Wakenya.... Kwanini mna lafudhi mbaya sana mazee??

Wakenya.... Kwanini mna lafudhi mbaya sana mazee??

Hehehe! Huwa mna nongwa sana nyie, hamkawii kuibuka na hizi mada za kupimana urefu wa dushe. Nimewaambia mara si haba kwamba Wakenya hatuwezi fugwa kwenye zizi la lugha moja kama mazombi, sisi ni wajanja wa lugha, tunaongea nyingi.
Tunapenda zetu za asili, na tunaongea pia za kigeni. Hii ndio sababu moja ambayo imetufanya kuwa wajanja zaidi ya raia wa nchi zote ukanda huu wote wa Afrika Mashariki na Kati. Wanasayansi walifanya utafiti uliodhihirisha kwamba mtu mwenye kuongea lugha kadhaa ana uawezo mkubwa kiakili na kimawazo.

Sasa nyie Wabongo mumefungiwa kwenye lugha moja, na hata hicho Kiswahili wengi hamkijui vizuri kwa ufasaha. Nikiangalia alivyoandika mleta mada, humo kuna makosa mengi ya kiufasaha halafu anajinadi kwamba yeye mtaalam wa Kiswahili. Vijana wa mjini kazi kuvaa milegezo na kuimba Bongo flava na kuomba omba buku jero mjini.
We unaongea poa kabisa mkuu
 
Kenya nchi iliyo kosa muelekeo wa kujitambua, mpaka mkijitambua ndio mtaelewa matatizo ya kutokuwa na lugha moja yana changia na mengine zaidi. Kikuyu wanatetea kikikuyu chao, kalenjin hivyo hivyo, Luo nao pia, pwani hawataki mchezo. Nchi zote za Ulaya na Marekani,China, Russia nk.... kila moja ina lugha yake ambayo wote wanaitumia na kuelewana. Lugha moja Imesaidia kuwaunganisha waTanzania ambapo kuna makabila 120, na kila kabila lina lugha yake ya asili, kiswahili kimetumika kama chombo cha kuunganisha makabila yote hayo na kupunguza ule
u-mimi ktk nchi. Hata kwenye nyanja muhimu kama usafiri wa anga wa kimataifa, wanatumia kingereza kuweza kuelewana nini kinafanyika. Fikiria jeshi au polisi kila mtu ana lugha yake, kungekalika hapo? Mpaka wakenya wakijielewa kwamba ni lugha gani wanaipenda zaidi, ndio wataitumia kutatua matatizo yao ya kijamii.
 
Back
Top Bottom