Wakenya, nikiwa mtanzania je naweza kuagiza gari lifikie kenya ila nilitumie Tz, huku hali imekuwa mbaya

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Hali ya Tz kwa sasa, Ukaguzi wa gari unafanyika hapa hapa Tanzania na sio kufanyikia kwenye nchi unayoagizia gari kama japan.

sheria mpya ni kwamba gari halikaguliwi kwenye nchi linapotoka, linakaguliwa likifika hapa tz.

Sasa mimi nataka gari ikaguliwe huko huko japan, sitaki gari niliyoagiza ianze kufunguliwa na kuchokonolewa kwajili ya ukaguzi huko bandarini na mwisho wa siku baada ya kusubiri almost 1 month ya inspection nitumiwe bili kwamba nahitaji kulipia spea mpya na matengenezo ili gari likidhi viwango wakati zamani gari likikaguliwa huko japan kama ni bovu napewa option ya kuchagua gari nyingine au litatengenezwa huko huko bila mimi kugharamika.


Gari hizi ni used na nyingi zimevuka hata kilimota elf 70, probanility ya gari used kuwa na matatizo ni kubwa,ni kitu ambacho kinaongeza uhakika kwamba gari ikifika bandarini automatically haitafikia good standards, so itakubidi ulipie gharama za matengenezo ambayo inaweza kuwa bei mno na mbaya zaidi ukishindwa hizo gharama automatically inabidi tu ulitelekeze.

Kwa bureacracies hizi mtu ukiona gari inatumia mda mrefu kukaguliwa au ukianza kuhofia
gharama kubwa za matengenezo unaanza kupata idea chafu za kutoa kitu kidogo which is really bad

references: TBS mnaandaa mazingira ya rushwa ukaguzi wa magari?
 
Hapo lazima ujitathmini sana usije ukaona km unaruka mikojo kumbe ukajikuta ndio umekwepa mikojo na kukanyaga kinyesi
 
Tena likipitia Mombasa Port itabidi ulipeleke mwenyewe Dar Port sijui Yard ya UDART likakaguliwe!😁

BTW:Hivi hao wanaotumia port ya Mombasa ukaguzi wa TBS utakuwa unafanyikia wapi?
 
TRA hawakwepeki. Tena ukipitishia bandari ya Mombasa ukifika hapo Namanga au Tarakea boda jiandae kupigwa mara mbili au tatu ya kodi za huku

Hakuna kitu kama hicho,calculator ya Tra iko wazi.

Inshu hapa ni je,TBS watakua na kituo chao huko mipakani au la!!
 
Sahv n mwendo wa kununua gari used humu humu,nyie wenye pesa zenu endeleen kujirusha mbele
 
Hakuna kitu kama hicho,calculator ya Tra iko wazi.

Inshu hapa ni je,TBS watakua na kituo chao huko mipakani au la!!
Exactly

Mimi nachokwepa ni hawa tbs.

Mi sijaelewa hadi sasa uamuzi wao wa kukagulia magari bandarini wakati zamani utaratibu ulikuwa mzuri ukaguzi unafanyikia japan na kama gari ni bovu utaambiwa uchague lengine au wakutemgenezee hilo bovu kwa gharama zao wenyewe.

Sasa haya mambo umeagiza gari yako, inspection unakuta inatumia hata mwezi alafu mwisho wa siku unaambiwa gari ni mbovu!!! unaambiwa bmw uliyoagiza inabidi uwekewe spea mpya na matengenezo jumla dola 2,000$, Holy cow!!!

Na hapo hata storage costs za kulaza gari yako huko gereji hazijaguswa, aisee!!

Na usalama wa spea zetu ni vp huko gereji??
 
Wewe toa hongo. Kwani unaogopa kutoa hongo? Hapa ni Africa na hongo haikwepeki. Toa hongo na uingize gari bila kusumbuliwa na yeyote. La sivyo pitia Mombasa.
 
Wewe toa hongo. Kwani unaogopa kutoa hongo? Hapa ni Africa na hongo haikwepeki. Toa hongo na uingize gari bila kusumbuliwa na yeyote. La sivyo pitia Mombasa.
Ni risk kubwa sana, huku tuna taasisi ya kupambana na rushwa na imenyakua wengi sana

unapotoa hio rushwa usiombee umpe mwenye long term goals kama anaetaka kupandishwa cheo na kupata publicity. atakurekodi na kukataa rushwa yako wazi wazi, akipeleka huo ushahidi kwenye taasisi mimi naenda jela yeye anapandishwa cheo na kupata headlines kwenye media.

Mambo ya rushwa huku yameweka watu wwngi ndani saizi, Ni kama mchezo wa russian roullete.
 
Na mafundi wenyewe wa kibongo unarudishiwa gari nati nyingine Amna na ubovu umeongezeka kwenye gari
 
Haya sawa basi. Una options mbili aidha uipitishie port za Tanzania au ya Mombasa. Naweza kukuhakikishia kwamba mzigo wako utakapofika kwenye port ya Mombasa hutalipa tax yoyote maana hio ni "good on transit". Utalipa tu storage fee. Halafu utalipa clearing and forwarding fee. Mambo ya ushuru utaenda kupambana na serikali yako mzigo utakapofika kwenye border.
 
Na mafundi wenyewe wa kibongo unarudishiwa gari nati nyingine Amna na ubovu umeongezeka kwenye gari
Dah, yani nakosa amani nikifikiria haya mambo, Unakuta fundi mwenyewe yupo field ya chuone, anajifunzia kwenye gari yako.
 
Hii inaitwa ukisimama nchale na ukikimbia nchale..
 
TRA hawakwepeki. Tena ukipitishia bandari ya Mombasa ukifika hapo Namanga au Tarakea boda jiandae kupigwa mara mbili au tatu ya kodi za huku
Utoe gari Mombasa ikapitie Namanga ?? , Afadhali hata tarakea Ila best ni horohoro Tanga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…