wake 4 rukhsa UK

Now I have another reason to move my base to somewhere near Leincester...

Nadhani inabidi ianze kampeni ya kuruhusu pia waume 4 kwa mke mmoja huko Arabia na kokote kule kwenye hizi sheria if that is to be the norm of life (which I dont see it this way) all over the world!
 
Mwafrika wa Kike,
Dada yangu gari kinaweza chukua abiria wanne lakini abiria wanne hawawezi beba gari moja, safari haitakuwepo!.... Haa haaa haaa!.... Mbwa ruksa kuwa na madume zaidi ya mmoja na sidhani kuna mwanamke atapenda kufananishwa naye...

Admin,
Please unaweza kuihaisha mada hii kule kwenye dini maanake sielewi kabisa inachoendelea hapa. Kuruhusiwa kwa waislaam kuwa na wake wanne na hayo ya Eastern Europe?... Navyojua mimi ni Turkey na Bosnia tu zenye waislaam lakini zilizobaki zote ni nchi zenye kikristu na pengine hakuna kabisa Muislaam isipokuwa mhamiaji.
Kuwa na wake wanne haikuanza jana toka Nabii Ibrahim, church za Katoliki ndio waliobadilisha as a fact ukitazama mti wa kizazi cha Ibrahim utakuta karibu mitume wote walikuwa na wake zaidi ya mmoja..Sasa hilo agano a kale tunachagua cha kufuatana vingine tuviache?
Tatizo kubwa la Uislaam ni kuendeleza yale yaliyokubaliwa na mwenyezi Mungu toka zamani hali dini nyingine zinatupa mabadiliko yaani changes kiasi kwamba najiuliza kumbe Mungu naye alikuwa akifanya makosa kiasi kwama binadamu wamepewa nafasi ya kurekebisha kipi halali na kipi haramu..damn!
Mtalia sana jamaa zangu, mbona mwala nguruwe na halali yenu nasi hatupigi kelele...
 

Haya Mkuu nimekuelewa katika hili! hasa mfano wa gari ambao sasa unadhihirisha kabisa kuwa hii mada inabidi iende kule kwenye dini au somewhere!
 
Mwafrika wa Kike,
Heee hee heeee! patamu hapo dada yangu.... Kwanza mimi naona wivu sana kuwa wanawake tu ndio wanaozaa..
 

Mtanzania,
Nashukuru sana kwa ufafanuzi wako. Hiyo habari aliyo quote Kibunango niliisoma kwenye gazeti la kila siku la huko (Daily Express), ndio sababu hasa nikaandika hayo. Nilikuwa UK wiki iliyopita na nilikerwa sana na habari hiyo.
 

Si Uingereza pekee yenye interest za kibiashara katika nchi hizo, kwa mfano hivi karibuni Nokia walipoamua kufunga kiwanda chao chta ujerumani, wafanyakazi waliandamana na zaidi chancellor wao alikuja juu. Lakini haikusaidia kitu.

Kuhusu hizo benefits kwa wakaazi, sina ufahamu mkubwa nazo, ila kwa macho na masikio yangu nimeona jinsi baadhi ya watanzania hapo UK wakizitegemea katika maisha yao ya kila siku. Hali hii imewafanya kuwa na familia kubwa ili kuweza kupata benefit nyingi zaidi.
 

Mtanzania,
Tunakuomba tufafanulie hii benefits inafanyaje kazi hapo kwenu UK, kwa sababu nimesikia kwamba wenyeji wengi hawafanyi kazi kwa kutegemea hizo pounds 200 kwa wiki ambazo huwawezesha kuishi bila shida. Hapa nilipo kuna hico kitu ila nahisi ni tofauti kidogo na hapo UK.
 
Haya Mkuu nimekuelewa katika hili! hasa mfano wa gari ambao sasa unadhihirisha kabisa kuwa hii mada inabidi iende kule kwenye dini au somewhere!

Kheeee heeee heeee,
baada ya kupewa dongo naona mbio mbio, unashauri mada ihamishwe. Mada hii zaidi ya hizo ndoa ilikuwa inazungumzia ubaguzi, siasa za ulaya na biashara.
 
Sasa hii issue ni kwa mwanaume ambaye atakuwa na wake wanne. Itakuwaje kwa mwanamke mwenye waume wanne?
 
Sasa hii issue ni kwa mwanaume ambaye atakuwa na wake wanne. Itakuwaje kwa mwanamke mwenye waume wanne?

Sasa hiyo ya mke kuwa na wanaume wanne tutaitaje, "tetra-gamy" ama itaendelea kuwa 'polygamy' kama ilivyo kwa mume mmoja kwa wake zaidi ya mmoja?
 
Suala la ubaguzi linazidi kushika kasi katika nchi nyingi sana za Ulaya. Miaka michache hapo nyuma walikuwa wakihaha kuwabagua Waafrika na wale Wahindi wekundu wa Amerika Kusini pamoja na Waasia kwamba wanajaza nchi zao na kuwamalizia rasilimali, sasa naona wameingilia kuwabagua wazungu wenzao. Hili suala kwa kweli linakera sana, hata mie nilikereka sana na maswali ya ajabu ajabu pale Stansted Airport Uingereza wiki iliyopita ambayo yamekaa kibaguzi baguzi sana. Lakini niliwajibu 'kinyodo' kwamba sikuwa na lengo la kuishi nchini mwao kwa namna yoyote ile kwa sababu za ubaguzi kama huo waliouonyesha hapo uwanja wa ndege, kwa hiyo siwezi kuishi kwa amani kama ilivyo nyumbani kwetu!
Wakabaki wameachama midomo na kutoamini kwamba Mwafrika anaweza kuiponda nchi "iliyoendelea" kama yao!.
Pumbavu zao!
 
Kaazi kweli kweli. Yaani nyie kazi zenu kuutukana tu Uislam. Mbona kuna Wakristo wengi tu wanazaa hovyo na vimada. Na cha ajabu siku hizi kanisa linahalalisha watoto wa nje ya ndoa.

Kama hujui kitu ni bora ukauliza ueleweshwe.

Kabla ya Uislam watu matajiri Middle East na duniani kote walikuwa wanaoa wake wasio na idadi kulingana na mfuko wa mtu 10, 20, 30, 100, nk. Wengine walikuwa wakichukuwa mabint na kuwabikiri basi hawawarudii tena. Lakini anaitwa mke wa fulani. Haki yake ya unyumba hapewi na anatakiwa kukaa hivyo hadi umauti umkute.

Uislam uliondoa tabia hii na ikaweka kiwango cha mwisho wake wanne kwa mwenye uwezo economically, physically.

Haitoshi kuoa mke halafu huduma muhimu pamoja na tendo la ndoa humtimizii. Utakuwa umekiuka maadili ya ndoa.

Sheria ya mke mmoja imeshindwa kuondoa uzinzi. KWa mfano mtoto wa Malkia wa Uingereza Prince nani sijui, angeruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja, asingemtaliki Diana. Angeweza kuwa nao wote Diana na Camila.

Ruhusa ya kuoa zaidi ya mmoja ina faida zake

1. Wake wote wanakuwa na haki sawa ukiondoa kuheshimiana kati ya aliyetangulia kuolewa na wake wanaofuta. Mume anatakiwa kutoa haki sawa kuanzia matunzo na hata unyumba. Ndiyo maana anatakiwa kila nyumba akae kwa siku sawa na nyingine. Sio leo kwa Bi Fatuma siku nne, kwa Wadiri saa moja, kwa Kidawa siku mbili.

2. Watoto wote wanaozaliwa wana haki sawa kwa baba yao. Hakuna cha mtoto wa nyumba kubwa wala nyumba ndogo

3. Uwajibikaji. Kuna tabia ya wanaume wakristo wanajidai wana ndoa ya mke mmoja, huku mitaani wana watoto kibao ambao wanawatelekeza. Mama anaogopa kwenda kudai haki ya matunzo ya mtoto kwa sababu ati ni mume wa mtu.

4. Imethibitika kuwa katika ndoa za mitala maradhi ya zinaa ni kidogo sana. kwa anayebisha atazame data za ukimwi duniani. Hata hapa Bongo kuna utafiti ulifanywa kwa waathoirika wa Ukimwi na ilionekana kuwa wengi wao wana ndoa za mke mmoja.

Najua kuna watakaobisha. Endeleeni tu kubisha
 

MaMkwe,
Yaani unaongea mno ukweli- ila angalia walokole wasije kukupiga madongo!

Kweli HIV infection kwa ndoa ya mke mmoja ni kubwa zaidi- hata Middle East pia HIV infection ni kidogo sana!

Tatizo la sisi Wakristo ni unaafiki- tunaenda kanisani na wakati tuna nyumnba ndogo!

hizi mila za mke mmoja ni za wazungu- ndo wanaweza- na sisi Waafrika kusema kweli tumeiga tu! Mababu zetu wote walioa mke zaidi ya mmoja!

Nimependa sana jinsi ulivyokuwa muwazi!
 
Hivi ni taratibu zipi mtu anatakiwa kuzifuata ili awe muislam...
 

MASATU ukitaka uingie ktk UISLA anzisha thread kule kwenye DINI...wapo akina Zomba..Best..Fundi Mchundo etc...

Nafikiri hicho ndicho wanachokiogopa wengine juu ya Mwelekeo ya UK na Media zake..
Canterbury Archbishop Supports Shari`ah

1. http://www.islamonline.net/servlet/...57694529&pagename=Zone-English-News/NWELayout

Hii habari ipo BBC, hata yahoo news...

2. Qaradawi No Hate Preacher: UK Muslims [Shekhe wa Kiislam Anyimwa VISA ya MATIBABU ya kuingia UK]

http://www.islamonline.net/servlet/...57690963&pagename=Zone-English-News/NWELayout

pamoja na UK kuwa kimbilio na waislam wengi, bado pia ni Kikwazo kwa waislam wengine.

News zote hizi zipo BBC,CCN, Yahoo, Google news....


Nimeunganisha hizi recent news kwa kwakuwa zote from UK na hasa zinawagusa kwa namna moja au ingine waislam lkn pia lina Taathira ktk maisha ya watu wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…