Wakazi awachimba mkwara mzito EFM

Wakazi awachimba mkwara mzito EFM

sinza pazuri

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2014
Posts
3,344
Reaction score
9,066
IMG_20241010_121321.jpg


Socialite maarufu kwenye mtandao wa X na shabiki wa muziki wa hip-hop ambaye anatrend sana kwa kuchambua wanamuziki maarufu aitwae Wakazi ametishia kuwapiga block kituo cha radio cha EFM.

Ametoa mkwara huo baada ya kuoneshwa video ambayo watangazaji wa EFM walikuwa wanacheka kusikia Wakazi ajulikani anaimba vitu gani.

Socialite huyo ambaye ugeuka mbogo akiulizwa hitsong yake ni ipi? Alionekana kujaa jazba na kutokuwa mvumulivu kusikia maoni kuhusu yeye kama yeye alivyojipa jukumu la kutoa maoni kuhusu kazi za wasanii wengine.

Tunamshauri Wakazi asifikie kuwablock EFM maana akifanya hivyo itaathiri sana biashara ya hiyo radio, yeye ni mtu muhimu sana kwenye hii game anahitajika sana na media kama EFM, maisha bila Wakazi yatakuwa magumu sana.

Atoe msamaha na kusahau yapite yanazingumzika.
 
😄😄 chawa umeandika kinafiki mno. Ila Wakazi kaonyesha kipaji kikubwa kwenye muziki wa mwambao yaani Taarab. Ni muda muafaka wa yeye kujiunga na kundi la Isha Mashauzi ili kutoa hit songs za taarab. Kimsingi Wakazi ana hela zake kwenye muziki wa taarab.
 
Dada Wakazi wa Kazi gani wakati hajulikani hata na Wazazi wake... Mshamba wakazi kutokea bush Mara huko, kakimbia kuchunga mbuzi bush kwao kaja dar kuwa dada wa kazi... 😅😂 Dada wakazi ni useless sasa awablock efm wakat hata hajulikan popote sana sana angeshukuru wamempa kiki kwa kumtag
 
ifike mahali huyu mwamba aachane na mziki awe blogger tu, he always sees negativity in everything. shame on you wakazi.
 
mm ni MDAU mkubwa wa muziki wa BONGO FLEVA na soon tu nafungua label ya muziki (CHANANJA_records).
japo umeandika ukiwa neutral(kinafiki).
wakazi hana influence yoyote ktk huu muziki wa TZ, anaungaunga tu maisha na muziki umemshinda.nafikiri ameathirika ki_SAIKOLOJIA,hana hit_song, anaumwa ugonjwa uitwao BIPOLAR kila akiwaza hilo. atafute kazi nyingine ya kufanya.
 
Usiwe na mtazamo huo ndugu, Zama zimebadilika sana, na kipindi hiki cha socha network mtu kama wakazi anaweza ku survive bila hata wao.
Kwani ni lini wakazi alisurvive kwenye mziki huyu kwenye mziki alikuja kupoteza muda tu ni kama yule dada kasoma USA kaja kufungua biashara ya makande
 
Wakazi ana Ngoma kibao nilimfahamu kipindi kile Cha Kilingeni,kazi mnayo watoto wa juzi
 
Kitu ambacho kinanisikitisha watu wengi wanamchukia sana, huyu jamaa ni rapper mzuri na uandishi flani unique.... Kuna Ngoma ameonyesha flow za ki-unyama sema TU watu hawamtaki na hawamzingatii. Jaribuni kusikiliza flow na uandishi wake kwenye hizi Ngoma

1. Dengue fever-Wakazi
2. Torati ya mtaa - Chindo Man ft Fid Q, Dully Sykes and Wakazi.
 
Back
Top Bottom