KERO Wakazi wa Pugu, Kinyerezi na Viwege tunalaza magari barabarani kutokana na ubovu wa miundombinu

KERO Wakazi wa Pugu, Kinyerezi na Viwege tunalaza magari barabarani kutokana na ubovu wa miundombinu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mzee wa Code

Member
Joined
Sep 23, 2024
Posts
61
Reaction score
91
Sisi Wakazi wa maeneo ya Viwege na Pugu Kinyamwezi, Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam tumekuwa na changamoto ya kuwa na barabara mbovu, ikinyesha mvua ndio kabisa hali inazidi kuwa mbaya kuliko maelezo.

Barabara za mitaani kwetu zimeharibika vibaya, hali inayotulazimu kulaza magari mbali na nyumbani maeneo ya barabarani na kulipia Tsh. 2,000 kwa siku.

Gharama hizo zimekuwa mzigo mkubwa kwetu kwa kuwa tunalipa hivyo kila siku, wakati wengine maeneo ya kuegema magari yapo kwenye makazi yetu lakini hatufiki kutokana na changamoto ya barabara.

Tunazitaka mamlaka husika ikiwemo TARURA kuingilia kati na kufanyia matengenezo barabara hiyo kwa haraka.

Hali hii imekuwa kero kwetu Wananchi na tunaiomba Serikali ichukue hatua haraka ili kurahisisha usafiri na kupunguza mzigo wa gharama.
 
Halafu kuna taahira linakuja kujisifu humu eti mama yake amevunja rekodi ya kukusanya mapato.

Mapato ya nyoko!
 
Halafu kuna taahira linakuja kujisifu humu eti mama yake amevunja rekodi ya kukusanya mapato.

Mapato ya nyoko!
Ngazi zetu za Mitaa kuna changamoto nyingi sana wananchi wangejua umuhimu wa wenyeviti wa mitaa nadhani wangesimama imara kulinda kura
 
Ngazi zetu za Mitaa kuna changamoto nyingi sana wananchi wangejua umuhimu wa wenyeviti wa mitaa nadhani wangesimama imara kulinda kura
Kwembe,king'az na malamba toka 2023 nov,watu wanalaza magari barabarani kutokana barabara kuharibika,na mwaka jana ccm imeshinda chaguzi za serikali za mitaa huku watu wakiwa awaamini
 
Back
Top Bottom