Ndugu wadau, nilikuwa nafuatilia 'issue' ya wakazi wa Kipawa kwenye luninga wiki iliyopita nikasikia kuwa Serikali inatumia Sheria ya Ardhi ya mwaka 1967 na siyo ya 1999. Kwanza, msemaji mmoja wa Wizara ya Ardhi alisema, "Wananchi wakilipwa kwa sheria ya 1967 watanufaika zaidi kuliko ya 1999."
Niliona kama kunufaika kwa wananchi ndiko kulikoifanya Serikali itumie sheria ambayo haitumiki tena, basi Serikali yetu inawajali sana watu wake. Lakini kadiri nilivyoendelea kusikiliza niligundua kuwa siyo kweli. In fact, kwa kutumia Sheria ya Ardhi ya 1999, wakazi hao wangenufaika zaidi na hivyo msemaji huyo wa Ardhi alikuwa anasema uongo.
Hoja yangu hapa ni kwamba kama hii itakuwa 'trend' ya kuchagua ni sheria gani itumike (kama hata hizo ambazo hazitumiki zinatumika tena), je kutakuwa na sababu gani ya kuendelea kutunga sheria mpya kama za zamani zinaweza kutumika tena?
Niliona kama kunufaika kwa wananchi ndiko kulikoifanya Serikali itumie sheria ambayo haitumiki tena, basi Serikali yetu inawajali sana watu wake. Lakini kadiri nilivyoendelea kusikiliza niligundua kuwa siyo kweli. In fact, kwa kutumia Sheria ya Ardhi ya 1999, wakazi hao wangenufaika zaidi na hivyo msemaji huyo wa Ardhi alikuwa anasema uongo.
Hoja yangu hapa ni kwamba kama hii itakuwa 'trend' ya kuchagua ni sheria gani itumike (kama hata hizo ambazo hazitumiki zinatumika tena), je kutakuwa na sababu gani ya kuendelea kutunga sheria mpya kama za zamani zinaweza kutumika tena?