inapovaliwa shingoni mwa Askofu inamaanisha pia “nira ya Kristo” kwani Kristo alisema “Jitieni nira yangu… Kwa maana nira yangu ni laini…” (Mt. 11:29, 30). Pallium zikishatengenezwa huweka chini ya altare ya Basilica la Mt. Petro karibu kabisa na kaburi la Mtume Petro. Kila tarehe 29 June ambayo ni Sherehe ya Watakatifu Petro na Paulo Mitume, Maaskofu Wakuu wapya walioteuliwa mwaka huo huenda Roma na kupatiwa Pallium hizo kama zawadi maalumu kutoka kwa Baba Mtakatifu. Kwa nini Pallium huwekwa karibu na kaburi la Mtume Petro? Na kwa nini Papa pekee ndiye huwapatia Pallium Maaskofu Wakuu? Hii ni kuonesha kuwa Maaskofu Wakuu wanapaswa kuwa na ushirika wa kipekee kabisa na Baba Mtakatifu ambaye ni halifa wa Mtume Petro. Wanapaswa kuonesha muungano na utii kwa Baba Mtakatifu ambaye ni halifa wa Mtume Petro. Pallium ni nyeupe ili kuonesha kuwa Askofu husika anapaswa kuwa na usafi wa maisha (innocence of life).

Maelezo Haya ni Kwa Mujibu wa Padre Kelvin Onesmo Mkama, Jimbo Kuu la Mwanza (Mimi Nimeyaandika tu)

ALFRED
Mkuuu unamfahamu huyu padre

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu sema hivyo vitu vilikuwa vinavaliwa wakati wa utawala wa Rumi au Roman impire hata kabla Yesu hajazaliwa,ila vimekuja kuingizwa kiujanjaujanja pamoja usisahau na utamaduni wa Sanamu wamekuwa nao Roman impare toka enzi na enzi jalibu kuangalia habari zako wangapi watakaozisoma sio kila mtu humu ndani labda hajui,kama kuvaa hayo mavazi basi angevaa Yesu mwenyewe ambaye alikuwa mtume wa Mungu.Lakini yesu mpaka anakufa pamoja na mitume wake walikuwa wanavaa kanzu simple tu,kama walizokuwa wanavaa mitume wengine waliowatangulia
Mkuu uzi kama unaona haukufai unaweza kuukimbia tu
 
kuna zile nyingine wanasema zina nembo za freemason, ni kweli wanavaa mavazi ya aina hiyo ?
 
Aisee sawa sawaa!
mkuu Alfred naomba unijuze jumbo LA Kayanga liko eneo/mkoa gani.kwangu limekuwa kama jipya. na pill kama unaweza niorodheshee majimbo yote katoliki Tanzania na maaskofu wake nilijaribu kutafuta.mtanfaoni bila mafanikio hats tec hawana taariga hizo mtandaoni
 
mkuu Alfred naomba unijuze jumbo LA Kayanga liko eneo/mkoa gani.kwangu limekuwa kama jipya. na pill kama unaweza niorodheshee majimbo yote katoliki Tanzania na maaskofu wake nilijaribu kutafuta.mtanfaoni bila mafanikio hats tec hawana taariga hizo mtandaoni

Jimbo Katoliki la Kayanga (kwa Kilatini "Dioecesis Kayangana") ni mojawapo kati ya majimbo34 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania na kama hayo yote linafuata Mapokeo ya Kiroma
Kikanisa linahusiana na Jimbo Kuu la Mwanza.
Askofu wake wa kwanza ni Almachius Vincent Rweyongeza.
 
mkuu Alfred naomba unijuze jumbo LA Kayanga liko eneo/mkoa gani.kwangu limekuwa kama jipya. na pill kama unaweza niorodheshee majimbo yote katoliki Tanzania na maaskofu wake nilijaribu kutafuta.mtanfaoni bila mafanikio hats tec hawana taariga hizo mtandaoni

Bishop Joachim (Alois) Ammann, O.S.B. †, Abbot Emeritus of Ndanda

Bishop Eugéne Cornelius Arthurs, I.C. †, Bishop Emeritus of Tanga

Bishop Aloysius Balina †, Bishop of Shinyanga

Bishop Anthony Banzi, Bishop of Tanga

Bishop Attilio Beltramino, I.M.C. †, Bishop of Iringa

Bishop Joseph-Marie Birraux, M. Afr. †, Superior General of Missionaries of Africa (White Fathers)

Bishop Joseph Blomjous, M. Afr. †, Bishop Emeritus of Mwanza
Archbishop Franco Brambilla †, Apostolic Nuncio Emeritus to Australia
Bishop Léonce Bridoux, M. Afr. †, Vicar Apostolic of Tanganyika
Archbishop Cornelius Bronsveld, M. Afr. †, Archbishop Emeritus of Tabora

Bishop Renatus Lwamosa Butibubage †, Bishop Emeritus of Mwanza.

Bishop Joseph James Byrne, C.S.Sp. †, Bishop Emeritus of Moshi

Father Francesco Cagliero, I.C.M. †, Prefect of Iringa
Bishop Jean-Baptiste-Frézal Charbonnier, M. Afr. †, Vicar Apostolic of Tanganyika
Bishop Evaristo Marc Chengula, I.M.C., Bishop of Mbeya
Archbishop Joseph Chennoth, Apostolic Nuncio to Japan
Bishop Arnold Ralph Cotey, S.D.S. †, Bishop Emeritus of Nachingwea

Archbishop Damian Denis Dallu, Archbishop of Songea

Father Stanislao dell’Addolorata, C.P. †, Prefect of Dodoma
Father Max Theodor Franz Donders, M. Afr. †, Superior of Tukuyu
Bishop Dennis Vincent Durning, C.S.Sp. †, Bishop Emeritus of Arusha

Father Bonifatius (Magnus) Fleschutz, O.S.B. †, Prefect of Southern Zanguebar {Zanguebar Meridionale}

Bishop François Gerboin, M. Afr. †, Vicar Apostolic of Unianyembé
Bishop Henry Aloysius Gogarty, C.S.Sp. †, Vicar Apostolic of Kilima-Njaro
Father Giuseppe Gerardo Grondin, M.M. †, Prefect of Musoma

Father Ludwig Haag, M. Afr. †, Prefect Emeritus of Tukuyu
Bishop Anthony Victor Haelg (Hälg), O.S.B. †, Abbot Emeritus of Ndanda

Father Maurus (Franz Xaver) Hartmann, O.S.B. †, Prefect Emeritus of Southern Zanguebar {Zanguebar Meridionale}
Bishop Nicodemus Atle Basili Hhando †, Bishop Emeritus of Mbulu

Bishop Bernhard Gerhard Hilhorst, C.S.Sp. †, Bishop Emeritus of Morogoro
Bishop Jean-Joseph Hirth, M. Afr. †, Vicar Apostolic Emeritus of Kivu, Burundi
Bishop James Holmes-Siedle, M. Afr. †, Bishop Emeritus of Kigoma
Bishop Burkhard Huwiler, M. Afr. †, Vicar Apostolic Emeritus of Bukoba

Bishop Matthias Joseph Isuja †, Bishop Emeritus of Dodoma

Bishop Patrick Iteka †, Bishop of Mahenge

Bishop Flavian Matindi Kassala, Bishop of Geita

Bishop William Pascal Kikoti †, Bishop of Mpanda.

Bishop Method Kilaini, Auxiliary Bishop of Bukoba

Bishop Joseph Kilasara, C.S.Sp. †, Bishop Emeritus of Moshi
Bishop Rogatus Kimaryo, C.S.Sp., Bishop of Same
Archbishop Beatus Kinyaiya, O.F.M. Cap., Archbishop of Dodoma
Bishop Nikasius Kipengele †, Bishop of Mahenge
Bishop Jacob Venance Koda, Bishop Emeritus of Same
Archbishop James Joseph Komba †, Archbishop of Songea
Bishop Maurus Gervase Komba †, Bishop Emeritus of Tanga
Bishop Damian Kyaruzi, Bishop Emeritus of Sumbawanga

Bishop Anthony Gaspar Lagwen, Bishop of Mbulu
Bishop Alfred Lanctôt, M. Afr. †, Bishop of Rulenge
Father Willibrord Lay, O.S.B. †, Prefect Emeritus of Lindi
Archbishop Josaphat Louis Lebulu, Archbishop Emeritus of Arusha
Bishop Adolphe Le Chaptois, M. Afr. †, Vicar Apostolic of Tanganyika
Bishop Henri Léonard, M. Afr. †, Vicar Apostolic Emeritus of Tabora
Bishop Maurus Libaba †, Bishop of Lindi
Bishop Salutaris Melchior Libena, Bishop of Ifakara
Archbishop Francisco-Javier Lozano Sebastián, Apostolic Nuncio Emeritus to Romania
Bishop Fortunatus M. Lukanima †, Bishop Emeritus of Arusha
Bishop Prosper Balthazar Lyimo, Auxiliary Bishop of Arusha

Bishop Bernard Mabula †, Bishop Emeritus of Singida
Bishop Alfred Leonhard Maluma, Bishop of Njombe
Bishop Edward Elias Mapunda, Bishop of Singida
Bishop Emmanuel A. Mapunda, Bishop Emeritus of Mbinga
Archbishop Edgar Aristide Maranta, O.F.M. Cap. †, Archbishop Emeritus of Dar-es-Salaam
Archbishop Agostino Marchetto, Secretary Emeritus of the Pontifical Council for the Pastoral Care of Migrants and Itinerant People, Roman Curia
Archbishop Isaac Amani Massawe, Archbishop of Arusha
Archbishop Anthony Peter Mayalla †, Archbishop of Mwanza
Bishop Edward Aloysius McGurkin, M.M. †, Bishop Emeritus of Shinyanga
Bishop Elias Mchonde †, Bishop of Mahenge
Bishop Titus Joseph Mdoe, Bishop of Mtwara
Bishop Bernardin Francis Mfumbusa, Bishop of Kondoa
Archbishop Mario Epifanio Abdallah Mgulunde †, Archbishop of Tabora
Bishop Joseph Georges Edouard Michaud, M. Afr. †, Vicar Apostolic of Uganda
Archbishop Marko Mihayo †, Archbishop Emeritus of Tabora
Bishop Ludovick Joseph Minde, ALCP/OSS, Bishop of Kahama
Bishop Adriani Mkoba †, Bishop Emeritus of Morogoro
Bishop Telesphore Mkude, Bishop of Morogoro
Bishop Joseph Roman Mlola, ALCP/OSS, Bishop of Kigoma
Bishop Gabriel Mmole, Bishop Emeritus of Mtwara
Archbishop Gian Vincenzo Moreni †, Apostolic Nuncio to Philippines
Bishop Charles Msakila †, Bishop of Sumbawanga
Bishop Amedeus Msarikie †, Bishop Emeritus of Moshi
Bishop Castor Paul Msemwa †, Bishop of Tunduru-Masasi
Bishop Michael George Mabuga Msonganzila, Bishop of Musoma
Archbishop Norbert Wendelin Mtega, Archbishop Emeritus of Songea
Bishop Marie-Joseph-Aloys Munsch, C.S.Sp. †, Vicar Apostolic Emeritus of Kilima-Njaro
Bishop Magnus Mwalunyungu †, Bishop Emeritus of Tunduru-Masasi
Bishop Raymond Mwanyika †, Bishop Emeritus of Njombe
Bishop Gervas John Mwasikwabhila Nyaisonga, Bishop of Mpanda
Bishop Christopher Mwoleka †, Bishop Emeritus of Rulenge

Bishop John Chrisostom Ndimbo, Bishop of Mbinga
Bishop Agapiti Ndorobo, Bishop of Mahenge
Bishop Tarcisius Ngalalekumtwa, Bishop of Iringa
Bishop Bernard Martin Ngaviliau, C.S.Sp. †, Bishop Emeritus of Zanzibar
Bishop Bruno Pius Ngonyani, Bishop of Lindi
Bishop Severine Niwemugizi, Bishop of Rulenge-Ngara
Bishop Placidus Gervasius Nkalanga, O.S.B. †, Bishop Emeritus of Bukoba
Bishop Renatus Leonard Nkwande, Bishop of Bunda
Bishop Alphonse Daniel Nsabi †, Bishop of Kigoma
Bishop Eusebius Alfred Nzigilwa, Auxiliary Bishop of Dar-es-Salaam

Bishop Anton Oomen, M. Afr. †, Vicar Apostolic Emeritus of Mwanza
Archbishop Francisco Montecillo Padilla, Apostolic Nuncio to Kuwait

Polycarp Cardinal Pengo, Archbishop of Dar-es-Salaam
Bishop Anthony Jeremiah Pesce, C.P. †, Bishop of Dodoma
Archbishop Luigi Pezzuto, Apostolic Nuncio to Bosnia-Herzegovina
Bishop John James Rudin, M.M. †, Bishop Emeritus of Musoma

Laurean Cardinal Rugambwa †, Archbishop Emeritus of Dar-es-Salaam
Archbishop Novatus Rugambwa, Apostolic Nuncio to Honduras
Archbishop Protase Rugambwa, Secretary of the Congregation for the Evangelization of Peoples, Roman Curia
Archbishop Jude Thadaeus Ruwa’ichi, O.F.M. Cap., Coadjutor Archbishop of Dar-es-Salaam
Archbishop Paul Runangaza Ruzoka, Archbishop of Tabora
Bishop Almachius Vincent Rweyongeza, Bishop of Kayanga
Bishop Desiderius M. Rwoma, Bishop of Bukoba

Bishop Justin Tetmu Samba †, Bishop of Musoma
Bishop James Dominic Sangu †, Bishop Emeritus of Mbeya
Bishop Liberatus Sangu, Bishop of Shinyanga
Archbishop Pierluigi Sartorelli †, Apostolic Pro-Nuncio Emeritus to Kenya
Bishop Castor Sekwa †, Bishop of Shinyanga
Bishop Augustine Ndeliakyama Shao, C.S.Sp., Bishop of Zanzibar
Bishop Matthew Shija †, Bishop Emeritus of Kahama
Bishop Joseph Sipendi †, Bishop of Moshi
Archbishop Marek Solczyński, Apostolic Nuncio to Tanzania
Bishop Cassian (Franz Anton) Spiess (Spieß), O.S.B. †, Vicar Apostolic of Southern Zanguebar {Zanguebar Meridionale}
Bishop Eberhard (Hermann) Spiess, O.S.B. †, Abbot Emeritus of Songea
Bishop Thomas (Franz Xaver) Spreiter, O.S.B. †, Vicar Apostolic Emeritus of Eshowe, South Africa
Bishop Gallus (Bernhard) Steiger, O.S.B. †, Abbot Emeritus of Peramiho
Bishop Joseph Franciskus Marie Sweens, M. Afr. †, Vicar Apostolic Emeritus of Victoria-Nyanza

Bishop Laurent Tétrault, M. Afr. †, Vicar Apostolic of Bukoba
Bishop Nestorius Timanywa †, Bishop Emeritus of Bukoba
Bishop William Joseph Trudel, M. Afr. †, Vicar Apostolic Emeritus of Tabora

Bishop Beatus Christian Urassa, ALCP/OSS, Bishop of Sumbawanga

Bishop Herman Jan van Elswijk, C.S.Sp. †, Bishop Emeritus of Morogoro
Bishop Antoon van Oorschoot, M. Afr. †, Bishop of Mbeya
Bishop Jan Cornelius van Sambeek, M. Afr. †, Bishop Emeritus of Kigoma
Bishop François-Xavier Vogt, C.S.Sp. †, Vicar Apostolic of Yaoundé, Cameroon

Bishop Bartholomew Stanislaus Wilson, C.S.Sp. †, Vicar Apostolic Emeritus of Sierra Leone
Father Henry J. Winkelmolen, C.S.Sp. †, Prefect of Same
Bishop Patrick Winters, S.A.C. †, Bishop Emeritus of Mbulu

Bishop Gabriel Joseph Maria Zeiger (Zelger), O.F.M. Cap. †, Vicar Apostolic Emeritus of Dar-es-Salaam
 
Write your reply...mkuu Alfred asante, ila nilikuwa nataks kujua jumbo LA kayanga geographical location au mkoa au wilaya
 
Back
Top Bottom