Wakazi wa Chumba Kimoja Tukutane Hapa

Wakazi wa Chumba Kimoja Tukutane Hapa

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,258
Baada ya Kuishi kwenye chumba kimoja huu ndio uzoefu wangu

  1. Ukitaka kumjua mkazi wa chumba kimoja mtembele kuanzia saa tatu hivi usiku, utakuta kila kitu ndani yakiwemo majiko, ndoo nk
  2. Ni ngumu sana kujua lilipo dirisha la chuma kimoja kwani aghalabu ndimo huegemezewa kabati la vyombo ama nguo
  3. Uvundo ndio mahakama ya chumba kimoja sababu ya mlundikano
  4. usistuke kuona panya ama mende kwenye chumba kimoja na hapo ni pale unapobahatika kwani unaweza kuondoka na wale jamaa
  5. ukiona kamba kwenye chumba kimoja imekatiza basi ujue siku hiyo kavaliwa........
  6. kuna mashuka ya mchana na ya usiku.................
  7. ...............ongeza........................
 
Baada ya Kuishi kwenye chumba kimoja huu ndio uzoefu wangu

  1. Ukitaka kumjua mkazi wa chumba kimoja mtembele kuanzia saa tatu hivi usiku, utakuta kila kitu ndani yakiwemo majiko, ndoo nk
  2. Ni ngumu sana kujua lilipo dirisha la chuma kimoja kwani aghalabu ndimo huegemezewa kabati la vyombo ama nguo
  3. Uvundo ndio mahakama ya chumba kimoja sababu ya mlundikano
  4. usistuke kuona panya ama mende kwenye chumba kimoja na hapo ni pale unapobahatika kwani unaweza kuondoka na wale jamaa
  5. ukiona kamba kwenye chumba kimoja imekatiza basi ujue siku hiyo kavaliwa........
  6. kuna mashuka ya mchana na ya usiku.................
  7. ...............ongeza........................
Pazia lazima lihusike hapo la mlangoni
 
Ole wako umwibukie usiku bila taarifa! Utakachokiona hutoamini. Utakuta mtu mchana anapigilia suti, lakini anapolala sasa mama yangu!
 
Chini ya vungu kumejaa sahani ya jana na kikombe cha wiki jana. Aisee nakomaa nimalizie geto hawa jamaa wa maliasili watataifisha mbao zangu sijui. Nimepasua mwenyewe kupunguza gharama
 
Hata wakazi wa chumba kimoja hawapendi kuishi vile wanavyoishi ni maisha tu yamewalazimisha kuwa hivyo walivyo, mfano mzuri mi nimeanzia huko na ndiko kulikonipa uchungu wa kutafuta maisha zaidi baada ya kuchukia maisha ya mkazi wa chumba kimoja,

“Intelligence without ambition is a bird without wings.”
 
Back
Top Bottom