Wakazi wa kijiji cha Ng'wan'holo Mwadui na hofu ya maradhi ya maji taka kutoka mgodini

Wakazi wa kijiji cha Ng'wan'holo Mwadui na hofu ya maradhi ya maji taka kutoka mgodini

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
majitakaapiic.jpg


Wakati Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) likiendelea kuzuia majitaka yenye tope yanayotoka katika mgodi wa Williamson Diamond kuingia kwenye makazi ya watu, wataalamu wa madini wameonya wananchi kutoyasogelea hadi watakapopewa taarifa yapo salama.

Maji hayo ambayo NEMC inaendelea kuyadhibiti, yametokana na bwawa la majitaka la mgodi huo unaomilikiwa na kampuni hiyo (asilimia 75) na Serikali (asilimia 25) kupasuka majuzi na kutiririsha maji hayo yenye tope kwenye makazi ya watu.

Akitoa tahadhari kwa wananchi, Mtaalamu wa Madini katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Karim Baruti alisema kama kuna mito katika maeneo ambayo tope hilo linatiririka, wananchi wanapaswa kuchukua tahadhari.

“Ni lazima tujue hayo maji yakitoka yanaelekea wapi, yatakuwa na athari kwenye eneo kubwa au dogo, lakini wananchi hawapaswi kuyasogelea au kuyatumia mpaka watakapoambiwa ni salama au sio salama,” alisema.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Sophia Mjema aliyezungumzia suala hilo juzi, tayari nyumba ambazo zimezingirwa na tope hili ni 13 na wananchi walioathirika ni 59 na watoto watatu walipata shida ya homa ya kutapika na wanaendelea na matibabu.

Kutokea kwa tukio hilo, wananchi katika kijiji hicho wameiomba Serikali iwasaidie kwa haraka ili kuepukana na maji hayo, kwa kuwa maji hayo yameingia pia katika bwawa lenye maji wanayotumia kupikia na kunywa.

Taarifa ya Petra Diamond, kampuni tanzu inayomiliki mgodi huo iliyotolewa katika mtandao wa Miningmx imesema kwa sasa uzalishaji umesimamishwa kutokana na ajali hiyo.

“Hakuna vifo vilivyothibitishwa kutokea kutokana na kupasuka kwa bwawa hilo,” imeeleza taarifa hiyo.
Wawakilishi wa kampuni pamoja na Serikali na huduma za dharura wanaendelea kuwaweka wanavijiji mbali na eneo lililoathirika,” imesema taarifa hiyo.

Mwananchi
 
Uzuri wa processing ya almasi haitumii kemikali sana kama kwenye dhahabu.
 
Back
Top Bottom