Wakenya hebu nifafanulieni kuhusu Ugavana, Useneta na Ubunge huko kwenu

Wakenya hebu nifafanulieni kuhusu Ugavana, Useneta na Ubunge huko kwenu

Dodoma leo

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2021
Posts
1,336
Reaction score
1,658
Naomba ufafanuzi kuhusu nafasi za kisiasa za ugavana, useneta na ubunge.
Kwa vigezo vifuatavyo.

Kiongozi yupi ni mkubwa kuliko wengine, magavana wapo wangapi nchi nzima, maseneta pia na wabunge.
 
Naomba ufafanuzi kuhusu nafasi za kisiasa za ugavana, useneta na ubunnge.
Kwa vigezo vifuatavyo.

Kiongoz yupi ni mkubwa kuliko wengine,
magavana wapo wangapi nchi nzima, maseneta Pia na wabunge.
Kila kiongozi ako jukumu lake la kikatiba. Ukubwa hatuujali vile ikiwa unatekeleza majukumu yako.

Maseneta na Wabunge ni wawakilishi. Seneta anawakilisha county/gatuzi, mbunge anawakilisha eneo bunge. Gavana ni msimamizi mkuu mtendaji wa kaunti. Kunao pia MCAs wanawakilisha ward ambayo ni maeneo madogo ya county. Hawa wote wanapigiwa kura na wananchi.
 
Kila kiongozi ako najukumu lake la kikatiba. Ukubwa hatuujali vile ikiwa unatekeleza majukumu yako.

Maseneta na Wabunge ni wawakiluishi. Seneta anawakilisha county/gatuzi, mbunge anawakilisha eneo bunge. Gavana ni msimamizi mkuu mtendaji wa kaunti. Kunao pia MCAs wanawakilisha ward ambayo ni maeneo madogo ya county. Hawa wote wanapigiwa kura na wanainchi.
Ok umenielewwsha kidogo. Nani anaweza mkoromea mwingne wajibu usipotimizwa au kila mmoja ni kambale??
Je uwiano wa wabunge kila kaunti uko Sawa au inategemea na ukubwa wa eneo
 
Kuna county/gatuzi.. Kila county Kuna governor anayeitawala. Gavana nikama rais wa county. Kuna county 47.

Kila county iko na seneta, na maseneta wengine 20 wameteuliwa, so 67 in total

Maseneta kazi yao ni kujadili mijadala inayohusu county, pia wanaweza kumtimua (impeach) raisi, naibu wa rais, gavana, naibu wa gavana. The seneta ni upper house

Kuna maeneo mbunge 300++ na kila eneo mbunge lina MP/Mbunge. Na pia kuna wambunge kadhaa wa kuteuliwa(appointed).

Kazi yao ni kujadili mambo yanayoihusu inchi. Kuna mijadala wanashirikiana na maseneta. Bunge lao ni Lower house.
 
Ok umenielewwsha kidogo. Nani anaweza mkoromea mwingne wajibu usipotimizwa au kila mmoja ni kambale??
Je uwiano wa wabunge kila kaunti uko Sawa au inategemea na ukubwa wa eneo
MCA watamkoromea gavana. Wabunbge na maseneta watamkoromea Rais. Maeneo bunge yote ni sawa, yako na idadadi sawa ya watu inchini. Ward pia ziko hivyo. Kaunti ndio tofauti kwa idadi ya watu na ukubwa lakini maseneta wako na kura sawa kwenye Seneti.
 
Ingawaje mimi siyo Mkenya lkn huenda huko mara nyingi nilivyoelewa ni kwamba Gavana ni kama Mkuu wa Mkoa lkn aliyechaguliwa na wananchi kwetu anateuliwa na kutenguliwa na raisi, MCA ni Diwani kwa huku kwetu tofauti MCA analipwa hela ndefu sana, Mbunge ni kama Mbunge huyo Seneta hatuna ulinganifu na hata mimi sijui kazi yake lkn wote hao wana mishahara mirefu na privileges zote kwa kifupi ni mfumo aghali sana na chaotic kwa maoni yangu lkn wameuchagua na wameona unawafaa hivyo ni sawa tu kwao!
 
Gavana ni yule ambaye ana kitambi kikubwaa, alafu ana kiburi kupindukia. 😄 Kisa eti anaitwa his excellency, mke wake first lady na yeye ni rais wa 1/47 ya taifa la Kenya. Ana mawaziri ambao anawateua kusimamia sekta tofauti kwenye gatuzi lake. Ana hela za bajeti ambazo anapokea kutoka kwa serikali kuu, 35% ya hela zote ambazo zinakusanywa nchini.

Yeye kupitia wawakilishi kwenye bunge la gatuzi lake, almaarufu MCA(madiwani), ndiye anayeamua masuala yote yanayohusiana na maendeleo kwenye gatuzi lake. Seneta naye ni mwakilishi wa gatuzi lake kwenye bunge la kitaifa, seneti(upper house).

Alafu hayo yote yanajirudia kwenye level ya kitaifa. Wabunge wakiwa kwenye ngazi ya chini, pamoja na wawakilishi wa kina mama, Women Rep. Wakiwakilisha maeneo bunge yao kwenye bunge la kitaifa, Lower House. Wakisimamia maendeleo, sheria, miradi ya serikali kuu chini ya rais, wizara tofauti na mihimili mingine ya serikali. Wote hao wanachaguliwa moja kwa moja na wananchi kwenye uchaguzi mkuu, kila baada ya miaka mitano.
 
Back
Top Bottom