Wakazi: Diamond Platnumz ni maarufu ila hajui kuimba, "ukweli unauma mpaka mnanipigia simu za vitisho"

Wakazi: Diamond Platnumz ni maarufu ila hajui kuimba, "ukweli unauma mpaka mnanipigia simu za vitisho"

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
Msanii kutoka Tanzania, Wakazi amesema kwamba Diamond Platinumz ni maarufu ila sio mzuri katika uiambaji.

Kupitia ujumbe aliochapisha kwenye ukurasa wake wa Twitter, Wakazi alisema kwamba kuna tofauti kubwa kati ya umaarufu na ubora wa msanii, na hivyo kuwa maarufu haimaanishi kuwa mzuri katika sanaa ya muziki.

Aidha, Wakazi alikubali kwamba Diamond Platinumz ni miongoni mwa watu watatu maarufu nchini Tanzania ila kwa usanii bado kuna mengi anayopaswa kuyafanya. Wakazi aliweka wazi kwamba kuna watu wanaoimba na kufanya zaidi ya Diamond Platinumz.

Baadhi ya wandani wa Diamond Platnumz walionekana kughadhabishwa na kauli hiyo huku wakitema cheche kali. "Huo umaarufu kaupata kwa sababu gani? Unaweza kuwa bora na watu wasikufahamu?" Wengine waliuliza.

Kauli hii inajiri baada ya Diamond Platnumz kusema kwamba hataki kushindanishwa na wasanii wa ndani ya Tanzania, na kwamba alitaka kushindana na wanamuziki wa kimataifa.

Aidha Wakazi ameweka wazi kuwa kutokana na kusema kauli hiyo amepigiwa simu za vitisho lakini ameonyesha kubaki na msimamo wa kauli yake.

1647426576332.png


======

1647425848901.png

Picha: Webiro Wakazi Wassira
Ameandika Webiro Wakazi Wassira katika akaunti yake ya Twitter

"Kuna tofauti kati ya UMAARUFU na UBORA wa Musicians. Being popular doesn’t necessarily translates to being The Best. That being said, nakubali kuwa Diamond Platnumz is Top 3 in popularity, ila kwa Ubora (artistry) that is a reach… Kuna watu wanaupiga mwingi zaidi yake".

"Nadhani mtazamo wa ukali wa msanii ndio unategemea ntu na ntu! Kwenye ubora, nazingatia vigezo vya kiufundi, pia kufanya kwa muda mrefu bila kushuka kiwango huku unaendelea kuzingatia vigezo hivyo. Ila kuwa “mkali” au “msanii pendwa” ni sikio lako. Umaarufu unatokana na mengi".

"Wanasema Ukweli unauma… Hii imeuma sana inaonyesha, hadi napigiwa simu za vitisho"?


Pia soma: Diamond Platnumz ahoji kwanini Ali Kiba (mkongwe) hana media yake? Atoa onyo kushindanishwa na wasanii wa Tanzania 'ni wadogo sana kwake'
 
Huyu nae anahamu ya kuongea, unapigiwa simu na watu baki unaogopa. Je zingekuwa simu za mashabiki wa Yanga na Simba, manake wale ndio wana maanisha.

Halafu hao wanamtisha si awaripoti vyombo vya usalama, mwisho wa siku watamwona kama anataka kiki.
 
Wakazi yuko sahihi Diamond hata atoe ngoma ya dakika mbili halafu humo ndani awe anacheka mwanzo mwisho utaona ngoma hiyo itavyokuwa trend na usikute ikapewa na tuzo

Hayo yote yamerahisishwa kutokana na jina (umaarufu) na ndio maana hata hawa ma underground wana amini wakipata nafasi ya kufanya kazi kwenye lebel yao watatoka tu, kwasababu kitachowafanya wajulikane sio ubora wa kile wanachokiimba

Means hata kwa level zao za huku chini wanaamini hata wakaze msuli namna gani bado ubora wa nyimbo hautakuwa kigezo wao kutoka

Nakubaliana na Wakazi
 
MOST OF THEM NI WIVU HILO HALINA UBISHI.ETI NI MAARUFU HUO UMAARUFU KAUPATA KUPITIA NINI???

NI UJINGA PIA KUCHUKIA MAFANIKIO YA MWENZIO.
Kuwa na mawazo hayo ni dhana mbaya sana ya kimasikini na yenye utabaka, kufikiria mwenye haki ya kukosolewa ni yule ambaye hana kitu, kuwa hata ukimkosea watu watasema ni sawa as long as hana kitu cha thamani cha kukufanya uonekane mkosoaji una wivu nacho

Kwamba mkosoaji amemuona Diamond kuwa ni tajiri sana kiasi cha kumonea wivu kuliko MO na Bakhresa ambao wako kwenye rank za matajiri Africa?
 
Wakazi yuko sahihi Diamond hata atoe ngoma ya dakika mbili halafu humo ndani awe anacheka mwanzo mwisho utaona ngoma hiyo itavyokuwa trend na usikute ikapewa na tuzo

Hayo yote yamerahisishwa kutokana na jina (umaarufu) na ndio maana hata hawa ma underground wana amini wakipata nafasi ya kufanya kazi kwenye lebel yao watatoka tu, kwasababu kitachowafanya wajulikane sio ubora wa kile wanachokiimba

Means hata kwa level zao za huku chini wanaamini hata wakaze msuli namna gani bado ubora wa nyimbo hautakuwa kigezo wao kutoka

Nakubaliana na Wakazi
Mfano ni baba Levo sijui anaimb nini jamani mnisaidie mnaomwelewa mim naona makelele tu
 
Kuwa na mawazo hayo ni dhana mbaya sana ya kimasikini na yenye utabaka, kufikiria mwenye haki ya kukosolewa ni yule ambaye hana kitu, kuwa hata ukimkosea watu watasema ni sawa as long as hana kitu cha thamani cha kukufanya uonekane mkosoaji una wivu nacho

Kwamba mkosoaji amemuona Diamond kuwa ni tajiri sana kiasi cha kumonea wivu kuliko MO na Bakhresa ambao wako kwenye rank za matajiri Africa?
Wasanii Tz ni wengi mno kwanini yeye ndo wanamkosoa kila siku?? Yani akitoa kitu lazima KWANINI ziwe nyingi??

Afu kingine sawa hajui kuimba huo umaarufu umetokana na nini??? JE HAO WANAOMZIDI KUIMBA MBONA HAWAWI MAARUFU KAMA YEYE?? HAWAPATI PESA KAMA YEYE???

NDO ILE YA MSUVA NA SAMATTA ETII OO MSUVA ANAJUA WAKATI ANAZEEKA HATA LIGI YA BELARUS HAJACHEZA😂😂😂
 
Msanii kutoka Tanzania, Wakazi amesema kwamba Diamond Platinumz ni maarufu ila sio mzuri katika uiambaji.

Kupitia ujumbe aliochapisha kwenye ukurasa wake wa Twitter, Wakazi alisema kwamba kuna tofauti kubwa kati ya umaarufu na ubora wa msanii, na hivyo kuwa maarufu haimaanishi kuwa mzuri katika sanaa ya muziki.
Nawe ukaona utuletee mambo ya Webiro.

Hivi huyu Diamond aliupata wapi huo umaarufu kama sio kwenye uimbaji wake mzuri, kucheza kwa kuburudisha, kujua soko linataka nini, na kutojikweza.
 
mfano ni baba levo sijui anaimb nini jamani mnisaidie mnaomwelewa mim naona makelele tu
Sasa huyu watu wanaweza kuku support kwasababu hamiliki rolls Royce, ila ukimgusa boss huo ni msala mwingine
 
Kuwa na mawazo hayo ni dhana mbaya sana ya kimasikini na yenye utabaka, kufikiria mwenye haki ya kukosolewa ni yule ambaye hana kitu, kuwa hata ukimkosea watu watasema ni sawa as long as hana kitu cha thamani cha kukufanya uonekane mkosoaji una wivu nacho

Kwamba mkosoaji amemuona Diamond kuwa ni tajiri sana kiasi cha kumonea wivu kuliko MO na Bakhresa ambao wako kwenye rank za matajiri Africa?
SAWA SWALI NI KWAMBA HAOOO WANAOMZIDI KUIMBA, HAO WENYE MELODY NZURI, HAO WENYE TUNGO KALI NA SAUTI YA KUVUTIA MBONA HAWAFIKI POPOTE??? MBONA KAZI ZAO HAZISONGI KAMA ZA HUYO WANAEMKOSOA???

NAJUA MNAJUA, NA TUNAJUA MNAJUA TUNAWAPIGAJE MNAJUA😂😂😂
 
Wasanii Tz ni wengi mno kwanini yeye ndo wanamkosoa kila siku?? Yani akitoa kitu lazima KWANINI ziwe nyingi??

Afu kingine sawa hajui kuimba huo umaarufu umetokana na nini??? JE HAO WANAOMZIDI KUIMBA MBONA HAWAWI MAARUFU KAMA YEYE?? HAWAPATI PESA KAMA YEYE???

NDO ILE YA MSUVA NA SAMATTA ETII OO MSUVA ANAJUA WAKATI ANAZEEKA HATA LIGI YA BELARUS HAJACHEZA😂😂😂
Nani alikuambia wasanii wengine hawakosolewi?

Wanakosolewa ila tatizo ni kwamba hawajafanikiwa kujenga fanbase kubwa ya utimu kufanya mashabiki wao wawe wanawatetea kipindi wanakosolewa

Swali lako la pili ni kituko na kuonesha kuwa kuna mambo lundo yanakupita, unamjua lil pump?

Ahh huko mbali tuanze hapa hapa Africa, kuna jamaa aliimba parakata tumba unamjua?
 
Sisi tunataka kujua huo umaarufu kaupata wapi ikiwa hajui chochote kwenye kuimba, kama mnavyodai?

Hao wanaojua kuimba ni nani na nani? Watajeni hapa kisha mtueleze kwanini wao sio maarufu kama Diamond.

Kuwa mwanamziki sio kujua kuimba tu, ukiachana na kuimba Mond kawazidi wengine vitu vingi sana kuhusu mziki.

Kuhusu wakazi, ni moja kati ya wasanii ambao wamedumu kuwa ma-underground kwa miaka mingi sana.
 
Wa kazi huwa namuelewa sana , mshikaj mziki hajui Ila mawazo yake (thinking capacity ) anawakalisha mpak TISS...!! Kuna tofauti kubwa Kati ya umaarufu na ubora , kuna shortcut nyingi za kufikia umaarufu Ila ubora ni scientific term
 
Msanii kutoka Tanzania, Wakazi amesema kwamba Diamond Platinumz ni maarufu ila sio mzuri katika uiambaji.

Kupitia ujumbe aliochapisha kwenye ukurasa wake wa Twitter, Wakazi alisema kwamba kuna tofauti kubwa kati ya umaarufu na ubora wa msanii,
Huyu nae ni kama demu wa kizaramo,amekosa significance sasa anatafuta kiki,kama hajuhi kuimba,amepata umaharufu vipi?
Mbona wengine hawana umaharufu,umaharufu hauji kwa kuota,lazima ufanye kazi,na kwa mond kazi yake kwa miaka 10+ ni muziki,sasa utasemaje hajuhi kuimba!!!wewe unaejua kuimba mbona hata umaharufu huna,ukipita Moro mjini,hakuna anaekufahamu,muacheni mtoto wa tandale apige pesa
 
Back
Top Bottom